YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Thursday 31 July 2014

AIBU KWA TAIFA: MSANII ANASWA CHINA NA MADAWA YA KULEVYA


HUKU modo maarufu Bongo, Jacqueline Fitzpatrick Cliff ‘Jack Patrick’, akisota jela nchini China kwa skendo ya kukamatwa na madawa ya kulevya (unga), mrembo mwingine ambaye aliwahi kujaribu kuchomoka kisanii kwenye muziki wa Kizazi Kipya almaarufu kwa jina la Winnie Mandela, naye amenaswa na polisi nchini humo.
Mrembo almaarufu kwa jina la 'Winnie Mandela' katika muziki wa kizazi kipya akiwa amenaswa na polisi China.

Tukio hilo lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kupitishwa kwa msako maalum wa kutokomeza biashara hiyo katika viunga vya Mji wa Hong Kong, China.
JUX, PETIT MAN WAPATA WAKATI MGUMU
Kwa mujibu wa chanzo chetu chenye maskani yake Hong Kong, Mbongo Fleva, Juma Khaleed ‘Jux Vuitton’ na meneja wa msanii wa Bongo Fleva aitwaye Mirrow, Petit Man nao walijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kunusurika kuunganishwa kwenye oparesheni hiyo ya ukamataji wa waingizaji wa madawa ya kulevya nchini China.

'Winnie Mandela' wa muziki wa kizazi kipya Bongo akiwa chini ya ulinzi mkali China.

MADAI YA KUBEBA UNGA
Ilidaiwa kwamba Winnie alijikuta mikononi mwa askari wa China akidaiwa kubeba mzigo wa unga tumboni hivyo kukamatwa na kutembezwa mitaani kuelekea kituo cha polisi.

APITA VIZUIZI, AKAMATWA
Ilisemekana kwamba Winnie ambaye ni msichana wa mjini Dar, alifanikiwa kupita vizuizi vyote lakini kwa hali ilivyo kwa sasa nchini humo ndipo akajikuta akikamatwa na kutembezwa mtaani kama mhalifu wa kivita.

“Unaambiwa ilikuwa kama vita kwani polisi wa China huwa wana silaha za kutisha sana. Unajua Winnie alikamatwa kwenye mitaa ambayo kuna Wabongo wengi hapa Hong Kong,” kilisema chanzo chetu kutoka Hong Kong.
Ilidaiwa kwamba askari hao walipokea agizo maalum kutoka kwenye kitengo cha kudhibititi madawa ya kulevya nchini humo kwani kwa sasa nchi hiyo imechafuka kwa uingizwaji wa madawa ya kulevya, jambo ambalo limeifanya serikali ya China ifanye oparesheni kubwa ya kuhakikisha wanatokomeza wimbi hilo.
KWA WABONGO CHINA
Chanzo chetu kilisema kwamba kwa sasa Wabongo wanaokwenda au wanaokaa China wanaishi kama digidigi kwani wamefikia hatua ya kutoonesha pasipoti  zao na hata wengine wanadiriki kukataa uraia wao kwa kuwa Wabongo ndiyo wanasakwa kwa wingi.

“Sasa hivi jamaa wakisikia huyo ni Mtanzania wanamfuatilia sana kwani ndiyo wenye sifa ya uingizaji wa dawa za kulevya nchini China,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
KAMA HUAMINI MUULIZE JUX AU PETIT MAN
“Hicho ndicho kilichomtokea Winnie. Nakwambia Wabongo wanazidi kukamatwa na madawa ya kulevya. Yaani ni aibu, huwezi kuamini.

“Wabongo wengi sana wamekamatwa Hong Kong na wengine familia zao Bongo hazijui.
“Kama Watanzania hawaamini wawaulize Jux na Petit Man ambao walishuhudia mtiti mwanzo mwisho.”

BALOZI WA TANZANIA CHINA
Ili kupata undani na idadi ya Watanzania wanaokamatwa kwa ishu za madawa ya kulevya nchini China, gazeti hili lilimtafuta Balozi wa Tanzania China, Luteni General Abraham Shimbo ambapo simu yake ya ofisini iliita bila kupokelewa.

