YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Friday 8 November 2013

DUNIA HII SIJUI INAELEKEA WAPI? HEBU CHEKI PICHA CHAFU ZA MSANII PENDO AKISAGANA NA MWENZAKE ZILIZO ACHIWA NA MTANDAO WA GHAFLA WA NCHINI KENYA


Thursday, 7 November 20130 comments




 
I limit my words becoz this photos by ghafla speakes. She is Pendo and she is a socialite...I'm am not shocked by this photos becoz thats all you have to do to maintain your title as asocialite. Now it time for photos....




Thank you Ghafla for promoting her coz she really needed this to remain relevant n' true to her title

PICHA:MZEE ALIYEZIKWA HAI AFUKULIWA AKUTWA AMEKUFA MWILI WAKABIDHIWA NDUGU NA KUUZIKA UPYA



MSAMARIA MWEMA ALIYEJITOLEA KUUTOA MWILI BAADA YA KUUKUTA 
MWILI WA MAREHEMU MWAIKASU AMBAYE ALIZIKWA AKIWA HAI UKIENDELEA KUIBULIWA KABURINI
KATIKATI MJANE WA ALIYEZIKWA HAI
MWILI UKIWA TAYARI KWA KUZIKWA UPYA
NDUGU WAKIWA NA SIMANZI. 
MOJA YA WANAUSALAMA AKIWASHUKURU NDUGU KWA UVUMILIVU WALIYOUONYESHA KATIKA MSIBA HUU MZITO.
ULITOKA KWA UDONGO UTARUDI KWA UDONGO NDIYO NDUGU WA MAREHEMU WALIVYOKUWA WAKISEMA.
SHUGHULI YA KUZIKA UPYA IKIENDELEA.
SHUGHULI YA MAZISHI IMEKAMILIKA KWA AMANI NA UTULIVU LAKINI HAKUNA WANAKIJIJI WALIYOJITOKEZA KATIKA MSIBA HUU HOFU KUKAMATWA NA DOLA. 
Picha na Ezekiel Kamanga
Mbeya yetu

MCHUNGAJI ATOA MAPEPO SEHEM ZA SIRI KAZI KWELI KWELI SIYO MOVIE KITU UKWELI MTUPU, CHEKI MWENYEWE HAPA


Katika mtazamo wa haraka haraka yawezekana ikaonekana kama filamu au mchezo wa kuigiza vili. La hii ni kweli imetokea huko pande za Nigeria,ambapo kuna mtumishi mmoja amekuwa akijipatia umaarufu kwa kuwatoa wanawake mapepo kunako sehemu za siri. Una maoni gani kuhusu hili?

AZAM TV NI NOMA, TAZAMA BASI LINALOONGOZA KWA MKWANJA MREFU LA STAFF WA AZAM TV:


HUYU NDO MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU ..ALIYE UWAWA KIKATILI NA MUMEWE KISHA MWILI WAKE KUUFICHA STOO


 
Marehemu Hamida Urembo
Ni kifo cha kusikikisha cha mwanamke huyo pichani Hamida Urembo na muhusika wa mauaji hayo ni mumewe wa ndoa waliyeishi kwa miaka mitatu.Hamida alikuwa mwanafunzi wa chuo kikuu na mwaka watatu na alikuwa anatarajia kugraduate mwezi huu chuoni hapo.
 
Hamida na mumewe yahaya walibahatika kupata mtoto wa kike mwenye miaka mitatu sasa.Kwa mujibu wa dada wa Hamida ndoa yao ilikuwa ya misuko suko sana.Mume alikuwa sio mwaminifu mara nyingi alikuwa akizini nje.Ukiacha hilo alikuwa akimpiga sana mkewe mpaka kumzimisha.

Matatizo ambayo ndugu walikuwa wakiyajua na walishasuluhisha mara nyingi na Hamida kurudi kwa mume kuendelea na maisha.Hii ya mwisho ndio ilikuwa kubwa zaidi.Mume alikuwa akimtongoza housegirl hapo nyumbani na alipokuwa kesho housegirl akamfahamisha mama.

