YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Sunday 14 April 2013

TAMKO LA CHADEMA KUHUSU NJAMA ZA KUKICHAFUA ZINAZOFANYWA NA GENGE LA VIONGOZI WAKUU WA CCM NA VYOMBO VYA DOLA, LIMETOLEWA JIJINI DAR ES SALAAM LEO, MACHI 14, 2013 NA MJUMBE WA KAMATI KUU NA MWANASHERIA WA CHAMA, MH. MABERE NYAUCHO MARANDO


Ndugu waandishi wa habari;
LEO tumewaita hapa ili kuwaomba mtufikishie ujumbe kwa Watanzania, kwamba nikiwa mwanasheria na mtu ambaye nimepata ujuzi wa kazi za ushushu, nimefanya uchunguzi matukio haya ya utekaji na utesaji na kugundua mambo mengi mno.

Uchunguzi huu nimeufanya kabla na baada ya kukamatwa kwa Mkurugenzi wetu wa Ulinzi na Usalama, Willifred Muganyizi Lwakatare, ambaye hivi sasa anashitakiwa mahakamani kwa tuhuma za kupanga ugaidi.

Nimefanya hivyo kwa kuangalia maslahi mapana ya taifa langu na chama changu. Katika uchunguzi wangu huo, nimegundua mambo mengi ikiwamo kuwapo kwa genge la watu ndani ya serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanaopanga mipango hii ya kishetani na kisha kuwasingizia watu wengine.

Angalieni mfano huu: Unaoitwa na polisi na Mwigulu Nchemba, “mkanda wa Lwakatare” unadaiwa uliwasilishwa jeshi la polisi Desemba mwaka jana. Lakini jeshi hilo halikumkamata yoyote wala kumhoji, hadi pale Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda, alipovamiwa na kuumizwa. 

Aidha, Nchemba amedai kumiliki video ile Desemba mwaka jana, lakini rekodi hiyo iliwekwa kwenye mitandao ya kijamii (YouTube na Jamii Forum) baada ya kutekwa kwa Kibanda. Hapa mtu makini anaweza kujiuliza, hiki kimelenga nini? 

Kwamba genge hili la kina Nchemba na wenzake, walipanga kumteka Kibanda, wakatimiza lengo lao hilo, baadaye wakaingia kwenye plani B ya kutaka kuihusisha Chadema. Wakamtumia Ludovick Joseph Rwezahula ambaye ni mshitakiwa wa pili katika kesi ya Lwakatare, kufanikisha mkakati wao huu wa kishetani. 


Bonyeza Read more kuendelea






Ndugu waandishi wa habari;
Huu ni mchezo mchafu na wahatari mno ambao kwa vyovyote vile, haupaswi kuvumiliwa. Kuanzia sasa nimeamua kwa dhati kabisa, kukomesha mchezo huu ambao unahatarisha uhai wa taifa letu.

Kwa kuanzia, kesho Jumatatu, nitaongoza jopo la mawakili sita wa Chadema kumtetea Bw. Lwakatare. Wenzangu wengine katika kesi hii, ni Profesa Abdallah Safari, Tundu Lissu, Edson Mbogoro, Peter Kibatara na Nyaronyo Kicheere. Huko mbele tutaongeza mawakili wengine, akiwamo mmoja anayewekwa na familia ya Lwakatare. 

Ndugu waandishi wa habari;
Mnaweza kujiuliza, kwa nini Chadema kimechukua uamuzi huu wa kuweka kundi kubwa la wanasheria katika kesi hii ya Lwakatare? Jibu ni kwamba tumegundua kuwa kesi hii imefunguliwa kwa lengo maalum la kuidhoofisha Chadema na kuinusuru CCM ambayo inakabiliwa na dhahama ya kushindwa katika uchaguzi mkuu ujao kutokana na kushamiri kwa makundi. 

Hivyo wameamfungulia kesi Lwakatare, kwa lengo la kutaka kuaminisha umma kuwa Chadema ni chama cha magaidi, kinapanga ugaidi na hivyo kichukiwe. Hilo ndilo lengo lao. Basi!

Ndugu waandishi wa habari; 
Pili, nitakwenda mahakamani kuwasilisha ombi maalum la kuomba amri ya mahakama kuagiza makampuni ya simu za mkononi kuwasilisha mahakamani statement za simu za watu kumi (10) ili kusaidia mahakama kutenda haki na jamii kujua ukweli wa mambo haya. 

Watu ambao nitaomba mahakama itoe amri ya kuletwa taarifa zao simu 
na meseji (sms) ni Naibu Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa nchini (TISS), Jack Zoka, anayetumia simu Na. 255756809535, Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mwigulu Lameck Nchemba, anayetumia simu tano zikiwamo 0754 008888, 0757 946223, 0714 008888 na 0787 513446 na Ludovick Joseph Rwezahula, ambaye simu zake ni,0715 927100 na 0753 927 100.

Mwingine ambaye mawasiliano yake yanahitajika, ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Emmanuel Nchimbi, anayetumia simu Na. 0754 003388, Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Mwananchi, Dennis Msaky anayetumia simu mbili, 0655 331010 na 0764 331010 na Bw. Sinbad Mwagha, ambaye ni afisa wa idara ya usalama wa taifa, anayetumia simu 0754 006355. 

