YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Tuesday 18 June 2013

NAPE: CHADEMA NI WAHUTUHUMIWA NAMBA MOJA


Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza  na waandishi wa habari leo mjini Dodoma.
Itakumbukwa tarehe 16/06/2013 ilikuwa ni siku ya uchaguzi mdogo wa madiwani kwa baadhi ya kata nchini. Uchaguzi huo umefanyika kwenye kata ishirini na mbili (22)  kati ya kata ishirini na sita (26) zilizotangazwa kufanya uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi wazi.

 Matokeo tuliyoyapata toka kwenye maeneo yaliyofanya uchaguzi yanaonyesha kuwa kati ya kata 22 zilizofanya uchaguzi CCM tumeshinda kata 16 sawa na asilimia 72.72% na wenzetu wamechukua kata 6 zilizobaki sawa na asilimia 27.28%.

 Tunawashukuru sana kote walikoonyesha imani yao kubwa kwa Chama chetu kwa kutupa dhamana ya kuendelea kuwatumikia. CCM inawaahidi utumishi uliotukuka. Hata wale 27.28% walioamua kuwajaribu wenzetu, tunawatakia kila lakheri, kwani wametumia haki yao ya kidemokrasia kuchagua wanaodhani watawasaidia kufikia malengo yao ya kimaendeleo. Uchaguzi kwenye kata hizi zote umeisha sasa tuwatumikie wananchi.

 Kata nne za jiji la Arusha hazikufanya uchaguzi baada ya kuahirishwa kufuatia tukio la kusikitisha la kulipuka kwa bomu kwenye mkutano wa kampeni wa Chadema mjini Arusha tarehe 15/06/2013.

 CCM tunalaani tukio hilo la mlipuko wa bomu na matukio yanayofanana na hayo katika nchi yetu. Tunawapa pole wale wote walioathirika na tukio hilo. Ni vizuri serikali ikalichunguza swala hili kwa kutumia muda mfupi na kuhakikisha waliohusika wanapatikana na kuchukuliwa hatua zinazostahili.

 Pamoja na kulaani na kuitaka serikali kukomesha vitendo hivi nchini, ni wakati muafaka kwa vyama vya siasa nchini kujitazama upya kwani kuna kila dalili kuwa tukio hili kama alivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari mhe. Mbowe Mwenyekiti wa Chadema Taifa kuwa ni la kupangwa, inawezekana limepangwa na Chadema wenyewe.

 Hali ya kisiasa jijini Arusha kuelekea uchaguzi huo ilikuwa wazi kuwa wana Arusha walishaamua kuzirudisha kata hizo nne kwa CCM, hasa baada ya kuchoshwa na maandamano na vurugu za kila siku jijini Arusha. Aidha kauli za kukata tamaa za viongozi wa Chadema na vitendo vyao ni dalili tosha kuwa tukio hili lilipangwa na Chadema wenyewe.

 CCM tunaendelea kusisitiza na kulaani juhudi za wenzetu kujaribu kujenga umaarufu wa chama chao juu ya damu za Watanzania. Juhudi hizi zinapaswa kulaaniwa na wazalendo wote ndani na nje ya nchi. Tukumbuke asiyekubali kushindwa, si mshindani. Si busara wala uungwana na ni kinyume na utu kutumia majanga ya kutengeneza kama mtaji wa kisiasa.

 Lakini CCM tunalaani pia kitendo cha viongozi wa Chadema kujaribu kutumia baadhi ya misiba na majeruhi wa tukio hili kisiasa na mwisho wa siku kwenda kuwatelekeza hospitali baadhi yao baada ya kuwaahidi kubeba gharama zote za matibabu na mazishi.Tunaipongeza serikali kwa kuingilia kati na kuwasaidia waathirika hawa na kuhakikisha wanapata huduma inayostahili.

 CCM inarudia kueleza masikitiko yake kwa waathirika wa tukio hili la kinyama na kikatili lisilostahili kuvumiliwa hata kidogo. Kama Chama tumeguswa sana na tukio hili pamoja na kulilaani, tunawasihi watanzania tushindane na kutofautiana bila kupigana na kuvunja tunu ya nchi yetu ya amani na utulivu. Katika demokrasia ya vyama vingi swala la kuvumiliana ni swala la msingi sana katika kufikia ukomavu wa demokrasia hiyo.

