YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Saturday 30 August 2014

KAMPUNI YA MATANGAZO YANAYOTEMBEA (TRIA) YAZINDULIWA RASMI TANZANIA


1qDIANA LAVENDER Meneja Mauzo na Masoko kampuni ya CONICA MINOLTA akisoma risala yake wakati wa uzinduzi wa matangazo hayo.
2q
TRUSHAR KHETIA Mkurugenzi mtendaji wa TRIA akikata utepe wakati akizindua rasmi matangazo hayo nchini Tanzania wa pili kulia ni ZULFIKAR MOHAMED Meneja Mkuu wa kampuni ya TRANSPAPER EXPRESS na mwisho kulia ni DIANA LAVENDER Meneja Mauzo na Masoko kampuni ya CONICA MINOLTA na kushoto ni AZDA AMANI Meneja wa Huduma Shirika la ndege la PRECISION AIRLINE ambao ni wateja wakampuni ya TRIA
.................................................................................
Kampuni ya matangazo kwa kutumia vifaa tembezi yaani matangazo yanayotembea imezinduliwa rasmi jijini Dar esSalaam.

Akiongea na waandishi wa habari pamoja na wageniwengine waliohudhuria katika hafla hiyo ya uzinduzi ulifanyika katika hanga la shirika la ndege la Precision yenye makao makuu yake eneo la uwanja wa ndege jijini Dar esSalaam, mkurugenzi mtendaji na muasisi wa TRIA bw. Trushar Khetia amesema kuwa TRIA ni kampuni ya kimataifa inayojishughulisha na matangazo yawekwayo juu, nje au ndani ya fifaa safirishi kama mabasi ya kusafiria ndani na nje ya miji, ndege na usafiri wa majini maarufu kama boti au meli.

“Tumezoea kuona ama kusikia matangazo malimbali ya kibiashara nay ale ya kijamii yaani matangazo yasiyo ya kibiashara yakifanyika kupitia kwenye TV REDIO magazeti na majarida hapa nchini lakini leo TRIA inawathibishia wafanya biashara wa Tanzania na wengine kuwa matangazo yanaweza kufanyika popote wakati wowote tena kwa gharama ndogo” alisema bwana Trushar na kuongeza kuwa TRIA ina lenga kuwainua watanzania hasa vijana wadogo na kuwafanya watambue fursa zao katika maisha sambamba na kuwaongezea matumaini makubwa wamiliki wa mabasi, ndege, daladala namakapuni ya usafirishaji katika kunufaika kutokana na biashara zao za usafirishaji.

Aidha bwana Trushar amesema kuwa kampuni yake pamoja na kwamba haitegemi kufanya biashara kwa hasara hailengi pia kutengeneza faida tu bali kuleta ufanisi na changamoto endelevu katika sekta ya masoko na matangazo ambapo vijana wadau na wateja wa huduma hiyo wataweza kupiga hatua za kimaendeleo kibiashara sambamba na kuongezeka kwa soko la ajira hususana kwa vijana wa kitanzania “TRIA Tanzania hailengi kutengeneza faida tu bali pia kuleta maendeleo yenye tija kibiashara kwa wale watakaokuwa wateja wetu na wadau kwa ujmla, lakini pia ajira kwa vijana wenye uwezo tofauti tofauti wa kufanya kazi pamoja na wale wenye utaalamu wa kuandaa na kutengeneza matangazo haya” alisema Khetia.