Wengine, ni Bw. Shaali Ali, afisa mwinge wa usalama wa taifa anayetumia simu Na. 0716990099, Saumu K. Malungu, mwenye kutumia simu 0719 541 434 na 0789 614 629, simu mbili zinazotumiwa na mtuhumiwa mkuu wa utekaji wa Dk. Steven Ulimboka, Bw. Ramadhani Abeid Igondo ikiwamo 0713 760 473, simu za Bw. Ridhiwani Kikwete ambazo ni 0754 566299, 0784 566 299, simu ya Dr. Steven Ulimboka, ambayo ni 0713 0713 731 610, pamoja na simu zote tatu za Willifred Lwakatare, ambazo ni 0786 774697, 0713 237869 na 0758 417169.
Ndugu waandishi wa habari; 
Mtu mwingine muhimu nitakayeomba mahakama itoe amri ya kutolewa kwa taarifa zake, ni mwandishi wa habari na mpigapicha wa magazeti ya serikali, Muhidini Issa Michuzi. Mwandani huyu wa Ikulu, ndiye aliyeandika ujumbe kwa njia ya emeili kuipongeza ofisi binafsi ya rais (OBR) na usalama wa taifa kwa kupata video ya Lwakatare. 

Pongezi za Michuzi kwa TISS ndizo zinanisukuma kuiomba mahakama kuagiza kupatikana taarifa zake. Michuzi anaipongeza TISS kwa kuibua njama za wahalifu, lakini mimi ninajua TISS ikipata njama za aina hiyo haraka inapeleka ushahidi polisi, lakini huu wa Lwakatare ulipelekwa Youtube, badala ya kwenye vyombo vya sheria.

Maneno ya Michuzi kwamba ni TISS imeibua hiyo video yanathibitisha ushiriki wa TISS kwenye mchezo huo mchafu, na kwamba Chadema kinajua kuwa Michuzi alishirikiana na watu wa usalama wa taifa katika kazi hiyo chafu. Software za video (editing) walizotumia zilitoka kwake. Fedha ya kuandaa hiyo video zilitoka usalama na Ikulu. Tunajua kuwa wale vijana wa Ada Estate na yule jamaa anayempelekea kigogo wa Jamii Forum, walilalamika sana kwa mmoja wa wamiliki wa JF. 

Ndugu waandishi wa habari;
Chadema kinajua kuwa mmoja wa watuhumiwa hawa, Mwigulu Nchemba anafanya mipango na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom ili kumsaidia kufuta taarifa zake. Nachukua nafasi hii, kuionya kampuni hiyo kuacha kucheza mchezo huo kwa kuwa ni kinyume cha sheria za mamlaka ya mawasiliano (TCRA).

Tunahitaji mawasiliano haya kwa kuwa Mwigulu – zinaonyesha mtuhumiwa huyo akifanya mawasiliano mfululizo na Ludovick, yakiwamo yale ya tarehe 4 Machi 2013. Hii ilikuwa siku moja kabla ya Kibanda kutekwa.

Ndugu waandishi wa habari;
Hawa niliowataja ni watu muhimu sana katika upangaji wa mkakati wa utengenezaji wa video ya Lwakatare na vitendo vya kihalifu vya utekwaji wa Kibanda na tukio la kutekwa na kisha kutupwa msutuni kwa mwenyekiti wa Jumuiya ya madaktari nchini, Dr. Steven Ulimboka.

Kwa mfano, simu ya Mwigullu Nchemba, namba 0714 008888, 0756 008888 na 0757 946223, zimefanya mawasiliano mara kadhaa na Ludovick Joseph, Saumu K. Malungu, Jack Zoka, Ali Shaali na Ramadhani Ighondo. Mawasiliano hayo yalifanyika katika kipindi ambacho mgomo wa madaktari ulishamiri; baadaye yakarudi tena kati ya 26 Desemba mwaka jana na 15 Machi mwaka huu.

Miongoni mwa mawasiliano ambayo tunaona yanahusika na ujambazi huu, ni yale ya 28 Desemba, siku ambayo mkanda wa Lwakatare umerekodiwa; tarehe 4 hadi 6 Machi 2013, siku moja kabla ya Kibanda kutekwa na yale ya usiku wa manane (saa 8:17) wa 13 Machi 2013, ambako mchana uliofuata Lwakatare alikamatwa. 
Huyu Mwagha ndiye aliyekuwa anatumika kuwasiliana na Saumu Malungu, ambaye tulimtaja kuwa ndiye aliyekuwa amepewa kazi na Mwigulu na usalama wa taifa, kurubuni vijana wetu kwa fedha ili kutoa ushahidi wa uongo juu ya video ya Lwakatare.

Vilevile, mawasiliano ya Mwiguluna Mwagha, katika kipindi hicho nayo tunayahitaji. Kwa sababu, huyu Mwagha anayetumia simu 0754006355, mbali na kuwasiliana na Mwigulu, ndiye aliyekuwa anawasiliana na mmoja wa waliomteka Ulimboka; na ndiye aliyewasiliana na Saumu kati ya 20Januari na Machi 6 mwaka huu.

Ndugu waandishi wa habari;
Ludovick alifanya mawasiliano ya mwisho na Joyece Agustine, ambaye anatumia simu Na. 0717 559210, mawasiliano ambayo yalifanyika saa 5:13 usiku. Hiyo ndiyo ilikuwa simu yake ya mwisho usiku huo; katika siku hiyo Ludovick aliwasilisna na Joyce mara tisa kuanzia saa 12: 54 asubuhi.

Kwa mujibu wa taarifa za kwenye mtandao wa Jamii Forum, ambako video ya Lwakatare ilitumwa, Ludovick alikamatwa Machi 15 mwaka huu. Hata hivyo, rekodi katika simu yake Na. 0715 927100 inaoyesha 17 Machi Ludovick alifanya mawasiliano na Joyce Augustino. Mawasiliano hayo yalifanyika saa 8: 9 usiku, wakati inadaiwa na polisi alishakamatwa.

Naye mhariri wa Mwananchi, Bw. Msaky ambaye anatajwa kutaka kutekwa na Ludovick na Lwakatare, amekuwa na mawasiliano kadhaa na Ludovick – mtu anayepanga kumteka. Ludovick na Msaky walifanya mawasiliano mfululizo kati 27 Desema 2012, siku moja kabla ya video ya Lwakatare haijarekodiwa na 7 Machi siku moja baada ya Kibanda kutekwa. 

