Gari la polisi likiwa na askari kadhaa waliojidhatiti tayari kuzuia maandamano ya CHADEMA |
Wednesday 24 September 2014
BREAKING NEWS!!!MAANDAMANAO YA AMANI YA CHADEMA MANISPAA YA BUKOBA YAFANIKIWA
MH. PINDA AHUDHURI IBADA YA KUWEKWA WAKFU ASKOFU MWAIPOPO WA DAYOSISI YA SUMBAWANGA
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Tunu (wapili kulia) wakisalimiana na Askofu Damian Kyaruzi wa Jimbo la Sumbawanga (kulia) katika Ibada ya kumweka wakfu Askofu wa Dayosisi ya Ziwa Tanganyika, Ambele Mwaipopo iliyofanyika kwenye kanisa kuu la kiinjili la Kilutheri la mjini Sumbawanga Septemba 21, 2014. Wapili kushoto ni Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Alex Malasusa.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Tunu (wapili kulia) wakimkabidhi zawadi Askofu wa Dayosisi ya Ziwa Tanganyika, Ambele Mwaipopo (wapili kushoto) katika ibada ya kumweka wakfu Askofu huyo iliyofanyika kwenye Kanisa Kuu la Kiinjili la Kilutheri mjini Sumbawanga, Septemba 21, 2014. Kulia ni mke wa Askofu huyo, Tunsume Mwaipopo na kushoto ni Askofu Israel Mwakyolile wa Dayosisi ya Konde.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza katika ibada ya kumweka wakfu Askofu wa Dayosisi ya Ziwa Tanganyika, Ambele Mwaipopo katika Kanisa kuu la Kiinjili la Kilutheri mjini Sumbawanga Septemba 11, 2014.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Tunu (kushoto) wakiwa katika Picha ya pamoja na Askofu wa Dayosisi ya Ziwa Tanganyika, Ambele Mwaipopo na mkewe Tunsume Mwaipopo (kulia) katika katika ibada ya kumsimika Askofu huyo iliyofanyika kwenye Kanisa kuu la Kiinjili la Kilutheri mjini Sumbawanga Septemba 11, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
DK. TIZEBA ATOA MISAADA KWA WAHANGA WA MOTO JIMBONI KWAKE
Naibu Waziri wa Uchukuzi ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Buchosa, Dk Charles Tizeba akipanda boti kuelekea kisiwa cha Nyamango kulikotokea ajali ya moto kwa ajili ya kukabidhi misaada.
Na Daniel Makaka, Sengerema
NAIBU Waziri wa Uchukuzi ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Buchosa Dk Charles Tizeba ametoa msaada kwa wahanga wa ajali ya moto na nyumba zilizoezuliwa na mvua ya upepo katika kisiwa cha Nyamango kijiji cha Lushamba kata ya Bulyaheke jimbo la Buchosa wilayani Sengerema mkoa wa Mwanza.
Misaada aliyoitoa kwa wahanga hao ni Blanketi mia tatu na Magunia manne ya Unga wa Mahindi na moja la Maharagwe vyote vyenye thamani ya shilingi million tatu na laki tano ambavyo vimetolewa kwa kaya hamsini na moja ambazo zilikumbwa na janga hilo Septemba 19 na 20 mwaka huu.
Akikabidhi misaada hiyo Dk Tizeba aliwataka viongozi kuhakikisha misaada hiyo inawafikia walengwa na siyo vinginevyo lakini pia aliwaasa wahanga hao hao kutumia misaada kwa lengo la kuwasaidia wakati kamati ya maafa wilaya ya Sengerema ikiwa bado inaendelea kufanya tathimini il iione namna ya kuwasaidia.
Naibu Waziri wa Uchukuzi ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Buchosa, Dk Charles Tizeba akiwa ndani ya boti kuelekea kukabidhi misaada katika kisiwa cha Nyamango jimboni kwake.
…..Serikali itaendelea kusaidia kadri iwezavyo si kwamba watapewa fidia bali ni misaada tu.
Awali Katibu wa kamati ya maafa wilaya Sengerema Bw. Benard Myatilo akitoa taarifa ya wahanga wa tukio hilo alisema kuwa matukio hayo yalitokea kwa nyakati tofauti ambapo Septemba 19 majira ya saa nane usiku kaya 40 ziliteketea kwa moto na chanzo cha moto huo ni kulipuka kwa Kibatari ndani ya nyumba na tukio la pili kaya 11 kuezuliwa na mvua ilyoambatana na upepo likiwemo jengo la kanisa Katoliki kisiwani humo.
