YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Tuesday 31 July 2012

MANENO YA MSG YA MH. ZITTO KWENDA KWA KATIBU MKUU WA NISHATI NA WAZIRI MHUSIKA

Katika Gazeti la leo la Majira kuna ujmbe unaodaiwa kuandikwa na Mh.ZZK kwenda kwaKatibu Mkuu wa Nishati na Waziri Mhusika wa Wizara Bw. Maswi na Prof.Muhongo. Naomba kuunukuu " Bw. Maswi alitumiwa na Bw. Zitto, unasomeka hivi; “Maswi, sijawahi gombana na wewe kwa kuwa nakuheshimu sana, tuhuma ambazo wewe na Waziri wako mnatoa dhidi yangu ni uwongo, uzushi na za kupikwa. Mwambie Waziri wako na wewe binafsi, sijawahi kushindwa vita ya kulinda credibility yangu, sipendi ujinga hata kidogo, mimi nina uhuru wa kusema ninachoamini, sina bei tupambane tu tuone nani ataumia,” ujumbe huo unasomeka hivyo

HII NDIO COPY YA BARUA YA UMOJA WA WASANII WALIOIANDIKA KWA KAMPUNI YA PUSH MOBILE

Hallow people...

MWEZI WA RAMSO BADO WATU WAJIRUSHA TU!!!

Wakuu wakikata vinywaji Mwezi Ramso..

Hwa nao wanacheza disco Mwezi Ramso...
Hallow people...

BAADA YA KUTOKA TANGA SASA NI ZAMU YA DSM, JIPANGENI SASA WAJA HAWA WATU.

Masta J kushoto, Madame Rita katikati, Salama kulia, makini kabisa kwa kuanza kazi iliowapeleka...

Monday 30 July 2012

TUNAJIVUNIA NINI KWENYE OLYMPIC WATANZANIA?

wanamichezo wa olympic wa kitanzania huko LONDON
Hallow people...

BAADHI YA MAGAZETI KWA SIKU YA LEO july 31, 2012

















Hallow people...

KAULI ZA BAADHI YA WABUNGE KUHUSU RUSHWA BUNGENI.


Baada ya kuwepo malalamiko ya rushwa kutembea bungeni na kusababisha kuvunjwa kwa kamati ya kudumu ya bunge ya Nishati na Madini mwishoni mwa wiki iliyopita, baadhi ya Wabunge wametaka majina ya wenzao wanaojihusisha na rushwa yawekwe wazi na wafukuzwe bungeni.
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari (CHADEMA)amesema pamoja na kwamba kamati ya nishati na madini imetajwa moja kwa moja, zipo kamati nyingine ambazo wabunge wake wanatajwa kuhusika na kuomba rushwa.
Amesema “zipo kamati kadhaa zinatuhumiwa kwa rushwa, Mh Spika nilikua naomba muongozo wako kwamba kwa nini ofisi yako isiamue kuzivuruga kamati kadhaa ambazo zinatuhumiwa kwa rushwa ikiwemo kamati ya kudumu ya bunge ya Serikali za mitaa inayoongozwa na Mh. Mrema na Kamati ya kudumu ya bunge ya Mashirika ya Umma inayoongozwa na Mh. Zitto Kabwe, hii ni kwa sababu wabunge wengi wamekua wanazikimbilia zile kamati ambazo zina mikataba lakini kamati kama ya maendeleo ya jamii ya huduma za jamii ambazo zina umuhimu mkubwa kwenye nchi kwa sababu hazina mikataba zinakimbiwa”
Mbunge wa Lindi mjini Salum Khalfan na mbunge wa Nkasi kaskazini Ally keissy Mohamed wamelitaka bunge kuwafukuza bungeni wabunge wote watakaogundulika kula rushwa, wanataka watajwe kwa sababu sasa hivi wabunge wengine kila wakipita barabarani wanakosa raha kutokana na hiyo kashfa ya rushwa iliyolichafua bunge.
Baada ya hayo Naibu Spika wa bunge Job Ndugai aliomba kamati ya uongozi wenyeviti wa kamati za bunge kukutana na Spika kulizungumza ili baadae wampe maelekezo zaidi.

Wednesday 25 July 2012

DENTI CHUO KIKUU ATAKWA NA AFARIKI DUNIA...


MWANAFUNZI wa Chuo Kikuu Cha Usimamizi wa Fedha, (IFM) jijini Dar es Salaam, Agnes B. King’unza (pichani), amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kuokotwa akiwa hajitambui katika ufukwe wa Bahari ya Hindi jirani na Coco Beach.
Habari za kipolisi zinasema Agnes alitekwa kisha akaokotwa na msamaria mmoja ambaye kwa taarifa za awali anatajwa kuwa ni mlinzi wa nyumba moja maeneo ya Coco Beach, ambako ndiko alikokutwa akiwa hajitambui.
“Polisi na hata watu wengine wanahisi kuwa msichana huyo alitekwa kisha kutupwa na watu wasiofahamika, baada ya kufanyiwa ukatili wa kutisha kwa kunyweshwa kitu kinachodhaniwa kuwa ni sumu,” kilisema chanzo chetu cha habari ndani ya jeshi la polisi.
Habari zinasema baadaye mwanafunzi huyo ambaye alikuwa akichukua shahada ya mambo ya kodi, alipelekwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay kisha askari hao wakamkimbiza Hospitali ya Agha Khan kwa matibabu.
Hata hivyo, habari zinasema madaktari wa Agha Khan baada ya kuona hali ya mgonjwa ilikuwa mbaya, walimpa rufaa na kumpeleka katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa uchunguzi na matibabu zaidi.
“Agnes alifariki jioni ya Julai 16, mwaka huu katika Hospitali ya Muhimbili na habari za kifo chake zilisababisha Chuo cha IFM kuzizima kwa wanafunzi kumlilia mwenzao,” kilisema chanzo hicho.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Charles Kenyela alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na akasema kwamba wasamaria wema walisema waliona Bajaj ikifika eneo alilotupwa Agnes wakadhani wanatupa mzigo.
“Walipokwenda kuangalia wakakuta ni mtu akiwa hoi hajitambui. Baada ya kupelekwa hospitali siku ya pili alikuja mama mdogo wa marehemu Agnes aitwaye Veronica Galus na akaleta taarifa kuwa binti yao huyo amefariki dunia. Polisi tunaendelea na uchunguzi kuwatafuta wahusika,” alisema Kenyela. Hata hivyo, kifo hicho kimeacha maswali mengi kuwa binti huyo alilishwa nini na nani?
Mzazi wa marehemu aliyetajwa kwa jina la Bernad King’unza mkazi wa Kimara Dar, hakupatikana kwa maelezo kwamba alikuwa safarini Iringa kwenye mazishi ya mpendwa wao huyo yaliyofanyika nyumbani kwao Kalenga, Iringa Julai 19, mwaka huu.

