YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Wednesday 25 July 2012

DENTI CHUO KIKUU ATAKWA NA AFARIKI DUNIA...


MWANAFUNZI wa Chuo Kikuu Cha Usimamizi wa Fedha, (IFM) jijini Dar es Salaam, Agnes B. King’unza (pichani), amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kuokotwa akiwa hajitambui katika ufukwe wa Bahari ya Hindi jirani na Coco Beach.
Habari za kipolisi zinasema Agnes alitekwa kisha akaokotwa na msamaria mmoja ambaye kwa taarifa za awali anatajwa kuwa ni mlinzi wa nyumba moja maeneo ya Coco Beach, ambako ndiko alikokutwa akiwa hajitambui.
“Polisi na hata watu wengine wanahisi kuwa msichana huyo alitekwa kisha kutupwa na watu wasiofahamika, baada ya kufanyiwa ukatili wa kutisha kwa kunyweshwa kitu kinachodhaniwa kuwa ni sumu,” kilisema chanzo chetu cha habari ndani ya jeshi la polisi.
Habari zinasema baadaye mwanafunzi huyo ambaye alikuwa akichukua shahada ya mambo ya kodi, alipelekwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay kisha askari hao wakamkimbiza Hospitali ya Agha Khan kwa matibabu.
Hata hivyo, habari zinasema madaktari wa Agha Khan baada ya kuona hali ya mgonjwa ilikuwa mbaya, walimpa rufaa na kumpeleka katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa uchunguzi na matibabu zaidi.
“Agnes alifariki jioni ya Julai 16, mwaka huu katika Hospitali ya Muhimbili na habari za kifo chake zilisababisha Chuo cha IFM kuzizima kwa wanafunzi kumlilia mwenzao,” kilisema chanzo hicho.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Charles Kenyela alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na akasema kwamba wasamaria wema walisema waliona Bajaj ikifika eneo alilotupwa Agnes wakadhani wanatupa mzigo.
“Walipokwenda kuangalia wakakuta ni mtu akiwa hoi hajitambui. Baada ya kupelekwa hospitali siku ya pili alikuja mama mdogo wa marehemu Agnes aitwaye Veronica Galus na akaleta taarifa kuwa binti yao huyo amefariki dunia. Polisi tunaendelea na uchunguzi kuwatafuta wahusika,” alisema Kenyela. Hata hivyo, kifo hicho kimeacha maswali mengi kuwa binti huyo alilishwa nini na nani?
Mzazi wa marehemu aliyetajwa kwa jina la Bernad King’unza mkazi wa Kimara Dar, hakupatikana kwa maelezo kwamba alikuwa safarini Iringa kwenye mazishi ya mpendwa wao huyo yaliyofanyika nyumbani kwao Kalenga, Iringa Julai 19, mwaka huu.

BREAKING NEWZZZ!!!!!!!

RAISI WA GHANA AFARIKI DUNIA NI RAISI, JOHN ATTA MILLS



Ni Raisi wa Ghana JOHN ATTA MILLS

HIZI NDIO STORI KUBWA ZA MAGAZETI LEO JULY 25, SAJUKI TENA, AZAM FC, VAN PERSIE, AJALI YA FM, NA ALIYEMTEKA ULIMBOKA HUYU HAPA











Hallow people...

HAWA NDIO WANAUME WATATU WALIOPOTEZA MAISHA KWA KUWAKINGIA VIFUA WAPENZI WAO.

Huyu ndio James Holmes mtuhumiwa wa mauaji ya watu 14 kwenye ukumbi huo wa Cinema, alijeruhi watu wengine 58 pia. hapa ni akiwa amefikishwa Mahakamani kwa mara ya kwanza.

Hallow people...

HAWA NDIO WANAOMVUTIA AFANDE SELE KUWA MBUNGE.