Kwa upande wake mwakili wa Conica katika hafla hiyo Bi Diana Lavender amesema Conoca imekuwa mteja mkubwa wa TRIA nchini Kenya na kwakutambua ubora wa kazi zinafanywa naTRIA Conica imeamua kuunga na TRIA kwakuendelea kufanya matangazo yake hapa chini “tumekuwa wateja wa hii kampuni mda mrefu sasa huko nchini Kenya na kutoka na mafanikio makubwa tumeweza kupata kupitia matangazo yetu yanayofanywa na TRIA tumeonelea kuwa ni vizuri kuja kufanya hayo matangazo hapa Tanzania hasa pale tuliposikia kwamba TRIA inaanzisha tawi hapa nchini” alisema Lavender na kuongeza kuwa kufanya matangazo kupitia mabasi, ndege, daladala, treni, vyombo vya usafiri wa majini ni sehemu ya mapambo ya mji na njia zake kwani matangazo haya hutengenezwa vizuri na kufanya kuvuta macho ya wengi kila ipitapo “ni ma mabasi yetu huko Kenya maarufu kama matatu ukipita ukiona vile inavutia lazima utafurahia na kwamba lazima unaweza kutaka kupanda hiyo basi” aliongeza.

Naye mwakilishi kutoka shirika la ndege la precision hapa nchini ambao ni moja kati ya wadau wa karibu kabisa na TRIA Bi Azda Amani amesema kuwa uwekezaji wa biashara mbalimbali hasa biashara ngeni kama hayo ni sehemu ya kuongeza na kukuza pato la taifa na kupitia kodi kwa kampuni husika lakini pia kwa wamiliki wa mabasi, ndege na vinginevyo pamoja na wale wamiliki wa matangazo yatakawekwa kwenye magari haya watalipia kodi “ni furaha kuona wawekezaji wakubwa na wadogo wakiingia kila siku hapa nchini kuwekeza kibiashara na kwakufanya hivi nchi yetu ina kuwa pia kiuchumi kupitia kodi kutoka kwa watoa huduma na wahudumiwa wa huduma hii muhimu kwa maendeleo ya uchumi na biashara nchini” alisema Amani

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo Zulfikar Mohamed kutoka Transpaper ameisifia TRIA kwa hatua iliyofikia na kuwataka watanzania kuiga mfano huo muhimu na kwenda kuwekeza pia katika nchi jirani hata kimataifa “ mimi nipewa fursa ya kuzindua tawi la TRIA hapa Tanzania na kwakweli nimefurahia fursa hii.

Naomba kuwapongeza sana wahusika wote waliokaa na kuona kwamba mimi naweza kuwa mgeni rasmi wa kuzindua mradi huu muhimu lakini pia nawasifia watanzania kwa kuwa waungwana wakubwa sana kuwapokea wawekezaji kutoka pande zote za dunia bila kujali rangi kabila wa udini, kwa hili mko vizuri sana na nawapongeza sana niwaombe tu kwamba igeni huu mfano mzuri na nyinyi mkawekeze biashara zenu katika nchi nyingine kwa manufaa ya watoto wenu na watanzania wote” alisema Mohamed nakuongeza kuwa maendele ya kiuchumi katka taifa lolote huletwa na wenye nchi kupitia biashara yenye tija na inayovuka mipaka na kuleta fedha za kigeni.

MWANAFUNZI ABAKWA HADI KUFA NA KUTOBOLEWA MACHO


Mazishi ya mwanafunzi aliyeuawa kikatili kwa kubakwa kisha kutobolewa macho na watu wasiofahamika kisha mwili wake kutupwa kichakani katika kijiji cha Nhelegani kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga yamefanyika katika makaburi ya familia katika kijiji cha Negezi kata ya Mwawaza katika manispaa ya Shinyanga.
Mwanafunzi huyo  aliyekuwa anasoma darasa la tatu katika shule ya Msingi Negezi iliyopo kata ya Mwawaza manispaa ya Shinyanga alikutwa ameuawa kwa kubakwa kisha kutobolewa Agosti 25 mwaka huu saa saba mchana katika kitongoji cha Kashampa kijiji cha Nhelegani kata ya Kizumbi.
Akizungumza wakati wa mazishi ya mwili wa marehemu  yaliyofanyika LEO MCHANA naibu meya wa manispaa ya Shinyanga David Nkulila alilaani kitendo cha kinyama alichofanyiwa mtoto huyo huku akiitaka jamii kushirikiana na jeshi la polisi katika kuwafichua wahusika wa mauaji hayo.
“Kifo cha mtoto huyu ni mapenzi ya mungu yaliyosababishwa na wanadamu wabaya,naomba suala la hili lifuatiliwe hatuhitaji siasa katika hili inauma sana kwani vitendo vya ukatili dhidi ya watoto vinatishia amani Shinyanga”,alieleza Nkulila.