Akamueleza jinsi gani muwewe amekuwa akimsumbua kumtaka kimapenzi.Hamida akamwambia anataka tu uthibitisho kama ni kweli.Siku ya siku Yahaya akamlazimisha Hamida kwenda kwao na Hamida akakubali akijua kuna jambo.Akasindikizana na mumewe mpaka kituoni mume akijua mkewe hayupo kumbe mke aligeuzia njiani akarudi nyumbani akajificha chini ya uvungu chumbani kwa housegirl wake.Baadae mume akawasilia na housegirl kuwa anarudi nyumbani,aliporudi akaendelea kuomba mambo tena akavua nguo kabisa akabaki na boxer.Wakati huo yupo chumbani kwao na mkewe.Housegirl akamwambia wahamie chumbani kwako hapo sio salama.Basi wakahamia chumbani na akawa ndio anamuinamisha dada ili amfanye Hamida akatoka chini ya uvungu ili kumuokoa dada na kumuonyesha mumewe kuwa alikuwepo na amejua usaliti wake.Na alipokuwa chini ya uvungu alikuwa akirekodi kila kitu kwenye simu na alipotoka na picha akapiga.
Huyu ndiye Yahaya  aliyekuwa mume wa marehemu Hamida 
Hamida alitoka hapo akashitaki kwao na kwao wakamwambia aende kwa mjomba wa mumewe kumueleza matatizo ya mtoto wao. Alipofika kwa mjomba akaambiwa wanaume ndivyo walivyo avumilie tu arudi kwa mumewe.

Hamida akarudii kwao akiwa hana hana raha lakini uamuzi aliouchukua ni kuachana na mumewe kwani alikuwa kashachoka. Wakawa wakivutana sana mume akimsihi arudi nyumbani walikokuwa wakiishi Mbagala ila Hamida hakuridhia.

Hamida alishaenda mpaka Bakwata ili mumewe aamriwe kutoa talaka.

Mwisho wa Hamida kuonekana nyumbani ni siku ambayo yeye na ndugu zake walikuwa waende kijijini kwao kwenye viwanja walivyopewa na babu yao.Ila siku hiyo Hamida alitoa udhuru kuwa haendi na akamtaarifu mama yake kuwa Yahaya kamuita akachukue vitu vyake vilivyobakia.Mama akamkatalia kwenda akamwambia kuna kaka zake wakubwa aache wataenda kuvifata kwani huyo mume ni mshenzi anaweza kumfanyia kitu kibaya.Hamida akamwambia mama anataka kwenda mwenyewe kwani kuna vyeti vyake muhimu akavichukue.

Basi mama akamuacha aende kishingo upande lakini mama akamwambia basi nenda hata na mdogo wako.Akaenda na mdogo wake lakini kufika kule mume akamkatalia mdogo mtu kuingia ndani.

Wakabishana sana kwa nini asiingie mdogo mtu kuepusha shari akaenda kukaa kwa jirani asubiri kuitwa. Akakaa na muda kupita kukawa kimya akajua wale wameelewana ndio maana hakuna makelele hivyo akaendelea kusubiri.

Akakaa weee mpaka jioni giza lilipoanza kuingia kidogo Yahaya akampigia simu kwa kutumia simu ya Hamida akimwambia aondoke tu arudi nyumbani wao wameshaondoka na vyombo wamebeba.

Mdogo mtu akaondoka kurudi nyumbani kwao Tabata akijua mke na mume wameelewana kumbe dada yake ameshakufa ndani.

Mdogo mtu akafika nyumbani saa mbili usiku na kumwambia mama jinsi Hamida alivyomuudhi kamuacha yeye kwa jirani na akaondoka na mumewe Yahaya.Mama machale yakamcheza akanyanyua simu akampigia Yahaya kumuuliza mwane yupo wapi.Yahaya akamjibu kuwa ameachana nae kitambo mama akamwambia sio kweli mwanangu hawezi kuchelewa kurudi nyumbani na hana kawaida hiyo.Yahaya akamjibu atarudi tu Hamida mtu mzima.