Wakati Jack Patrick akisubiri kupandishwa kizimbani kwa mara nyingine mwezi ujao, ripoti zinaonesha kwamba wapo Watanzania wengi waliofungwa na wengine kunyongwa kwa msala wa madawa ya kulevya

DUNIANI KUNA MAMBO JAMANI, UNAAMBIWA MISUKULE YA GWAJIMA YATINGA POLIS... NDUGU WATHIBITISHA KUHUSU VIFO VYAO




msukule1

Baada  ya  hivi  karibuni  kutoa  waraka  mzito  unaowalenga  watumishi  wa  mungu  kwa  kile  alichodai  kuwa  ni  ukiukwaji  wa  sheria  za  mungu, Nabii Hosea  Chamungu  ametangaza  rasmi  kuiwasilisha  ripoti  ya  misukule  feki  mikononi  mwa  jeshi  la  polisi  ili  hatua  za  kisheria  zichukuliwe…
.
Akiongea  kwa  kujiamini, Nabii  Cha Mungu  alimuonyesha  mwandishi  baadhi  ya  picha  za  misukule  ikiwmo  iliyowahi  kuonyeshwa  ndani  ya  kanisa  la  ufufuo  na  uzima  linaloongozwa  na  mchungaji  Josephat  Gwajima…..
“Unapofanya  kazi  ya  mungu  hutakiwi  kuwa  mwoga  kwa  lolote  kwani  yeye  ndiye  anayetulinda  sisi  sote, kondoo  wa  bwana  wamekuwa  wakipotea  siku  hadi  siku  huku  wachungaji  tukiwaangalia  bila  kuwaokoa.Mimi  sikubaliani  na  hii  miujiza  ya  kutoa  misukule  inayotangazwa  kila  siku  wakati  hatujui  hao  misukule  walifia  wapi….
msukule1
“Baada  ya  kufunuliwa  na  mungu  juu  ya  jambo  hili, nimeanza  kukusanya  taarifa  kuhusiaa  na  hili  jambo  na  tayari  uelekeo umeshapatikana, watu  hawataamini  siku  nitakapoliweka  wazi  hili  suala  kwani  nitaliomba  jeshi  la  polisi  liwashitaki  wote  waliorubuniwa  na  kujifanya  misukule  pamoja  na  wale  walioinjinia  ishu  nzima.Kama  kuna  watu  wenye  uwezo  wa  kufufua  watu  kwa  nini  vifo  vinaendelea  kutokea  kila  siku?”,alisema  Cha Mungu
Cha  Mungu  alidai kuwa  zoezi  hilo  litafikia  hitimisho  mwishoni  mwa  mwezi  ujao.
Aidha, alitoa  wito  kwa  ndugu, jamaa  na  wazazi  ambao  kwa  namna  moja  au  nyingine  wamehusika  na  kuficha  siri  za  ndugu, jamaa  au  watoto  wao  waliojihusisha  na  zoezi  la  kumdhihaki  Mungu  la  kujifanya  wao  ni  misukule  wangali  wakijua  si  kweli  wajisalimishe  kabla  hajawaumbua….
msukule
“Nitakapokamilisha  details  nitawataja  kwa  majina, mahali  walipo  na  jinsi  walivyohusika, kwa  wale  ambao  wanaogopa  vitisho  waje  nitawaombea  na  roho  ya  woga  itaondoka  na  hakuna  atakayewadhuru,” alisema
Jitihada  za  kumpata  mchungaji  Gwajima  kuongelea  suala  hilo  ziligonga  mwamba  kutokana  na  simu  yake  kutopatikana.