Pia alisema kati ya wahanga hao hakuna mtu aliyejeruhiwa katika matukio hayo licha mali zote zlizokuwemo kuteketea ambapo hadi sasa kaya saba hazina mahali pakuishi huku zilizobaki zikihifadhiwa na baadhi ndugu na jamaa wanaoishi katika kisiwa hicho.
Muonekano wa baadhi ya nyumba zilizoteketea kwa moto katika kisiwa cha Nyamango wilayani Sengerema mkoa wa Mwanza.
Kanisa la Roman Katoliki katika kisiwa cha Nyamango lililoezuliwa na upepo ulioambatana na mvua.
Naibu Waziri wa Uchukuzi ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Buchosa, Dk Charles Tizeba (mwenye suti ya kijivu) akikabidhi misaada ya mablanketi 300 kwa Mwenyekiti wa kijiji cha Lushamba, Deus Bitulo (kulia kwa naibu waziri) huku Mwenyekiti wa CCM tawi la Nyamango, Japhet Kafula akishuhudia tukio hilo
AMERICAN COUPLE GET MARRIED ON MOUNT KILIMANJARO
The newly expected couple sitting together with their Patron Ansigar Mtandika and Matron Neema Njau.
The newly expected couple Richard Miller and Kara Lee from America poses in a picture at Shira Cave point shortly before descending to a place where they exchanged vows in Mount Kilimanjaro yesterday.
Chief Park Warden for Kilimanjaro National Park Erastus Lufungulo (right) and TANAPA’s Corporate Communications Manager Pascal Shelutete (second left) poses in a picture with the newly expected couple at Shira Cave point shortly before they exchanged vows in Mount Kilimanjaro.
POSTED BY JOSEPHAT LUKAZA
MWANAMUZIKI RAPPA MAHIRI KUTOKA NCHINI MAREKANI T.I KUSAMBAZA UPENDO NDANI YA TAMASHA LA FIESTA OKTOBA 18,2014 JIJINI DAR
Mmoja wa Marappa mahiri kutoka nchini Marekani atambulikae kwa jina la Clifford Joseph Harris,'T.I' ni mmoja wa wanamuziki watakaoangusha bonge la shoo la kusambaza upendo kwa wakazi wa jiji la Dar na vitongoji vyake,katika onesho la Fiesta 2014 linalotarajiwa kufanyika ndani ya
Viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam Oktoba 18.
T.I atafanya makamuzi pamoja na wasanii wengine mahiri wa hapa
nchini,watakao pangwa kushusha bonge la burudani kwa wale watakaobahatika kupangwa kwenye orodha ya Oktoba 18, mwaka huu jijini
Dar.
Nguli huyo mwenye albamu nane ambazo ni I'm Serious, Trap Muzik, Urban
Legend, King, T.I. vs. T.I.P., Paper Trail, No Mercy na Trouble Man:
Heavy Is the Head ambapo nyingi kati yake zimefanya vyema katika
soko la muziki. T.I ameshinda tuzo tatu za Grammy tangu aanze safari yake ya muziki.
Baadhi ya singo kali alizoachia mkali huyo na kufanya vyema ni "Bring
Em Out", "What You Know", "Big Shit Poppin' (Do It)", "Swagga Like Us"
(FT Kanye West, Jay-Z na Lil Wayne), "Dead and Gone" (FT Justin
Timberlake), "Ball" (FT Lil Wayne) na "No Mediocre" (FT Iggy Azalea).
Viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam Oktoba 18.
nchini,watakao pangwa kushusha bonge la burudani kwa wale watakaobahatika kupangwa kwenye orodha ya Oktoba 18, mwaka huu jijini
Dar.
Nguli huyo mwenye albamu nane ambazo ni I'm Serious, Trap Muzik, Urban
Legend, King, T.I. vs. T.I.P., Paper Trail, No Mercy na Trouble Man:
Heavy Is the Head ambapo nyingi kati yake zimefanya vyema katika
soko la muziki. T.I ameshinda tuzo tatu za Grammy tangu aanze safari yake ya muziki.