Mamam tayari alishajua kuna jambo akampigia simu baba Hamida aliyekuwa Arusha kumtaarifu kilichotokea. Baba Hamida akampigia Yahaya lakini hakupokea simu.Wasiwasi ukazidi kutanda na ndugu kupeana taarifa zaidi.Asubuhi kulipokucha wakaenda Mbagala kwa Yahaya lakini wakatoa taarifa polisi.Polisi wakawaondoa wasiwasi kwamba hao wanajuana wenyewe labda wameamua kukumbushiana.

Ndugu hawakuridhika wakaenda kwa mjumbe awaruhusu wavunje nyumba waingie ndani pengine kamfungia ndani maana ilikuwa kawaida yake kufanya hivyo kumfungia Hamida ndani.Basi mjumbe akaruhusu mlango uvunjwe walipoingia ndani palikuwa patupu hawakuona kitu wala dalili za mauaji.Kuna chumba ambacho ni stoo hicho walishindwa kufungua na mjumbe akawaambia hiyo ni stoo wanawekaga mavitu yamejazana humo basi wakakiacha wakaondoka.

Hawakuishia hapo bado waliendelea kumsaka Hamida bila mafanikio.

Hamida alipotea toka jumapili iliyopita,jumanne juzi kila mtu wakapanga kila mtu akamtafute popote pale anapoona anaweza kumpata.Mama akaenda kwenye maombi kanisani wakati muislam,dada akaenda blue pearl kazini kwa Yahaya na huku majirani Mbagala wakaanza kuona inzi na harufu kali ikitoka nyumbani kwa Yahaya.Ikabidi mjumbe apige simu kwa mama Hamida kumueleza kinachoendelea polisi wakaitwa,nyumba ikavunjwa ili kutafuta harufu inatokea wapi.Wakavunja kile chumba cha stoo na kukuta mwili wa Hamida umeshaanza kuharibika.Kanyongwa na kamba ya katani na kitenge kafungwa puani na mdomoni.Mwili wake ukawekwa kwenye mfuko akajaziwa mito na manguo nguo na tendegu la kitanda kawekewa shingoni.

Ndugu, polisi wakachukuwa mwili kwa ajili ya msiba na mazishi wakati huo Yahaya alishakimbia siku nyingi hajulikani alipo.

Hamida alizikwa jana kule kwa babu yake Mzenga uzaramuni walipokuwa waende  kwenye mashamba waliyopewa. Msiba upo nyumbani kwao Tabata. Mrehemu ameacha mtoto wa kike wa miaka mitatu anaitwa Tayana.

Habari hii inaendelea tena kesho katika heka heka za leo ndani ya leo tena ya clouds fm.

Na kwa sasa kama nilivyo report hapo mapema leo kwamba mthumia Yahaya anatafutwa na police kwa kosa la mauwaji ya mkewe Hamida.

R.I.P Hamida na tunatoa pole kwa familia nzima ya Urembo kwa msiba

WANAFUNZI WAWILI WA CHUO ZA CBE DODOMA WAFARIKI PAPO HAPO KWA AJALI YA PIKI PIKI:



Wanafunzi wawili wa chuo cha biashara CBE Dodoma jana(06/11/2013)  majiria ya jioni walipata ajali ya piki piki maeneo 
ya nje kidogo na mji wa Dodoma ambapo walipoteza uhai papo hapo, kwa mujibu wa ripota wetu chanzo cha ajali hiyo ilikuwa ni mwendo mkali wa chombo hicho cha moto piki piki waliokuwa wamepakizana wanafunzi hao na gafla bila kutegemea walilivaa gari kubwa lililokuwa limaegeshwa pembeni ya bara bara na kusababisha mauti wa wanafunzi hao wawili ambaye ni GEORGE LULANDALA  wa ODPS  pamoja na RAMADHANI LESSO wa  ODMK:
''BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE''