YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Sunday 20 January 2013

AJALI YA BASI LA NGANGA, MMOJA AFARIKI PAPO HAPO NA MAJERUHI ZAIDI YA 40 WAPELEKWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA


BASI LA NGANGA LILILOKUWALINATOKEA MBEYA KWENDA DSM LIMEPINDUKA ENEO LA IMEZU  MBEYA AJALI HIYO IMETOKEA MAJIRA YA SAA MBILI ASUBUHI ABIRIA MMOJA AMEFARIKI PAPO HAPO NA ZAIDI YA MAJERUHI 40 WAMEPELEKWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA ABIRIA ALIYEFARIKI AMETAMBUWA KWA JINA LA ENOCK LWILA MKAZI WA MAMA JOHN MBEYA NA NIMFANYABIASHARA MWANJELWA
BAADHI YA WAKAZI WA IMEZU WAMESEMA AJALI HIYO IMESABABISHWA NA MWENDO KASI
MWILI WA MAREHEMU ENOCK LWILA  UKIWA UMELAZWA CHINI KUSUBIRI WANA USALAMA KUJA UCHUKUA
MAREHEMU ENOCK LWILA AMEKUTWA NA ZAIDI YA SHILINGI MILION 15 KATIKA SOKSI NA KWENYE MIFUKO YAKE YA SURUALI INASEMEKEANA ALIKUWA ANAENDA DSM KUNUNUA BIDHAA MBALIMBALI ZA DUKANI KWAKE
HAPA WANAUSALAMA WAKIHESABU PESA WALIZOZIKUTA KWENYE MWILI WA MAREHEMU ENOCK HUKU WANANCHI WAKISIMAMIA KWA MAKINI ZOEZI HILO LA KUHESABU HIZO HIZO PESA ZAIDI YA SHILINGI MILION 15  ALIKUWANAZO MAREHEMU 

Saturday 19 January 2013

MAWAZIRI WAGUNDUA UHUNI BANDARINI JANA.


wabaini kuondolewa kipengele cha mkataba

DK-HARRISON-MWAKYEMBEMAWAZIRI wanne wamebaini kuondolewa kipengele ndani ya mkataba kinachomtaka mkandarasi wa Kampuni ya ujenzi ya Leinton ya Singapore kuiachia Mamlaka ya Bandari (TPA) vifaa vyenye thamani ya sh bilioni 3 baada ya kumaliza ujenzi.

Mkandarasi huyo ambaye amemaliza ujenzi wa mtambo wa mafuta bandarini, alitakiwa kuviacha vifaa hivyo.
Mawaziri waliobaini kuondolewa kwa kipengele hicho kilichokuwepo ndani ya mkataba, ni Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe; Waziri wa Viwanda na Biashara, Abdallah Kigoda;  Waziri wa Fedha na Uchumi, Wiliam Mgimwa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene.
Hayo yalibainika jana baada ya mawaziri hao kufanya ziara bandarini na kupata taarifa fupi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Madeni Kipande.
Akizungumza na wafanyakazi wa bandari, Dk. Mwakyembe alisema wamefanya ziara hiyo ya kawaida ya kutembelea chombo hicho muhimu katika kukuza uchumi wa taifa.

Alisema yeye na wenzake wamekubaliana kuwa wanahitaji maelezo haraka kuhusu watu hao waliondoa kipengele hicho kwenye mkataba, kwani hiyo ni hujuma na endapo mtambo huo utapata hitilafu watashindwa kufanya kazi.
Dk. Mwakyembe aliitaka bodi iitishe kikao cha dharura ili hadi leo lipatikane jibu kwani ana imani watu hao wanajulikana na hawapo mbali.

“Ni kitu cha kushangaza kuona mkataba uliokwishasainiwa unavunjwa kiujanja… kama mnavyofahamu mkataba ukishaafikiwa hakuna wa kuuvunja, sasa tunaomba hadi Jumatatu mtuletee jibu ili tulifanyie kazi kwa pamoja,” alifafanua Dk.  Mwakyembe.

Alisema wanasheria wapo na kama inavyofahamika mkataba ukishapitishwa hauguswi tena, hivyo kama yupo aliyekichomoa kipengele hicho basi atambue kuwa na yeye atachomolewa.
Mbali na hilo, akizungumzia mashine ya utambuzi wa mizigo kwenye makontena (Scan), inayosimamiwa na Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA), Dk. Mwakyembe alisema hawaelewi kulikuwa na sababu gani za msingi mashine hiyo kupelekwa Tanga ambako ni zaidi ya miaka miwili sasa haifanyi kazi.
 “Sasa kama haifanyi kazi imepelekwa kufanya nini au inacheza taarab?” alihoji Dk. Mwakyembe.

Aliiagiza TPA kuirudisha mashine hiyo ili ziweze kuwa mbili katika kuimarisha utendaji kazi wa Bandari ya Dar es Salaam.
Vilevile amewataka wafanyakazi hao kujijengea tabia ya uadilifu kwani hiyo ni moja ya njia itakayosaidia kuwajengea imani wateja wao wa ndani na nje ya nchi.