AIBU KUBWA HII: MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI AFUMWA AKILIWA URODA GESTI MCHANA KWEUPE


Askari wa jeshi la polisi na wasamaria wema wakiwa wamemdhibti binti anayedaiwa kuwa ni mwanafunzi wa darasa la saba moja ya shule ya msingi Manispaa ya Morogoro,
binti huyo anadaiwa kukurupushwa katika moja ya nyumba ya kulala wageni eneo la Mawenzi wakati akipelekwa kituo kidogo cha polisi. Kwa kile kinachodaiwa kujihusisha na mapenzi na masomo.
Wasamalia wema wakiwa wamemdhibti binti anayedaiwa kuwa ni mwanafunzi wa darasa la saba Manispaa ya Morogoro baada ya kumnusuru na kipigo

Sunday 27 July 2014

RAIS KIKWETE ATUNUKU WAHITIMU WA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI KATIKA MAHAFALI YA KOZI YA PILI


 Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Kanali
James Ruzibiza Stashahada ya Usalama na Stratejia (Diploma in Security
and Strategic Studies) katika mahafali ya Kozi ya Pili ya Chuo Cha Taifa
cha Ulinzi (NDC) chuoni hapo Kunduchi jijini Dar es salaam leo Julai
26, 2014. Kanali Ruzibiza, ambaye anatokea Rwanda, ni mmoja wa washiriki
tisa wa kozi waliotoka nchi za nje. Washiriki wengine kutoka nje y nchi
walitoka Kenya, Malawi, Namibia, Nigeria, Uganda, zambia na Zimbabwe.
Jumla ya wahitimu 30, wakiwemo maafisa wandamizi katika utumishi wa
umma, ambapo 11 wametoka JWTZ na 10 kutoka vyombo vingine vya usalama na idara mbalimbali. 
 Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku Luteni Jenerali
C.L. Makakala Shahada ya Uzamili ya Falsafa ya Usalama na Stratejia
katika mahafali ya Kozi ya Pili ya Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC)
chuoni hapo Kunduchi jijini Dar es salaam leo Julai 26, 2014. Luteni
jenerali Makakala, ambaye ni Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi wa
kwanza, amekuwa mtunukiwa wa kwanza wa Shahada hiyo hapo chuoni.
 Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia baada ya kutunuku shahada katika  mahafali ya Kozi ya Pili ya Chuo Cha Taifa cha Ulinzi  (NDC) chuoni hapo Kunduchi jijini Dar es salaam leo Julai 26, 2014.Jumla ya wahitimu 30 wamehudhuria kozi hiyo wakiwemo maafisa wandamizi katika utumishi wa umma, ambapo 11 wametoka JWTZ na 10 kutoka vyombo vingine  vya usalama na idara mbalimbali. Washiriki wengine tisa wametoka  nchi  za nje ambazo ni Kenya, Malawi, Namibia, Nigeria, Rwanda Uganda, Zambia  na Zimbabwe.
 Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwaambia kuwa sasa ni
zamu yao kupiga picha ya kumbukumbu bila yeye wahitimu wa Kozi ya Pili
ya Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC) chuoni hapo Kunduchi jijini Dar es
salaam leo Julai 26, 2014.

NEWS ALERT : BASI LA HOOD LAPATA AJALI MBAYA ASUBUHI HII LIKITOKEA MBEYA


Muda mchache baada ajali kutokea 
 Askari wa usalama wa barabarani wakiwa wamefika eneo la tukio  na baadhi ya Mashuhuda wakishuhudia ajali hiyo
 Basi la Hood limepata ajali asubuhi hii likitoka Mbeya haijafahamika mara moja lilikuwa linaelekea wapi na haijafahamika kama kuna watu waliojeruhiwa, endelea kufutilia hapa kupata taarifa kamili hii ni taarifa ya awali. Picha na Mbeya yetu Blog

