YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Thursday 23 August 2018

TRUMP AKANA TUHUMA DHIDI YAKE


kutoka kushoto: Michael Cohen, Donald Trump, Stormy Daniels na Karen McDougalHaki miliki ya picha
Image captionkutoka kushoto: Michael Cohen, Donald Trump, Stormy Daniels na Karen McDougal
Rais wa Marekani amekana vikali tuhuma za kuhusika kwake katika kutumia fedha wakati wa mikutano ya kampeni kuwalipa wanawake wawili ambao wanasadikiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi naye.
Katika kesi iliyosikilizwa katika mahakama moja mjini New York mapema wiki hii , mwanasheria wa zamani wa rais Trump, Michael Cohen, amesema kuwa Trump alimpa maelekezo kutoa fedha kwa lengo kuu la kuwashawishi wanawake hao kukaa kimya wakati wa uchaguzi wa rais wa 2016.
Ingawa katika mahojiano na kituo cha runinga cha Fox News, Raisi Trump alitoa ufafanuzi kuwa malipo hayo yalitoka katika fedha zake binafsi na hazikuwa fedha za kampeni kama inavyodhaniwa.
Na kuarifu kuwa alikuja kutanabahi juu ya malipo hayo baadaye, ingawa hakubainisha kuwa miamala hiyo ilifanyika wakati gani.
Raisi Trump amekuwa akimshutumu bwana Cohen kwa kupika mambo dhidi yake kwa lengo la kupata huruma na kuepuka kifungo.
Ikulu ya white house, imesisitiza kuwa kuvunja sheria ya fedha za kampeni kwa Michael Cohen hakumaanishi kuwa basi Rais trump naye atawajibika, msemaji wa white house sarah sanders amekataa kusema ni lini Rais Trump alijua juu ya malipo ya wacheza filamu wawili wa ngono
''kama rais alivyosema katika matukio tofauti tofauti, hajafanya kitu chochote kibaya, hakukua na madai yoyote dhidi yake katika hili, na kwasababu tuu Michael Cohen amekiri makossa yake haimaanishi inamgusa rais''
Katika kukiri makosa yake siku ya jumanne bwana Cohen alisema kuwa ametumwa na Trump kufanya malipo hayo lakini white house imekataa madai haya.
Malipo yafanywayo kwa siri kwa niaba ya mwanasiasa ama mgombea yeyote yanaweza kuchukuliwa kama ukiukwaji wa sheria za kampeni za nchini Marekani

MBUNGE BOBI WINE KUSOMEWA MASHITAKA LEO

Bobi Wine akiwa na wafuasi wake

Haki miliki ya picha
Image captionBobi Wine akiwa na wafuasi wake
Mbunge ambaye aliwahi kuwa mwanamuziki nchini Uganda Robert Kyagulanyi jina maarufu Bobi Wine leo anatarajiwa kurudishwa katika mahakama ya kijeshi mjini Gulu kaskazini mwa Uganda.
Taarifa hiyo imewashtua mawakili wake ambao awali walijuzwa kuwa kesi itasikilizwa katika kambi ya kijeshi ya Makindye anakozuiliwa mjini Kampala.
Wakati huo huo Mtandao wa haki za binadamu za wanahabari nchini Uganda umetoa saa 48 kwa jeshi kuwatambulisha askari wake waliowajumu wanahabari.
Kwa upande mwingine, Wanamuziki wakubwa wakiwemo Chris Martin , Angelique Kidjo na Damon Albarn, wametoa wito wa kuachiwa kwa Mbunge Bobi wine ambaye ana wiki sasa tangu kukamatwa kwake na mbunge mwezake na zaid ya watu 30. Wasanii hao wamejaza waraka wa kutaka mbunge huyo wa upinzani kuachiwa.
Haki miliki ya picha
Wakili wa Bobi Wine anasema kuwa mteja wake ameteswa sana na jeshi, lakini jeshi kwa upande wao wanakataa kumtesa.
Anatarijiwa kufikishwa mahakamani juu ya madai ya kumiliki silaha kinyume na sheria.
Waraka huo umeanzishwa na Rikki stain aliekua msimamizi wa zamani wa mawamuziki fella kuti ambae alikua mkosoaji mkubwa wa serikali ya Nigeria
Anasema kuwa likua akipigwa hata kwa kuzungumza.
Jeshi ambalo ndilo linamzuia Wine linasema kuwa hajateswa na Rais Yoweri Museveni ametupilia mbali madai hayo na kuzitaja kuwa habari za uongo.
Bobi WineHaki miliki ya picha
Image captionBobi Wine

