YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Monday 25 July 2016

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUFUNGULIWA KWA MFUMO WA UDAHILI WA PAMOJA (CAS) UNAORATIBIWA NA BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE) NA KUTANGAZWA KWA MAJINA YA WAOMBAJI UDAHILI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KOZI ZA CHETI NA DIPLOMA


 
Baraza linapenda kutoa taarifa kuwa Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) umefunguliwa tena kuanzia tarehe 22 Julai 2016 ili kujaza nafasi za udahili zilizo wazi baada ya Baraza kuchagua waombaji udahili waliowasilisha maombi yao kuanzia tarehe 4 Machi 2016 hadi tarehe 3 Juni 2016. Mwisho wa kuwasilisha maombi ni  tarehe 5 Agosti 2016 saa sita usiku.

Waombaji wapya na baadhi ya waombaji walioshindwa kukamilisha maombi yao kupitia mtandao ilipofika tarehe 3 Juni 2016, wanaarifiwa kuanza kuwasilisha maombi ya udahili kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) ili kujaza nafasi zilizo wazi. Waombaji wanahimizwa kutumia muda huu wa nyongeza ili kuwasilisha maombi.

Baraza linapenda pia kuwaarifu waombaji udahili na umma kwa ujumla kuwa vikao vya Kamati za kuidhinisha majina ya waombaji udahili kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) vilipitisha orodha ya majina  ya wenye sifa za udahili kulingana na nafasi za udahili kwa kila kozi zitolewazo na vyuo husika kati ya tarehe 18 Julai 2016 na 21 Julai 2016. Majina ya waombaji waliochaguliwa kwa kila kozi itolewayo na chuo husika yamekabidhiwa vyuoni kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS). Waombaji waliochaguliwa nao wamearifiwa kupitia kurasa (profile) zao binafsi au kwa kubofya hapa. Waombaji ambao hawakuchaguliwa wamejulishwa sababu zilizowafanya wasichaguliwe kupitia kurasa (profile) zao pia.  

Kwa waombaji wa Shahada ya Kwanza waliowasilisha maombi yao kupitia NACTE, Baraza linapenda kuwaarifu kuwa, mashauriano kati ya NACTE na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) yanaendelea kufanyika ili kufanikisha udahili wa waombaji wa kozi za Shahada ya Kwanza kama Serikali ilivyoagiza.

Imetolewa na
Ofisi ya Katibu Mtendaji
NACTE
Tarehe: 22 Julai, 2016 

Monday 18 July 2016

MANENO YA MUHESHIMIWA BAADA YA KUUPINGA USHOGA.

Ushoga umepingwa na vitabu vya dini, haipo kisheria najua watanitukana sana lakini nguvu niliyonayo hakuna wa kunisimamisha" - Mkuu wa Mkoa wa Dsm - Paul Makonda

DEMBA BA AVUNJIKA MGUU AKIWA UWANJANI

Demba Ba atarudi tu coz bone healing may takes from 8 weeks to 12 weeks but physically kuwa fit may take up to 10 months sema atakuwa muoga huyoo kama kunguru

Thursday 30 June 2016

WAKUU WA WILAYA WAKILA KIAPO HIO JANA IKURU DSM.

Baadhi ya Wakuu wa wilaya wapya wakila kiapo cha uadilifu Ikulu, jijini Dar es salaam jana kabla ya kwenda kwenye vituo vyao vya kazi.

Wednesday 29 June 2016

WATOKA BUNGENI KWA MABANGO YENYE UJUMBE MZITO.

Leo hii wabunge wanaounda umoja wa ukawa wameendelea kutoka nje ya ukumbi wa bunge kwa kuonyesha mabango yenye ujumbe mzito kama yanavyo onekana katika picha.




Tuesday 28 June 2016

USAJIRI BARANI ULAYA. TETESI.





TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE 28.06.2016
Chelsea wanajiandaa kuingia katika mbio za kumwania kiungo wa Roma Axel Witsel, 27, ambaye yuko Ufaransa na timu yake ya taifa ya Ubelgiji katika Euro 2016 (Daily Mail), Barcelona huenda wakamnyatia beki wa Arsenal Hector Bellerin, 21, baada ya Dani Alves kuondona Barca na kwenda Juventus (London Evening Standard), Crystal Palace wamekubaliana ada ya uhamisho ya pauni milioni 31.6 ya kumsajili mshambuliaji wa Ubelgiji Mitchy Batshuayi, 22, anayechezea Marseille (Guardian), Manchester City huenda wakawazidi kete Manchester United na Benfica katika kumsajili winga Marlos Moreno, 19, anayeichezea Atletic Nacional ya Colombia kwa pauni milioni 8 (Daily Mail), Real Madrid wanapanga kumtoa mshambuliaji wake Jese, 23, kwa mkopo msimu ujao, licha ya mchezaji huyo kusakwa na Chelsea na Manchester United kwa mkataba wa kudumu (AS), meneja wa Hull City Steve Bruce anafikiria kumsajili mshambuliaji kutoka Paraguay anayecheza Augsburg Raul Bobadilla, 29, anayedhaniwa kuwa na thamani ya pauni milioni 5 (Daily Mirror), Leicester City wapo kwenye mazungumzo ya kumsajili kiungo Nampalys Mendy, 24, kwa pauni milioni 13, kutoka Nice (Leicester Mercury), Zlatan Ibrahimovic, 34, atafanya vipimo vya afya Old Trafford wiki ijayo kabla ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja (Sky Sports), beki wa Chelsea Baba Rahman, 21, anasakwa na Lazio ambao tayari wametoa dau la pauni milioni 13 kumtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Ghana aliyenunuliwa na Chelsea msimu uliopita kwa pauni milioni 21.7 (Daily Mirror), Napoli wamekubaliana maslahi binafsi na Hector Herrera, 26, anayesakwa na Liverpool, lakini klabu hiyo ya Italia bado haijakubaliana na Porto ada ya uhamisho wa kiungo huyo (Tutto Mercatto), Arsenal wamepanda dau kumtaka mshambuliaji Gabriel Barbosa, 19, ambaye kifungu chake cha uhamisho ni pauni milioni 40, katika klabu yake ya Santos ya Brazil (ESPN Brazil), meneja wa Everton Ronald Koeman anajiandaa kumsajili kipa Maarten Stekelenburg, 33, ambaye alikuwa Southampton msimu uliopita kwa mkopo akitokea Fulham (Liverpool Echo). Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Cheers!

Monday 27 June 2016

MAGAZETINI LEO 28/6/2016 STORI KUBWA ZA UTEUZI NA MAMBO MENGINE

 

















 






 

RAISI KUTETA NA LIONEL MESSI


OMBI LA RAIS WA ARGENTINA BAADA MESSI KUTANGAZA KUJIULU  SOKA LA KIMATAIFA:
Rais wa Argentina Mauricio Macri amemwita nyota wa soka wa nchi hiyo Lionel Messi kwa lengo la kumuomba atengue maamuzi yake ya kujiuzulu kucheza soka la kimataifa.

Messi alifikia maamuzi hayo baada ya timu yake kushindwa kwa mara ya pili mfululizo katika fainali za Copa America huku akiwa miongoni mwa wachezaji waliokosa mikwaju ya Penalti. ''Amemwita na kumueleza namna anavyoona fahari kwa kiwango kizuri kilichoonyeshwa na timu yake katika michuano hiyo huku akimtaka asisikilize maneno ya watu'' ilisema msemaji wa Rais Macri.
Ndani ya miaka mitatu Messi ametinga katika fainali tatu tofauti moja ikiwa ni ya kombe la dunia nchini Brazili mwaka 2014 ambapo walipoteza dhidi ya Ujerumani,na nyingine mbili za Copa America moja ikiwa mwaka 2015 na 2016 zote timu yake ikipoteza dhidi ya Chile.


KARIAKOO MIAKA YA 80'S

Kama hukupata bahati ya kuiona Kariakoo miaka hio sasa ilikuwa inafanana hivi.  Na hapa ni mtaa maalufu sana na wenye msongamano mkubwa wa watu mtaa wa kongo.

KITWANGA AKABIDHI OFISI RASMI KWA NCHEMBA

KITWANGA AKABIDHI OFISI : Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu  Nchemba (wa pili kushoto) akipokea taarifa ya makabidhiano kutoka kwa aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo, Charles Kitwanga kwenye ofisi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, jijini Dar es salaam leo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira. Picha na  Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

HT: Iceland 2 - 1 England

Timu ya England mpaka sasa ipo nyuma kwa bao mbili moja kwa dhidi ya Icelanf. Matokeo yakendelea kuwa mama yalivyo Engla itakua imejitoa EURO kwa mara ya pili.