 Kwa upande wake Intelijensia mkoa wa Shinyanga Bundala Maige alisema suala la ulinzi kwa watoto ni jamii nzima na kwamba wahalifu wako ndani ya jamii hivyo kuitaka jamii kuwafichua wahalifu hao ili kukomesha vitendo vya ukatili vinavyoendelea mkoani Shinyanga.


Naye mwenyekiti wa mtaa wa Masekelo kata ya Masekelo yalikofanyika mazishi ya mtoto huyo bwana Peter Juma Kitundu alisema kifo cha mtoto huyo kinatia simanzi kubwa kwani kimesababishwa na binadamu huku akiiomba serikali kulifanyia uchunguzi wa kina tukio hilo  na lisiingizwe suala la siasa.

Kwa upande wake mwinjilisti  Emmanuel Donald Kaswalala aliyeendesha ibada ya mazishi alilaani vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa watotot huku akiiomba jamii kumrudia mwenyezi mungu kwa

AJALI MBAYA YAUWA WATU 10 WAFARIKI DUNIA KATIKA ILIYOTOKEA MCHANA HUU


Watu kumi wakiwemo watoto wawili, 
wamefariki dunia papo hapo na wengine 
saba wamejeruhiwa vibaya katika ajali 
iliyohusisha magari mawili.

Ajali hiyo imehusisha gari ndogo ya abiria 
maarufu daladala lenye namba za usajili T 
237 BFB aina Toyota Hiace na gari kubwa 
aina ya Fuso lenye namba za usajili T 158 
CSV.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo 
wamemwambia paparazihuru kuwa ajali hiyo imetokea maeneo ya Mbalizi baada ya Hiace iliyokuwa ikitokea 
Mbeya mjini kuelekea Mbalizi kulivaa Fuso 
ilikuwa ikiingia barabarani.
Hata hivyo majina ya majeruhi na marehemu 
hayajaweza kupatikana mara moja kutokana 
na kuwa katika hali mbaya ambapo Dereva 
wa Fuso akitokomea mara baada ya tukio.
R.I.P All na pole sana kwa familia

Thursday 28 August 2014

BONGE LA AIBU: MADAKTARI WANASWA LIVE WAKIMTOA MIMBA DENTI! SHUHUDIA MWENYEWE ILIVYOKUA HAPA!


Written By Jo Cyberspace on Thursday, 28 August 2014 | 08:33

IMEBUMA kwao! Madaktari wawili, Hamis Chacha na Shengena wa zahanati moja iliyopo Yombo Buza jijini Dar wamejikuta katika wakati mgumu baada ya polisi kuwaibukia na kuwaweka chini ya ulinzi kwa madai ya  kufanya jaribio la kumchoropoa mimba msichana mmoja aliyedaiwa kuwa ni denti wa chuo f’lani cha digrii za juu, Dar.
Madaktari wawili, Hamis Chacha (kushoto) na Shengena wanaotuhumiwa kwa jaribio la utoaji mimba.
Tukio hilo la aina yake lilijiri Agostii 25, mwaka huu katika zahanati hiyo ambayo jina tunalihifadhi kwa sasa.Awali, Operesheni Fichua Maovu  ‘OFM’ ya Global Publishers  ikiwa katika pitapita zake ilinasa tukio hilo ambapo polisi walikuwa ndani ya zahanati hiyo wakiwaweka chini ya ulinzi madaktari hao.
OFM ilifanikiwa kuzama ndani ya zahanati hiyo na kuingia kwenye chumba cha kilichodaiwa hutumika katika zoezi hilo.

