YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Wednesday 13 August 2014

DEREVA WA BODABODA ASAKWA KWA KUUA.

Jeshi la polisi Mkoani Iringa linamtafuta dereva wa pikipiki kwa tuhuma ya kusababisha kifo cha mtembea kwa miguu kwa ajali ya barabarani kisha kukimbia baada ya kutokea kwa tukio hilo.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa jeshi la polisi Mkoani Iringa ACP Ramadhani Mungi amesema Mfaume Kilangi ambaye pia ni mwenyekitio wa kijiji cha Idodi wilaya ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa akiwa anaendesha pikipiki ambayo haijafahamika namba zake za uasjili ilimgonga na kusababisha kifo cha Laurent Kafwela umri miaka 40.

Aidha ameongeza kuwa marehemu amefariki muda mfupi akiwa anakimbizwa katika hospitari ya Mapogoro wilaya ya Iringa Vijijini Mkoa wa Iringa na chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi na uzembe wa dereva wa kutochukua tahadhari kwenye makazi ya watu.Hata hivyo Kamanda Mungi amesema ajari hiyo imetokea katika eneo la Mapogoro katika barabara ya Idodi-Tagamenda wilaya ya Iringa Vijijini pia ametoa wito kwa wamiliki na madereva kuwa makini wawapo barabarani kwa kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajari zinazoweza kuepukika

RIHANA ASHAULIWA NA DROGBA KUINUNUA LIVERPOOL

Rihanna anataka kuinunua Liverpool FC, ashauriwa na Drogba

posted 4 hours ago by admin
Mapenzi ya Rihanna kwenye soka yameingia katika hatua nyingine na sasa hataki kuwa shabiki tu bali mmiliki halali wa timu kubwa duniani, na kwa kuanza anataka kuinunua Liverpool FC!
Kwa mujibu wa gazeti la Hispania, El Mundo Deportivo mwimbaji huyo alianza mpango huo muda mfupi baada ya kuisha kwa fainali za kombe la dunia nchini Brazil ambapo alionekana akitweet mara kwa mara kuhusu mechi zilizokuwa zinaendeelea.
Gazeti hilo limeeleza kuwa Rihanna amekuwa akipata ushauri kutoka kwa marafiki zake wa karibu akiwemo mchezaji wa Chelsea, Didier Drogba ili kufanya maamuzi sahihi katika ununuzi wa club ya mpira wa miguu.
Kwa sasa Liverpool inamilikiwa na John W. Henry na hana mpango wa kuiuza timu hiyo ya soka.
Huwezi jua, endelea kutembelea www.timesfm.co.tz kufahamu kitakachoendelea

WANAWAKE WAPINGA JESHI KUPELEKA WAUME ZAO VITANI.

Wanawake wayazuia magari ya jeshi yaliyokuwa yakiwapeleka waume zao kupigana na Boko Haram

posted 1 day ago by admin
Ripoti kutoka Nigeria zinaeleza kuwa Jumamosi iliyopita kundi kubwa la wanawake lilijitokeza na kuzuia magari ya jeshi yaliyokuwa yamewabeba wanaume wao na wake zao yakielekea katika mji wa Gwosa, sehemu ambayo inadhibitiwa na kundi la Boko Haram.
Kwa mujibu wa Prime Times ya Nigeria, wanawake hao walizua geti la barracks katika mji wa Borno huku wengine wakilala barabarani kushinikiza waume zao wapewe vifaa vya kisasa na imara zaidi ndipo waende vitani kupambana na kundi hilo.
Hali hiyo imekuja baada ya kuripotiwa kuwa karibu wanajeshi 60 waliuawa Jumatano iliyopita katika eneo la Gwosa linalomilikiwa na Boko Haram na kudaiwa kuwa sababu kubwa ni zana duni walizokuwa nazo kulinganisha na zana za kisasa za kijeshi za kundi hilo.
Chanzo kimeiambia Prime Times kuwa wanawake hao walieleza kuwa hawataki kubaki wajane na yatima kama wenzao kwa sababu ya vita hiyo.
“Mwanamke mmoja alisema ‘hatutaki kuwa kundi lingine la wajane, wapeni waume zetu zana bora zaidi za kivita, silaha na magari bora zaidi la sivyo hawaendi kokote’.”
Wanajeshi wengine pia walionekana kuunga mkono madai ya wanawake hao na kusukuma lawama kwa maafisa wa serikali.
We are ever ready to tackle Boko Haram terrorists but our superior officers are the ones killing us by not giving us the right arms to execute the war. How could I go and face Boko Haram with AK47 that is charged with only three cartridges when the enemy is brandishing modern GPMG, AA, RPG and so on.”Alikaririwa mwanajeshi mmoja.
Kundi la Boko Haram bado linawashikilia mateka wanafunzi wa kike zaidi ya 200 na wanawake wengine huku likitekeleza mauji ya kutisha katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 13.08.2014