RAISI MSTAAFU WA AWAMU YA PILI ATOA NENO KWA BAKWATA.

#Habari:Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi ameutaka uongozi wa baraza kuu la waislamu BAKWATA kuunda mfuko maalum wa fedha kwa ajili ya kugharamia shughuli mbalimbali za kimaendeleo kwa waumini wa kiislaam.

WAKUU WA WILAYA NA MIKOA WAPYA HAWA HAPA.


Rais Magufuli ateua maDC 139 na kupangua maRC

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.
Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam ambako atapangiwa majukumu mengine.
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.
Dkt. Charles F. Mlingwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stanslaus Magesa Mulongo ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Wakuu wapya wa mikoa walioteuliwa wataapishwa tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam na mara baada ya kuapishwa watakula kiapo cha maadili ya uongozi.
Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 139.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika uteuzi huo Rais Magufuli amezingatia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na umri ambapo kwa wale ambao umri wao ni zaidi ya miaka 60 ameamua wastaafu.
Mhe. Rais amewashukuru sana kwa utumishi wao mzuri na amesema pale ambapo itahitajika, serikali itaendelea kuwatumia katika majukumu mengine.
Katika uteuzi huo, Wakuu wa Wilaya waliopo sasa ambao wamebaki katika nafasi zao ni 39. Pia Rais Magufuli amewateua Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri 22 kuwa Wakuu wa Wilaya kutokana na utendaji wao mzuri.
Aidha, nafasi 78 za uteuzi wa Wakuu wa wilaya zimejazwa na watanzania wengine ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza wengi wao wakiwa ni vijana, wenye elimu ya kutosha na uzoefu katika maeneo mbalimbali.
Walioteuliwa kuwa wakuu wa wilaya ni kama ifuatavyo (Orodha imepangwa kulingana na mikoa)
ARUSHA
1. Arusha - Mrisho Mashaka Gambo
2. Arumeru - Alexander Pastory Mnyeti
3. Ngorongoro - Rashid Mfaume Taka
4. Longido - Daniel Geofrey Chongolo
5. Monduli - Idd Hassan Kimanta
6. Karatu  - Therezia Jonathan Mahongo
DAR ES SALAAM
1. Kinondoni - Ally Hapi
2. Ilala  - Sophia Mjema
3. Temeke - Felix Jackson Lyaviva
4. Kigamboni - Hashim Shaibu Mgandilwa
5. Ubungo - Hamphrey Polepole
DODOMA
1. Chamwino - Vumilia Justine Nyamoga
2. Dodoma - Christina Solomon Mndeme
3. Chemba - Simon Ezekiel Odunga
4. Kondoa - Sezeria Veneranda Makutta
5. Bahi  - Elizabeth Simon
6. Mpwapwa - Jabir Mussa Shekimweli
7. Kongwa - John Ernest Palingo
GEITA
1. Bukombe - Josephat Maganga
2. Mbogwe - Matha John Mkupasi
3. Nyang'wale - Hamim Buzohera Gwiyama
4. Geita  - Herman C. Kipufi
5. Chato  - Shaaban Athuman Ntarambe
IRINGA
1. Mufindi - Jamhuri David William
2. Kilolo  - Asia Juma Abdallah
3. Iringa  - Richard Kasesela
KAGERA
1. Biharamulo - Saada Abraham Mallunde
2. Karagwe - Geofrey Muheluka Ayoub
3. Muleba - Richard Henry Ruyango
4. Kyerwa - Col. Shaban Ilangu Lissu
5. Bukoba - Deodatus Lucas Kinawilo
6. Ngara  - Lt. Col. Michael M. Mtenjele