Msacky alitumia simu zake hizo mbili (0764 331010 na 0655 331010) kuwasiliana na Ludovick, huku Ludovick akitumia 0753927100. Mawasiliano ya 31 Desemba yalifanyika Ludovick akiwa Tegeta, jijini Dar es Salaam. Mawakala hawa wawili wa usalama wa taifa (Ludovick na Msaky), walikutana 31 Desemba 2012, katika hoteli ya Tamal, Mwenge jijini Dar es Salaam.

Ndugu waandishi wa habari;
Baada ya kupitia taarifa hizi za mawasiliano ya simu za Mwigulu Nchemba, Ludovick Joseph, Ramadhani Ighondo na Saumu Malungu tumegundua yafuatayo: Kwamba, Ramadhani Ighondo, amefanya mawasiliano mara nyingi na Mwigulu, Mwagha na Zoka; naye Mwagha amefanya mawasiliano na Mwigulu na Saumu; naye Saumu amefanya mawasiliano na Mwagha, Mwiguluna Shaali Ali, ambaye ni afisa usalama wa taifa.

Tumegundua vilevile, kuwapo mawasiliano kadhaa kati ya Ludovick na Msaky; Ludovick na Mwigulu; Msaky na Nchimbi; Msaki na Mwagha, Samu na Mwagha na Ramadhani Ighondo Abeid, anayetuhumiwa kumteka Dk. Ulimboka na Mwanga na Mwigullu.

Tumegundua pia kuwapo mawasiliano kati ya Ulimboka na Ramadhani; Zoka na Ighondo na Ridhiwani na Ighondo. Mawasiliano haya yalifanywa mfululizo usiku wa Juni 2012 siku ambayo Dk. Ulimboka alitekwa.

Tumepata kufahamu pia kwamba baadhi ya watu waliotajwa na gazeti la MwanaHALISI kuwa waliwasiliana na Ighondo usiku wa Juni 26, mwaka 2012, wamefanya mawasiliano pia na Mwigulu, Mwagha na Shaali Ali.

Ndugu waandishi wa habari;
Mwagha ni afisa usalama wa taifa anayefanyakazi makao makuu ya idara hiyo. Ndiye yule anayetumika kuendesha michezo ya kuhonga wanasiasa wa CCM na upinzani. Ni Mwagha anayepanga wabunge na kuwapanga waongee nini kwa maslahi ya CCM. Ushenzi wote anaoongea Mwighulu bungeni, hupewa na Mwagha kwa maelekezo ya Jack Zoka.

Naye Shaali ndiye aliyekutana na afisa wetu wa usalama, Ahmed Sabula na mwenzake, Machi 29 mwaka huu katika hoteli ya See Cliff jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo kati ya Sabula, kijana wetu wa usalama na afisa usalama wa serikali Bw. Shaali alitaka Sabula akubali kutumika kwa kutoa taarifa za vikao vya chama, kuwasilisha kwake nyaraka za kamati kuu na kueleza mipango ya chama katika kesi ya Lwakatare. 

Kwenye mpango huu, afisa huyo wa usalama wa taifa ambaye ninamfahamu vizuri, alimuahidi Sabula kiasi cha Sh. milioni 30 na kwamba fedha hizo angelipwa wiki iliyopita. Aliahidiwa pia kwamba kila nyaraka atakayopeleka atalipwa ujira. 

Aidha, Sabula aliahidiwa kulipwa shilingi 500,000 (laki tano) kila mwezi; afisa wetu huyu ameripoti tukio hilo kwa viongozi wake wa chama. Yule mwenzake aliandaliwa kuwa shahidi wa kesi ya Lwakatare; aliambiwa akikubali dili hiyo atalipwa kila mwezi Sh. 500, lakini akaombwa kuwa mvumilivu kwa kuwa atalazimika kupotea kwa miezi kama mitano hadi sita.

Ndugu waandishi wa habari;
Kitendo cha Mwigulu kuwasiliana Ramadhani Ighondo, Mwigulu kuwasiliana na Ludovick, Saumu kuwasiliana na Mwigulu, Ighondo kuwasiliana na Ulimboka, Zoka kuwasiliana na Ighondo, tena katika muda uleule ambao Ighondo amewasiliana na Ulimboka na Saumu kuwasiliana na Mwagha, ni uthibitisho tosha kwamba usalama wa taifa wako nyuma ya mipango hii ya michafu ya kupanga utekaji na kisha kutaka kukichafua Chadema.

Aidha, kitendo cha Ludovick kuwasiliana Msaky; Ighondo kuwasiliana na Mwagha, Ridhiwani Kikwete kuwasiliana na Ighondo, tena kila baada ya Ighondo kuwasiliana na Ulimboka na Jack Zoka, ni uthibitisho mwingine kuwa genge hili la wahalifu linashirkiana na baadhi ya watu kutaka kuangamiza taifa.

Ni uthibitisho tosha kwamba hawa ndiyo wanaowahonga wanachama wa Chadema na watu wengine ili watoe ushahidi feki dhidi ya Lwakatare, na kwamba ni usalama wa taifa walioandaa ile video uchwara inayopigiwa chapuo na Mwigulu.

Ndugu waandishi wa habari;
Chama Cha Mapinduzi kinajua kwa hali ya sasa hakiwezi kushinda uchaguzi wa mwaka 2015 huku Chadema ikiwa katika hali nzuri ya kisiasa tunayoiona sasa. Wanajua kabisa CCM imegawanyika, kundi lolote litakalopita ndani ya CCM, litahujumu kundi jingine. Ni kama ilivyotokea uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki.

