YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Saturday 1 September 2012

YALIYOJIRI YA KIMICHEZO LEO. PICHA ZAIDI NDANI














MTUHUMIWA WA MAUAJI YA NORWAY AFUNGWA MIAKA 21


.


http://s1.reutersmedia.net/resources/r/?m=02&d=20120824&t=2&i=645573356&w=460&fh=&fw=&ll=&pl=&r=CBRE87N0N8A00

OSLO-NORWAY,
 Mahakama nchini Norway imemkuta na hatia na kumhukumu kifungo cha miaka 21 jela, mtuhumiwa wa mauaji ya watu 77 nchini Norway Bw.Anders Behring Breivik. Matuhumiwa huyo alidaiwa kuhusika na mauaji ya watu 77 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 240 wakati alipotega bomu katikati ya mji wa Oslo na baadae kuwapiga kwa risasi vijana waliokuwa katika kambi moja huko Camp Island.

Mtuhumiwa huyo alikiri kufanya makosa hayo na kukataa kuitwa mkosaji akitetea uamuzi wake kuwa ni sahihi kwa kuwa alikuwa akizuia kuenea Uislam Norway.Kesi hiyo ambayo imedumu kwa miezi kadhaa ilikuwa na mvutano ambapo licha ya kuonekana na hatia mawakili na serikali walikuwa na mvutano ikiwa mtuhumiwa huyo yupo timamu au ana matatizo ya akili hali iliyokuwa ikileta utata juu ya hukumu anayostahili, ingawa hatimaye serikali imajiridhisha kuwa mtuhumiwa huyo anastahili hukumu.

Hukumu hiyo imewekwa wazi ambapo itaweza kuongezwa kwa miaka zaidi ya 21 ikiwa mtuhumiwa huyo ataonekana bado ni hatari kwa jamii yake hata baada ya kumaliza kifungo chake.

Familia na ndugu wa Marehemu na waathirika wa tukio hilo wameridhishwa na hukumu hiyo,"Amepata anachostahili," alisema Alexandra Peltre, 18,ambaye alipigwa risasi na kujeruhiwa na mtuhumiwa huyo.Bi. Per Balch Soerensen,  ambaye binti yake aliuawa katika shambulio hilo alisema anashukuru hukumu hiyo imefika mwisho kwa sababu watakuwa na amani na utulivu tena.

Mtuhumiwa huyo akivalia sare kama za polisi alilipua bomu pamoja na kuwapiga risasi vijana waliokuwa katika kambi huko Norway, na kusababisha vifao vya watu 77 hapo mwezi Julai Mwaka jana.


SHAMBULIO LA RISASI LAUA WATATU MAREKANI





NEW YORK-MAREKANI 
Mwanaume mmoja aliyetambulika kwa jina la Terence Tyler, (23) amewapiga na kuwaua wafanyakazi wanzake kwa risasi na kujiua mwenyewe katika duka la New Jersey wanapofanya kazi leo hii mjini nje kidogo ya Jiji la New York huko Marekani.Waliouawa wametambuliwa kuwa ni binti wa miaka 18, Cristina LoBrutto na kijana Bryan Breen mwenye umri wa miaka 24.

Terence ambaye aliwahi pia kuwa mwanajeshi wa jeshi la maji la Marekani alikuwa akifanya kazi katika duka hilo kwa muda unaokadiriwa kuwa wiki 2, na imedaiwa kuwa chanzo cha mauaji hayo ni kukosana na mmoja wa wafanyakazi wenzake.Polisi wamesema Terence alikwaruzana na mfanyakazi mwenzake leo asubuhi na akatoka na baadaye kurudi na bunduki pamoja na bastola ambapo aliwapiga risasi wafanyakazi wenzake wawili kabla ya kujipiga mwenyewe.

Wafanyakazi wenzake walifunga milango wakati akirudi ingawa alifanikiwa kuwapiga risasi kupitia dirishani.