MWIMBAJI BAHATI BUKUKU APATA AJALI MBAYA YA GARI


Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kwamba, mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili hapa nchini, Bahati Bukuku amenusurika kifo baada ya gari alilokuwa akisafiria kupata ajali mbaya katika eneo la Kongwa, mkoani Dodoma usiku wa kuamkia leo.
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari, mwimbaji huyo alipata majeraha makubwa sehemu mbalimbali mwilini na kwamba chanzo cha ajali hiyo kinadhaniwa kuwa ni mwendokasi.
Chanzo hicho hakijaweza kueleza zaidi kwamba Bukuku alikuwa akielekea ama kutoka mkoani Dodoma na kama ndani ya gari hilo kulikuwamo na abiria wengine.
Pia haikuweza kufahamika mara moja kama mwimbaji huyo alikuwa akiendesha mwenyewe gari hilo, ingawa kilithibishwa ajali hiyo na kwamba Bukuku alijeruhiwa vibaya.
Endelea kuperuzi blogu hii kwa habari zaidi ya tukio hilo.

DUNIA HAIISHUI VITUKO:KUTANA NA BINTI ALIEOMBA KU-DATE NA UHURU KENYATA....WALINZI WAKAMBANIA...SOMA STORY NZIMA HAPA


Binti huyu ni rafiki wa Uhuru Kenyatta  huko Facebook..sasa alimuomba KU-DATE na kupitia hukohuko FB na kukubaliwa..SOMA  HAPO CHINI ISHU ILISHINDIKANA VIP...
SOMA HAPA

Saturday 26 July 2014

MFANYAKAZI WA NDANI ABAKWA HADI KUFA HUKO DODOMA,ALIPOTEA TANGU JUMAMOSI ILIYOPITA


Kinamama walio karibu na familia ya marehemu Isabela Andrew aliyebakwa hadi kufa wakiangua kilio baada ya kushuhudia mahali mwili wake ulipokutwa huko Area C mjini Dodoma jana. 
Mfanyakazi wa ndani, Isabella Andrew (18), amefariki dunia na kifo chake kikidaiwa kusababishwa na kubakwa na watu wasiojulikana.

Mwili wa msichana huyo ulikutwa ukiwa umeharibika katika moja ya pagale, lililopo Area C, Dodoma Mjini na mwandishi wetu alishuhudia ukitolewa hapo kwa machela huku polisi wakiwahoji mashuhuda wa tukio hilo.

Mkazi wa Mtaa wa Kiwanja cha Ndege, Jackson Coy aliyekuwa akiishi na binti huyo alisema msichana huyo alipotea tangu Jumamosi iliyopita.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime, alisema mwili huo uliokotwa jana saa mbili asubuhi na kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo chake.

Mwili huo ulibainika baada ya mama mmoja, Rehema Msambile kufika katika pagale hilo alipokuwa akifuatilia nyendo za mtoto wake ambaye juzi alipigwa kwa tabia ya utoro shuleni.

“Niliamua leo (jana) kumfuatilia, nikaanza katika mapagale.Nilipofika hapa ndipo nikaona mwili wa marehemu ikabidi nimuite jirani hapo aje aone,” alisema.

Diwani wa Kata ya Kiwanja cha Ndege, Henry Kandenga alisema mazingira yanaonyesha kuwa binti huyo alibakwa kwa sababu walikuta nguo za ndani zikiwa pembeni.

“Hakuna yowe iliyosikika kwamba kuna mtu anauawa ukizingatia kwamba nyumba ziko jirani na hata nyumba aliyokuwa akiishi ni jirani na mahali alipokutwa,” alisema .

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma

HUSSEIN MACHOZI AFUMANIWA KENYA NA MKE WA MTU,

Hussein Machozi afumaniwa akizini na mke wa mwanasiasa maarufu Kenya

posted 3 hours ago by admin
Hit maker wa  ‘Kwa Ajili Yako’, Hussein Machozi aliyekuwa ameweka kambi na kukubalika sana nchini Kenya anadaiwa kuwa amefumaniwa na mke wa mwanasiasa wa nchini humo na kupewa masaa 24 kuvuka mpaka wa Kenya.
Kwa mujibu wa gazeti la The Star la Kenya, Hussein Machozi alikuwa anatembea na mwanamke wa mwanasiasa huyo wa Mombasa kwa muda mrefu kwa siri huku wakiwa na mipango mikubwa ikiwa ni pamoja na kununua nyumba.
Lakini mapenzi ni kikohozi, siri hiyo ilimfikia mwanasiasa huyo baada ya kushtukia pale alipoona ujumbe usio wa kawaida kwenye simu ya mkewe kwa njia ya WhatsApp.
Mwanasiasa huyo ambaye anadaiwa kuwa mtu anaesafiri mara kwa mara  kufanya biashara na kushughulikia mambo ya siasa aliamua kuweka mtego ambao ulimnasa mwizi wake na kumtia mikononi mwake.
Gazeti hilo linaeleza kuwa liliongea na rafiki wa karibu wa Hussein Machozi wa Mombasa anaefahamika kwa jina maarufu Notystee na alikiri kutokea kwa tukio hilo.
“Nilishtuka pale nilipopokea simu kutoka kwa Hussein Machozi akiniambia kuwa alikuwa katika tatizo. Aliniambia mapema kuwa anaenda kukutana na mwanamke ambaye alikuwa mpenzi wake lakini sikujua kitu ambacho kingetokea.”
Hata hivyo, Hussein Machozi anaonekana bado yuko nchini Kenya kwa mujibu wa chanzo chetu

MAUZAUZA NDANI YA KABURI LA ADAMU KUMBIANA...YALIYOTOKEA HAPA NI ZAIDI YA YALIYOKUTWA KWA RECHO


SIKU chache baada ya kukutwa mauzauza katika kaburi la mwigizaji Rachel Haule ‘Recho’, kaburi la mwigizaji Adam Kuambiana (pichani)limekutwa limetoboka kimaajabu.

Gazeti la Risasi Jumamosi toleo la Julai 19, mwaka huu lilikuwa na babari yenye kichwa cha habari kisemacho: ‘Uchawi kaburini kwa Recho.’ Kwenye habari hiyo, ilielezwa kuwa katika kaburi la Recho kulikutwa tunguri iliyoviringishwa shanga, kitambaa cha kanga chakavu, manyoya ya kuku, yai moja na vitu vingine ambavyo havikujulikana ni nini.

Baada ya habari hiyo, siku mbili baadaye, chanzo kingine kiliwapigia simu waandishi wetu na kuwaeleza kuwa mbali na tukio la Recho, kaburi la Kuambiana limetoboka kimaajabu na kuzua mtafaruku miongoni mwa watu walioshuhudia kwa mara ya kwanza tukio hilo.

“Jamani haya ni mambo ya kishirikina, huwezi amini kaburi hili limetoboka ghafla kimaajabu maana juzi tu nilikuja kutembelea makaburi haya, lilikuwa halijatoboka,” kilisema chanzo hicho.

Mapaparazi wetu walifika katika makaburi hayo na kujionea kaburi hilo likiwa limetoboka huku watu wengi waliokuwepo eneo hilo walidai kuwa tukio hilo si la kawaida kwani limetokea wakati ambao mvua hazijanyesha.

Walisema kama tukio hilo lingetokea wakati ambao mvua zinanyesha basi wasingekuwa na mashaka lakini kwa jinsi ambavyo limetoboka wakati wa jua kali ni dhahiri kutakuwa na ‘mkono wa mtu’.
“Hapa bwana tusidanganyane kuna mkono wa mtu, haiwezekani kaburi lisitoboke kipindi kile cha mwanzomwanzo lije kutoboka sasa wakati kuna jua kali namna hii, lazima kuna mkono wa mtu tu,” alisema shuhuda mmoja.

Wengine walikwenda mbali zaidi kwa kuhoji kulikoni matukio hayo yawe kwa mastaa pekee na si kwa watu wengine?“Hii si bure hapa wachawi watakuwa na shida yao binafsi, haiwezekani iwe kwa mastaa tu ndiyo kunakuwa na mauzauza,” alisikika shuhuda mwingine.
Alipoulizwa mmoja wa walinzi wa eneo hilo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini, alisema hata yeye hajui kwa nini inatokea katika makaburi ya mastaa.“Mimi hata sijui kwa nini lakini yamefululiza, juzi tumeona kwa Recho na leo kwa Kuambiana, tumuombe sana Mungu atuepushe na mabaya,” alisema mlinzi huyo.

Hata hivyo, licha ya watu wengi walioshuhudia kaburi hilo kuamini katika uchawi, mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo ambaye alionekana ni mcha Mungu alisema hakuna uchawi wowote zaidi ya ardhi kutitia na kusababisha mmomonyoko wa udongo.

“Jamani siyo uchawi, hivi vitu vinatokea. Hapa itakuwa wakati wa kuzika, kulikuwa na uwazi umeachwa hivyo ardhi iliposhuka kuziba uwazi huo ndipo iliposababisha tobo,” alisema shuhuda huyo mcha Mungu.
Kuambiana alikutwa na umauti Mei 17, mwaka huu alipokuwa akipelekwa katika Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge, Dar baada ya kuugua ghafla akiwa hotelini alipokuwa amepanga kwa ajili ya kuandaa filamu.

PICHA; AJARI YA FUSO HUKO SHINYANGA

25

  • Jul2014


Miili ya marehemu ikiwa katika eneo la dharura katika hospitali ya mkoa wa shinyanga
Hapa ni katika eneo la dharura katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga ambapo majeruhi 29 hadi sasa wamepokelewa kufuatia ajali ya gari aina ya fuso iliyokuwa imebeba watu wengi pamoja na mizigo kuelekea katika mnada wa Mhunze uliopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.Ajali hiyo imetokea asubuhi ya leo Alhamis.Pichani majeruhi waliendelea kuhudumiwa na wataalam wa afya katika hospotali ya mkoa wa Shinyanga
Kwa mujibu wa kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga Dkt Maguja Daniel ameiambia malunde1 blog kuwa mpaka sasa wamepokea miili miwili ya marehemu na majeruhi 29
Huduma inaendelea kutolewa katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga
Baadhi ya majeruhi wameiambia malunde1 blog kuwa gari aina ya fuso waliyokuwa wamepanda tena kwa kujazana ilikuwa inafukuzana na fuso nyingine na ghafla walijikuta wakiwa wameshapinduka
Kulia ni kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga Dkt Maguja Daniel akichukua maelezo kutoka kwa askari wa usalama barabarani
Majeruhi akipelekwa wodini
Kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga Dkt Maguja Daniel akizungumza na waandishi wa habari hivi punde-Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

ANGALIA PICHA ZA MAKAHABA WA KICHINA WAKIKIMBIZWA NA ASKARI DAR





Tag : AIBULAANAMAJANGA

MAMBO ANAYOYAFANYA SHILOLE NA WENZIE






 

