BREAKING NEWZZZ!!!!!!!

RAISI WA GHANA AFARIKI DUNIA NI RAISI, JOHN ATTA MILLS



Ni Raisi wa Ghana JOHN ATTA MILLS

HIZI NDIO STORI KUBWA ZA MAGAZETI LEO JULY 25, SAJUKI TENA, AZAM FC, VAN PERSIE, AJALI YA FM, NA ALIYEMTEKA ULIMBOKA HUYU HAPA











Hallow people...

HAWA NDIO WANAUME WATATU WALIOPOTEZA MAISHA KWA KUWAKINGIA VIFUA WAPENZI WAO.

Huyu ndio James Holmes mtuhumiwa wa mauaji ya watu 14 kwenye ukumbi huo wa Cinema, alijeruhi watu wengine 58 pia. hapa ni akiwa amefikishwa Mahakamani kwa mara ya kwanza.

Hallow people...

HAWA NDIO WANAOMVUTIA AFANDE SELE KUWA MBUNGE.


Siku zikiwa zinahesabika ili msanii Mfalme wa Rymes Afande selle kutangaza chama atakachogombea nacho Ubunge 2015 Morogoro Mjini, mkongwe huyu amekubali kuwataja wanasiasa ambao ndio wanamvutia, wanampa hamu na ushawishi wa hiyo kazi kutokana na wanayoyafanya.
Afande anaesema anayajua machungu ya wanamoro amekiri kwamba wanaomvutia kwenye siasa ni wengi lakini wachache wao sana sana ni Zitto Kabwe Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Halima Mdee wa Kawe na Burhani wa Lindi.
Amesema “mtu kama Zitto Kabwe ni mtu ambae ananipigia simu mara nyingi nikiwa na masahibu yangu ananishauri, namuheshimu sana na nafasi hii naitumia kumshukuru, yuko dada Halima Mdee wananionyesha kitu flani ambacho ninaweza kukifanya vilevile, kuna wabunge vijana kama Baruani kutoka Lindi japo ni Albino lakini ameonyesha kwamba Albino anaweza kuwa kiongozi mzuri kuliko hata watu wasio na ulemavu, wako wengi wananivutia hasa kutoka vyama vya upinzani”
Kwenye interview yake ya May 2012 na AMPLIFAYA, Afande alisema kuna vyama saba vya kisiasa vilivyomuita ajiunge navyo kugombea Ubunge lakini viwili ndio vyenye nafasi kubwa, kimoja kati ya CHADEMA au C.U.F
Alisema “kimsingi ndio vyama ambavyo hata namna ya kuvionganisha ningetamani siku moja viwe na sera moja na kuungana kuipigania nchi hii kwa sababu siamini kama kimoja bila kingine kati ya hivyo viwili kinaweza kuliangusha hili dudu kubwa ambalo lipo madarakani”

HII NDIO STORI KAMILI KUHUSU MWENYEKITI WA CCM MISUNGWI KUPIGWA CHINI.


Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi mkoa wa Mwanza imetengua na kumvua nafasi Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi Benard Pollycarp baada ya kukaidi maagizo na maelekezo yaliyotolewa na kamati hiyo kwa kamati ya siasa ya wilaya ya Misungwi hivi karibuni.
Katibu wa siasa na uenezi wa CCM Mwanza Simon Mangelepe amesema kutokana na maagizo iliyokua imeyatoa kwa kamati ya siasa ya wilaya ya Misungwi, ilimwita na kumuhoji Mwenyekiti huyo kisha kumtaka apime uzito wa tuhuma na kujiuzulu.
Pollcarp anatuhumiwa kwa kuhusishwa na ubadhilifu na wizi wa fedha za Halmashauri ya wilaya ya Misungwi kwenye taarifa ya mkaguzi mkuu wa hesabu CAG Ludovick Uttouh iliyozitaja halmashauri 33 nchini ambazo zimeripotiwa kutafuna fedha kinyume na taratibu.
Wakati uongozi wa CCM Mkoa ukichukua hiyo hatua tayari kuna stori za chinichini kwamba mwenyekiti huyo amekua akiendesha mipango ya chini kwa chini kuwahamasisha baadhi ya madiwani 26 wanaomuunga mkono waendelee kujiandaa kukihama chama hicho na kujiunga na chama kimoja cha siasa kwa madai kwamba taarifa ya CAG iligushiwa na kuchakachuliwa kwa lengo la kisiasa ikidaiwa kufanywa na kigogo mmoja wa ngazi ya kitaifa ambae anatoka kwenye wilaya ya Misungwi.