YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Saturday 18 May 2013

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MAY 19, 2013








 








Mtoto aliyepigwa mapanga na baba yake juzi, afariki dunia

polisi-amcharanga-mapanga-mwanae-miaka-4-picha-0Mtoto Devotha Gerald (4) aliyepigwa mapanga na baba yake, polisi mstaafu Samson Bwire Amefariki dunia baada ya jitihada za madaktari kuokoa maisha yake kushindikana.

Mtuhumiwa wa tendo hilo ambaye naye alipigwa vibaya na wananchi wenye hasira yuko mikononi mwa jeshi la polisi.
Tendo hili lilitokea mkoani Shinyanga. Kama haukuona habari hiyo ya kusikitisha, ya kushambuliwa mtoto huyo, iliyotokea juzi usiku,
 
KAMA ULIIKOSA HABARI HIYO BOFYA HAPA CHINI
  
 

MFANYABIASHARA AFARIKI KWA KUPIGWA RISASI JIJINI DAR ES SALAAM



542239_526484784032714_436209060_nMfanyabiashara wa jijini Dar es salaam anayejulikana kwa jina la Ayoub Mlay ameuwawa kwa kupigwa risasi usiku wa kuamkia leo  katika klabu ya  AMBROSIA CLUB iliyoko Kunduchi jijini Dar es salaam.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kinondoni Charles Kenyela ameithibitishia Fullshangweblog  kwa njia ya simu, kutokea kwa tukio hilo , huku akisema uchunguzi zaidi unaendelea kujua chanzo cha kupigwa risasi kwa mfanya biashara huyo
Kamanda Kenyela ameongeza kwamba watu hao walikuwa wakinywa ndipo mojawapo alipochukua bastola yake na kumpiga mwezake Ayoub Mlayambaye alifariki usiku wa kuamkia leo

Rais kikwete akutana na Askofu mkuu wa Canterbury mjini Dodoma


8E9U6389Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Askofu Mkuu wa Canterbury Justin Portal Welby katika ukumbi wa St.Gaspar mjini Dodoma leo(picha na Freddy Maro). 8E9U6409Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Askofu Mkuu wa Canterbury Justin Portal Welby muda mfupi baada ya kufanya naye  mazungumzo katika ukumbi wa St.Gaspar mjini Dodoma.Askofu huyo alishiriki katika ibada ya kutawazwa kwa askofu mkuu mpya wa Kanisa la Anglikana nchini Tanzania Dkt.Jacob Erasto Chimeledya.

TUNAOMBA RADHI KWA PICHA, AIBU NYINGINE:PICHA ZA USHENZI ZA WASANII WA KOMEDI ZAFUJA,WAZAZI WAJA JUU KWA UDHALILISHAJI WA WATOTO WAO:



 Mmoa wa wasichana hao aliyejitambulisha kwa jina la Happy akiwa na kingua cha aibu kabla ya kukivua kabisa.

 Hapa tayari akiwa amechojoa nguo

 Hapa Master Face akiwa na Happy kama anavyoonekana huku wakitomasana

 Hapa Happy na Master Face na Happy wakiwa wamedata kwa mahaba.Ilikuwa ni aibu mbele ya watu

 Haya Master Face umepewa "mgongo" huo kazi kwako habati hiyooooooooo kakaangu!

 Hapa Happy akiwa na msanii mwingine wa kundi hilo Manaiki Sanga kama anavyoonekana kwenye picha.

 

Katika hali isiyokuwa ya kawaida na kushtua picha zinazowaonesha wasanii wa kundi la Ze Komedi wakiwa kwenye fukwe moja ya huko Kigamboni zimezusha balaa kubwa mtaani huku familia za wasichana hao zilikija juu.

Picha hizo ambazo blog hii ilizinasa kwa gharama kubwa toka kwa mmoja wa wafanyakazi wa fukwe ya Chadibwa zilikopigwa bila kundi hilo kutambua kama walikuwa wanafotolewa picha hizo.

Habari zaidi zilisema kuwa picha tangu zimewekwa kwenye blog hii zimeanza kusambaa hadi kuwafikia wanafamilia ambao wamekuja juu huku wengine wakitaka kuchukuwa hatua za kuwashtaki wasanii hao kwa udharirishaji wa watoto wao.

