YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Wednesday 20 August 2014

BREAKING NEWS!!! TANESCO KAGERA YAKAMILISHA MIPANGO YA KUFIKISHA UMEME KWA VIJIJI 400 MKOANI HUMO.


Meneja TANESCO KAGERA mhandisi Martine Madulu akieleza jinsi mradi huo unavyokamilishwa

Transformer mpya yenye MVA15
Transformer ya zamani inayotumika sasa yenye MVA5
Mtaalamu kutoka makao makuu Tanesco Dar es salaam anayefunga Transformer hiyo Bwana AMON GAMBA, akitoa ufafanuzi wa kitaalamu.
Fundi msaidizi kulia akiendelea kukunjua waya unaotumika kuweka mawasiliano ya umeme katika transformer hiyo mpya.
Mwonekano wa Transformer mpya ya kufua umeme kwa MVA15.


Meneja wa shirika hilo mkoa wa kagera mhandisi MARTINE MADULU akiongea na waandishi wa habari, amesema wananchi mkoani kagera wanatarajiwa kuondokana na kukatikakatika kwa umeme kutokana na kufungwa transfoma  mpya ya kusambaza umeme katika mkoa wa kagera.

Bwana madulu amesema kuwa serikali imeamua kufanya kuleta transfoma hiyo mpya iliyogharimu zaidi ya bilioni 1.4 kutokana na kuongezeka kwa wateja na kusababisha transfoma iliyokuwepo kushindwa kutoa huduma iliyokuwa inahitajika.

Mhandisi madulu ameongeza kuwa  taransfoma hiyo itakuwa na uwezo wa kuhudumia wateja zaidi ya elfu 22 wa mkoa wa kagera kuliko hii ambayo ilikuwepo.

Pia amewataka wananchi kuendelea jkushirikiana na tanesco katika kutoa taarifa kwa wanahoujumu miundo mbinu ya shirika hilo.
  

PICHA 10 ZA MAWE YA MWANZA YALIVYOPOROMOKA NA KUUA NDUGU WATU WANNE.




Natoa pole sana kwa ndugu waliopoteza ndugu zao wanne baada ya mvua kunyesha kisha nyumba zao kuporomokewa na haya mawe makubwa maeneo ya Mabatini Sinai mtaa wa Nyerere A.




HIVI NDIVYO WAKAZI WA GONGO LA MBOTO WALIVYOFAIDI MAFUTA YA BURE

19

  • Aug2014

Na Father Kidevu Blog.
Bomba la mafuta linalotumika kusafirisha mafuta kutoka Bandari ya Dar es Salaam Tanzania hadi Nchini Zambia lijulikanalo kama TAZAMA limetobolewa na mafundi waKampuni ya Raddy Fiber Solutution Ltd ya jijini Dar es Salaam wakati wakichimba chini ya barabara kupitisha awamu ya pili ya kebo za mkongo wa taifa wa mawasiliano katika eneo la Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Meneja Mkuu wa kampuni ya Raddy, Rajab Mikumwo amesema mafundi wake walitoboa bomba hilo kwa bahati mbaya majira ya saa nane alasiri leo wakati wakifanya kazi ya kuchimba njia ya kupitisha bomba.
 Sehemu inayoonesha mafuta ya kimiminika baada ya bomba hilo kutobolewa chini. 
 Wakazi wa Gongo la mboto wake kwa waume wakiwa katika pilika za kuchota mafuta hayo machafu ya Diseli.
Mkazi wa Goms akiondoka na dumu lake la mafuta. 
Mafuta hayo yakitiririka katika mtaroni mithili ya maji.
chanzo

SOMA ALICHOSEMA DIAMOND PLATINUMZ KUHUSU CHID BENZ




Picha pamoja na ujumbe wa Diamond Platinumz

Baada ya CHID BENZ kufanya ngoma kwa kushirikina na Diamond pamoja na AY hatimaye jana katika ukurasa wa Instargram Diamod aliandika ''Mimi na wewe wote ni viumbe na ndiomaana wakati mwingine tunatereza na kukosea.... lakini naamini tukiweza kusameheana tukapendana na kushirikiana basi umoja wetu utaleta nguvu na maendeleo makubwa katika tasnia yetu.... Tafadhari let's support our brother@chidibeenz na mkono wake huu mpya #MpakaKuchee ...download ngoma kwa kubonyeza link iliyo kwa BIO yangu hapo juu, kisha uniambie ni line gani iliyokukosha zaidi....''


