YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Thursday 5 June 2014

MAGAZETI YA LEO JUNE 5, 2014

.
.
Ni utaratibu wa millardayo.com kukupatia stori kubwa za Magazeti ya Tanzania kila siku kabla ya saa mbili kamili asubuhi kutoka kwenye kurasa za kila gazeti kuanzia ya Udaku, Michezo na hardnews kurasa za mwanzo na mwisho.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

LIJUE DENI LA TAIFA NA DENI LA KILA MTANZANIA

fedha
Bunge la bajeti linaendelea bungeni mjini Dodoma ambapo sasa ni zamu ya wizara ya fedha na uchumi. Bajeti yake imewasilishwa na waziri wa fedha Saada Mkuya Salum ambapo bajeti yake imepita huku suala la deni la taifa likiendelea kuumiza vichwa vya wabunge wengi kwa kuendelea kukua siku hadi siku.
Suala hilo limeonekana kuwashtua wabunge wengi akiwemo Mheshimiwa Christina Lissu ambaye anasema fedha zinazokopwa na kuongeza deni la taifa zimekuwa hazitumiki katika miradi ya maendeleo.
Picha no 6(2)
Mhe. Lissu anasema “Mheshimiwa spika deni la taifa, tumeangalia hotuba ya kamati ya wizara hii ikieleza kwamba deni la taifa limekua kutoka trilioni 21 hadi 29 ikiwa ni ongezeko la trilioni 8 tu kwa miaka 7, kukopa ni sahihi na nchi yoyote inakopa lakini je fedha tunazokopa zinaenda katika miradi ya maendeleo? Mbona ukuaji huu wa deni hauendani na fedha zinazoelekezwa katika miradi ya maendeleo?.”
“Kwa mwaka huu karibu miradi yote ya maendeleo imepelekewa fedha chini ya asilimia 50, mbona ukuaji wa deni hauendani na fedha zilizoenda kwenye matumizi ya maendeleo? inawezekana tunakopa na tuaambiwa deni ni stahimilivu lakini kama fedha haiendi kupunguza matatizo ya wananchi inakuwa haina maana kukopa.”
Suala la kuchelewesha fedha zinazotengwa kwa ajili ya bajeti ya miradi mbalimbali limeonekana kuwagusa wabunge wengi ambapo Mhe. Asupta Mshana anasema;
“Kumekuwepo na tatizo kubwa la fedha tunazoidhinisha kama bunge kutotolewa kwa wakati na kufanya kazi kama zilivyopangiwa, tatizo ni kwamba tunaandaa bajeti kwa kutabiri bila kuwa na fedha mkononi. Ni vyema tukabadilisha utaratibu wa kuandaa bajeti zetu badala ya kuwa na Cash bajeti tuwe na Capital bajeti”
Pamoja na jitihada za serikali kupitia kukusanya kodi je mikakati ya ukusanyaji kodi inatosha? Mhe. David Kafulila anasema;
“Tufike mahala tuwe na mkakati wa kutosha kuhakikisha maeneo yote ambayo hatukusanyi kodi tunakusanya. Tumezungumza mara kadhaa juu ya watanzania kuashiriki kwenye uchumi wa nchi yao kwa kupitia masoko ya mitaji katika soko la hisa DSE ili watanzania washiriki kwenye uchumi wao, tusiwanyime fursa wazawa kushiriki katika uchumi wao.”
Wakati Serikali ikiendelea kubanwa juu ya suala hilo, Waziri Kivuli wa Fedha, James Mbatia amesema ukiligawanya deni hilo kwa idadi ya Watanzania milioni 45, kila mwananchi atakuwa anadaiwa Sh600,000.