Bobi Wine ni nani?

Nyota huyo wa mtindo wa Afrobeats aliingia katika taaluma ya muziki katika miaka ya 2000, hna anaelezea kipaji chake kuwa ni cha kuelimisha na kuburudisha. Mojawapo ya vibao vyake vya awali Kadingo, inahusu usafi wa mwili.
Jina lake rasmi Wine, ni Robert Kyagulanyi Ssentamu, alichaguliwa kuwa mbunge katika uchaguzi mdogo baada ya kusimama kama mgombea huru mwaka jana wilayani Kyadondo mashariki, Uganda ya kati.
Aliwashinda wagombea kutoka chama tawala National Resistance Movement (NRM) na chama kikuu cha upinzani Democratic Change (FDC).

Tuesday 21 August 2018

BAADA YA VIDEO KUSAMBAA, JESHI LAOMBA RADHI


Uganda PolitictsHaki miliki ya picha
Image captionMwanzoni mwa wiki hii waandamanaji waliingia katika mitaa ya Kampala kudai kuachiliwa kwa mbunge Bobi Wine.
Jeshi la Uganda limeomba msamaha ambao ni nadra sana kutokea baada ya askari wake kuonekana kwenye mkanda wa video wakimpiga mwandishi wa habari ambaye alikuwa akitimiza wajibu wake kwenye maandamano ya kushutumu kukamatwa kwa mbunge Bobi Wine mnamo Jumatatu .Katika tukio hilo waandishi wengine nao walipigwa walipokuwa wakiarifu jamii juu ya maandamano hayo kupitia vyombo vyao vya habari.
Taarifa iliyotolewa na jeshi la polisi, ilieleza kuwa kitendo hicho kilichofanywa na askari wake kuwa si cha weledi na kusema kuwa watakamatwa kwa muujibu wa sheria za jeshi nchini humo.
Kumekuwa na mvutano wa kisiasa nchini Uganda baada ya mbunge Bobi, na wabunge wanne wa upinzani, kukamatwa wiki iliyopita.
Bobi ni maarufu nchini Uganda awali kutokana na kujihusisha na tasnia ya muziki kabla ya kuchaguliwa kama mbunge mwaka jana, amefanikiwa kuteka umaa wa wana Uganda miongoni mwao vijana, na kuendesha harakati za kisiasa dhidi ya raisi Yoweri Kaguta Museveni anaarifu mwandishi wa BBC aliyeko mjini Kampala Catherine Byaruhanga.
Uganda PolitictsHaki miliki ya picha
Image captionBobi Wine alikishinda chama tawala katika jimbo alilogombea na kuwa mbunge
Vijana wengi walioko sasa nchini Uganda walikuwa hawajazaliwa wakati raisi Museveni alipotwaa madaraka mnamo mwaka 1986.
Mapema wiki hii chama cha kutetea haki za binaadamu kilichoko mjini New York, kimewataka polisi na jeshi nchini Uganda kusitisha mara moja mashambulizi yao dhidi ya vyombo vya habari na waandishi habari nchini humo na kuheshimu haki za waandamanaji.
Katika video iliyorushwa mtandaoni, mwandishi wa habari wa shirika la Reuters James Akena, anaonekana akipigwa kwa fimbo na askari wawili mtaani katika mji mkuu, wa Kampala.
Kipigo kiliendelea kumuangukia mwandishi Akena hata alipoamua kusalimu amri na kuweka mikono yake juu huku akiwa amepiga magoti.
Shirika hilo la kutetea haki za binadamu linasema kupigwa na kukamatwa kwa waandishi wa habari ni ushahidi tosha kuwa wa mamlaka nchini Uganda wanataka kuficha mwenendo wa vikosi vya usalama nchini humo.Katika taarifa yake, Jeshi limejitetea kuwa awali lina uhusiano mzuri baina yake na vyombo vya habari nchini humo.
Mbunge Bobi, ambaye jina lake kamili ni Robert Kyagulanyi, bado anaendelea kusalia kizuizini na kwamba anatarajiwa kufikishwa katika mahakama ya kijeshi siku ya Alhamisi kujibu mashtaka ya umili wa silaha kinyume cha sheria.
Familia ya mbunge huyo inadai kuwa alishambuliwa vikali, lakini jeshi, ambalo linamshikilia Mbunge huyo , limekana vikali madai hayo.
Naye raisi Yoweri Museven amekanusha taarifa kuwa Bobi Wine ameumia na kwamba ana majeraha mabaya, na kuziita taarifa hizo kuwa ni habari za kupikwa.