.
23_45aae.jpg
2_af633.jpg

21_8f720.jpg
4_14e1c.jpg 3_f7699.jpg
22_736c8.jpg
04_6bac1.jpg
37_65b2d.jpg
5_301d6.jpg

31_cdf56.jpg6_2baf6.jpg
30_568a1.jpg
7_b2b38.jpg
38_85748.jpg
11_51f64.jpg
36_622b3.jpg
12_69ac7.jpg
35_558f6.jpg
39_48121.jpg

Sunday 10 August 2014

VIDEO YA DIAMOND NA NEY WAKIFANYA YAO FIESTA


Diamond Mwanza Aug 9Japokuwa ni show ya kwanza kufanyika kwenye msimu huu wa Serengeti Fiesta 2014, inaonekana itakuwa miongoni mwa show zitakazovunja rekodi kwenye idadi ya mahudhurio.
Show ilifanyika CCM Kirumba kwa amani huku ukaguzi ukifanywa mlangoni na Polisi kwa kila aliekua akiingia ambapo miongoni mwa wakali waliochukua nafasi kwenye stage ni Diamond Platnumz na Nay wa Mitego na hit song yao ya ‘muziki gani’ ambayo unaweza kutazama walichofanya hapa chini on AyoTV
Kuwa Mwanafamilia wa millardayo.com na utumiwe kila stori inayonifikia usiku au mchana kwa kubonyeza hapa

BAADA YA GWAJIMA KUNUNUA HERIKOPTA, KAKOBE ASEMA HAYA..

Screen Shot 2014-08-11 at 6.23.39 AM
Gazeti la KIU Aug 1 2014
Kama sehemu ya vyanzo vyako vya habari ni mitandao kama vile website, blogs, facebook, twitter na Instagram inawezekana hii stori ya Gwajima ambae ni Muhubiri wa Injili kununua Helikopta uliiona hata zaidi ya mara moja.
Hata hivyo Muhubiri mwenzake Askofu Zacharia Kakobe Aug 10 2014 amenukuliwa na gazeti la Nyakati na kuizungumzia hiyo Helikopta akisema ‘kitendo cha Gwajima kununua helikopta kwa ajili ya kazi zake za Injili kinastahili kufurahiwa na Wakristo wote wa kweli, tujifunze kupongezana.. nampongeza sana’
‘Kumiliki kwake Helikopta kutachangia katika kufuta dhana potofu ambayo imedumu kwa muda mrefu ya kuyaita Makanisa ya kilokole…. makanisa ya vichochoroni, Helikopta sio starehe na hata muundo wake sio wa starehe bali ni kazi, itamwezesha pia kufika maeneo ambayo gari sio rahisi kumfikisha kutoa neno la Mungu’ – Kakobe
Screen Shot 2014-08-11 at 6.36.10 AMKuhusu Askofu Kakobe kununua Helikopta yake, amesema >>> ‘mimi sio mtu wa mashindano na pia kila mtu anakwenda sawa kutokana na ono aliloitiwa, haya sio mambo ya kushindana… hicho ndicho kinacholeta shida mara kwa mara, Gwajima ana Helikopta ni kwa manufaa ya Ufalme wa Mungu, mimi nina chakwangu ni kwa utukufu wa Mungu, hakuna haja ya kuigana’

