YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Sunday 9 March 2014

SIKILIZA TAHARIFA ZA MAGAZETI YA LEO TAREHE 10/3/2014 LIVE

on_air11Kwa kutumia teknolojia ya kisasa nimekurekodia magazeti haya yakisomwa na kuchambuliwa  Redioni kwako mtu wangu wa nguvu,hivyo kama ulimis kwa bahati mbaya waweza kuyasikiliza hapa,Sikiliza kupitia 104.4 Clouds Fm Dodoma.
Bonyeza play kusikiliza.

Use

AKIWA STUDIO YA RADIO MAARUFU:SHOGA ANAEJIITA ANTI SUZY AVAMIWA NA KUPEWA KICHAPO NUSU YA KUFA


 
BAADA ya shoga maarufu jijini Dar es Salaam, Ibrahimu
Mohamed ‘Anti Suzy’ (25), kutoboa siri kwenye vyombo vya habari jinsi watoto wa kiume wanavyoharibiwa na wanaume na kueleza namna alivyobwagiwa mtoto wa mwaka amtunze, mwanamume aliyembwagia mtoto ameibuka na kumjeruhi kwa visu akitaka kumuua.

Mwanamume huyo mwenye mke, awali alikuwa akiishi na Anti Suzy kama mume na mke eneo la Jangwani, baada ya kumkimbia mkewe na alikorofishana na shoga huyo baada ya kumfanyia fujo na kumuibia.

Akizungumza na gazeti la Habari Leo jana nyumbani kwake, ‘Anti Suzy’ aliyejitangaza kuwa ni muathirika wa Virusi Vya Ukimwi kwa zaidi ya miaka 10 sasa, alisema mwanamume huyo alikuwa akimsumbua warudiane, lakini yeye alikataa na kumtaka aishi na mkewe na kutunza watoto badala ya kumng’ang’ania.

“Nilimwambia simtaki, vituko alivyonifanyia ukiacha kuniletea mtoto wa mwaka na nusu wa kike nimlee hapa nyumbani, alikuwa akinipiga, kunitukana na aliniibia vitu vyangu vyote. Kwanza nilishamwambia nimeathirika na Ukimwi ananifuata nini?” Alihoji shoga huyo.

“Jana (juzi) alinipigia simu akinitaka turidiane nikamwambia asinifuate kwanza nimeshaenda kwenye vyombo vya habari.”

Alisema alimwambia hivyo ili asimfuate, lakini baada ya kumweleza hayo, alimvamia nyumbani juzi kati ya saa nne na tano asubuhi akiwa na panga na visu akimtishia kumuua kama hawatarudiana na kama ataendelea kwenda kwenye vyombo vya habari kumuanika mambo yake.

“Nilikimbilia ndani na yeye akanifuata humo, akarusha panga anikate shingoni huku akisema ataniua, nikakwepa, lakini likanijeruhi shingo, kama haitoshi akachukua kisu alichokuwa nacho akanikata vidole.

“Damu ikaanza kutoka nyingi, alivyoona hivyo akanikaba kooni ili aninyonge, majirani waliposikia nakoroma, wakavunja mlango na kuniokoa,” alidai Anti Suzy.

Shoga huyo aliyeanza vitendo hivyo akiwa mkoani Mwanza, alisema aliamua yeye na mama mwenye nyumba kwenda Kituo Kidogo cha Polisi Jangwani kutoa taarifa na kupewa hati yenye namba MS/RB/10695/2011.

Alisema baada ya kwenda Polisi, aliandika maelezo na kutoa vielelezo likiwemo panga na kisu alivyovitumia kumjeruhi na aliandikiwa hati ya matibabu (PF3) na kwenda Hospitali ya Mnazi Mmoja kwa matibabu.

Polisi katika Kituo cha Jangwani walithibitisha kutokea kwa tukio hilo, lakini walisema mlalamikaji alijitaja kwa jina la kike ambalo ni Suzana Mohamed na tayari taarifa za suala hilo zimepelekwa Kituo cha Polisi Msimbazi kwa hatua za juu zaidi. Mkuu wa Kituo cha Msimbazi hakuwa tayari kutoa taarifa kuhusu suala hilo.