Vifaa vilivyokusudiwa kutumiwa na madakta hao katika zoezi la utoaji wa mimba.
Daktari Shengena alipoona kamera ya OFM alitaka kukimbia licha ya kuwepo kwa askari ndani ambapo walitumia nguvu za ziada kuwadhibiti vyema na kuingizwa ndani ya chumba alichokuwemo mwenzake ambaye naye alinaswa akiwa na vifaa vilivyodaiwa ni vya kuchomolea mimba akiwa amevificha kwenye mfuko wa rambo.
Madaktari wakiwa chini ya ulinzi wa makamanda wa OFM.
Baada ya maafande kuwaweka chini ya ulinzi, madaktari hao walizua kituko kufuatia kuzitupa chini shilingi 40,000 walizopewa na denti huyo kama malipo ya kazi hiyo wakidhani ni za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ‘Takukuru’.
kiasi cha fedha cha Shillingi arobaini elfu walicholipwa madaktari kwa ajili ya kufanikisha zoezi la utoji mimba.
Wakizungumza na waandishi wetu baada ya kuulizwa nini kilikuwa kikiendelea chumbani humo, Dokta Chacha alidai kuwa mgonjwa huyo ana tatizo kwenye kizazi hivyo alikuwa akitaka kusafishwa na si kutoa mimba maelezo yalikosolewa na denti huyo aliyedai kuwa alikwendwa kwa mapatano ya kumchoma mimba ili akaendelee na masomo chuoni.
Binti (denti) aliyekusudiwa kutolewa mimba.
 Akijibu kuhusu kwa nini alivificha vifaa va kutolea mimba kwenye mfuko, Dokta Chacha alijiumauma na kusema denti huyo alifuata taratibu zote kama wagonjwa wengine, lakini alishindwa kuonesha risiti au cheti cha kumsajili mgonjwa huyo kwa ajili ya matibabu.
Zahanati iliyotumiwa na madaktari hao katika jaribio la utoaji mimba.
 Kichekesho kingine kilikuwa wakati OFM na wanausalama wakitoka nje ya zahanati hiyo na watuhumiwa na kukuta kwenye maeneo mengine kukiwa kweupe na kusemekana kuwa, madaktari na manesi walioshuhudia wenzao wakitaitiwa walitoka nduki kwa kuogopa ushahidi. 

Mwishowe watuhumiwa hao walifikishwa katika Kituo cha Kidogo cha Polisi Buza na kufunguliwa jalada lenye Kumbukumbu Na. BUZ/RB/32/2014 kabla ya baadaye kufikishwa Kituo cha Polisi Chang’ombe, Dar kwa ajili ya mahojiano ya kina kuhusiana na sakata hilo.

SASA KILA KITU KIKO WAZI, ZITTO AANIKA UHUSIANO WAKE NA DIVA WA CLOUDS FM



KWA mara ya kwanza Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Zuberi Kabwe ameibuka na kuzungumzia uhusiano wake na mtangazaji wa Clouds FM, Loveness Malinzi ‘Diva’ na kufuta uvumi mzito uliokuwa ukizagaa kuwa wawili hao ni wapenzi.


Mtangazaji wa Clouds FM, Loveness Malinzi ‘Diva’.
Zitto alifunguka hayo juzi kupitia kipindi cha Mkasi kinachorushwa na Televesheni ya East Africa ambapo alikanusha kuwa hana uhusiano wowote wa mapenzi licha ya kudaiwa kutungiwa wimbo na mtangazaji huyo kama ishara ya penzi lao.“Mh! Kama yeye amenitungia wimbo sijui lakini mimi sina uhusiano naye wowote wa kimapenzi,” alisema Zitto.
Katika mahojiano hayo, mheshimiwa huyo alifungukia skendo nyingine inayomhusisha kutembea na staa wa Bongo Fleva, Mwasiti Almasi na kudai hakuna ukweli wowote juu ya ishu hiyo.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Zuberi Kabwe.
Alisema anaumia zaidi kusikia watu wanavyomhusisha kutembea na Mwasiti kupitia mitandao ya kijamii wakati hakuna ukweli wowote ambapo msanii huyo wanaheshimiana na kufanya naye kazi kwa karibu ili kumsaidia katika harakati zake za muziki.
“Naumia sana kusikia wakinisema na Mwasiti wakati yule ni dada yangu na mbaya zaidi ni mtu ambaye mara kwa mara nimekuwa nikimsaidia katika shughuli zake za muziki, hakuna kitu kingine zaidi ya ukaka na udada,” alisema Zitto.
Aidha, mheshimiwa huyo mbali na kungumzia mikakati yake ya kisiasa katika kipindi hicho, aliweka bayana kuwa ni baba wa mtoto mmoja kwa mkewe aliyemtaja kwa jina moja la Jack, wanamlea mtoto wao vizuri lakini suala la ndoa bado halijatimia

Wednesday 27 August 2014

AVUNJA REKODI KIJANA AUVUA NGUO KILELENI MLIMA KILIMANJARO.

KIJANA AVUA NGUO ZOTE NA KUBAKI MTUPU BAADA YA KUFIKA KILELE CHA MLIMA KILIMANJARO


 
KIJANA Ben Boleyn aliamua kuvua nguo baada ya kufika kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro nchini chenye joto la kati ya sentigrade 10 hadi 12.

Ben Boleyn akiwa kilele cha Mlima Kilimanjaro.

Ben alifanya hivyo baada ya kuwekeana dau la shilingi 500 na mwenzake miongoni mwa aliopanda nao mlima huo.


Ben akivua nguo baada ya kuwekeana dau na mwenzake.

Kijana huyo mwenye miaka 18 alipanda mlima huo katika kuchangisha fedha kusaidia watoto wa kituo cha kulea watoto cha Acorns Children's Hospice kilichopo jijini Worcester nchini England.

Kwa kupanda mlima huo, Ben alikusanya pauni 600 ila baada ya kuvua nguo zake na kuweka picha yake mitandaoni alichangisha fedha nyingi zaidi.

Ben baada ya kuvua nguo. Ben ambaye hujitolea katika kituo hicho alipanda futi 19,341 za Mlima Kilimanjaro kwa siku 9 akiwa na wenzake 7.
Ben ambaye ni mwenyeji wa Kingswinford, England alisema: Kila mtu alifurahia kitendo nilichokifanya katika kilele cha Mlima Kilimanjaro na kuchukua picha zangu

Wazazi wangu walipigwa na mshangao mwanzoni, ila walipoona watu wanazidi kuchangia kwa wingi walinielewa maana nilifanya kitu tofauti.

MCHEZAJI MPYA WA MAN U DI MARIA ALIVYOPOKELEWA OLD TRAFORD


Excitement: United fans chase after the car with Di Maria inside outside Carrington on Tuesday
Spotted: Di Maria sat on the left side of the back seat on his way into Manchester United's training ground
Got him! Angel di Maria poses with Manchester United boss Louis van Gaal upon signing
New motor: Di Maria poses in front of a Chevrolet car outside Aon Training Complex
Long-term man: Di Maria signs on a five-year deal from European champions Real Madrid
Chief coup: Executive vice-chairman Ed Woodward poses with Di Maria

On the look out: Di Maria peers out of his United car as he arrives for the completion of his transfer 
World class: Di Maria has been a key figure for both Real Madrid and Argentina over the past few years

All smiles: Manchester United boss Louis van Gaal (right) was spotted with agent Jorge Mendes on Tuesday
Deal to be done: Mendes is pictured leaving the Lowry Hotel in Manchester on Tuesday


Creative: The winger should bring a new spark to Van Gaal's side, which has been lacking this season
Pedigree: Di Maria was a crucial member of Real's Champions League winning side last season
In the zone: Manchester United assistant Ryan Giggs looks focused as he made his way to the training ground
Serious: Injured midfielder Marouane Fellaini drove into United's Aon Training Complex
You might also

VIDEO, UKISTAAJABU YA ISIS UTASHANGAA YA BOKO HARAM

POSTED BY TANZANIA CLASSIC ON 11:02 AM | NO COMMENTS
.com/magazine/wp-content

BEKI ADAKA PENATI NA KUIVUSHA TIMU YAKE UEFA BAADA YA GOALKEEPER KUPATA KADI NYEKUNDU.