BOWE NA KINANA WATETA KWA SIRI DAR.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe

AZIZA MASOUD NA AGATHA CHARLES
IMEDHIHIRIKA kuwa viongozi waandamizi wa vyama vikubwa vya siasa vilivyo na uwakilishi katika Bunge Maalumu la Katiba, wanapanga njama za kulivunja bunge hilo baada ya kushindwa kufikia maridhiano ya muundo wa serikali.
Kuvuja kwa taarifa hizi kumekuja ikiwa ni siku chache baada ya kufanyika vikao kadhaa vilivyowashirikisha viongozi wa vyama vikilenga kutafuta maridhiano ya muundo wa serikali unaopaswa kuandikwa katika Katiba mpya.
Taarifa zilizolifikia MTANZANIA Jumapili kutoka vyanzo vya kuaminika ndani ya vyama vya CCM, Chadema, CUF na NCCR- Mageuzi, zimeeleza kuwepo kwa mikutano ya siri ya viongozi wakuu wa vyama hivyo inayojadili mwenendo wa Bunge la Katiba na hatima ya upatikanaji wa Katiba mpya.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, mwelekeo wa vikao vya viongozi hao unaonyesha mchakato wa kufanikisha upatikanaji Katiba mpya utafanywa na rais wa awamu ya tano atakayeingia madarakani kwa kutumia Katiba ya sasa ambayo itafanyiwa marekebisho.
MTANZANIA Jumapili limedokezwa kuwa vikao hivyo vinafanyika katika hali ya usiri mkubwa na kuhudhuriwa na wenyekiti watatu wa vyama vya upinzani vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wanaotajwa kuwa ni Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF, James Mbatia wa NCCR-Mageuzi na Freeman Mbowe wa Chadema huku CCM ikiwakilishwa na Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana.
Imeelezwa kuwa ili kuweka hali ya usiri wa mazungumzo na makubaliano yatakayofikiwa katika vikao hivyo, wasaidizi wa wanasiasa hao na hata watendaji wengine wanaofanya nao kazi kwa karibu, wamezuiwa kuhudhuria.
Taarifa zilizopatikana kutoka Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, zimeeleza kuwa katika kikao cha kwanza kilichofanyikia Dodoma, Kinana aliondoka Dar es Salaam kwa ndege hadi mkoani humo Alhamisi wiki iliyopita kwa ajili ya kiwafuata Mbowe, Lipumba na Mbatia.
Kwamba katika kikao hicho cha kwanza, ajenda mama ilikuwa kupata suluhu ya kutatua mgogoro wa kikatiba unaoendelea baina ya vyama.
Taarifa zinadai, makubaliano yaliyofikiwa ni pamoja na Kinana kwenda kuongea na Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta ili kumtaka asitishe shughuli za bunge hilo mpaka hapo itakapotangazwa vinginevyo.
Makubaliano mengine ni kuitaka serikali ipeleke muswada wa marekebisho madogo ya Katiba ya Jamhuri katika mkutano wa bunge unaotarajiwa kuketi mwezi Novemba yatakayohusu Katiba kumtambua mgombea binafsi, kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi na kuanzishwa kwa mahakama ya juu (supreme court) itayosikiliza mashauri ya kupinga matokeo ya urais mahakamani.
Muswada huo ambao utaandaliwa na tume ya Makatibu wakuu wa vyama vya siasa na kuwekwa katika lugha ya kisheria na utaratibu wa kiserikali pia utaeleza umuhimu wa ajenda ya Katiba Mpya kujadiliwa baada ya uchaguzi mkuu wa mwezi Novemba 2015.
Alipotafutwa Kinana kupitia simu yake ya kiganjani ili kuzungumzia kuwepo kwa vikao hivyo alilitaka gazeti hili kuzungumza na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye aliyeeleza kuwa ndiye mzungumzaji w mambo yote yanayohusiana na Ukawa.
“Mpigie Nape, tafuta ufafanuzi kutoka kwa Nape wa majibu yeyote unayoyataka,” alisema Kinana.
Naye Mbatia alipopigiwa simu alisema ameshitushwa na taarifa za kuwa mmoja wa wajumbe kwenye kikao hicho na kudai kuwa si za kweli.
“Sio kweli kwamba mimi nilishiriki kikao wala sijasikia kikao chochote, ndio kwanza nakusikia wewe,” alisema Mbatia.
Gazeti hili lilipomtafuta pia Profesa Lipumba lakini simu yake ya kiganjani iliita bila majibu na hata alipotumiwa ujembe mfupi wa maneno hakujibu.
Hata hivyo, hoja za kuvunjwa kwa Bunge la Katiba hivi karibuni zilionekana kupata nguvu kutokana na kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda pamoja na ile ya Jumuiya ya Tawala za Mitaa (ALAT) katika kikao na Mameya wa Majiji, Manispaa na Wenyeviti wa Halmashauri za Miji na Wilaya nchini mjini Tanga waliokaririwa wakisema akisema uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu kwa kutegemea hatma ya mchakato wa Katiba mpya.
Kwa upande mwingine, ALAT mbali na kusisitiza kuwa uchaguzi huo utafanyika mwezi Oktoba, pia Aprili mwaka huu ilitoa tamko kuwa vikao vya Bunge Maalumu la Katiba vinavyoendelea mjini Dodoma ni batili.
ALAT ilisisitiza kuwa vikao hivyo ni batili kutokana na kuwatenga wawakilishi wa wananchi wengi ambao ni jumuiya hiyo.
Uamuzi huo wa ALAT kuwa uchaguzi wa Serikali za Mitaa utafanyika kama ulivyopangwa mwezi Oktoba, unaipa nguvu hoja ya kuvunjwa kwa Bunge la Katiba ili kupisha Bunge la Jamhuri ya Muungano kuketi kwa ajili ya marekebisho ya sheria za uchaguzi.
Kwa mujibu wa mwenendo wa taratibu za uchaguzi, maboresho yanayofanywa na Tume ya Uchaguzi katika daftari la kudumu la wapiga kura, yanatoa hitaji la kufanyika kwa mabadiliko ya sheria ya uchaguzi.
Kutoka na kuwepo kwa hitaji hilo la kisheria, Bunge la Jamhuri litalazimika kuketi ili kufanya marekebisho ya sheria hiyo kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa, Oktoba, mwaka huu.
Mabingwa wa shughuli za kibunge wanaeleza kuwa Bunge la Jamhuri litakapoketi litalazimisha kusitishwa kwa shughuli za Bunge Maalumu la Katiba na ikiwa kinyume chake, uchaguzi wa Serikali za Mitaa hautafanyika kama ulivyopangwa.
Katika mwelekeo wa kukazia hoja ya kuvunjika kwa Bunge hilo, mapendekezo yaliyotolewa katika kikao kinachodaiwa kukaliwa na viongozi wakuu wa vyama vya siasa vikubwa nchini, pia yametolewa na chama cha ACT-Tanzania ambacho kimetaka Bunge hilo kuvunjwa.
Akizungumza jana katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Hoteli ya JB Belmont jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa ACT, Samson Mwigamba, alisema  moja ya mapendekezo yao ni kuona Tume ya Uchaguzi inakuwa huru na ionekane wazi.
Mwigamba pia alisema Katiba ya sasa inapaswa kuruhusu mgombea binafsi na wabunge ‘kukatisha kapeti’ (kuhama chama kimoja na kwenda kingine bila kupoteza ubunge) kwa madai ya kudhibiti ubabe wa vyama vya siasa.
“Pia kushusha umri wa mgombea urais ili kuwapa vijana haki na fursa ya kugombea katika nafasi hii muhimu, hasa ukizingatia kwamba karibu theluthi mbili (65%) ya wapiga kura wote Tanzania wapo chini ya umri wa miaka 40, na ukweli kwamba takwimu za Tume ya Marekebisho ya Katiba zinaonyesha kuwa wananchi walio wengi (53.7%) waliotoa maoni kuhusu umri wa mgombea urais, walitaka umri huo ushushwe,” alisema Mwigamba.
Alisema ATC inapendekeza pia kuwepo kwa masharti kwamba ili mgombea atangazwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, lazima apate angalau asilimia 50 ya kura zilizo halali.