Siku zikiwa zinahesabika ili msanii Mfalme wa Rymes Afande selle kutangaza chama atakachogombea nacho Ubunge 2015 Morogoro Mjini, mkongwe huyu amekubali kuwataja wanasiasa ambao ndio wanamvutia, wanampa hamu na ushawishi wa hiyo kazi kutokana na wanayoyafanya.
Afande anaesema anayajua machungu ya wanamoro amekiri kwamba wanaomvutia kwenye siasa ni wengi lakini wachache wao sana sana ni Zitto Kabwe Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Halima Mdee wa Kawe na Burhani wa Lindi.
Amesema “mtu kama Zitto Kabwe ni mtu ambae ananipigia simu mara nyingi nikiwa na masahibu yangu ananishauri, namuheshimu sana na nafasi hii naitumia kumshukuru, yuko dada Halima Mdee wananionyesha kitu flani ambacho ninaweza kukifanya vilevile, kuna wabunge vijana kama Baruani kutoka Lindi japo ni Albino lakini ameonyesha kwamba Albino anaweza kuwa kiongozi mzuri kuliko hata watu wasio na ulemavu, wako wengi wananivutia hasa kutoka vyama vya upinzani”
Kwenye interview yake ya May 2012 na AMPLIFAYA, Afande alisema kuna vyama saba vya kisiasa vilivyomuita ajiunge navyo kugombea Ubunge lakini viwili ndio vyenye nafasi kubwa, kimoja kati ya CHADEMA au C.U.F
Alisema “kimsingi ndio vyama ambavyo hata namna ya kuvionganisha ningetamani siku moja viwe na sera moja na kuungana kuipigania nchi hii kwa sababu siamini kama kimoja bila kingine kati ya hivyo viwili kinaweza kuliangusha hili dudu kubwa ambalo lipo madarakani”

HII NDIO STORI KAMILI KUHUSU MWENYEKITI WA CCM MISUNGWI KUPIGWA CHINI.


Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi mkoa wa Mwanza imetengua na kumvua nafasi Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi Benard Pollycarp baada ya kukaidi maagizo na maelekezo yaliyotolewa na kamati hiyo kwa kamati ya siasa ya wilaya ya Misungwi hivi karibuni.
Katibu wa siasa na uenezi wa CCM Mwanza Simon Mangelepe amesema kutokana na maagizo iliyokua imeyatoa kwa kamati ya siasa ya wilaya ya Misungwi, ilimwita na kumuhoji Mwenyekiti huyo kisha kumtaka apime uzito wa tuhuma na kujiuzulu.
Pollcarp anatuhumiwa kwa kuhusishwa na ubadhilifu na wizi wa fedha za Halmashauri ya wilaya ya Misungwi kwenye taarifa ya mkaguzi mkuu wa hesabu CAG Ludovick Uttouh iliyozitaja halmashauri 33 nchini ambazo zimeripotiwa kutafuna fedha kinyume na taratibu.
Wakati uongozi wa CCM Mkoa ukichukua hiyo hatua tayari kuna stori za chinichini kwamba mwenyekiti huyo amekua akiendesha mipango ya chini kwa chini kuwahamasisha baadhi ya madiwani 26 wanaomuunga mkono waendelee kujiandaa kukihama chama hicho na kujiunga na chama kimoja cha siasa kwa madai kwamba taarifa ya CAG iligushiwa na kuchakachuliwa kwa lengo la kisiasa ikidaiwa kufanywa na kigogo mmoja wa ngazi ya kitaifa ambae anatoka kwenye wilaya ya Misungwi.

Tuesday 24 July 2012

AJARI!!!! AJARI!!!! AJARI!!!

calvin
BASI LA DAR EXPRESS NA SIMBA MTOTO YAMEGONGANA LIVE. ila hakuna mtu aliepoteza maisha kuripotiwa, basi la simba mtoto lilikua linaenda Tanga na Basi la Dar express lilikua linatoka Arusha. Majeruhi wamepelekwa katika hospitari ya chalinze na ajari yenyewe imetokea eneo la Wami.....

BODABODA IKIWA IMESHONA ABIRIA, HAPA KWETU VIPI?

dereva na abilia wake....

WANYAMA UNYAMANI....

TID kushoto akiwa na MANGWAIR.
Hallow people...

KWELI NDIVO ITAKAVOKUA MWAKA 2015? MIMI NA WEWE HATUJUI..

Yalaiti watu wengine wanapenda ingekua kama inavoonekana hapo, lakini tusubiri tuone..

KAMA WATAKA KWENDA JESHI JIANDAE NA MAZOEZI KAMA HAYA

BAADHI YA MAZOEZI YA WANAJESHI KABLA NYA KUPATA CHAKULA CHAO CHA KILA SIKU.

MAMBO YA MAAKULI MCHANA HUU,

Kilichoandaliwa hapa sitaki hoji hasa kwa wenzetu waliofunga mwezi mtukufu...

CHOO CHA KILIPIA JAMANI BEI NAFUU TU Tsh. 50

Hallow people...HAYA YAPO MTAANI KWETU TU PESA YAKO ITAKUFANYA UKAMILISHE HAJA YAKO..

LEO MTOTO HATUMWI DUKANI, NI MECHI KALI KATI YA AZAM NA SIMBA .

hghghbhb


NOKIA EAST AFRICA WANAKULETEA "DONT BREAK THE BEAT

The winner of the grand final will take home Kshs. 250,000. Plus everyone who attends will have a chance to win Nokia Asha phones and more great giveaways! 

If you want to battle for the grand prize you will need to audition before the event and there are prizes available for spectators. Claim your spot today!

WAZIRI KUJIUZULU WADHIFA


0

.njhbvg
Ikiwa ni siku ya sita toka kuzama kwa MV SKAGIT huko Zanzibar na kusababisha vifo vya watu 78 mpaka sasa, Waziri wa Miundombinu na mawasiliano wa serikali ya mapinduzi Zanzibar HAMAD MASOUD HAMAD ambae pia ni mwakilishi wa jimbo la Ole Kaskazini Pemba, ameamua kujiuzulu.
Baada ya kujiuzulu nafasi yake imechukuliwa na RASHID SEIF SULEIMAN ambae ni mwakilishi wa jimbo la Ziwani mkoa wa kusini Pemba.
Mwandishi Khaleed kutoka Zanzibar amesema “ni kweli nimepata taarifa za kujiuzulu kwa Waziri huyo, aliandika barua ya maombi ya kujiuzulu kwa Mh Rais na barua hiyo leo ndio amejibiwa rasmi, alishajiuzulu toka saa 12 leo jioni ambapo wananchi wa Zanzibar walimuandama sana ndio kisa cha kujiuzulu”
“Wananchi walifurahi sana kwa kujiuzulu kwake kwa sababu hana umuhimu kwenye utendaji kazi wake, kila mtu kafurahi sana na mpaka sasa zinafanywa sherehe mbalimbali kwa kujiuzulu kwa waziri huyo, kulikua kuna vurugu la uamsho lakini mpaka sasa tunamshukuru Mwenyezi Mungu Zanzibar hali ni shwari hakuna vurugu ya aina yoyote wala barabara kuchomwa na kupangwa mawe” Khaleed.

YALIOJIRI KATIKA MAGAZETI YA LEO








Hallow people...

Monday 23 July 2012

KESI YA ELIZABETH MICHAEL_LULU BADO KUNA UTATA!


Kesi inayomkabili msanii wa kike wa filamu Lulu juu ya kifo cha aliyekuwa msanii mwenzake Steven Kanumba aliyefariki April 7 mwaka huu bado imegubikwa na utata baada ya hii leo tena kupigwa kalenda. Akisikiliza kesi hiyo mapema leo msajili wa mahakama kanada ya Dar es salaam Ndugu Amir Msumi aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 20 kutokana na kutokuwepo kwa jaji Fauz Twaib anayesikiliza kesi hiyo kwa kuwa yuko kwenye mitihini ya sheria anayoifanya kwenye chuo anachosoma hivyo kesi hiyo imepigwa kalenda hadi mwezi ujao