Ndiyo maana wanapanga kila mbinu kutaka kuiangamiza Chadema. Nasi tunasema katu hatutakubali kuona Chadema kinakufa. Tutapambana usiku na mchana. Juna na mvua. Hadi tushinde hila hizi.Tunawaambia wanachama wetu na wale wanaotuunga mkono, Chadema ni chama kikubwa. Kina mtandao kila mahali, kuanzia Ikulu hadi polisi; na hivyo hakitakufa au kuzorota kwa mambo ya kupikwa.

Ni imani yangu kwamba amri ya mahakama itawafichua wote hawa ni kuirudisha Tanzania katika amani yake. Ni lazima tufikike mahala watu hawa wafahamike mbele ya umma, tunataka wafahamu kuwa maisha ya mwanadamu yana thamani kuliko siasa chafu na ufisadi wanaouendeleza. 

Nawashukuru kwa kunisikiliza.

Mabere Marando,
Dar es Salaam

Mwandishi akamatwa tuhuma za kushambuliwa kwa Kibanda





Posted  Jumapili,Aprili14  2013  saa 24:56 AM
KWA UFUPI
Habari zilizolifikia gazeti hili jana mchana na baadaye kuthibitishwa na polisi zinasema Mjengwa alikamatwa muda wa asubuhi na kwamba alikuwa akihojiwa na makachero wa jeshi hilo hadi alasiri kuhusu tukio la kuteswa kwa Kibanda.

Dar es Salaam:  Mwandishi wa safu katika magazeti mbalimbali nchini, Majid Mjengwa amekamatwa na polisi kwa tuhuma za kuhusika na tukio la kushambuliwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana mchana na baadaye kuthibitishwa na polisi zinasema Mjengwa alikamatwa muda wa asubuhi na kwamba alikuwa akihojiwa na makachero wa jeshi hilo hadi alasiri kuhusu tukio la kuteswa kwa Kibanda.
Msemaji Mkuu wa Polisi Advera Senso aliliambia Mwananchi kwamba:
“Ni kweli kwamba tunaye, tunaendelea kumhoji, tunachoomba ni kwamba mtupe nafasi ili tufanye kazi yetu na kukiwa na jambo lolote tutawajulisha.”
Hata hivyo, Senso hakuwa tayari kueleza kwa undani muda aliokamatwa Mjengwa wala sababu za kukamatwa na kuhojiwa kwake, lakini chanzo chetu ndani ya Jeshi la Polisi kilithibitisha kwamba pamoja na mambo mengine kuhojiwa kwake kulihusu uteswaji wa Kibanda.
Jumatatu wiki hii, Kaimu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Nchini, Issaya Mngulu alisikika akizungumza na Kituo cha Radio One cha Dar es Salaam kwamba kesho Jumatatu (April 15, 2013) polisi watatoa taarifa rasmi ya hatua waliofikia katika upepelezi wa kesi ya Kibanda.
Kwa upande wake Mia Mjengwa ambaye ni mke wa Mjengwa, alisema mumewe alipata wito kutoka polisi makao makuu Alhamisi na kwamba juzi Ijumaa alisafiri kutoka Iringa kwenda Dar es Salaam kuitikia wito huo.
“Ninachojua ni kwamba aliitwa kwenda polisi na leo (jana) alinipigia simu kama saa 7:00 mchana na aliniarifu kwamba yupo polisi, sasa tangu wakati huo sijaongea naye tena na wala simu zake hazipatikani,” alisema Mia na kuongeza: “Kwa hiyo mimi kwa kweli sifahamu kwamba anahojiwa kwa sababu gani.”
Taarifa za kukamatwa kisha kuhojiwa kwa Mjengwa ambaye pia ni mmiliki wa Mjengwa Blog, zimekuja siku chache tangu msaidizi wake katika Blog hiyo, Joseph Ludovick akamatwe, kuhojiwa kisha kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za ugaidi.
Ludovick alifikishwa mahakamani pamoja na Mkurugenzi wa Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Willifred Lwakatare wakikabiliwa na tuhuma za ugaidi na kupanga kumteka Mhariri Mtendaji wa Mwananchi, Dennis Msacky.
Kuteswa Kibanda
Machi 5, mwaka huu saa 5.30 usiku, Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Kampuni ya New Habari (2006) Ltd, alinusurika kifo baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana nyumbani kwake kisha kupigwa na kujeruhiwa vibaya.

MAAJABU HUKO GEITA, ALIYEFARIKI MIAKA ILIYOPITA AONEKANA AKIWA HAI.


mwanamke anayedaiwa kufariki miaka mitano iliyopita 


Posted  Jumapili,Aprili14  2013  saa 24:51 AM
KWA UFUPI
Inadaiwa kwamba Flora Onesmo (45) alifariki Februari 28, 2008 katika Hospitali ya Wilaya ya Geita na kuzikwa katika Kijiji cha Nakasenya, Kata ya Butundwe, lakini juzi alfajiri alikutwa ameketi nje ya nyumba ya dada yake aitwaye Monica James, anayeishi Kasamwa.

MBOWE NA DR SLAA WAKATAA HUJUMA KWA CHADEMA.



Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akizungumza kwenye kongamano la chama hicho lililofanyika jana jijini Dar es Salaam. Picha na Fidelis Felix. 