Na kwamba kuwe na msingi wa kikatiba kuwa wagombea hao wa urais wafanye midahalo takribani mitatu katika kipindi cha kampeni.
“Kuondoa suala la mafuta na gesi katika mambo ya Muungano ili kuruhusu Zanzibar kuendelea na utafutaji wa mafuta na gesi asilia kwa uhuru na bila kuingiliwa na Tanzania bara, huku ikiruhusiwa kuwa na ushirikiano wa kimataifa  kwa faida za maendeleo yake,” alisema.
Mbali na masuala hayo ya Zanzibar, Mwigamba alisema kuwe na mipaka ya mashitaka ya kesi za rushwa ili kuruhusu TAKUKURU kufanya uchunguzi na kuendesha kesi, hususani zinazohusu ufisadi wa mali za umma pasipo kupitia kwa Mkurugenzi wa Mashitaka.
Sambamba na hilo, alisema kuwepo na msingi wa kisheria wa tangazo la mali na madeni ya viongozi kuwa wazi kwa umma, na uthibitisho wa uhalali wa mali ambazo mtu anamiliki uwe upande wa mtuhumiwa.
Pia alitaka marekebisho hayo kuweka misingi ya kikatiba kwa uhuru wa kupata habari kwa wananchi na kupiga marufuku vyombo vya habari kufungiwa isipokuwa kwa amri ya mahakama.
Mbali na hayo, lakini pia hoja ya theluthi mbili bado haifikiwi katika Bunge hilo la Katiba linaloendelea na vikao vyake Dodoma.
Hofu ya kupatikana kwa theluthi mbili iliibuliwa pia na mjumbe ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Mwigulu Nchemba.
Mwigulu ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha,  aliungwa mkono na baadhi ya wabunge wa CCM alipotaka Bunge Maalumu la Katiba lijitathmini kama lina ulazima wa kuendelea wakati hakuna uhakika wa kupatikana kwa theluthi mbili.
Hali hiyo ya kukosekana kwa theluthi mbili, ilijitokeza pia hivi karibuni wakati wa Bunge hili kwa kamati namba mbili inayoongozwa na  Shamsi Vuai Nahodha kukosa idadi hiyo katika ibara 19 na 22 zinazohusu maadili na miiko ya uongozi na utumishi wa umma.
Na kwamba ili theluthi mbili ipatikane katika Bunge hilo, wanahitajika wajumbe 16 kutoka upande wa Zanzibar.
Viongozi wa juu wa  Ukawa pamoja na wale wa CCM  walishakutana zaidi ya mara mbili wakiwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kwa lengo la kutafuta maridhiano bila mafanikio.
Katika vikao walivyofanya na Jaji Mutungi ambavyo havikuzaa matunda, cha mwisho kilifanyika Agosti mosi katika Hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam.
Viongozi hao pia waliwahi kuitwa  na wajumbe wa Kamati ya Maridhiano ya Bunge Maalumu la Katiba, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta jijini Dar es Salaam, lakini wajumbe wa Ukawa waligoma kufika katika mkutano huo.
Mkutano huo ulikuwa na lengo la kuikutanisha kamati hiyo pamoja na wajumbe hao kwa ajili ya kutafuta suluhu ya mvutano uliotokea katika Bunge hilo lililopita ambapo Ukawa walitoka nje.
Kamati hiyo iliyoteuliwa na Sitta kabla ya kuanza kwa awamu ya pili ya mjadala wa Katiba Agosti 5 kwa ajili ya kutafuta suluhu ya mvutano huo, ilijumuisha wajumbe kutoka vyama, taasisi na mashirika yote yaliyowakilishwa katika Bunge hilo.
Hata hivyo, katika mkutano huo, wajumbe waliohudhuria takribani wote ni viongozi, hasa mawaziri na baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo walioko kwenye kamati hiyo kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) na taasisi mbalimbali, huku vyama vya upinzani aliyehudhuria ni Peter Mzirai kutoka chama cha APPT-Maendeleo.