Baadhi ya singo kali alizoachia mkali huyo na kufanya vyema ni "Bring
Em Out", "What You Know", "Big Shit Poppin' (Do It)", "Swagga Like Us"
(FT Kanye West, Jay-Z na Lil Wayne), "Dead and Gone" (FT Justin
Timberlake), "Ball" (FT Lil Wayne) na "No Mediocre" (FT Iggy Azalea).
Tuesday 23 September 2014
SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA (NHC) LAWAKOMBOA VIJANA MKOANI PWANI
Meneja wa Shirika la Nyumba mkoa wa Pwani Pauline Mrango akisoma Hotuba ya makabidhiano ya mashine 28 za kufyatulia matofali kwa vikundi vya vijana katika halmashauri zote za mkoa wa Pwani.
Shirika la Nyumba la Taifa limetoa mashine hizo zenye gharama ya zaidi ya shilingi milioni 12 pamoja na mafunzo kwa vijana ya wiki mbili ambapo baada ya kumaliza mafunzo Shirika litatoa msaada wa shilingi laki tano kwa kila kikundi kama mtaji , yMakabidhiano hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Kibaha wakati wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu .Abdulrahman Kinana.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimpa mkono wa pongezi Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa mkoa wa pwani Pauline Mrango kwa kutoa mashine 28 za kuwasaidia vijana. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kuashiria makabidhiano ya mashine za kufyatulia matofali zilizotolewa na shirika la nyumba la Taifa kwenda kwenye halmashauri zote za mkoa wa Pwani. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokea risala kuashiria makabidhiano ya mashine za kufyatulia matofali zilizotolewa na shirika la nyumba la Taifa kwenda kwenye halmashauri zote za mkoa wa Pwani. Hizi ni baadhi ya mashine Baadhi ya wafanyakazi wa NHC.
ELEWA KUMUHUSU KAKOBE
TUNAENDELEA KUWALETEA MFULULIZO WA MAZUNGUMZO KATI YA ASKOFU KAKOBE NA MWANDISHI WETU kuhusu alipotokewa na yesu, mambo yalikuwaje?
MJADALA NA MKEWE
Askofu Kakobe: Baada ya hapo nilijadiliana na mke wangu Hellen, nilimwambia nitashindwa kuhubiri au kuwa mchungaji. Sina maono kabisa ya kuanzisha shughuli ya kiroho, lengo langu ni kutumia fedha zangu kwa shughuli za kueneza wokovu wa Yesu Kristo. Nilimuambia mke wangu kwamba kama Yesu atanipa nafasi ya kuzungumza nitamuambia sitamani kuwa mchungaji au mhubiri, nitamuomba anipe uwezo wa kuwa tajiri ili niweze kuwasaidia wahubiri wa wokovu.
Mwandishi: Kwa nini uliamua hivyo?
Askofu Kakobe: Nilifanya uamuzi huo kujiunga na huduma kwa kutoa msaada katika Kanisa la Tanzania Assemblies of God. Nilimsaidia Askofu Moses Kulola kueneza mahubiri yake kwa kuyarekodi katika mitambo yangu ya kurekodia ya kieloktoniki na kusambaza kanda zake kwa watu kwa gharama zangu. Nikawa mmoja wa washirika wake. Kwa kweli sikupendelea kuwa mhubiri.
Mwandishi: Ukiwa unaabudu katika Kanisa la Assemblies of God, uliwahi kuhubiri angalau kwa siku moja kanisani?
Askofu Kakobe: Hapana. Hata siku moja sikuwahi kuhubiri au hata kupewa jukumu la kufundisha dini, nilikuwa muumini wa kawaida tu.
Mwandishi: Ulipofanya uamuzi huo wa kutohubiri au kuwa mchungaji, Yesu hakukutokea tena?
Askofu Kakobe: Baada ya miaka michache alinitokea katika nyumba yangu (pichani juu) iliyopo Kijitonyama, Dar na alikuja kwa njia ileile kama alivyofanya mwanzo. Lakini safari hiyo hakuchukuwa muda mrefu. Alinieleza mipango ya Mungu kwangu na huduma nitakayotoa huku akitilia mkazo na akasema itachukuwa muda mrefu kunirudia tena na baada ya hapo, akatoweka.
Mwandishi: Ujio huo wa pili wa Yesu ulikubadili mawazo?
