YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Saturday 1 September 2012

WALIMU WAISHUKIA SERIKALI TENA



DAR ES SALAAM-TANZANIA,
http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2012/07/Gratian-Mukoba.jpgSerikali imedaiwa kupuuza amri ya  Mahakama iliyotakakuktana na Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ili kujadili maslahi ya walimu chini ya mshauri ambaye ni mtaalamu wa sheria za kazi.
Akiongea na waandishi wa habari hapo jana Rais wa chama cha walimu (CWT) Bw.Gratian Mkoba amesema licha ya agizo hilo la mahakama serikali haijawa tayari kukutana na walimu kusikiliza madai yao.

Mukoba kwa niaba ya CWT ameitaka serikali kukutana na walimu kabla ya Septemba 10, siku ambayo shule zinafunguliwa vinginievyo chama chake kitachukua hatua kitakazoona zinafaa.



Mukoba alisema Agosti 2, mwaka huu chama chake kilimwandikia Katibu Mkuu  Kiongozi barua yenye kumbu namba CWT/004/IKULU/VOL.1/48  nia yao ya kukutana naye kujadili madai hayo 
ambapo aliwajibu atajadiliana na wenzake kuhusu suala hilo.
ukoba aliongeza kuwa agosti 6 waliandika tena barua ingawa haijapewa majibu mpaka sasa.

“Kitendo cha serikali kukaa kimya kwa muda wa siku 27 bila ya kuonesha kujali kutekeleza kwa amri ya mahakama kunatafsiriwa na CWT kama ni kukosekana kwa nia njema ya serikali kusikiliza madai ya walimu tofauti na propaganda zilizoendelezwa wakati wa mgomo juu ya utayari wao wa kujadiliana na walimu,” alinukuliwa Mukoba.

Mukoba aliitaka pia serikali kuwarudishia madaraka walimu iliowavua madaraka na kufuta mashitaka yote dhidi ya walimu inayodai walishiriki katika mgomo.Pia rais huyo ameitaka serikali kumaliza tatizo hilo mapema ili kuwapa matuamaini walimu kala ya shule kufunguliwa.

No comments:

Post a Comment

gfjythfghgfhdfgergdfgbvdfgrfdgdfrgdrgdfrgrdegedrgdrfg