Romanian defender does his best Mike Magee impression, saves two penalties in shootout | THE SIDELINE

Mike Magee, eat your heart out.
You may remember the now-Chicago Fire star putting on an exemplary display as an emergency goalkeeper while with the LA Galaxy in 2011. But as far as field players in goal go, Magee may have been one-upped by Cosmin Moti, a Romanian center back playing for Bulgarian side Ludogorets Razgrad.
After the Ludogorets goalkeeper was sent off in the 118th minute of extratime in their UEFA Champions League qualifier against Steaua Bucharest, with all three substitutes already used and the aggregate score knotted, Moti was selected to don the No. 1 jersey for the remaining few minutes of the game and the looming penalty shootout.
What happened next was history:
You saw that right: Moti made two saves, including the decisive one, in the 6-5 shootout win, one that will be worth millions to the Bulgarians now that they've made it to the group stages.
Though Magee certainly had to deal with more during his famous stint between the sticks, the shootout drama and high stakes on Tuesday night may top what we saw at Buck Shaw Stadium a few years ago. Whose emergency goalkeeping was better? Make your voice heard in the comments below!

KARIBU UTAZAME VIDEO YA WIMBO MPYA YA VICTORIA KIMANI FEAT DIAMOND AND OMMY DIMPOZ - PROKOTO



 
Audio ya wimbo huu umefanywa hapa hapa Tanzania na producer wa Kitanzania anaitwa Tudd Thomas ambaye ni mkali aliyetengeneza hit single kadhaa za wasanii mbalimbali ikiwemo singo ya Ndagushima ya Ommy Dimpoz na Mdogo Mdogo ya Diamond Platnumz. 

 
Hapa kashiriki kuutengeneza wimbo huu kutoka kwa mwanadada anaewakilisha 254 Victoria Kimani,hii single inaitwa Prokoto ambapo upande wa audio imetolewa miezi michache iliyopita.

 
Video imefanywa na Director kutoka Kenya Kevin Bosco Jnr ambaye kwa taarifa fupi ni kwamba ameshiriki pia kutengeneza video ya Mtanzania Ney wa Mitego ya Mr. Ney ambayo bado haijatoka.

Bonyeza play kutazama.

TAZAMA PICHA ZA KILICHOJIRI KATIKA PARTY ILIYOANDALIWA NA DIVA WA CLOUDS FM PALE MAISHA CLUB



  

Juzi ndani ya Club Maisha dar es salaam, kulikua na Party kubwa iliyoandaliwa na Mtangazaji wa Kituo cha Clouds Fm Ala za Roho, Party hii ilihudhuriwa na wajanja wengi wa Town na burudani ilitolewa na Rapper Chidi Benz ambaye kwa muda mrefu hajaonekana kwenye Majukwaa na sasa hivi anai promote Ngoma yake mpya Mpaka Kuchwee aliyo washirikisha Diamond na Ambwene Yesaya (A.Y) Chidi alipokelewa na vizuri na mashabiki waliohudhuria usiku huo, wengine walioperform ni Bob Junior Sharobaro mwenye nyota ya chips Mayai, Kassim Mganga kutoka Manza Bay Tanga, Shilolole Kiuno pamoja na Mpenzi wake Nuh Mziwanda wao ndio walifunga kazi  kabisa kwa kula denda on stage, Godzilla pia aliperform pamoja na Wadananda, Party hii iliisha mida ya saa kumi na moja alfajiri.