SIKUKUU ZA EID

Decorated Sheep at a market

Haki miliki ya picha
Image captionkatika sikukuu ya Eid ul-Adha ,familia nyingi hutoa mbuzi au kondoo kwa ajili ya marafiki na wahitaji
Waumini wa dini ya Kiislamu duniani kote wanasherehekea sikukuu ya Eid ul-Fitr. Hii ni moja ya sikukuu za idi? Baadhi ya watu, hasa wasio waamini wa dini hiyo wamekuwa wakikanganyikiwa kati ya Eid ul-Fitr na Eid ul-Adha.
Lakini hizi ni sikukuu tofauti.

Eid ul-Fitr

Eid ul-Fitr maana yake ni "sikukuu ya kumaliza mfungo" na kutumiwa kuadhimisha mwisho wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Sacrificed meat being distributedHaki miliki ya picha
Image captionSikukuu hii ya Eid-ul-Adha ya mwaka 2018 kuna waliosheherekea tarehe 21 na wengine tarehe 22 Agosti.
Siku hii huwa ni siku rasmi ya mapumziko katika mataifa mengi yenye waumini wengi wa Kiislamu. Hata hivyo idadi ya siku za mapumziko huwa tofauti katika nchi mbalimbali.
Waislamu huanza sherehe hizi kwa kukusanyika kwa maombi ya kila mwaka ambayo hufanyika muda mfupi baada ya macheo.
Eid
Ni kawaida kuwaona Waislamu wakikusanyika katika misikiti na viwanja vya wazi kwa maoni ya pamoja.
Kabla ya ibada hiyo, huwa wanatoa sadaka kwa maskini (huitwa Zakat) ambayo ni moja ya nguzo kuu katika dini ya Kiislamu.
Ni kawaida kwa miji mikuu mataifa ya Kiislamu kupambwa sana na sherehe kubwa kuandaliwa, watoto kununuliwa nguo mpya na kupewa zawadi mbalimbali.
Siku hii huadhimishwa baada ya kuonekana kwa mwezi wa Shawwal .
Mwezi huu ulionekana Alhamisi jioni katika baadhi ya mataifa yakiwemo ya Afrika Mashariki na uarabuni.
Bujumbura
Image captionWaislamu wakiwa uwanja wa Nyakabiga, Bujumbura wakati wa kusherehekea Eid ul-Fitr
Ndio maana sikukuu ya Eid ul-Fitr inaadhimishwa leo Kenya, Uganda na Tanzania nan chi kama vile Qatar, UAE, Saudi Arabia, Indonesia, Uturuki, Morocco, Algeria, Tunisia, Libya na Malaysia wanasherehekea Eid leo.
Mwezi haukuonekana India na Pakistan Alhamisi hivyo wao watasherehekea Eid ul-Fitr Jumamosi Juni 16 sawa na New Zealand na Australia.