Posted  Jumapili,Aprili14  2013  saa 24:41 AM
KWA UFUPI
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa wamesema “hawatakubali wala kuvumilia” hujuma dhidi ya chama chao.
SHARE THIS STORY
 
 
0
Share
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa wamesema “hawatakubali wala kuvumilia” hujuma dhidi ya chama chao.
Dar es Salaam. Viongozi hao kwa nyakati tofauti jana walisema hujuma hizo zimekuwa zikifanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na Serikali ambayo imekuwa ikitumia vyombo vya dola na kwamba sasa wanapanga ugaidi wa kuwateka maofisa wa ngazi ya juu wa Chadema.
Suala la ugaidi liliibuka kwa nguvu katika wiki ya kwanza ya Bunge la Bajeti na sasa limehamia nje ya chombo hicho cha kutunga sheria kutokana na Chadema kuwatuhumu CCM na Serikali yake kwamba wanapanga njama za kuwateka maofisa wakuu wa chama hicho.
Jana Dk Slaa alipokuwa akimkaribisha Mbowe kufungua  Mkutano wa Mafunzo na Mipango ya Vuguvugu la Mabadiliko ‘M4C’ na Kongamano la Katiba Mpya kwa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, alisema taarifa walizonazo zinaonyesha kuwa CCM ndiyo wanaofanya vitendo vya kigaidi wakishirikiana na Serikali.
“Tuna taarifa zote zinazoonyesha kwamba CCM ndiyo magaidi wakishirikiana na  Serikali yake, lakini sisi tuko makini kuliko hata Serikali ya CCM na tuko makini kuliko hata Usalama wa Taifa na umakini huu ndiyo utakaotupeleka Ikulu mwaka 2015,”alisema Dk Slaa.
Hata hivyo Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alipotafutwa kujibu tuhuma hizo alisema hakuna jipya ambalo Chadema wamelisema.
“Kuna jipya katika hilo, ni yale yale ya kawaida na jana (juzi) Mwingulu alizungumza vizuri sana bungeni. Hiyo ni sawa na mchawi anapomwangia mtu na kufa anakuwa wa kwanza kwenda kulia msibani, nchi siku yoyotete haijengwi kwa ngonjera za maneno bali inajengwa kwa mipango,”alisema Nape.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alipotakiwa kutoa msimamo wa Serikali juu ya tuhuma hizo alisema, “Mimi siwezi kuzungumza ila mtafute Waziri (Dk Emmanuel Nchimbi),”alisema Silima.
Alipotafutwa Dk Nchimbi kupitia simu yake ya  mkononi, ilikuwa ikiita bila kupokewa.
Kauli ya Mbowe
Kwa upande wake Mbowe alisema, CCM imekuwa ikitumia mbinu mbalimbali kuhakikisha inakisambaratisha chama hicho bila mafanikio.
“Watu wa Usalama wa Taifa wakishirikiana na CCM wamekuwa wakifanya mipango ya kutaka kuwateka maofisa wetu. Hawa watu ni wepesi sana na msiwaogope hata kidogo,”alisema Mbowe huku akishangiliwa na wanachama na makada waliofurika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Blue Pearl.
Mbowe alisema: “Ukiona chama chochote tawala kinatumia jeshi la polisi kutengeneza ushahidi wowote wa kihalifu hiyo ni dalili ya hatari kwa mustakabali wa usalama wa nchi.”
Mbowe alisema mbinu za sasa za CCM zinatokana na kushindwa kukivuruga chama hicho kwa propaganda kuwa ni chama cha familia, ukabila, ukanda na baadaye udini.
Katiba na Elimu
Kuhusu mchakato wa Katiba Mpya, Mbowe alisema ikiwa itafika Aprili 30 mwaka huu bila hatua zozote kuchukuliwa, watamwamuru mjumbe wa tume hiyo kutoka Chadema, Profesa Mwesiga Baregu kujiondoa.

MAGAZETI JUMAPILI APRIL 14 2013


0
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
..
..
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

HAWA NDIO WANAMUZIKI 10 MATAJIRI AFRIKA, WA AFRIKA MASHARIKI YUKO MMOJA TU, KOFFI OLOMIDE JE?


1
.
Wa mwisho ni Jose Chameleone.
Stori imeandikwa na mtvbase.com
Unaweza kuwa karibu na mimi kupitia instagram.com/millardayo twitter.com/millardayo na facebook.com./millardayo ili kupata Breaking News, stori za michezo na mengine ya fastafasta

VIDEO INAYOONESHA MALUMBANO KATI YA TUNDU LISSU NA MWIGULU KUHUSU UGAIDI LEO BUNGENI



KWA WALE WALIOKOSA KUANGALIA SAKATA LA MWIGULU  NA  TUNDU  LISSU KUHUSU UGAIDI WANAWEZA KUBOFYA HAPO NA KUJIONEA HALI ILIVYOKUWA.

Thursday 11 April 2013

AJARI YAUA WAANDISHI WA HABARI NA OFISA UHAMIAJI TANGA


Hussein-Semdoe-wa-MwananchiWAANDISHI wa habari wawili pamoja na Ofisa Uhamiaji wa Wilaya ya Handeni wamefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea leo majira ya saa nne asubuhi nje kidogo ya Mji wa Handeni. Waliofariki dunia ni Hussein Semdoe wa mwandishi wa gazeti la Mwananchi, Hamis Bwanga wa Radio Uhuru na Abood pamoja na Mariam Hassan ambaye ni Ofisa Uhamiaji Wilaya ya Handeni.




Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo pamoja na vifo vya marehemu hao. Akizungumza na thehabari.com mchana huu, Mkuu wa Wilaya hiyo alisema ajali hiyo imetokea wakiwa kwenye …read more
Source: thehabari.com

HII NI KAULI YA NAIBU WAZIRI MULUGO KUHUSU WANAOSEMA KAGUSHI VYETI VYA ELIMU YAKE

2
.
hii habari imeandikwa na mtanzania.co.tz unaweza kuingia na kusoma habari nyingine pia.

MAMBO YA GOAL TECHNOLOGY SASA YAMEFIKA HAPA.