 Imetolewa;
Nape Moses Nnauye
Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi.
17/06/2013
Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi

MBOWE:MABOMU YAMERUSHWA NA POLISI KWA MAAGIZO



"Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema polisi wanahusika na milipuko katika mkutano wa CHADEMA na kuua watu watatu.

Mh Mbowe amesema ana ushahidi na picha za video za tukio hilo.

Mh Mbowe alisema hayo akihojiwa na ITV" From Jamii forums

Pia nape nae amekaririwa akisema chadema wenyewe ndio wamehusika na bomu hilo...
Sasa hapo sijui tumwamini nani ?
My take 
---------
Hapa inawezekana hakuna kati yao aliyehusika but ni mtu we pembeni sasa havi amekaa anakunywa kahawa akichekelea jinsi wanavyozozana....Hivyo wasubiri uchunguzi wa Dola ..haya wanayoyasema bila uchunguzu yanatuchanganya tu ..

Monday 17 June 2013

VIDEO HII IKIMUONYESHA MSICHANA ALIYEKAMATWA NA KILO 5 ZA HEROIN EGYPT AFANYIWA MAHOJIANO LIVE.





Msichana anaejulikana kwaJina la Fatma aka Brown Berry Aliyekamatwa Egypt na madawa ya Kulevya Afanyiwa Mahojiano, Angalia na sikiliza kwa makini mahojiano ya Fatma a.k.a brown Berry hapo chini

TOA MAONI YAKO HAPA

GERALD HANDO WA CLOUDS FM NUSURA AFUMULIWE NA BASTOLA LEO



MTANGAZAJI maarufu wa Clouds FM, Gerald Hando leo alfajiri alizua kizaazaa na kupelekea kutishiwa bastola na mtu ambaye jina lake halikufahamika mara moja.
Chanzo cha Saluti5 kimesema Hando aligonga gari la mtu huyo maeneo ya Kwa Kopa, jambo lililopelekea mtu huyo ashuke kwenye gari lake bastola ikiwa mkononi na kutishia kumfumua Hando.
Kama mtu huyo alidhani kutoa bastola ndio suluhisho basi alikosea sana, Gerald Hando anayetangaza kipindi cha "Power Breakfast" naye alishuka kwenye gari lake na kufungua shati lake na kuanza kumuamrisha mtu huyo afyatue bastola.
Huku akiporomosha matusi kwa ukali Hando alisema: “Piga hiyo bastola yako, shoot me.”
Hando aliendelea kuwa mkali huku akipigapiga kifua chake hali iliyovuta watu wengi kwenye tukio hilo ambao waliwasihi wote wawili kutuliza mzuka na kumfanya mtu huyo aliyekuwa na gari aina ya Rav 4 arudishe bastola yake kwenye gari na kutafuta njia nyingine ya kulimaliza tatizo lililotokea.

MSIKILIZE MR SUGU AKIONGEA ALIPOKUWA JUKWAANI KATIKA SHOW YA LADY JAY DEE



Mr II Sugu akiingia kwenye jukwaa la Machozi Band kwenye show ya miaka 13 ya Lady Jay Dee .. Video
TOA MAONI YAKO HAPA

MACHANGUDOA WANAOFANYA BIASHARA YAO SINZA WAKAMATWA





Mgambo wa jiji la Dar es Salaam wakiwa katika zoezi la kuwakamata Madada wanaofanya biashara ya kuuza miili yao wajulikanao kama Machangudoa katika eneo la Sinza. Picha mbalimbali zikionyesha namna walivyokuwa wakipakiwa ndani ya Gari tayari kwa kupelekwa katika vyombo vya sheria

PICHA MBALI MBALI YA KINACHIJIRI KATIKA KUANDAA UTARATIBU WA KUMUAGA LANGA


You might also like:

MAPENZI YA JINSIA MOJA YADAIWA KUSHAMIRI HALMASHAURI YA MOROGORO


HALMASHAURI ya Manispaa ya Morogoro inakabiliwa na changamoto ya kukua kwa maambukizi ya Ukimwi, baada ya kushamiri kwa biashara ya mapenzi ya jinsia moja. Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa, Naibu Meya Manispaa ya Morogoro, Lidya Mbiaji, alisema kuwa kumekuwa na tatizo kubwa la kushamiri kwa vichocheo vya ngono, hali inayochangia kukua kwa kiwango cha maambukizi ya Ukimwi katika mkoa huo.