BAADA YA MUDA MFUPI AKAJITOKEZA MWENYEWE NA KUSEMA KUA HAJAFA

EDDIE MURPHY
I Ain't Dead ... Yet

Bado sijafa jamani, ni maneno ya mwenyewe...Eddie Murphy

TETESI ZA KIFO CHA MWIGIZAJI MASHUURI EDDIE MURPHY

Actor - Eddie Murphy Dies In Snowboard Accident

        


THIS STORY IS STILL DEVELOPING...
Actor Eddie Murphy is reported to have died shortly after a snowboard accident earlier today - July 24, 2012.
The actor & novice snowboarder was vacationing at the Zermatt ski resort in Zermatt, Switzerland with family and friends. Witnesses indicate that Eddie Murphy lost control of his snowboard and struck a tree at a high rate of speed.

Eddie Murphy was air lifted by ski patrol teams to a local hospital, however, it is believed that the actor died instantly from the impact of the crash. The actor was wearing a helmet at the time of the accident and drugs and alcohol do not appear to have played any part in his death.

DADA WA DIAMOND QEEN DARLIN AIBUKA NA KUMUUNGA MKONO MDOGO WAKE DIAMOND KWAMBA BABA YAO ALIWATOSA WALIPOKUA WADOGO

Diamond akiwa na dada yake Qeen Darlin
Hallow people...

UNYAMA!!! UNYAMA!!! UNYAMA!!!

Huu ni unyama ambao unapigwa marufuku sana na vituo vingi vya haki za binadamu. Wivu wa mapenzi unapozidi matokeo yake ndo kama hivi yaliomkuta huyu mwanamke baada ya kuhisiwa na mumewe kua anatoka nje ya ndoa. Sio vizuri kabisa kwa vitendo kama hivi kuendelea kutokea hapa nchini kwetu na duniani kote.

Ajali ya MV Skagit: Waziri Zanzibar ajiuzulu

Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu mjini Zanzibar,  Hamad Masoud amejiuzulu wadhifa wake baada ya kuwepo kwa shinikizo la kuachia ngazi lilitoka kwa wananchi.
 Hatua hii imekuja kufuatia madai ya wananchi kuwa ajali za meli zimekuwa zikiongezeka mjini Zanzibar bila yeye kuchukua hatua.

NYIMBO MPYA YA BARNABA BOY, “SIJUTII KWA NILIYEMPATA”


Kama unafuatilia ninachokiandika hapa ndani ya BC,bila shaka unatambua kwamba naamini kabisa kwamba Barnaba ni miongoni mwa vocalists wanaotisha sana tulionao nchini Tanzania hivi sasa.Kijana ana uwezo wa hali ya juu wa kuimba…according to me at least.
Lakini kama huamini,ngoja nijaribu kukufanya nawe uamini.Msikilize hapa katika wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina Sijutii Kwa Niliyempata


“MADEMU”-MPOKI Feat.BARNABA

calvin
Unajua kwamba Mpoki ni mchekeshaji. Na pengine,bila shaka, unaelewa kwamba Mpoki ni mwanamuziki…tena mshindi wa Tuzo za Kilimanjaro.Anazo kofia nyingi katika vipaji.Of course hili la kipaji cha muziki,bado lipo maabara.Kuna Hey na kuna Nah.Lakini,well,anakata mbuga.
Kuthibitisha kwamba bado yupo na ataendelea kuwepo,huu hapa ni ushirikiano wake na Barnaba ambaye kwa mapana na marefu ni miongoni mwa waimbaji wazuri zaidi waliowahi kuwepo nchini Tanzania.There is no doubt about that.Wimbo unaitwa Mademu.…yes Mademu.Umesoma sahihi.Ni production kutoka wa Lamar pale FishCrab. Usikilize hapo chini;

.

FUTARI IKO TAYARI KWA WOTE WALIOKUA KWENYE MFUNGO SIKU YA LEO

calvin
mambo ya maakulikwa wote wafungao...
Hallow people...