AMWAGIWA UJI KWA TUHUMA ZA KUCHEPUKA NA BOSI WAKE

MSICHANA mmoja mkazi wa eneo la Minga katika Manispaa ya Singida (muuza duka), amenusurika kifo baada ya kumwagiwa uji wa moto na mke wa tajiri yake na kumsababishia maumivu makali kutokana na kile kinachosadikiwa kuwa ni wivu wa kimapenzi.
Muuguzi wa zamu katika Hospitali ya mkoa wa Singida, wodi namba mbili ya wanawake, Anna Sprian ameifahamisha FikraPevu kuwa binti huyo amejeruhiwa sehemu za sikio la upande wa kulia na mgongoni, ambapo amesema hali ya mgonjwa huyo inaendelea vizuri kutokana na matibabu anayoyapata hospitalini hapo.
Mhudumu
Akizungumza na FikraPevu leo Agosti 10, 2014 kwa tabu, binti huyo Jackline Lasway (23), maarufu kwa jina la Pendo, amesema majeraha ya moto katika sehemu ya sikio la upande wa kulia na mgongoni.
Singida 1
Majeruhi, Jackline Lasway, akiwa amelazwa katika wodi ya wanawake katika Hospitali ya mkoa wa Singida, baada ya kujeruhiwa kwa kumwagiwa uji wa moto wakati akiwa dukani kwa bosi wake katika Manispaa ya Singida
Pendo amesema kuwa tukio hilo limetokea jana Jumamosi Agosti 9, 2014 saa nane mchana wakati akiwa dukani kwa bosi wake aliyemtaja kwa jina la, Charles Kamnde.
Amesema akiwa anaendelea na kazi zake za kuuza bidhaa mbalimbali dukani hapo, gafla alitokea mke wa bosi wake akiwa na chupa yenye uji wa moto na kuwa alimmwagia usoni ambapo baada ya kumwagiwa uji huo alitaka kujiokoa ili usimmwagikie usoni na ndipo ulimuunguza kwenye sikio la kulia na mgongoni na kuwa baada ya mke wa bosi wake kumkosa uso alitoa kisu kutaka kumchoma kifuani.
“Mimi sikuwa na ugomvi naye wala sijui chanzo cha yeye kufika dukani na kunifanyia vile jana, maana kama ni kazi mimi ninafanya kulingana na maelekezo kutoka kwa bosi wangu Chale lakini sijui kilichomfanya afikirie kunifanyia huu unyama” alisema.
Aidha, amesema katika purukushani za kujiokoa kuwa asichomwe kisu hicho, alifanikiwa kumkamata mkono mwanamke huyo na kupiga kelele za kuomba msaada ambapo watu walifika na kumwokoa baada ya muda mchache ambapo alichukuliwa na bosi wake hadi Kituo cha Polisi mjini Singida na kupewa PF3 kwa ajili ya matibabu na kupelekwa katika hospitali hiyo ambako amelazwa huku akiwa ma majeraha mwilini.
Kwa upande wake, mmiliki wa duka hilo Chale Kamnde alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa hayuko tayari kulizungumzia kwani maelezo aliyotoa binti huyo yanajitosheleza.
Wakiongea kwa nyakati tofauti na FikraPevu baadhi ya majirani wa familia hiyo, wameonyesha masikitiko yao juu ya tukio hilo na hatua ya mwananmke huyo kummwagia uji msichana huyo huku wakihusisha tukio hilo na wivu wa kimapenzi baina ya mfanyakazi huyo na mume wa mtuhumiwa.
“Kama aliona kama kuna sehemu kamkosea angemuonya au kama ameshindwa kueleweka basi angemshitaki hata polisi kwani kitu alichokifanya hakiendani na haki za binadamu kwakuwa ni kumdhalilisha huyu msichana ambaye alikuwa akifanya kazi kwa ajili ya kujipatia kipato chake na familia yake.
Kamanda wa Polisi Mkoani hapa, Geofrey Kamwela, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwa wanamshikilia mtuhumiwa kwa mahojiano na mara baada ya upelelezi kukamilika atafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma hizo

MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 11.08.2014


1_1d4dc.jpg

2_e6a33.jpg
03_0a6c2.jpg
3_f526a.jpg
4_6137e.jpg
5_e44f3.jpg
6_b9a5c.jpg
7_89a91.jpg
8_d120f.jpg
9_0ea2f.jpg
10_fb001.jpg

AJABU NA KWELI, SAMAKI MTU AINA YA NGUVA AONEKANA LAIVU

LI

FM KIBONDE WA CLOUDS AJIFANYA MJANJA KUMBE.... POLISI WAKOMAA NAYE MWANZO MWISHO



Mtangazani Mahiri wa Redio Clouds FM Ephrahim Kibonde akidhibitiwa na Askari wa Usalama barabarani.

Mtangazani Mahiri wa Redio 88.5 Clouds FM kupitia kipindi cha Jahazi, Ephrahim Kibonde akidhibitiwa na Askari wa Usalama barabarani wakati alipotakiwa kutii sheria bila shurti,mapema asubuhi hii jijini Dar es salaam.
Kibonde anadaiwa kusababisha ajali asubuhi hii eneo la Makumbusho, ikiwa gari aliyokuwa akiendesha kuigonga gari ya dereva mwingine kwa nyuma. Trafiki walifika eneo la tukio na kupima ajali, Kibonde alipoona hivyo akarudi nyuma na kuendesha gari lake kuondoka eneo la tukio bila kufuata taratibu za usalama barabarani,hali iliyomlazimu yule Trafiki katumia gari lililogongwa kumfukuzia.

Walifanikiwa kumkamata eneo la Mwenge na Trafiki aliingia katika gari lake na kumwomba arudi eneo la ajali ili wakapime na kuchora mchoro wa ajali. Kibonde aligoma na kumtaka trafiki ashuke katika gari lake,Trafiki naye hakutana kufanyi kwa maana ya kuwa aligoma kushuka na kumuamuru Kibonde arudi eneo la tukio.

Kibonde aliondoa gari na kuendelea na safari yake huku yule Trafiki akiwa ndani ya gari hiyo, Trafiki aliwasiliana na wenzake ambao walianza kuifuatilia gari hiyo ya Kibonde kama walivyopewa maelekezo na mwenzao aliopo ndani ya Gari hiyo.
Mara Kibonde akatokea maeneo ya mataa ya Ubungo, hapo kulikuwa na Trafiki mwingine aliyekua eneo hilo akaipiga mkono gari ya Kibonde na ambapo inasemekekana hakusimama na badala yake ikaja gari nyingine na kuichomekea kwa mbele na hapo ndipo alipotiwa mbaroni!
Aligoma kuendesha gari ikabidi livutwe hadi polisi Urafiki na yeye kuwekwa chini ya ulinzi na baadae akahamishiwa Kituo cha Oystabay ambako yupo mpaka sasa.
Inadaiwa kuwa Kibonde alikuwa amelewa sana,hali iliyopelekea kufanya hayo yote ikiwa ni pamoja na kuwajibu vibaya Askari hao.

TAZAMA PICHA ZAIDI YA 52 MWANZO MWISHO KWENYE SHOW YA MATUMAINI JANA , AKIWEMO SHILOLE, ROMA, YEMI ALADE NA WASNII WENGINE KIBA


Mwanadada mwigizaji na mwanamuziki Zuwena Mohamed 'Shilole' akicheza kwa kujiachia katika Tamasha la Usiku wa Matumaini 2014 usiku wa kuamkia leo.
Zuwena Mohamed 'Shilole' akiongea na mashabiki wake.
Wacheza show wa msanii wa Shishi Baby wakifanya yao.
Add caption
Add caption
Shishi Baby akifanya makamuzi.