Kila mtu ana maoni yake kuhusiana na ujumbe huo, je wewe unahisi ni kwanini Diamond aliamua kuandika hivyo?

HUU HAPA NDIO UKWELI KUHUSU KUNDI LA ORIGINAL COMEDI KUMWAGWA


KUNDI maarufu la vichekesho ambalo kwa sasa ni kama halipo, limepata pigo kubwa baada ya aliyekuwa meneja wao, mtangazaji nyota wa zamani wa televisheni, Christina Mosha maarufu kama Seven, kuwamwaga na hivyo kuachana nao.
Baadhi ya waigizaji wa kipindi cha orijino Komedi kutoka kushoto ni Joti, Wakuvanga, Mpoki, Masanja mkandamizaji na Maclegan.
Akizungumza na gazeti hili juzikati, Seven alisema ameachana nao baada ya mkataba wake wa sasa kumzuia kufanya kazi na watu wengine zaidi ya walio chini ya mwajiri wake mpya.
“Hivi sasa niko na Sony, wao wananizuia kufanya kazi na wasanii ambao hawako nao, hivyo baada ya mkataba wangu na wao kumalizika, nimeamua kuachana nao.
Aliyekuwa meneja wa kundi la Ze Comedi, mtangazaji nyota wa zamani wa televisheni, Christina Mosha maarufu kama Seven akifafanua jambo.
Mimi ni mwakilishi wa Sony barani Afrika, ninashughulika na wasanii toka nchi tofauti za Afrika, kama Senegal, Kenya na kwingineko kasoro Afrika Kusini,” alisema.

VIDEO MBILI ZA KUONYESHA JINSI EBOLA INAVYOENEZWA




BONYEZA PLAY HAPA CHINI KUZITAZAMA VIDEO HIZO!

AJALI MBAYA YAUA 16 NA KUJERUHI 75 JANA MKOANI TABORA


 

WATU 16 wamepoteza maisha huku 75 wakijeruhiwa baada ya basi la AM lililokuwa likitoka Mwanza kuelekea Mpanda kugongana uso kwa uso na basi lingine la Sabena linalofanya safari zake Mbeya - Tabora katika eneo la Mlogoro, Sikonge mkoani Tabora jana.

Basi la basi la AM baada ya kugongana uso kwa uso na basi la Sabena katika eneo la Mlogoro, Sikonge mkoani Tabora jana.
Baadhi ya wananchi wakiwa eneo la ajali.
Kushoto ni baadhi ya miili ya abiria waliopoteza maisha katika ajali hiyo. Kulia trafiki na wananchi wakiwa eneo la ajali.
Uso kwa uso: Hivi ndivyo ajali hiyo ilivyokuwa na kuondoa uhai wa wananchi 16 na kujeruhi 75.

LIVE!!! CHADEMA YAKANA KUHUSIKA NA KIFO CHA DAUDI MWANGOSI


Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Chadema, John Mnyika, akizungumza na waandishi wa habari
Baadhi ya viongozi wa Chadema kutoka kushoto ni Ofisa Habari, Tumaini Makene, Mbunge wa Ubungo Mh. John Mnyika, Ofisa Mwandamizi Mafunzo na Uendeshaji, Mohamed Mtoi, na mwenye gwanda ni Katibu Mtendaji, Ofisi ya Katibu Mkuu, Victor Kimesera.

LIVE! MSANII WA BONGO FLEVA ANASWA NA MACHANGUDOA WA SINZA AFRICASANA



Ramadhan Shaban 'Wabibi' akiwa na changudoa mwingine.WAKATI wasanii wakitakiwa kuwa mstari wa mbele katika kuenzi maadili mema kwa jamii ya Kitanzania, mambo yamekuwa kinyume, baada ya nyota wa muziki wa kizazi kipya, Ramadhan Shaban 'Wabibi' kukutwa live, akipatana bei na wanawake wanaojiuza katika eneo maarufu kwa machangudoa la Sinza Africasana jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.