Askofu Kakobe: Hapana, niliendelea na mwenendo wangu uleule kwa miaka kadhaa. Lakini mwaka 1987 Novemba, alikuja mhubiri maarufu wa kimataifa Reinhard Bonnke, alifanya mkutano mkubwa wa kiroho Dar es Salaam ambao uliwavutia watu wengi nami nilikuwa mmoja wapo, wengi wakajitoa kwa Yesu na miujiza mingi ilitokea pale (viwanja vya Jangwani).
Wakati mhubiri huyo anamalizia mahubiri yake, nilifikiria umati ule uliojitoa kwa Yesu ambao ulikuwa ni utukufu kwa Bwana katika jiji na kwa taifa kwa ujumla. Nikasikia sauti ikiniambia, ‘Mwanangu, mhubiri anaaga sasa, nani sasa atachukuwa nafasi yake? Nani atatangaza utukufu wangu baada ya huyu kuondoka?
ATETEMEKA MWILI MZIMA
Mwandishi: Sauti hiyo uliyoisikia bila shaka ni ya Yesu, je, ulifanya nini baadaye?
Askofu Kakobe: Sauti ile ilipasua moyo wangu na mifupa yangu ilianza kutetemeka, sikujiweza, wakati umati wa watu ukiimba nyimbo za kumalizia mkutano kwa furaha, mimi sikuweza kuimba nilikuwa nikilia sana kwa sauti ya juu. Nilijilaumu kwa kutotii agizo la bwana lakini nilimshukuru kwa kunivumilia, nikajitoa kwa Yesu na kumuambia Bwana kwamba nitumie mimi upendavyo.
Mwandishi: Ikawaje baada ya kujitoa rasmi kwa Yesu?
Askofu Kakobe: Moyo wangu ghafla ukajazwa Roho Mtakatifu, nikavutiwa katika kupenda kuhubiri Neno la Mungu na kuombea wagonjwa na wenye mahitaji. Sikungoja tena hata siku moja kuingia katika kazi ya bwana, yaani kuhubiri na kuingia katika miujiza ya uponyaji.
KUANZA KUHUBIRI RASMI
Mwandishi: Kwa hiyo baada ya hapo ukawa mhubiri wa Neno la Mungu?
Askofu Kakobe: Ni baada ya maandalizi ya kiroho, siku ikafika Agosti 3, mwaka 1988, nikaanza rasmi safari yangu ya kuhubiri utukufu wa Mungu na timu iliyokuwa ikiitwa The Gospel Evangelistic Team (GET). Nilienda na timu hiyo mikoani na kuanza mikutano ya uponyaji baada ya kualikwa na makanisa ya Kipentekoste.
Nilifanya mikutano kumi sehemu za wazi katika Miji ya Tanga, Kilimanjaro, Tabora, Mbeya, Pwani na Dar es Salaam.
Mwandishi: Nini maoni yako kuhusu mikutano hiyo kumi ya mwanzo?
Askofu Kakobe: Baada ya mikutano hiyo nakumbuka mchungaji mmoja mwandamizi alisema, mikutano hii imethibitisha wito niliopewa na Mungu. Katika mikutano hiyo watu waliohudhuria walikuwa wengi kuliko matazamio yetu. Watu wengi wakaamua kumfuata Yesu na katika mikutano yote miujiza ya uponyaji ilitokea.
Askofu Kakobe: Baada ya hapo nilijadiliana na mke wangu Hellen, nilimwambia nitashindwa kuhubiri au kuwa mchungaji. Sina maono kabisa ya kuanzisha shughuli ya kiroho, lengo langu ni kutumia fedha zangu kwa shughuli za kueneza wokovu wa Yesu Kristo. Nilimuambia mke wangu kwamba kama Yesu atanipa nafasi ya kuzungumza nitamuambia sitamani kuwa mchungaji au mhubiri, nitamuomba anipe uwezo wa kuwa tajiri ili niweze kuwasaidia wahubiri wa wokovu.
Askofu Kakobe: Nilifanya uamuzi huo kujiunga na huduma kwa kutoa msaada katika Kanisa la Tanzania Assemblies of God. Nilimsaidia Askofu Moses Kulola kueneza mahubiri yake kwa kuyarekodi katika mitambo yangu ya kurekodia ya kieloktoniki na kusambaza kanda zake kwa watu kwa gharama zangu. Nikawa mmoja wa washirika wake. Kwa kweli sikupendelea kuwa mhubiri.