Mwandishi wetu ilimtafuta kiongozi wa kundi hilo Mtanga ili kuzungumzia ambapo alipatikana na kueleza kwa ufupi " Kaka hali ya Mungu mimi sijaiona hizo picha hivyo nashindwa kueleza chochote,Isipokuwa kama kuna malalamiko yoyote toka kwa wanafamilia hao wafike ofisini kwetu tuweke sawa" Alisema Mtanga

Wednesday 15 May 2013

WABUNGE WA CCM WANATAKA KUCHAPANA MAKONDE BUNGENI


 
WABUNGE wa CCM, juzi walizua tafrani nje ya Ukumbi wa Bunge baada ya kukasirishwa na kitendo cha mwenzao wa Nkasi Kaskazini, Ali Keisy kupinga Bajeti ya Wizara ya Ujenzi wakati akichangia hotuba ya wizara hiyo.   
Katika mchango wake, Keisy alisema haungi mkono hoja kwa sababu Barabara ya Sumbawanga hadi Kanazi-Mpanda mpaka Kibaoni haijajengwa kwa kiwango cha lami.
Pia alisema zilitengwa Sh27 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo lakini mpaka sasa Wachina waliopewa zabuni ya ujenzi huo wamekosa fedha na wameamua kuuza kokoto.


Mara baada ya Bunge kuahirishwa, Keisy akiwa nje ya ukumbi huo alifuatwa na Mbunge wa Urambo Mashariki, Profesa Juma Kapuya, Omary Nundu (Tanga Mjini), Mendrady Kigola (Mufindi Kusini) na Rita Kabati (Viti Maalumu) na kumzonga.
 
Baada ya wabunge hao kumzonga, Profesa Kapuya ambaye amewahi kuwa waziri serikalini alihoji kitendo cha mbunge huyo kupinga bajeti... “Kwa nini umekataa kuunga mkono hoja? Ulikuwa unalidanganya Bunge wakati unachangia si kweli huko Rukwa hakuna barabara, barabara mnazo.”
 
Kessy alionekana kukerwa na swali hilo na kumjibu kwa hasira: “Nyinyi na mimi nani ni mbunge Nkasi? Mimi sina unafiki napinga kutokana na yaliyopo jimboni kwangu sipo hapa bungeni kuwafurahisha nyinyi na wala Serikali. Nipo kwa masilahi ya wananchi wangu.”
 
Baada ya majibu hayo, mbunge huyo aliondoka haraka eneo hilo. Baadaye jioni mwandishi wetu alimfuata ili kupata ufafanuzi juu ya msimamo wake.“Hakuna barabara kwangu, kwa nini niunge mkono hoja? Namshangaa sana Kapuya kwa tabia aliyonionyesha pale... Mbona mama Margaret Sitta amesema Tabora hakuna barabara hawakumfuata ?.”
 
Alisema wabunge hao hawana haki ya kuhoji kwa nini hakuunga mkono hoja kwa kuwa kila mmoja amekuja bungeni kutokana na kushinda katika jimbo lake. Akichangia hotuba ya bajeti hiyo, Kessy alisema haungi mkono hoja kwa asilimia 100 hadi pale atakapoelezwa lini barabara hizo zitajengwa.    Alisema zaidi ya vijiji 30 vya mwambao wa Ziwa Tanganyika na Barabara ya Kipili hadi Bandarini ni mbovu kwa kiasi kikubwa na muda wake wa ujenzi kumalizika umeshapitiliza miezi mitatu iliyopangwa.
 
Alisema nchi imegawanyika kwani baadhi ya majimbo ya wabunge yana lami hadi mlangoni lakini Nkasi hawajawahi kuiona akitoa mfano wa Jimbo la Waziri Mkuu, Mizengo Pinda (Mpanda Mashariki) Same Mashariki kwa Anna Kilango.

KILIZA HAPA WIMBO MPYA WA MWANA FA FT. NJENJE, MANDOJO NA DOMOKAYA - KAMA ZAMANI

SI

Mwana FA


AJALI MBAYA YA PIKI PIKI YATOKEA ASUBUHI HII BUGURUNI ROZANA, DAR


Ajali mbaya imetokea asubuhi hii ikihusisha pikipiki na daladala hii ambazo zilikutana uso uso lakini Kwa BAHATI nzuri dereva wa pikipiki Hiyo (mwenye helmet chini) alipona baada ya kuruka kwenye pikipiki na pikipiki kuharibika vibaya baada ya kukanyagwa na gari. Picha kwa hisani ya mwanaharakati mzalendo blog. Ajali za aina hii zimekuwa nyingi mno jijini Dar es salaam na kwengineko kufuatia wimbi kubwa la bodaboda kila mahali na uendesshaji usiofuata sheria
Balaa asubuhi

Askari wa trafiki wakiwa kazini baada ya ajali hiyo, huku dereva wa pikipiki akisubiri pembeni
Dereva wa pikipiki aliyenusurika
Polisi jamii na wasamaria wema wakijaribu kuinasua pikipiki uvungumi mwa daladala.Picha Kwa Hisani ya Michuzi Blog