Awali Mkurugezi wa TPA, Kipande, alisema nchi inayotegemea usafirishaji wa mizigo kwa kutumia barabara iko hatarini kufilisika.
Alisema TPA inaomba serikali kuimarisha ujenzi wa reli zinazoelekea kwenye bandari zake zote zikiwemo zile maziwa.

MAWAZIRI WAGUNDUA UHUNI BANDARINI JANA.


wabaini kuondolewa kipengele cha mkataba

DK-HARRISON-MWAKYEMBEMAWAZIRI wanne wamebaini kuondolewa kipengele ndani ya mkataba kinachomtaka mkandarasi wa Kampuni ya ujenzi ya Leinton ya Singapore kuiachia Mamlaka ya Bandari (TPA) vifaa vyenye thamani ya sh bilioni 3 baada ya kumaliza ujenzi.

Mkandarasi huyo ambaye amemaliza ujenzi wa mtambo wa mafuta bandarini, alitakiwa kuviacha vifaa hivyo.
Mawaziri waliobaini kuondolewa kwa kipengele hicho kilichokuwepo ndani ya mkataba, ni Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe; Waziri wa Viwanda na Biashara, Abdallah Kigoda;  Waziri wa Fedha na Uchumi, Wiliam Mgimwa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene.
Hayo yalibainika jana baada ya mawaziri hao kufanya ziara bandarini na kupata taarifa fupi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Madeni Kipande.
Akizungumza na wafanyakazi wa bandari, Dk. Mwakyembe alisema wamefanya ziara hiyo ya kawaida ya kutembelea chombo hicho muhimu katika kukuza uchumi wa taifa.

Alisema yeye na wenzake wamekubaliana kuwa wanahitaji maelezo haraka kuhusu watu hao waliondoa kipengele hicho kwenye mkataba, kwani hiyo ni hujuma na endapo mtambo huo utapata hitilafu watashindwa kufanya kazi.
Dk. Mwakyembe aliitaka bodi iitishe kikao cha dharura ili hadi leo lipatikane jibu kwani ana imani watu hao wanajulikana na hawapo mbali.

“Ni kitu cha kushangaza kuona mkataba uliokwishasainiwa unavunjwa kiujanja… kama mnavyofahamu mkataba ukishaafikiwa hakuna wa kuuvunja, sasa tunaomba hadi Jumatatu mtuletee jibu ili tulifanyie kazi kwa pamoja,” alifafanua Dk.  Mwakyembe.

Alisema wanasheria wapo na kama inavyofahamika mkataba ukishapitishwa hauguswi tena, hivyo kama yupo aliyekichomoa kipengele hicho basi atambue kuwa na yeye atachomolewa.
Mbali na hilo, akizungumzia mashine ya utambuzi wa mizigo kwenye makontena (Scan), inayosimamiwa na Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA), Dk. Mwakyembe alisema hawaelewi kulikuwa na sababu gani za msingi mashine hiyo kupelekwa Tanga ambako ni zaidi ya miaka miwili sasa haifanyi kazi.
 “Sasa kama haifanyi kazi imepelekwa kufanya nini au inacheza taarab?” alihoji Dk. Mwakyembe.

Aliiagiza TPA kuirudisha mashine hiyo ili ziweze kuwa mbili katika kuimarisha utendaji kazi wa Bandari ya Dar es Salaam.
Vilevile amewataka wafanyakazi hao kujijengea tabia ya uadilifu kwani hiyo ni moja ya njia itakayosaidia kuwajengea imani wateja wao wa ndani na nje ya nchi.

Awali Mkurugezi wa TPA, Kipande, alisema nchi inayotegemea usafirishaji wa mizigo kwa kutumia barabara iko hatarini kufilisika.
Alisema TPA inaomba serikali kuimarisha ujenzi wa reli zinazoelekea kwenye bandari zake zote zikiwemo zile maziwa.

HAYA NI BAADHI YA MAGAZETI YA LEO NA STORI ZAKE KUBWA.



Posted: 19th January 2013 by MillardAyo in News
0
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

HAYA NI BAADHI YA MAGAZETI YA LEO NA STORI ZAKE KUBWA.



Posted: 19th January 2013 by MillardAyo in News
0
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

MWANDISHI WA GAZETI LA MWANAHALISI, SAED KUBENEA AJIPANGA KUGOMBEA UBUNGE KWA TIKETI YA CHADEMA


Mwandishi wa habari wa gazeti la Mwanahalisi Saed Kubenea, inasemekana amejapanga kugombea Ubunge Jimbo la Kibaha Mjini kupitia CHADEMA mwaka 2015. kwa hivi sasa Jimbo hilo linaongozwa na Silvestry Koka [CCM].