Pia alisema ongezeko la nyumba za kulala wageni nalo limekuwa kichocheo kikubwa cha kushamiri kwa biashara ya ngono zembe.

Aliionya jamii kuepukana na mila na desturi zinazochangia kuleta vichocheo vya kuongezeka kwa maambukizi ya ukimwi, ikiwemo ngoma za unyago zijulikanazo kwa jina maarufu la kunemwa pamoja na mabanda ya kuonyesha video ambayo nje yamekuwa yakionyesha mechi za soka, lakini ndani ya mabanda hayo huonyesha picha za ngono na kusababisha kuleta hamasa ya watu kufanya ngono.

Pia aliviomba vyombo vya habari kusaidia kuelimisha jamii namna ya kujiepusha vitendo vinavyochangia maambukizi ya ukimwi, kwani hali si shwari kutokana na makundi ya watu wanaofanya biashara ya ngono kuvamia Manispaa ya Morogoro.

Alisema hata kwa wasomi wa vyuo vikuu, hali pia si shwari, kutokana tafiti kuonyesha kuwa wana kiwango cha juu cha kufanya ngono zembe, hivyo kulitisha taifa kupoteza wasomi wake mara baada ya kumaliza masomo yao.

“Kumekuwa na makundi makubwa ya jamii yanayoingia katika hatari ya kupata maambukizi…ukiangalia kundi la wanafunzi, watu masikini na wanawake, hasa wajane changamoto hii inawagusa moja kwa moja,” alisema Mbiaji.

Saturday 15 June 2013

BREAKING NEWS......! WATU SABA WAMEJERUHIWA VIBAYA BAADA YA BOMU KULIPUKA HUKO ARUSHA





6510_197909020362132_1935330081_n
Takriban watu saba wamejeruhiwa na kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu, kilicholipuka eneo la Soweto, jijini Arusha, ambako mkutano wa CHADEMA ulikuwa ukifanyika. Tukio hili limetokea muda mfupi tu baada ya mwenyekiti wa CHADEMA, kumaliza kuhutubia wananchi waliokuwa kwenye eneo hilo na inasemekana Watu 6 Wamepoteza Maisha Na Wengine Kujeruhiwa,,

Wananchi Arumeru wateketeza shamba la mwekezaji



Tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 3.30 usiku nyumbani kwa mwekezaji huyo, Ikbar Abdalah (53)ambaye ni mkulima mwenye asili ya Kiasia na mkazi wa kijiji hicho.

Arusha. Wananchi zaidi ya 1000 wa kijiji cha kwa Ugoro wilayani Arumeru, wamevamia shamba la mwekezaji na kuliteketeza kwa moto na kupora bidhaa mbalimbali mali za mwekezaji huyo zenye thamani ya mamilioni ya fedha.
Tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 3.30 usiku nyumbani kwa mwekezaji huyo, Ikbar Abdalah (53)ambaye ni mkulima mwenye asili ya Kiasia na mkazi wa kijiji hicho.
Katika tukio hilo wanakijiji hao walichoma nyumba yake,mabanda mawili, trekta moja chakavu,mashine ya kusaga nafaka,spea za magari na kupora vitu mbalimbali ikiwamo pikipiki moja aina ya Honda.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas ,chanzo cha uharibifu huo ni mgogoro wa muda mrefu kati ya wanakijiji hao na mwekezaji wa kugombea eneo lenye ukubwa wa zaidi ya hekari 100 linalomilikiwa na mwekezaji huyo.
Alifafanua kuwa viongozi wa eneo hilo walidai kuwa mgogoro huo umedumu kwa muda mrefu, kiasi cha kufikisha suala hilo ngazi ya mahakama na kwamba kesi hiyo ilishawahi kutolewa uamuzi mara mbili na sasa iko ngazi ya rufaa.
Hata hivyo, polisi ilifanikiwa kumnasa mwanakijiji mmoja (jina linahifadhiwa na polisi) anayeshikiliwa katika kituo cha polisi jijini hapa huku wengine wakiendelea kusakwa kutokana na kutenda kosa la kujichukulia sheria mkononi.
Wakati huo huo, Kamanda Sabasi ametoa onyo kali kwa mtu ama kikundi chochote cha watu watakaojihusisha na matukio ya kuvuruga uchaguzi mdogo wa madiwani utakaofanyika Juni 16 mwaka huu
.

Video: mwanamke anaswa akivunja amri ya sita vichakani huku akiwa na mtoto mchanga mgongoni




Mwanamke mmoja amenaswa akifanya uchafu porini huku akiwa na mtoto mchanga mgononi...

Tukio hilo la kusikitisha liliwanasa wawili hao wakiridhishana chini ya kichaka huku mtoto mchanga akionekana kulia kwa huzuni.....

Haijafahamika mara moja kama watu hao ni mtu na mume au ni wazinzi tu...!!!

VIDEO HAPO CHINI

MAMA WEMA SEPETU ATISHIA KUMCHOMA MTU KISU KISA MWANAE...




VIDEO inayomuonesha mama wa Wema Isaac Sepetu, Miriam Sepetu akizua timbwili ‘hevi’ nyumbani kwa mwanaye huyo huku akitishia kumchoma mtu kisu imevuja, Ijumaa limeinasa.

Kwa mujibu wa video hiyo, mama Wema alitimba nyumbani kwa mwanaye huyo Kijitonyama, Dar kwa lengo la kuwasambaratisha marafiki wanafiki wa Wema ambao alidai wanamharibu mwanaye.
Pamoja na matusi yanayosikika kwenye video hiyo, mzazi huyo alikuwa akitoa vitisho kwa Maila ambaye ni mmoja wa mashosti wa karibu wa Wema.

“Nitammaliza huyu…(tusi), hana kwao, hana chochote,” sauti ya mama Wema inasikika na kuongeza:
“Nina data, mimi nilipigiwa simu, huyu sijui Maila, sijui nani kuwa alishikwa na begi lenye vipisi vya bangi Airport (uwanja wa ndege).
“Hawamshauri Wema chochote, wanamharibu ili maisha yake achanganyikiwe. Ningekuwa na kisu ningemchoma…ningekuwa na kisu leo ningemchoma visu…potelea mbali.”

Mbali na vitisho hivyo, mama Wema anaonekana akibinua vitu vya ndani kama makabati na makochi ikidaiwa kuwa alikuwa akisaka bangi aliyoletewa mwanaye na rafiki zake.

Kwa mujibu wa watu walioiona video hiyo walisema marafiki wa Wema kama Kajala Masanja, Snura Mushi, Martin Kadinda, Jamila na wengine kibao wanapaswa kuwa makini na mama huyo kwani anaonekana kuwa na hasira nao.

Baada ya kuinasa video hiyo, Ijumaa lilimsaka mama Wema ili kupata mzani wa habari hiyo lakini simu yake ya kiganjani iliita bila kupokelewa.
Mwandishi Wetu alikwenda nyumbani kwa mama huyo Sinza-Mori, Dar ili kuzungumza naye ‘laivu’ lakini alipogonga tu getini alitokea binti aliyedai mama Wema hakuwepo.

PICHA ZAIDI MIAKA 13 YA LADY JAYDEE



Umati wa watu unaoshuhudia show ya Lady J Dee sasa hivi hapa Nyumbani Longe.

Lady J Dee anatoa burudani ya kutosha kwa mashabiki.

Professa Jay akiwa back stage anajiandaa kupanda jukwaani kutoa burudani nzuri kwa mashabiki

Miaka 13 ya Lady j Dee#sasa hivi ndiyo Mh.Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu ameingia

Lady J Dee anatoa burudani ya kutosha kwa mashabiki.

Lady J Dee anatoa burudani ya kutosha kwa mashabiki.

Team Times Fm 100.5 (Dj Jors Bless,Ndimbo na Mariam)

Sugu na Mkoloni wanatoa burudani kali kwa mashabiki.

Mama mzazi wa Lady J Dee naye amekuja kushuhudia show ya mwanae.

Juma Nature anatoa burudani kwa mashabiki

Sugu akitoa burudani kali kwa mashabiki

M 2 The P akiongea machache baada ya kukaribishwa kwenye jukwaa na Juma Nature.