2
.
.
Kampuni ya Uingereza ya Hawk Eye imepewa mkataba wa kufunga na kuendesha mifumo ya teknolojia ya mstari wa goli maarufu kama Goal Line Technology kwa timu zinazoshiriki ligi kuu ya England.
Maamuzi hayo yamefanyika kwenye mkutano wa vilabu vya ligi hiyo ambavyo vimeridhia matumizi ya teknolojia hiyo kuwasaidia waamuzi kutambua pale goli linapofungwa.
.
.
Mara ya mwisho kampuni hiyo ambayo inatoa huduma kama hiyo kwenye michezo ya Cricket na Tenis ilishindwa na kampuni ya Goal Control ya Ujerumani ambayo imezawadiwa tenda ya kufunga mifumo ya Goal Line Technology kwenye michuano ya Kombe la mabara na tayari imeanza kufanya kazi ya majaribio ya kufunga camera kwenye uwanja wa St Mary’s wa timu ya Southampton.
Tayari chama cha soka cha England FA kimepitisha matumizi ya teknolojia hiyo kwenye uwanja wa Wembley ambapo itaanza kutumika kwenye mchezo wa ngao ya Jamii mwezi Agosti 2013.

KUTANA NA MWANZILISHI WA BLOG TANZANIA NA MAHOJIANO MAFUPIPI NA MWANDISHI.

MEET THE PIONEER BLOGGER OF TANZANIA..!

The Michuzi Blog is the pioneer blog in Tanzania. 
After only six years on air, the Michuzi Blog is not only the most popular blog in Tanzania; it is the most read Kiswahili blog on earth. In it you will find an eclectic mix of content including: news issues not covered anywhere else, political discussions and debates, entertainment news and much more. The Michuzi Blog is widely accepted to be the best blog platform for Tanzanian’s to exchange views and share news.
 
SPORAH: Although the name Issa Michuzi is so popular but our readers would like to hear from the man himself.  So who is Issa Michuzi?
 
MICHUZI: He is a journalist who unexpectedly happened to become a popular blogger whose blog has a worldwide readership, bearing in mind that I initially took blogging as a hobby, before I decided to take it seriously.

 I remember I started in 1980, using my brother-in-law’s camera, which my in-law’s younger brother and I ‘stole’ in order to use it to take snaps at different locations. Eventually I found myself falling in love with photography. Five years later, a friend of mine gave me a Pentax Spotmatic as a gift which ironically didn’t even know how to operate. Fortunately, by then there were some photography classes at Goethe Institute (at the IPS Building).

I recall my first instructor was Tom Mwewuka from the US Info Services. The practical part of the studies led me to taking snaps on the streets, and I eventually found myself at the YMCA Hall where popular DJs Kalikali, Negre Jay, and others were deejaying. Most people have no idea that the pictures I used to take by then were basically for the sake of earning enough money to develop the films (and not to make any profit) and for my photography class practicals. After finishing my course I continued going to the YMCA to take pictures, as well as doing so in the streets where I would photography whoever wanted my service. I think people were impressed with the quality of the pictures I took that they kept on demanding my service. I remember my first pictures ever to be used in a newspaper were taken at a building which collapsed at Msimbazi Street and two people lost their lives. A popular newspaper by then, Mfanyakazi used four of the pictures I sent them.

But establishing myself as a photographer really took shape when one day in 1989, Jah Kimbuteh and his Roots and Culture band performed at the YMCA, and I was asked to do a photo shoot. Among those in attendance to the event was Attilio Tagalile from the Daily News, who just happened to come without a photographer. He then asked me to give him one of the pictures I took, and that was the first time ever the paper used an artist’s picture on the front page. I think they were very impressed with how I photographer Jah Kimbuteh with his dreadlocks ‘flying in the air’ while singing with deep emotions. Since then, Tagalile encouraged me that I would make a good photojournalist.

Moreover, the Daily News’s chief photographer, the late Vincent Urio, who owned his own photo studio known as ‘Studio Laura’ was impressed by my skills and contracted me. I then continued with my practices with the best of the best in photography, who taught not only taught me the art of photography but also dark room techniques, especially on how to develop black and white films and printing.

I officially joined the Daily News on January 1st, 1990, and two years later I was offered a scholarship to go to Berlin, Germany to gain further skills in photography. When I came back, I joined the Tanzania School of Journalism (I was there from 1994to 1996).Upon completion; I was offered another scholarship to go to Cardiff, Wales for advanced training in political photojournalism. We were among the first to be taught about digital photography by then. I recall Canon and Kodak were working in partnership to make the first digital camera, which they eventually brought it at the college, offering us a rare opportunity to participate in their quest for developing digital photography.
 
   SPORAH: What encouraged you to start a blog (bearing in mind that in those days blogging was still a foreign thing to majority of Tanzanians)? Also, as an undisputedly most popular Tanzanian blogger, could you give us a brief history of your blog?
 
MICHUZI: I think I was encouraged by my friend Fidelis Tungaraza who is living in Helsinki, Finland. Each time he sent me an email, he challenged me that Tanzanian journalist were not catching up with global trends, and as a result were denying Tanzanians in the Diaspora opportunities to know more about what was happening in their country.

He never got tired of pressuring me to pioneer efforts to bridge the information gap that existed by then. I then happened to travel to Finland to cover The Helsinki Conference in 2005, accompanying President Jakaya Kikwete (who was by then the Minister for Foreign Affair), the UN Deputy Secretary General, Dr Asha Rose Migiro (Minister for Community Development, Women and Children, by then), and other government officials.

While in Helsinki I met a U-S-based friend of mine, who was invited to the Conference as a blogger. I got so much excited, especially as there was virtually no blog in Tanzania. A handful of bloggers from the country-like Boniface Makene, Da’Mija, Marco Polo, John Mwaipopo, and others- were by then all foreign-based. With technical support from Ndesanjo Macha adding up on top of the encouragement from Tungaraza, I decided to start blogging on September 8, 2005.When I got back home; I continued blogging passionately, providing timely coverage of local news and events. The wealth of pictures and news has have successfully made my blog uniquely popular within and outside Tanzania.
 
  
SPORAH: How do you manage to balance your time between serving your employer (to whom you work as a photojournalist) and your blog which you seem to work in full time? Secondly, how do you draw a line between your employer’s interest and your blog’s (for instance, which pictures to appear in your blog and which in the newspaper you work as a photojournalist)?
 