Mwandishi: Ukiwa unaabudu katika Kanisa la Assemblies of God, uliwahi kuhubiri angalau kwa siku moja kanisani?
Askofu Kakobe: Baada ya miaka michache alinitokea katika nyumba yangu (pichani juu) iliyopo Kijitonyama, Dar na alikuja kwa njia ileile kama alivyofanya mwanzo. Lakini safari hiyo hakuchukuwa muda mrefu. Alinieleza mipango ya Mungu kwangu na huduma nitakayotoa huku akitilia mkazo na akasema itachukuwa muda mrefu kunirudia tena na baada ya hapo, akatoweka.
Mwandishi: Ujio huo wa pili wa Yesu ulikubadili mawazo?
Mwandishi: Sauti hiyo uliyoisikia bila shaka ni ya Yesu, je, ulifanya nini baadaye?
Askofu Kakobe: Sauti ile ilipasua moyo wangu na mifupa yangu ilianza kutetemeka, sikujiweza, wakati umati wa watu ukiimba nyimbo za kumalizia mkutano kwa furaha, mimi sikuweza kuimba nilikuwa nikilia sana kwa sauti ya juu. Nilijilaumu kwa kutotii agizo la bwana lakini nilimshukuru kwa kunivumilia, nikajitoa kwa Yesu na kumuambia Bwana kwamba nitumie mimi upendavyo.
Mwandishi: Ikawaje baada ya kujitoa rasmi kwa Yesu?
Mwandishi: Kwa hiyo baada ya hapo ukawa mhubiri wa Neno la Mungu?
Askofu Kakobe: Ni baada ya maandalizi ya kiroho, siku ikafika Agosti 3, mwaka 1988, nikaanza rasmi safari yangu ya kuhubiri utukufu wa Mungu na timu iliyokuwa ikiitwa The Gospel Evangelistic Team (GET). Nilienda na timu hiyo mikoani na kuanza mikutano ya uponyaji baada ya kualikwa na makanisa ya Kipentekoste.
Mwandishi: Nini maoni yako kuhusu mikutano hiyo kumi ya mwanzo?
Askofu Kakobe: Baada ya mikutano hiyo nakumbuka mchungaji mmoja mwandamizi alisema, mikutano hii imethibitisha wito niliopewa na Mungu. Katika mikutano hiyo watu waliohudhuria walikuwa wengi kuliko matazamio yetu. Watu wengi wakaamua kumfuata Yesu na katika mikutano yote miujiza ya uponyaji ilitokea.
Thursday 18 September 2014
POLISI WAIMALISHA ULINZI MANISPAA YA DODOMA BAADA YA KUZUIA MAANDAMANO YA CHADEMA
Jeshi la polisi limeimalisha ulinzi katika maeneo yote ambayo yalitajwa na chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwa ndiyo watapitia wakiandamana kwenda kwenda Bungeni kuanzia saa 4 asubuhi ya leo.(Picha na John Banda wa Pamoja Blog)
Polisi wakiwa wamefunga kamba kati barabara ya mzunguko ya stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani na chuo cha biashara CBE kwaajili ya kuwazuia waandamanaji hao waliopanga kwenda Bungeni
Polisi wapanda farasi wakiimalisha ulinzi katika viwanja vya nyerere Squere ambapo Chadema wamepanga kuanzia maandamano kuelekea bungeni.
Askali polisi wakiwafanya mawasiliano kwenye gari lao ambalo lilikuwa limepakia mbwa kwa ajili ya kuimalisha ulinzi katika viwanja vya Nyerere Dodoma kwa ajili ya kuwazuia waandamanaji wa Chadema walipanga kuandamana kwenda Bungeni.
Kwa Hisani ya Pamoja Pure Blog
SHUHUDIA MSHIKEMSHIKE WA POLISI NA WAFUASI WA CHADEMA DAR MUDA HUU
Jeshi la polisi jijini Dar es Salaam limetumia mbwa na virungu kuwatanyama mamia ya wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Manendeleo Chadema ambao walifurika Makao Makuu ya Jeshi hilo kwa lengo la kumsindikiza Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, ambaye aliitwa kwa mahojiano.
MTOTO ALIYEZAMIA KWEYE NDEGE, ATOWEKA TENA NYUMBANI! SOMA ZAIDI HAPA!