Friday 30 May 2014

PICHA ZA GARI ALILOKUWEMO MAREHEMU TYSON WAKATI WAKITOKA MKOANI DODOMA NA KUPATA NALO AJALI

IMG_4162
Marehemu Geogre Tyson pichani hapa alikuwa yupo kijiji cha Chilonwa Chamwino kwenye utoaji wa madawati katika shule ya msingi Chaula iliyopo Dodoma. Baada ya kumaliza shughuli hii huku akiwa kama producer wa The Mboni Show mauti yalimkuta majira ya saa 12 jioni masaa 4 tu toka tuanze safari ya kurudi Dar es Salaam maeneo fulani hivi kama unataka kukaribia GAIRO mjini.
Katika gari hilo walikuwa watu 8 ila yeye pekee ndio aliyepoteza maisha na wengine kupata majiraha mwilini pamoja na dereva wa gari hilo. Kwa sasa mwili wa marehemu umehifadhiwa Morogoro katika  hospital ya mkoa Morogoro, baadae asubuhi mwili utaanza safari ya kuelekea Dar es Salaam.
IMG_4166 IMG_4213IMG_4214IMG_4215
Kweli ajuae mwisho wetu ni Mungu pekee. Tunaishi kama vile tunajua maisha yetu yataisha lini kumbe tunajidanganya. Haya matukio yote ni kwa ajili yetu kuamka na kujifunza kitu. Tumrudieni Mungu, tuungame dhambi zetu maana hakuna ajuae siku wala saa yake itakuwa lini. R.I.P Tyson na wote mliotutangulia.
Picha zote kutoka DJ Choka Music

SAD NEWS: MUONGOZAJI MAHIRI WA FILAMU NA VIPINDI TANZANIA GEORGE TYSON AFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA GARI ILIYOTOKEA MKOANI MOROGORO

George Tyson enzi za Uhai wake

Taarifa zilizotufikia katika meza yetu ya habari Usiku huu ni kuwa Muongozaji mahiri katika Tasnia ya Filamu Nchini na Mzazi Mwenza wa Msanii Nguli wa Filamu nchini Vyonne Cherry Au Monalisa, Bwana George Tyson amefariki Dunia mara baada ya kupata ajali ya gari Mkoani Morogoro Katika Eneo la Gairo wakati wakitokea Mkoani Dodoma ambapo walienda kwaajili ya Kuadhimisha Miaka Miwili ya Kipindi Cha Mboni Show.

Bw Tyson Mauti yamemfika mara baada ya Gari walilokuwa Wakitumia kusafiria Kutoka Mkoani Dodoma Kupasuka Matairi na kupelekea Kupoteza maisha na kupelekea hali ya watu wengine wanne waliokuwemo katika Gari hilo kuwa mbaya baada ya Kuumia vibaya na kukimbizwa katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwaajili ya Matibabu.

Ajali hiyo imetokea majira ya Saa Moja Usiku katika Eneo la Gairo

Tutaendelea Kupeana taarifa zaidi kadri tunavyozipata

Tunapenda kutoa Pole kwa Mmoja wa Majaji wa Shindano la Tanzania Movie Talents ambae ni Mzazi Mwenza wa Marehemu George Tyson, Bi Vyonne Chery Kwa kuondokewa na Mzazi mwenzie ambae walibahatika Kupata Mtoto Mmoja aitwaye Sonia.

Timu nzima ta TMT inatoa Pole kwa Msiba Huu

BREAKING NEWSSS:::MWANAMKE AUAWA VIBAYA KWA KUKATWA KICHWA HUKO GEITA KWA IMANI ZA KISHIRIKINA TUNAOMBA RADHI KWA PICHA

 Mwili wa Lushiku Tenganija ukiwa chini baada ya mauji hayo


Mwanamke mmoja ameuawa kikatili kwa kukatwa katwa na mapanga sehemu mbalimbali za Mwili wake kwa kudhaniwa kuwa anaimani za Kishirikina, Mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la Lushiku Tenganija  Sono Msukuma aliyekuwa na Umri wa Miaka 59 wa kitongoji cha Senga kata ya Bugando Mkoani Geita ameuawa na mwili kuonekana muda wa Saa moja asubuhi jana  ukiwa kwenye barabara ya mtaa umbali wa mita kama mia tatu kutoka nyumbani alipokuwa akiishi Marehemu pamoja na wajukuu zake watatu.
Maremu amekatwa shingo kabisa na kutenganishwa na Mwili, mkono wa kushoto na kulia pamoja na bega la kulia. Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Bwana Joel Saanane (42) amethibitisha kutokea kwa Tukio hilo na kudai kuwa msako mkali unaendelea dhidi ya wauaji hao.