AFUMWA NA KUTEMBEZEWA KICHAPO LAIVU

TIMBWILI la aina yake lilifumuka ndani ya gesti moja iliyopo Mbezi Afrikana jijini Dar es Salaam (jina kapuni), kufuatia kijana aliyefahamika kwa jina moja la Kelvin kumkuta chumbani mtu aliyedai ni mjomba wake, Joseph akiwa na mkewe wa ndoa, Emiliani.
Mjomba wa Kelvin(Joseph) akimsihi Mpwa wake amsamehe mara baada ya kukutwa gesti na mke wa Kelvin.
Mkasa huo wa ajabu ulijiri usiku wa Jumamosi iliyopita kwenye gesti hiyo iliyopo Mbezi ya Afrikana jijini Dar es Salaam.
MPISHI WA FUTARI AUZA ISHU OFM
Mama mmoja aliyedai ni mpishi wa futari maeneo hayo, alipiga simu kwa makamanda wa Oparesheni Fichua Maovu (OFM) na kusema:
Kelvin (kulia)'akidili' kisawasawa na mjomba wake. 
“Mimi ni mpishi wa futari hapa Mbezi Afrikana kuna baba mmoja na ndugu zake wanachakazana, kisa wamefumaniana kwenye gesti ya (akaitaja jina). Ipo hapahapa jirani njooni muwahi.”
Mlinzi wa gesti akijaribu kumzuia Kelvin asizidi kumjeruhi mjomba wake.
OFM KAZINI, AIBU!
Kufuatia taarifa hiyo, mkuu wa zamu wa OFM aliwaagiza mapaparazi wake wanaotumia pikipiki ziendazo kasi ambao walitumia muda usiozidi robo saa kutoka walipokuwa kufika eneo la tukio ambapo walimkuta Kelvin amemvaa mjomba ‘ake chumbani ambapo timbwili zito lilitifuka. Walikuwa wakigaragazana huku mjomba mtu huyo akiwa kama alivyozaliwa na damu chapachapa jambo lililomtia aibu!
Mjomba akiwa chumba cha gesti mara baada ya mkong'oto 'hevi' kutoka kwa mpwa wake.
PICHA ZA TUKIO
Mapaparazi wetu bila kuzubaa nao walianza kuchukua picha za tukio  hatua kwa hatua. Wakati Timbwili likiendelea, Joseph alikuwa akipiga mayowe kumuomba mpwa wake huyo amsamehe ili wayamalize kimyakimya na kumsihi asisambaze habari hizo zikafika mpaka nyumbani kwa mke wake.
MKE ATIMKA KINYEMELA
Katika hali ya kushangza, wakati wawili hao wakiendelea kuangushana chumbani, mke huyo alipata upenyo na kuchoropoka, akatimua mbio kwa kuhofia kipigo na kukwepa kamera za OFM.
...Mjomba taratiiibu 'akirejesha' mavazi mwilini mwake.
MLINZI WA GESTI
Timbwili la wajomba hao lilitulizwa na mlinzi wa gesti hiyo (jina halikujulikana)  ambaye alitumia mabavu na kufanikiwa kuwadhibiti na kuwaweka kitako.
MJOMBA MTU AGOMA KWENDA POLISI
Baada ya kutulizwa, Kelvin aling’ang’ania waende polisi lakini mjomba mtu alikataa katakata akimbembeleza mpwa wake kwamba wayamalize na kuahidi kutorudia tena mchezo huo huku akisema mwanamke huyo alimuwekea mtego wa makusudi.
Mjomba akiomba msamaha kwa mpwa wake.
CHONDECHONDE KELVIN
Baadhi ya waungwana waliofika kushuhudia tukio hilo walimsihi Kelvin kumsikiliza mjomba ‘ake na kupokea fidia kidogo kwani kuyasongesha mbele mambo hayo ni aibu kwa familia yao na kumtia matatani mjomba huyo kwa mkewe.
MJOMBA ‘AJIKOMITI’ KIMAANDISHI
Kufuatia maombi ya watu, akiwemo mlinzi wa gesti hiyo, Kelvin alikubali kumsamehe mjomba wake ambaye naye ‘alijikomiti’ kimaandishi (kopi tunayo) kumlipa Kelvin fidia ya shilingi laki tano (500,000) na kuahidi kutorudia kummendea mke wake.
Sehemu ya nyaraka ikionyesha mjomba 'akijikomiti' kimaandishi.
Katika barua hiyo aliyoaindika Joseph kwa mkono, alikiri kukutwa na mke wa Kelvin na kusema anatoa shilingi laki tatu (300,000) siku hiyo kisha kiasi kinachobaki atatoa siku inayofuata.
MGONI AGEUKA NA KWENDA KUFUNGUA KESI
Hata hivyo, taarifa zilizotufikia wakati tunakwenda mitamboni zinadai kuwa, Joseph alikwenda kituo cha polisi (jina halijajulikana) kumfungulia kesi mpwa wake Kelvin na mkewe Emiliani akidai walipanga kumfanyia fumanizi.
KUTOKA KWA MHARIRI
Kwa sababu kisa hiki kinadaiwa kufikishwa polisi na Joseph, magazeti pendwa ya Global yataendelea kukifuatilia ili kujua mwisho wake. Endelea kusoma.