Mtoto Happiness Rioba(10) aliyedaiwa kuzamia kwenye ndege kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar bila kugundulika, ametoweka tena nyumbani kwao baada ya kukutanishwa na mama yake mzazi Sara Zefhania.
Happiness ambaye ni mkazi wa eneo la Mkokozi, Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani inadaiwa ametoweka katika mazingira ya kutatanisha.
Akizungumza na Mwananchi jana, Sara alisema mwanawe alitoweka jana saa sita mchana na kutokomea kusikojulikana.
Alisema asubuhi mtoto wake aliamka salama bila tatizo lolote na muda wote walikuwa pamoja kwa kuwa alikuwa na wageni kutoka kituo cha televisheni cha ITV, waliomuahadi kumtembelea nyumbani kwa lengo la kumuona Happines
“Aliamka vizuri tu na muda wote alikuwapo nyumbani, lakini ilipofika saa sita mchana, nilipigiwa simu na waandishi wa habari wa ITV kuwa nikawachukue katika kituo cha daladala... kabla sijaondoka nilimwambia mwanangu nakwenda kupokea wageni, lakini niporejea nyumbani na wageni hatukumkuta,”
alisema Sara.
Alisema baada ya kumkosa alianza kumtafuta akishirikiana na waandishi hao pamoja na majirani, lakini hawakufanikiwa kumpata ndipo alipotoa taarifa kwa mjumbe wa Serikali za Mitaa na kuwataarifu ndugu, jamaa na marafiki.
Aidha, aliongeza mwanawe alipokuwa Zanzibar alifanya mambo ya ajabu likiwamo kuongea na paka, kula chakula kwa kutumia mkono wa kushoto, kutokuongea na watu pamoja na kutoweka katika mazingira ya kutatanisha.
UNAAMBIWA JAJI ALIYETOA MAAMUZI KATIKA KESI YA MWANARIADHA OSCAR PISTORIUS ATISHIWA KUUWAWA
Mashirika ya kisheria nchini Afrika Kusini, yameelezea wasiwasi kuhusu vitisho dhidi ya jaji aliyetoa uamuzi katika kesi inayomkabili mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius.
Jaji Thokozile Masipa alimpata Pistorius na hatia ya kuua bila kukusudia wala sio mauaji ya kusudi.
Jaji huyo amekuwa akikosolewa tangu kutoa uamuzi wake kuwa Pistorius alimuua mpenzi wake kwa bahati mbaya.
Baadhi ya matamshi yaliyotolewa ni ya chuki , kumlimbikizia lawama na hata kwenda kinyume na mahakama.
Bi Masipa amewekewa ulinzi tangu kutoa uamuzi wake, kwa mujibu wa jarida la City Press.
Maafisa wa polisi wamekuwa wakishika doria nje ya nyumba yake na pia wamekuwa wakimsindikiza kila anapokwenda.
Pistorius alikana kosa la kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp kwa kukusudia.
Wataalamu wa maswala ya kisheria wamekosoa uamuzi wa jaji Masipa ambaye alichukua wadhifa wake mwaka 1998 na kuwa mwanamke wa pili mweusi kuwahi kushikilia wadhifa huo.
Taarifa ya wanasheria hao ilisema kuwa uamuzi wa jaji Masipa ilikuwa sawa kuambatana na sheria na pia kulingana na ushahidi uliotolewa Masipa.
Viongozi wa mashitaka walilaani uamuzi wa jaji Masipa wakisema kuwa Pistorius alipaswa kupataikana na hatia ya kumuua mpenzi wake kwa kukusudia.
EXCLUSIVE: CHRIS BROWN KUTUA BONGO KWENYE SERENGET FIESTA
BASI LA SHAKILA LATUMBUKIA MTO PANGANI MKOANI TANGA
Basi la Shakila likiwa limetumbukia katika Mto Pangani wakati likiwa kwenye kivuko cha MV Pangani.
CHADEMA WATANGAZA KUMSINDIKIZA MBOWE KESHO HADI MAKAO MAKUU YA POLISI ,WANACHAMA NAO WATAKIWA KUJITOKEZA
MWANASHERIA MKUU WA CHADEMA AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI MUDA HUU |
Chama cha democrasia na maendeleo CHADEMA leo kimetangaza kuwa mwenyekiti wao keshoi ataenda polisi makao makuu kuitikia wito wa jeshi hilo ambao ulikuja kwa barua ukimhitaji mwenyekiti huyo kufika makao makuu ya jeshi hilo.