MICHUZI: I am a quite a well-organised person. Also, courtesy of my benefactors, I have been able to get a lot of support and assistance from reputable journalists from almost certainly every corner of Tanzania, who frequently send me news and pictures. We also get a lot of pictures and news from oversees. Additionally, I have a strong team of people who edit the news and pictures sent to me, and they also have their own material to be published in the blog. Some I am not working alone. Behind me is a strong team of journalists. Combined with pictures and news sent from ‘wadau’ (informal stakeholders) all over the world, I certainly am not overburdened.

I have successfully managed to draw a fine line between my role as a blogger and as a TSN Journalist, mostly because I am not a photographer at the Daily News but a sub-editor. Prior to that, I was an on-line editor, managing the Daily News’s website. I still do the photographing but not as my primary role, as there are other photographers doing the job. For that matter, there’s no chance of any conflict of interest. And if there is a need to choose which picture should be used in the newspaper, then the decision is my bosses’. The pictures I use in my blog are either sent by my associates and member of the public, if not taken by myself.
 
 
SPORAH: How do you interact with your blog readers?
 
MICHUZI: Ah, that’s so easy. As you know, social media networks are quite different from radio, TV or newspapers in the sense that in social media there is a place for readers/visitors to comment. Therefore, the interaction is automatic, and if there’s a section on my blog where readers/visitors can leave their queries or share whatever news they might have. Furthermore, my email address issamichuzi@gmail.com is widely known. So I engage my audience by either writing to them to seek their opinion or criticism. On average, I receive at least 1000 emails and I do my best to respond them all of them.
 
They says, Eating and drinking while standing, walking, driving or watching TV means that you will probably eat more than if you were sitting at a table..! 
 
SPORAH: You once created Michuzipost.com but it is no longer working. What happened?
 
MICHUZI: Michuzipost.com is no longer there because it’s not ready yet. I just introduced it to the public to gauge opinion, and I realised that the public is in favour of the blog. Therefore, to come up with a complete website, Michuzipost.com is now in the hands of professionals, and when it’s back it would be a force to be reckoned with as it would have online TV and radio. When? Soon…Watch this space.
 
 
SPORAH: One of the reasons given for unpopularity of Tanzania is the usage of Swahili (which in itself is not a problem). What’s your view on this, and just as the first few posts in Michuzipost.com were in English, do you have any plans in the future to use other language(s) than Swahili (for the sake of reaching a wider audience, especially those who are not fluent in the language)?
 
MICHUZI: I have repeatedly been asked this question, and at times people seeking my opinion as to whether they should use Swahili or English or any other language (remember I am also fluent in German and French...).But because majority of the people visiting my blog speak Swahili, and in appreciating our national language, I have decided to continue blogging in Swahili.
I strongly believe that sooner or later the logic behind this decision would be understood by many. For those who are not fluent in Swahili I just advise them to learn the language, bearing in mind that soon the language would be among the official languages used in AU’s and UN’s meetings. Also, I have been told that most of our foreign embassies have been using my blog as a reference point for our local news, and that’s something that has really encouraged me to continue blogging in Swahili.
 
Issa Michuzi on point..!
SPORAH: How do you work with other bloggers?
 
MICHUZI: Co-operation among Tanzanian bloggers is really impressive. First of all, I feel so proud of being a pioneer in encouraging others to start blogging. Also, I have played a big role in creation of most of the (Tanzanian) blogs you find today. I wouldn’t get into naming names without their consent but all I can say is my role was there. I’m quite proud that the people I inspired to blog are doing really well. Moreover, I never hesitate to be of help whenever someone starts a blog, and asks me to publicise it.

I also tend to advise new bloggers about their blog design or even content, sometime well before I publicise them. Additionally, I tend to share some news items which some blogger have not had access to. I am also quite willing to let other bloggers to use my blog’s content with expectation that they would cite my blog as a source. I work closely with both locally- and foreign-based bloggers, for instance, Washington DC-based Dj Luke’s ‘Vijimambo,’ Urban Pulse (Reading UK), Freddy Macha (London), Da’Subi of wavuti.com, Francis Godwin (Iringa) Bongo Celebrity, Mbeya Yetu, my brother Israel Isaria’s (London) Tanzaniasports and many more, including you guys   (The Sporah show), Jestina George and brother Ayub Mzee’s Swahili Diaries (London), and Da’ Chemi’s Swahili Times. I work very closely with all of them.
 
 
Issa Michuzi himself.!
SPORAH: As a Government employee, how do you make sure that your blog does not seem to be the State’s mouthpiece?
 
 MICHUZI: They are all my readers.
 
 
SPORAH: A question related to the previous one, how do you manage to publish news (or pictures) which your employer (the Government) might have preferred they receive less or no publicity?
 
MICHUZI: Fortunately, my blog’s policy is strictly not to hurt people’s feelings. Adhering to this policy assures me of not running into problems. Mind you ‘what’s good for the goose is bad for the hen’. Therefore, it’s not all about my employer. There are sections of the society that might not like some of the stuff which others do. It’s all about common sense and applying journalism ethics and standards, in denying gossips, and other unfounded stories a place in my blog, and that really helps.
 
Issa Michuzi having a laugh with The President  of Republic Of Tanzania His Excelence Jakaya Mrisho Kikwete.
 
  SPORAH: What’s your opinion on an influx of Tanzanian blogs, most of which seem to share same themes?
 
MICHUZI: I do not have any issues with what you call an influx of Tanzanian blogs; bearing in mind that blogging in our country is at its infancy. We therefore have to leave the situation as it is. I only hope for a brighter future, and it’s up to the readers to judge the blogs they visit I usually encourage those who want to create blogs to focus on their areas of expertise, rather than just copying and pasting other bloggers’ works. If it’s a journalist, I usually advise them to come up with news blogs, but for those who are not journalists I tend to recommend they create blogs about stuff they are familiar with. For instance, a carpenter creates a blog about carpentry, not starting a news blogs lest he ends up copying other people’s works. It’s also worth knowing what potential visitors to your blog expect from you. And is it uniquely yours? If there’s another blog dwelling on same theme, do you have the guts to deliver more than they do, lest your blogs look similar?
 