Aidha, Muuguzi aliyekuwa zamu juzi katika Hospitali ya Mnazi Mmoja ambaye hakupenda kutaja jina gazetini, pia alithibitisha kumhudumia mgonjwa, Suzana Mohamed (25) mkazi wa Jangwani aliyejeruhiwa shingo na vidole kwa kukatwa na visu akiwa na PF3.

Mama mwenye nyumba anakoishi ‘Anti Suzy,’ Manju Machu maarufu kama Bi Manju, alithibitisha jana kutokea kwa tafrani hiyo iliyosababisha mpangaji wake huyo akimbie kunusuru maisha yake.

“Alikuja hapa huyo mwanamume akamvamia akitaka kumuua, alikuwa na panga na kisu, tuliingilia maana alikuwa anasema lazima amuue, nikasema akimuulia hapa kwangu na mimi nitakuwa matatani, na nchi hii ina sheria, kama una kosa na mtu polisi si ipo? Sisi tulimpeleka huyu Polisi kutoa taarifa” alisema Machu.

Majirani wa Mohamed ‘Anti Suzy’ nao walithibitisha jana kushuhudia vurugu hizo na kumshauri shoga huyo kurudi kwao Mwanza ikiwa vitisho vitaendelea.

Mwishoni mwa wiki iliyopita, Mohamed alifanya mahojiano na gazeti la Habari Leo na kueleza namna vigogo aliowataja kwa jina la mapedejee wanavyowatumia wao kwa gharama yoyote, wawatafutie watoto wadogo walioko shuleni na mitaani akiwataka wazazi, serikali na jamii kuwa macho na watoto hasa wa kiume.

Aidha, pia aliwaonya wanaume wasimfuate kwa kuwa yeye ni mwathirika wa Ukimwi na kwamba mashoga kama yeye wameathirika na ugonjwa huo. Usikose makala maalumu ya mahojiano ya ana kwa ana baina ya gazeti la Habari Leo na Mohamed “Anti Suzy” katika gazeti hilo keshokutwa Jumatano.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 10/3/2014 YA HABARI,UDAKU,MATUKIO,MICHEZO NA BURUDANI


 
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

PICHAZ..KUFURU KUBWA YA BONGO MOVIE AMBAYO INASHIKA REKODI MPAKA SASA...ILIKUWA NI FULL AIBU AISEEE....!!


ILITOKEA NA SIDHANI KAMA ITAKUJA TOKEA TENA KAMA HII, MAYBE BAADAE SANA..SHUKA NAYO HAPA CHINI
Ziara ya mastaa wa filamu Dodoma ni kufuru, fedha ilitumika, wasanii wajiachia kimapenzi wao kwa wao, wengine nusu wazipige.
The Biggest IQ, Ijumaa Wikienda lina ‘full nondoz’ hatua kwa hatua ndani ya Dom kama ifuatavyo.


FULL KUJIACHIA
Baada ya mechi na wabunge iliyochukua nafasi kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dom, wasanii walijigawa makundi mawili.
Kundi A ambalo lilitinga mjengoni na magari ya kifahari lilibaki na kugeuka Dar asubuhi ya Jumatatu (Juni 20), wakati Kundi B, walinyanyuka himahima Jumapili (Juni 19) saa 6:00 mchana.
Kundi B lilikuwa na wanaume wengi zaidi, wao waliambiwa wawahi Dar kwa sababu basi dogo walilokuwa wanalitumia lilikuwa linahitajika jijini.

Baada ya Kundi A kuondoka, Kundi A walijiachia ‘kinoma noma’ kwenye bwawa la kuogolea la Hoteli ya African Dream ambayo walifikia.
Katika bwawa hilo, mastaa ‘walishoo lavu’ kwa kuoga pamoja na kufurahi kwa michezo mbalimbali.

Wale waliokuwa hawataki kuingia majini, walisukumwa bwawani na nguo zao.
Mtiti uliibuka pale mchekeshaji Steven Mangere ‘Steve Nyerere’ alipomvaa Aunt Ezekiel ‘Gwantwa’ na kutaka kumtupia majini.
Vincent Kigosi ‘Ray’ naye aliongezeka kumsaidia Steve lakini baadaye timbwili hilo lilimalizwa na Mwenyekiti wa Klabu, Hartmann Mbilinyi aliyewatawanya.

TIMBWILI LA POSHO
Wasanii wote walipanga kuondoka Dom Jumatatu ya Juni 20 lakini tangazo kuwa basi dogo ni lazima liondoke Jumapili, liliwanyong’onyesha wengi, kwa hiyo ulianza mvutano wa nani atangulie, nani abaki.
 
 
Baada ya viongozi kubainisha wanaopaswa kutangulia na wengine wabaki, wale walioambiwa waondoke siku hiyo na basi, baadhi yao walianzisha timbwili la kudai posho.
Madai ya posho yalichochea hasira kwa viongozi na kusababisha Kiongozi wa Nidhamu, Issa Musa ‘Cloud’ kutaka kuzipiga na Soud Ally lakini Katibu, Salum Mchoma ‘Chiki’ alitumia busara kuwatuliza.
 
 
WAHESHIMIWA MACHO JUU
Kwa muda ambao wasanii hao walikuwa Dom, baadhi ya wabunge walikosa utulivu, wakipigana vikumbo jinsi ya kunasa mapenzi.
Baadhi ya wasanii walikamatika kutokana na uhuru uliokuwepo, kwani hakukuwa na kizuizi cha mtu kutoka na kwenda kupiga misele anapopataka.

NANI ANASEMA WASANII WA KIKE WANAUZWA?
Uchunguzi umeonesha kuwa baadhi ya wasanii wanajiuza wenyewe na wakati mwingine hutangaza ‘teni pasenti’ kwa mtu anayewasaidia kuwaweka kwa wafanyabiashara au wanasiasa wenye fedha.

Mbunge mmoja aliliambia gazeti hili kuwa alipigiwa simu na mrembo mmoja wa Klabu ya Bongo Movie akaomba kuwa naye karibu.

“Ni kama shule, kuna watu wazuri lakini wengine wabaya sana. Kuna mtoto nilikuwa namheshimu lakini alinipigia simu ananitongoza. Amenikera kweli, nilitaka kusaidia klabu yao lakini nimevunjika moyo kusaidia watu wa aina hiyo,” alisema mbunge huyo anayotokea moja ya majimbo ya Mkoa wa Morogoro.
 
 
JACK WOLPER BALAA
Jacqueline Wolper alitisha, kwani alitinga Dom akiwa na gari matata aina ya Toyota Land Cruiser V8, namba T 798 AXY na ndiye alikuwa ‘bei mbaya’ kuliko wenzake, kwani hata kambini alikuwa hakai.

SIKU MBILI WEMA HAONEKANI
Ijumaa (Juni 17) usiku, Bendi ya FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’ walitinga Dom na kudondosha ‘shoo’ kwenye Ukumbi wa Kilimani, kwa hiyo wasanii wote waliingia kuona mambo wazee wa mjini.

Baadhi ya wasanii hao, walipotezana na Wema Sepetu kuanzia muda huo, siku iliyofuata ambayo ndiyo mechi ilifanyika Uwanja wa Jamhuri hakuonekana mpaka Jumapili.
Gazeti hili lilimnasa msanii Zuwena Yusuf ‘Shilole’ akimhoji Wema: “Ulikuwa wapi? Siku mbili hatujakuona.”
Wema alijibu kwa kifupi kuwa hakuwepo lakini mwandishi wetu alipomhoji ni kwa nini hakuonekana siku ya mechi na wabunge ambayo ndiyo iliyowapeleka Dom alijibu: “Nilikuwa naumwa mafua.”
Mwandishi: Hayo mafua ni jana tu, mbona leo mzima?
Wema: Aah bwana yaache hayo.

RATIBA YAO
Mbunge wa Mvomero, Amos Makalla alikata zaidi ya shilingi 2,500,000 kulipia malazi ya wasanii hao kwenye hoteli hiyo.
Kila siku mchana, wasanii hao walikuwa wanakwenda kula nyumbani kwa Makalla mjini humo.Siku ya mechi, baada ya Bongo Movie kupokea kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Bunge Soka na 17-7 dhidi ya Bunge Netiboli, walialikwa nyumbani kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambako walikula chakula cha usiku pamoja na kuzungumza mpaka usiku mkubwa ambapo walirejea hotelini