Tukio hilo ambalo limetokea kabla ya kufunguliwa duka hilo, limekuwa ni mwendelezo wa matukio ya upiganaji risasi nchini humo baada ya lile lililotokea katika jumba la makumbusho la Sikh temple ambapo watu 6 waliuawa pamoja na lile lililotokea katika filamu ya Batman ambapo watu 12 waliuawa hali inayoongeza shinikizo juu ya sheria za uuzaji wa silaha nchini Marekani.

WALIMU WAISHUKIA SERIKALI TENA



DAR ES SALAAM-TANZANIA,
http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2012/07/Gratian-Mukoba.jpgSerikali imedaiwa kupuuza amri ya  Mahakama iliyotakakuktana na Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ili kujadili maslahi ya walimu chini ya mshauri ambaye ni mtaalamu wa sheria za kazi.
Akiongea na waandishi wa habari hapo jana Rais wa chama cha walimu (CWT) Bw.Gratian Mkoba amesema licha ya agizo hilo la mahakama serikali haijawa tayari kukutana na walimu kusikiliza madai yao.

Mukoba kwa niaba ya CWT ameitaka serikali kukutana na walimu kabla ya Septemba 10, siku ambayo shule zinafunguliwa vinginievyo chama chake kitachukua hatua kitakazoona zinafaa.



Mukoba alisema Agosti 2, mwaka huu chama chake kilimwandikia Katibu Mkuu  Kiongozi barua yenye kumbu namba CWT/004/IKULU/VOL.1/48  nia yao ya kukutana naye kujadili madai hayo 
ambapo aliwajibu atajadiliana na wenzake kuhusu suala hilo.
ukoba aliongeza kuwa agosti 6 waliandika tena barua ingawa haijapewa majibu mpaka sasa.

“Kitendo cha serikali kukaa kimya kwa muda wa siku 27 bila ya kuonesha kujali kutekeleza kwa amri ya mahakama kunatafsiriwa na CWT kama ni kukosekana kwa nia njema ya serikali kusikiliza madai ya walimu tofauti na propaganda zilizoendelezwa wakati wa mgomo juu ya utayari wao wa kujadiliana na walimu,” alinukuliwa Mukoba.

Mukoba aliitaka pia serikali kuwarudishia madaraka walimu iliowavua madaraka na kufuta mashitaka yote dhidi ya walimu inayodai walishiriki katika mgomo.Pia rais huyo ameitaka serikali kumaliza tatizo hilo mapema ili kuwapa matuamaini walimu kala ya shule kufunguliwa.

WAASI WATEKA NA KUHARIBU VITUO CHA NDEGE ZA JESHI SYRIA



 

SYRIA,
Waasi wameteka kituo kimpja cha jeshi la anga la Syria na kuharibu vituo vingine viwili mashariki mwa Syria asubuhi ya leo. Mashambulizi hayo yamekuwa ni ya kulipiza mashambulizi ya majeshi ya serikali ambayo kwa sasa yameongeza masahambulizi ya anga dhidi ya waasi hao.

Kwa mujibu wa mashuhuda Waasi hao wameteka kituo cha ndege za kijeshi na kuwakamata mateka 6 na vifaa vya kijeshi katika jimbo la Deir al- Zor karibu na mpaka wa nchi hiyo na Uturuki huku pia wakishambulia na kuaribu vituo vingine viwili vya Hamdan na Albu Kamal mashariki mwa Syria karibu na mpaka wa nchi hiyo na Iraq.

Katika taarifa nyingine imedaiwa kuwa waasi hao wameitungua na kuiangusha helkopta ya kijeshi pamoja na ndege aina ya Jet Fighter zote za jeshi la serikali.

Waasi wameendeleza mashambulizi dhidi ya majeshi ya serikali ambayo yameongeza kasi ya kuwashambulia kwa ndege baada ya kupata upinzani mkubwa katika mapigano ya ardhini.

Rais Al Assad amekuwa katika upinzani mgumu kutoka kwa wananchi na sasa waasi kwa takribani miezi 17 ambapo watu zaidi ya 20,000 wameuawa.

YALIYOJIRI KATIKA MAGAZETI YA LEO September Mosi 2012




0
.
.
.
.
.
.
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.