Kauli hiyo imetangazwa muda huu makao makuu ya chama hicho na wanasheria mkuu wa chama hicho mbunge TUNDU LISSU wakati akizungumzia wito wa jeshi la polisi kumhitaji mwenyekiti wao kwa kile ambacho ameadi kuwa hakijawekwa wazi wanamwitia nini.
"Tumepokea barua ya jeshi la polisi makao makuu wakimtaka mwenyekiti wetu kufika makao makuu ya polisi kwa maelezo,kamati kuu ya chama imeridhia mwenyekiti aende ila hawezi kwenda mwenyewe hivyo wanasheria wote wa chama walioko mkoani Dar es salaam watamsindikiza kwa ajili ya kujua mwenyekiti wetu ameitiwa nini.hivyo tunaomba wanasheria wote wa chama kesho tukutane polisi makao makuu saa tano kwa ajili ya kumsindikiza.
Naibu katibu mkuu wa chama JOHN MNYIKA akizungumza |
Aidha naibu katibu mkuu wa chama hicho mh JOHN MNYIKA NAYE naye amewataka wananchi na wapenzi wa chama hicho kujitokeza kesho kumsindikiza mwenyekiti wao kwa ajili ya kusikiliza kile ambacho mwenyekiti wao ameitiwa nini na jeshi la polisi.
KAZI IMEANZA: JESHI LA POLISI MKOA WA DODOMA LAZUIA MAANDAMANO YALIYOPANGWA NA CHADEMA
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) EMMANUEL G. LUKULA |
Na Sylvester Onesmo wa Jeshi l
a Polisi Mkoa wa Dodoma.Jeshi la Polisi mkoani Dodoma limetoa tamko la kuzuia maandamano ya Chama cha CHADEMA hapo tarehe 18/09/2014 na kuwataka wananchi kuyapuuza.
Akiongea na waandishi wa habari, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishina Msaidizi wa Polisi EMMANUEL G. LUKULA (ACP) alisema kuwa; Kufuatia Viongozi wa CHADEMA kutaka kufanya maandamano kuelekea viwanja vya Ofisi za Bunge Mkoani Dodoma kwa ajili ya kupinga Bunge la Katiba siku ya tarehe 18/09/2014 linaloendelea, kuwa maandamano hayo ni batili na akiwataka wananchi wakazi wa Dodoma kuyapuuza kwa kuwa yanakiuka Sheria iliyoliweka Bunge hilo.
Kamanda LUKULA alitaja sababu za msingi za kuzuia maandamano hayo kuwa ni:-
1. Siku ya maandamano ya tarehe 18/09/2014 ni siku ya kazi ikiwa ni pamoja na muda wa maandamano hayo ni masaa ya kazi saa 04:00 asubuhi hadi saa 06:00 mchana yataathili ufanisi wa watu waliopo makazini/maofisini.
2. Bunge maalumu la Katiba linaloendelea kwa sasa lipo Kisheria na hakuna tamko lolote lililotolewa na Mahakama yoyote kulisitisha, hivyo moja ya kazi ya Jeshi la Polisi ni kulinda Sheria na wale wanaofuata sheria. Hivyo kufanya maandamano yanayopinga Bunge la Katiba ni kukiuka Sheria iliyoliweka Bunge hilo.
3. Kuna kesi Mahakamani ya kupinga Bunge hilo kuendelea, hadi sasa shauri hilo linaendelea Mahakamani. Hivyo kwa CHADEMA kuandamana ni kuingilia Uhuru wa Mahakama.
4. Baadhi ya Wilaya barua za kufanya maandamano zimechelewa kufika kwa Wakuu wa Polisi Wilaya kabla ya saa 24 kisheria.
Aidha Kamanda Lukula alitoa wito kwa wananchi wa Dodoma kupuuza maandamano yoyote ya kupinga uwepo wa Bunge la Katiba kwani ni batili. Aidha aliwashauri viongozi wa CHADEMA Mkoa na Wilaya za Dodoma wayasitishe maandamano hayo na wasipo ridhika, wakate rufaa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwa maelekezo zaidi.
Subscribe to:
Posts (Atom)