Eid ul-Adha

Eid al-Adha ndiyo sikukuu kuu zaidi ya kidini miongoni mwa Waislamu kote duniani na pia huwa ni siku ya mapumziko mataifa mengi yenye Waislamu.
Nchini Kenya Eid ul-Fitr huwa ni siku ya mapumziko lakini Eid ul-Adha huwa si siku ya mapumziko ya taifa miaka yote.
Kijana mdogo aliyevalia vazi la Spider-Man na kofia ya balagashia akiwatazama kondoo wakati wa Eid al-AdhaHaki miliki ya picha
Image captionKondoo , waliopangwa tayari kwa kutolewa kafara, wakitazamwa na muislam mjini Beijing, Uchina mwaka 2017
Eid al-Adha maana yake ni "sikukuu ya kutoa kafara" kwa Kiarabu na hutumiwa kukumbuka wakati nabii Ibrahimu alipotaka kumtoa kafara mwanawe Ishmael alivyoamriwa na Allah, lakini akapewa kondoo na Mungu amtoe kafara badala yake.
Sikukuu ya Eid ul-Adha huadhimishwa kuanzia siku ya 10 tangu kuonekana kwa mwezi wa Dhu al-Hijjah.
Ibada ya Hajj kwenda Mecca huanza siku mbili kabla ya Eid al-Adha na tarehe yake huthibitishwa baada ya kuoenakana kwa mwezi huo wa Dhu al-Hijjah.
Eid al-Adha ina majina mbalimbali katika mataifa ya Kiislamu:
Mecca during HajjHaki miliki ya picha
Image captionMamilioni ya waislamu huhuudhuria Ibada ya Hijjah huko Mecca kila mwaka
Waislamu pia huvalia mavazi yao mazuri na ya kupendeza siku hii na huenda msikitini kwa maombi.
Baadhi humchinja ng'ombe, mbuzi au kondoo kukumbuka kitendo cha imani cha nabii Ibrahimu.
Hula chakula chenye nyama na huwapa jamaa, majirani na maskini nyama ya mnyama waliyemchinja.
Katika baadhi ya mataifa na miji hairuhusiwi watu kuwachinja wanyama kwao nyumbani hivyo vichinjio hutumiwa. Waislamu pia hutoa pesa za hisani kipindi hicho.
Waislamu hutumia Eid ul-Adha kusherehekea utiifu kamili wa nabii Ibrahimu kwa amri ya Mungu na kuwakumbusha wenyewe kuwa tayari kutoa kafara chochote ili kutimiza maagizo ya Mungu na kumfuata.

Eid Mubarak

An Eid dish containing dates, almonds, dried fruit and mint teaHaki miliki ya picha
Image captionChakula au mlo wa pamoja ndio kitu kinachozingatiwa zaidi wenye sikukuu hii
Eid Mubarak kwa Kiarabu maana yake ni "sherehe au sikukuu njema au yenye Baraka".
Ni salamu za kawaida wakati wa sikukuu za Eid.
Wakati wa Eid ul-Fitr, salamu nyingine maarufu ni