Hii itakuwa habari njema kwa tasnia ya habari kujiingiza katika masuala ya uongozi wa kisiasa, Kubenea kapata msukumo wa kugombea Ubunge baada ya kushauriana na Dr Slaa na kumuakikishia kuwa anaweza kushinda Ubunge Jimbo la Kibaha Mjini kama akijipanga vizuri na kupata msaada wa CHADEMA.

Kila la Heri Saed Kubenea

WAKE ZA WATU 13, WANAFUNZI 18, MAHOUSE GIRL 7 NA MABAAMEDI 5 WANASWA WAKIJIUZA



HAIWEZI kuwa aibu mpaka siri ifichuke, kwa wake za watu 13 walionaswa wakijiuiza, kwao imekuwa zaidi ya kuumbuka, wametia fedheha ndani ya familia zao.

Wake hao za watu, walinaswa usiku wa Jumanne iliyopita, Barabara ya Shekilango, kuanzia Afrika Sana mpaka Mori, Sinza, Dar es Salaam, wakati jeshi la polisi lilipofanya msako maalum wa kushtukiza.
 Pamoja na wake hao za watu, vilevile wanafunzi 18 wa vyuo mbalimbali nchini, mahausigeli saba na mabaamedi watano, arobaini yao ilifika siku hiyo, walipokamatwa na kupelekwa Kituo cha Polisi Kijitonyama, Mabatini kabla ya kupandishwa kizimbani, Mahakama ya Jiji siku iliyofuata.

Katika msako huo, zaidi ya makahaba 60 walikamatwa na katika mahojiano na polisi, ikabainika kuwapo kwa wake hao za watu, wanafunzi, wahudumu wa baa na wafanyakazi wa ndani.

WAKE ZA WATU.......
Jeshi la polisi likichukua maelezo ya mmoja baada ya mwingine, askari mmoja alimfikia mwanamke aliyefahamika kwa jina la Suzan Moses ambaye katikati ya mahojiano, alijieleza kwamba ni mke wa mtu.

Suzan ambaye baadaye ilibainika kwamba hujulikana pia kwa jina la Mamaa Suzy, alijieleza kuwa anaishi na mume wake  Tandale, Dar es Salaam na wana watoto wawili.

Askari aliyekuwa anamhoji Suzan, aliuliza: “Mke wa mtu kweli na watoto wawili unajiuza, huoni kama ni hatari?”

Suzan: “Hatari naijua ndiyo maana simruhusu mwanaume yeyote aniingilie bila kondomu, nipo makini juu ya hilo.”

Askari: “Mumeo anajua kama unajiuza?”

Suzan: “Hajui, japokuwa hata yeye tulikutana viwanja. 

Nilimdanganya mimi ni mhudumu wa Corner Bar, akaniachisha kazi lakini baada ya kuona hanitimizii mahitaji muhimu, nikamwambia narudi kazini, kwa hiyo mpaka leo anajua nahudumia baa.”

Baada ya wote kuhojiwa, ikabainika kuwa katika wanawake hao 60 waliokamatwa, mbali na Suzy, walikuwepo wengine 12 ambao ni wake za watu.

Mwanamke mwingine, Jessica Mashaka alidai kuwa aliamua kujiuza baada ya kubaini kwamba mume wake analelewa na mwanamke mmoja tajiri jijini Dar es Salaam.

“Anachokifanya mume wangu ni sawa na mtu anayejiuza. Akipewa fedha na mwanamke wake ananinyanyasa ndani ya nyumba, nikaona na mimi nijiuze nipate fedha zangu mwenyewe ili aache kuninyanyasa.”
 
Hata hivyo, Leila Madaha alidai yeye na mume wake walikubaliana ajiuze ili wawe wanapata fedha za kujikimu.

 Alisema: “Mume wangu huwa ananisisitiza kutumia kondomu kwa kila mteja, yeye hana kazi tangu alipofukuzwa bandarini miaka minne iliyopita.”
 WANAFUNZI......
Wanafunzi 18 kutoka vyuo vya Dar es Salaam, Dodoma na Iringa, walijitambulisha katika mahojiano na hayo na polisi.

Wanafunzi wa mikoani walisema kuwa hali ni mbaya kibiashara huko tangu iingie Januari ndiyo maana wamekuja Dar kujaribu kutafuta kipato.

MABAAMEDI NA MAHAUSIGELI.......
Katika wanawake hao, ilibainika wapo mabaamedi watano ambao walidai kuwa vipato vyao ni vidogo ndiyo maana kila baa wanazofanyia kazi zinapofungwa saa 5:00 usiku, hulazimika kuingia mitaani kuuza miili waweze kupata fedha zaidi za kuwawezesha kuishi.


Vilevile, wapo mahausigeli saba ambao maelezo yao yalikuwa sawa na yale ya mabaamedi kwamba hulipwa ujira mdogo na mabosi wao ndiyo maana hulazimika kujiuza ili kuongeza vipato.