Nyota wa muziki wa kizazi kipya, Ramadhan Shaban 'Wabibi' akitega 'mingo' kujiopolea machangu maeneo ya Sinza Africasana jijini Dar.



Wabibi anayetamba na kibao chake cha Kitenge kwenye vituo mbalimbali vya redio na runinga nchini, usiku wa saa saba alikuwa akivinjari katika viwanja hivyo, akichagua kama wafanyavyo wateja wa nguo dukani.



Msanii Ramadhan Shaban 'Wabibi' akipatana bei na mmoja wa machangudoa.
Bila kuchelewa paparazi wetu alifika eneo la tukio na kumkuta staa huyo akiendelea na chaguachagua yake kwa akinadada waliovalia kihasara ili kuwavutia wanaume wakware.
Mwanga wa kamera zetu hata hivyo haukuonekana kumshtusha sana msanii huyo ambaye alijichekesha na kujifanya kuendelea na shughuli nyingine, kama walivyokuwa wakifanya watu wengine katika eneo hilo linalosifika kwa biashara ya ukahaba jijini Dar.
Baada ya kujipatia picha za kutosha za tukio hilo na kuondoka eneo hilo,paparazi wetu hawakwenda kulala, bali waliendelea na uchunguzi wao katika mitaa mbalimbali.Katika hali isiyotarajiwa, saa mbili baadaye, msanii huyo kwa mara nyingine alikutwa na paparazi akiwa anaendelea na biashara yake ya sagulasagula ya machangudoa, lakini hivi sasa akiwa amehamishia kambi katika eneo la Sinza ya Mapambano.
Akiwa amevutiwa na mwanadada mmoja na kuanza kufanya naye mapatano ya bei, paparazi wetu alimuwahi kwa kumpiga picha, ambapo safari hii alishtuka zaidi na chapchap, akachukua Bajaj na kutokomea.

'Wabibi' akikurupushwa katika eneo la tukio.
Wabibi aliwahi kuwa memba wa kundi la muziki la Suba Mkole, akijulikana kama Wambua Classic ambao walitoa albamu iliyotamba kwa jina la Sonde.

Tuesday 19 August 2014

HUU HAPA NDIO UJUMBE ALIOTOA HASHEEM THABEET KWENDA KWA MASHABIKI WAKE WOTE


http://larrybway91.files.wordpress.com/2014/07/hasheem-thabeet.jpg
NINGEPENDA KUANZA KWA KUSEMA ASANTENI SANA KWA KUSHOW LOVE KWENYE HILI PAGE LANGU. BINADAMU WOTE TUMEUMBWA TOFAUTI, NA TUMEBARIKIWA TOFAUTI. 

SOTE TUNA MAPUNGUFU NA SOTE TUNA MAMBO AMBAYO NDIYO YANAYOTUFANYA TUWE WATU AMBAO TULIVYO SASA. KWA HIYO KAMA ULISHAWAHI KUONGEA NA MIMI UTANIJUA NI MTU WA AINA GANI.

NA KAMA TULISHAWAHI KUKUTANA NA LABDA HATUKUELEWANA KAULI ZETU NAOMBA UNISAMEHE MIMI NI BINADAMU NA NAKOSEA KAMA WATU WENGINE TU. NA NINA MAMBO MENGI YANAENDELEA NIKIWA KAMA BINADAMU NA SIO KUWA NARINGA KWA AJILI YA USTAA AU KITU GANI.

MWISHO WA SIKU SOTE TUNAPITA TU HAPA, JANA ILIKUWA WAO, LEO MIMI, KESHO KUNA WENGINE WANAKUJA. HILO MUNGU NDIO ANAJUA.

NA KAMA HAUJAPATA HIYO NAFASI SIKU MOJA TUTAKUTANA. INSHALLAH

Monday 18 August 2014

MAGAZETI YA LEO TAREHE 19/8/2014

.
.
Kama kawaida millardayo.com inakupa vichwa vya habari vya magazeti yote ya kila siku. Leo pia kuna headline mpya kwenye magazeti mbalimbali. Chukua muda wako kupitia kila kilichoandikwa kwenye kurasa za mbele za magazeti ya leo.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
,
,
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
Ni