TOFAUTI YA MASIKINI NA TAJIRI


Picha za kupigwa kutoka angani kwa kutumia ndege ndogo zisizo na rubani maarufu kama drone zimefichua tofauti kubwa iliyopo baina ya matajiri na maskini ambao ni majirani katika miji mingi duniani.
Mpiga picha Johnny Miller amefichua tofauti kubwa ya makazi na maisha kati ya maskini na mabwanyenye katika miji iliyo Afrika Kusini, Mexico na India.
Picha hizi zingepigwa Dar es Salaam, Mombasa, Nairobi na Mwanza au Dodoma taswira ingekuwa tofauti?
Santa Fe, Mexico City.Haki miliki ya picha
Image captionSanta Fe, Mexico City.
Picha hizo ni sehemu ya mradi wa Bw Miller wa Taswira Zisizo Sawa ambao aliuanzisha Aprili 2016 kuwahamasisha watu kutokubali tena ukosefu wa usawa katika jamii.
Mpiga picha huyo mwenye makao yake Afrika Kusini anasema: "Punde tu unapotua Cape Town, unazingirwa na vibanda na makazi duni.
"Vyumba vya maskini huuzingira uwanja wa ndege, ambavyo inakulazimu kupitia katikati ya vyumba hivyo kwa dakika kumi hivi ukitumia gari kabla ya kufika maeneo wanamoishi watu matajiri na watu wengine wenye mapato ya wastani, maeneo wanamoishi watu waliobahatika (mimi nikiwemo)."
Vukuzenzele, Sweet Home, Cape Town.Haki miliki ya
Image captionVukuzenzele, Sweet Home, Cape Town.
Bw Miller anaendelea: "Hii ndiyo hali halisi ya mambo yalivyo Cape Town, Afrika Kusini, na katika maeneo mengi duniani, lakini ni hali ambayo hainipendezi kamwe.
"Kwa kumnukuu Barack Obama, ninaamini kwamba ukosefu wa usawa na changamoto ambayo kizazi za sasa kinafaa kukabiliana nayo."
Santa Fe, Mexico City.Haki miliki ya picha
Image captionSanta Fe, Mexico City.
Grey line
Casey Park, Johannesburg.Haki miliki ya picha
Image captionCasey Park, Johannesburg.
Picha za kupigwa kutoka juu angani, zinaonesha vitu vinavyowatenganisha maskini na matajiri.
Wakati mwingine ni barabara, kwingine ukuta au uzio na kwingine ni chemchemi au mto au bahari. Upande mmoja kuna majengo duni na upande ule mwingine majengo ya kifahari.
Mumbai.Haki miliki ya picha
Image captionMumbai.
Grey line
Mumbai.Haki miliki ya picha
Image captionMumbai.
Grey line
Papwa Sewgolum Golf Course, Durban.Haki miliki ya picha
Image captionUwanja wa Golf wa Papwa Sewgolum, Durban.
Grey line
Ixtapaluca, Mexico City.Haki miliki ya pich
Image captionIxtapaluca, Mexico City.
Grey line
Tembisa, Johannesburg.Haki miliki ya picha
Image captionTembisa, Johannesburg.
Ili kupata maeneo mazuri ya kupigia picha zake, Bw Miller hufanya utafiti sana.
Hutumia picha za awali, takwimu kutoka kwa sensa, taarifa katika vyombo vya habari na pia kuzungumza na watu.
"Ninapotambua maeneo ninayotaka kupiga picha zangu, huwa naangalia muonekano wake utakuwaje kwa kutumia huduma ya ramani ya Google Earth, na kujaribu kuandaa njia ambayo droni yangu itapitia. Hii ni pamoja na kuzingatia msukumo wa hewa angani, sheria, usalama, muda ambao betri inaweza kudumu ikiwa na chaji, hali ya hewa, ni wakati gani ufaao, na mambo mengine mengi."
Lake Michelle, Masiphumelele, Cape Town.Haki miliki ya picha
Image captionLake Michelle, Masiphumelele, Cape Town.
Grey line
Otto's Bluff, Pietermaritzburg.Haki miliki ya picha
Image captionOtto's Bluff, Pietermaritzburg.
Grey line
Kya Sands, Bloubosrand.Haki miliki ya picha
Image captionKya Sands, Bloubosrand.