Shishi Baby akiagana na Mashabiki wake baada ya kufanya makamuzi ya ukweli katika Tamasha la Usiku wa Matumaini 2014 usiku wa kuamkia leo.

Roma Mkatoliki akiwarusha vilivyo wapenzi wa burudani waliofurika katika Tamasha la Usiku wa Matumaini 2014 usiku wa kuamkia leo.
Roma Mkatoliki akiongea na mashabiki wake.
Mashabiki wakiendelea kucheza na Roma.
Roma Mkatoliki akiendelea kufanya makamuzi.

Staa kutoka nchini Nigeria, Yemi Alade akipiga shoo usiku huu katika Tamasha la Usiku wa Matumaini 2014 ndani ya Uwanja wa Taifa jijini Dar.


Staa kutoka nchini Nigeria, Yemi Alade akipiga shoo katika Tamasha la Usiku wa Matumaini 2014 ndani ya Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Makamu wa Rais Mh. Mohamed Gharib Bilali akisalimiana Makamu wa rais Mh.Mohamed Gharib Bilali akisalimiana na Miongoni mwa matukio yaliyosisimua kwenye tamasha hilo ni pale mechi za mpira wa miguu zilipokuwa zikichukua nafasi.

Yemi Alade akipiga shoo.
BONGO MOVIES VS BONGO FLEVA
Wakati mechi hiyo ilipokuwa ikikaribia kuanza, umati ulilipuka kwa shangwe baada ya kumuona Mfalme wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba alipokuwa alipoonekana akipasha misuli na wenzake.

Mwanamuziki H-Baba akijaribu kuwatoka wachezaji wa Bongo Movies.
Wengi walikuwa wakishangilia wakidai ni siku nyingi hawajamuoana uwanjani, huku wengine wakishangilia kwa kuimba wimbo wake mpya wa Mwana.
Mchezaji wa Bongo Fleva, Ali Kiba akimtoka msanii wa Bongo Movies, Issa Mussa 'Cloud 112'.
Kama hiyo haitoshi haitoshi, shangwe zaidi liliongezeka baada ya Kiba kufunga bao ambalo lilidumu hadi mwisho wa mchezo na kuwafanya Bongo Fleva waibuke kidedea kwa mara nyingine hivi kumfanya kuwa nyota kwenye tamasha hilo.
Nyomi iliyokusanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Dar kwa ajili ya Tamasha la Usiku wa Matumaini 2014.
BONGO MOVIES WACHEZA KIDUKU
Licha ya kufungwa, mashabiki wa Bongo Movies ndiyo walionesha kushangilia zaidi ya mashabiki wa Bongo Fleva ambao ndiyo walikuwa washindi.

Wananchi wakifuatilia matukio mbalimbali katika Tamasha la Usiku wa Matumaini 2014.
Walicheza staili ya kiduku ile mbaya huku wakishangiliwa na umati uliofurika uwanjani hapo.
Bondia Mada Maugo amemshushia kichapo bondia Thomas Mashali katika mpambano wao kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini 2014 ndani ya Uwanja wa Taifa jijini Dar.
WABUNGE SIMBA VS YANGA
Wakati wa mechi ya wabunge, vituko ndiyo ilikuwa balaa. Kuna wakati baadhi ya waheshimiwa wabunge walikuwa wamechoka kiasi cha kushindwa kusogea lakini mwisho wa siku ilikuwa ni burudani kwani waliweza kubadilishana, wengine wakachukua nafasi. Hadi mtanange unamalizika, wabunge wa Yanga waliibuka kidededea kwa ushindi wa mabao 3 kwa 2.

Yanga wakishangilia bao lao.
Matukio mengine yaliyosisimua siku hiyo ni kama wasanii wa Bongo Fleva, Juma Nature, Shilole na wengineo ambao walipanda stejini kwa nyakati tofauti na kutoa burudani baab’kubwa.
Tamasha la Usiku wa Matumaini mwaka huu lilikuwa noma sana!

Ridhiwan Kikwete akishangilia ushindi wa Yanga dhidi ya Simba.