  SPORAH: There’s a view that some Tanzanian blogs seem to avoid focusing on variety of problem facing the country/society(for instance, corruption, poverty, diseases, etc) and they instead seem to prefer pictures and entertainment news. What’s your opinion on this?
 
MICHUZI: You would see that I already answered this question if you read carefully my answer to your previous question. My opinion is for those with expertise in such matters to come forward, and start blogging. They should not be scared because Rome wasn’t built in a day. One day they could become as popular as I am.
 
 
SPORAH: Is there any (local or international) blogger who you admire? Additionally, which blog/blogger you look upon as your role model?
 
MICHUZI: I like all bloggers whose work is original, I mean those who don’t copy&paste other bloggers’ pictures and/or news but they endeavour to look for original material to publish in their blogs. There are lots of such bloggers, and they do really impress me.
 

 

SPORAH: Two of your brothers are also established bloggers. Is blogging something that runs in your family or is it just a case of your young brothers getting inspired by you?
 
MICHUZI: I think what runs in our blood is a strong desire to share news and information through blogging. Initially, my younger brothers started by helping me with gathering news and pictures. Later on I encouraged them to have their own blogs. They followed my advice and they certainly are doing really well. They are still in my team, and for that matter nothing is missing in my blog even when I am away. I really like my younger brothers, Ahmad and Othman, and I truly value their hardworking attitude and spirit. Without them, I would really struggle to manage the workload. The good thing is they have both emerged as among the best photographers that I do not hesitate asking them to work for me. The public has warmly accepted their works, and I do not regret having them on board.
 
 
SPORAH: As a reputable blogger, how do you envision the future of blogging in Tanzania?
 


MICHUZI: The future of blogging in Tanzania is very bright, putting aside minor issues as I explained before. Also, I’m quite impressed now blogs have won recognition as reliable source of news and information, although there are still few people, especially those the conservatives, whose first encounters with social media left them with negative attitude towards blogs (for instance, first blogs they ever came across were filthy). They therefore still harbour a misguided impression that the whole social networks thing is filthy too. However, such misconceptions are gradually disappearing, and I strongly hope the future is bright.
 
 
SPORAH: There is a perception that using the domain “blogspot.com” is for new or unpopular blogs, and it creates an impression of a ‘personal’ blog as compared to such a prominent blog like yours (perhaps such perceptions are due to the fact that the domain ‘blogspot.com’ is used for free). Do you have plans to have something like “michuzi.com” which could probably create a more professional impression?
 
MICHUZI: Such perceptions are more theoretical than practical, although they have an element of truth. Especially you guys who are based overseas. Here in Tanzania, it’s just a habit. Most people here are getting used to blogs, easily having wider access to news. Many access blogs while they are at work. For them, a ‘one-page blog’ (i.e. reading news on same page without necessarily turning pages) is more convenient, and they don’t have to read a lot. Some might just be lazy or they are not well-used to searching for content in a comprehensive site. I witnessed myself in Michuzipost.com. The more sections a site has the further the number of visitors to the site diminished. Blogs in Kenya and Uganda, or even in Rwanda and Burundi, are quite less popular and only websites with professional touch seemed to hit it off together with readers. Perhaps that’s how the readers were exposed to accessing news online.
 


 
SPORAH: Because blogs are part of social media, and because you are among the first pioneers to embrace the trend, how would you describe the role of social media in Tanzania, and how it evolves?
 
MICHUZI: Social media has truly inspired an information revolution in our country. Gone are days when you had to wait until the following day to know what happened today. Although it might take some time, but the mainstream media would have to work really hard. And the ‘traditional’ media outlets which ignore the presence and effectiveness of social media must understand that they might be digging own graves. Nowadays a ‘normal’ reader could become a self-made journalist by using social media. Gone too are days when people were ‘spoon-fed’ with one-sided stories without a reader having an opportunity to comment on the news. This is a new era in which news could be easily access on your mobile phone, which does not necessarily have to be the priciest ones. I heard some of you guys living abroad do not buy newspapers and just get news from the internet. Such a trend is gradually becoming prominent in the Third World.
 
 
SPORAH: A related question, apart from blogging, do you use other social media such as Twitter, Facebook, YouTube, Tumblr, etc?
 
MICHUZI: Yes, I do frequently use them. I am on Facebook, I Skype, I am on Google+, and I have my own YouTube channel (mdauwalibeneke). My blog is connected to all these services, and that really helps to bring more readers to it.
 
 
SPORAH: A blog with few readers but achieving your aims for creating it in the first place, or a blog with massive number of visitors but not necessarily meeting your aims?
 
MICHUZI: Both. My aims and my readers’ expectations, needs, etc. As a journalist, my aim and role is to impart information to meet the needs of the public.
 


 
SPORAH: In conclusion, what would you like to tell our readers, yours and the public in general?
 
MICHUZI: I can’t find anything that I have not said or mentioned. Perhaps I should give a massive ‘THANK YOU’ to all who visit Michuzi Blog, and I would like to tell them I am their humble servant, and should not hesitate to tell me how best I can serve them. I respectably promise to fulfil their wishes/needs. I wouldn’t be here without them; they have been with me through highs and lows, thick and thin. To every reader of your magazine, I just want to let them know they made the right decision to choose it, and they should keep supporting it. Although you might not know, you are doing our nation an exceedingly great service. History will certainly tell that.


SPORAH: Thank you Issa for your time.


THANKS TO:
Issa Michuzi
Evarist Chahali
The Sporah Show' Crew.