7. Missenyi - Lt. Col Denis F. Mwila
KATAVI
1. Mlele  - Rachiel Stephano Kasanda
2. Mpanda - Lilian Charles Matinga
3. Tanganyika - Saleh Mbwana Mhando
KIGOMA
1. Kigoma - Samsoni Renard Anga
2. Kasulu  - Col. Martin Elia Mkisi
3. Kakonko - Col. Hosea Malonda Ndagala
4. Uvinza  - Mwanamvua Hoza Mlindoko
5. Buhigwe - Col. Elisha Marco Gagisti
6. Kibondo - Luis Peter Bura
KILIMANJARO
1. Siha  - Onesmo Buswelu
2. Moshi  - Kippi Warioba
3. Mwanga - Aaron Yeseya Mmbago
4. Rombo - Fatma Hassan Toufiq
5. Hai  - Gelasius Byakanwa
6. Same  - Rosemary Senyamule Sitaki
LINDI
1. Nachingwea - Rukia Akhibu Muwango
2. Ruangwa - Joseph Joseph Mkirikiti
3. Liwale  - Sarah Vicent Chiwamba
4. Lindi  - Shaibu Issa Ndemanga
5. Kilwa  - Christopher Emil Ngubiagai
MANYARA
1. Babati  - Raymond H. Mushi
2. Mbulu  - Chelestion Simba M. Mofungu
3. Hanang' - Sara Msafiri Ally
4. Kiteto  - Tumaini Benson Magessa
5. Simanjiro - Zephania Adriano Chaula
MARA
1. Rorya  - Simon K. Chacha
2. Serengeti - Emile Yotham Ntakamulenga
3. Bunda  - Lydia Simeon Bupilipili
4. Butiama - Anarose Nyamubi
5. Tarime - Glodious Benard Luoga
6. Musoma - Dkt. Vicent Anney Naano
MBEYA
1. Chunya - Rehema Manase Madusa
2. Kyela  - Claudia Undalusyege Kitta
3. Mbeya  - William Ntinika Paul
4. Rungwe - Chalya Julius Nyangidu
5. Mbarali - Reuben Ndiza Mfune
MOROGORO
1. Gairo  - Siriel Shaid Mchembe
2. Kilombero - James Mugendi Ihunyo
3. Mvomero - Mohamed Mussa Utali
4. Morogoro - Regina Reginald Chonjo
5. Ulanga  - Kassema Jacob Joseph
6. Kilosa  - Adam Idd Mgoyi
7. Malinyi - Majula Mateko Kasika
MTWARA
1. Newala - Aziza Ally Mangosongo
2. Nanyumbu - Joakim Wangabo
3. Mtwara - Dkt. Khatibu Malimi Kazungu
4. Masasi  - Seleman Mzee Seleman
5. Tandahimba - Sebastian M. Walyuba
MWANZA
1. Ilemela - Dkt. Leonald Moses Massale
2. Kwimba - Mhandisi Mtemi Msafiri Simeon
3. Sengerema - Emmanuel Enock Kipole
4. Nyamagana - Mary Tesha Onesmo
5. Magu  - Hadija Rashid Nyembo
6. Ukerewe - Estomihn Fransis Chang'ah
7. Misungwi - Juma Sweda
NJOMBE
1. Njombe - Ruth Blasio Msafiri
2. Ludewa  - Andrea Axwesso Tsere
3. Wanging'ombe - Ally Mohamed Kassige
4. Makete  - Veronica Kessy
PWANI
1. Bagamoyo - Alhaji Majid Hemed Mwanga
2. Mkuranga - Filberto H. Sanga
3. Rufiji  - Juma Abdallah Njwayo
4. Mafia  - Shaibu Ahamed Nunduma
5. Kibaha - Asumpter Nsunju Mshama
6. Kisarawe - Happyness Seneda William
7. Kibiti  - Gulamu Hussein Shaban Kifu
RUKWA
1. Sumbawanga - Dkt. Khalfan Boniface Haule
2. Nkasi  - Said Mohamed Mtanda
3. Kalambo - Julieth Nkembanyi Binyura
RUVUMA
1. Namtumbo - Luckness Adrian Amlima
2. Mbinga - Cosmas Nyano Nshenye
3. Nyasa  - Isabera Octava Chilumba
4. Tunduru - Juma Homela
5. Songea - Polet Kamando Mgema
SHINYANGA
1. Kishapu -  Nyambonga Daudi Taraba
2. Kahama - Fadhili Nkulu
3. Shinyanga - Josephine Rabby Matiro
SIMIYU
1. Busega - Tano Seif Mwera
2. Maswa  - Sefu Abdallah Shekalaghe
3. Bariadi - Festo Sheimu Kiswaga
4. Meatu  - Joseph Elieza Chilongani
5. Itilima  - Benson Salehe Kilangi
SINGIDA
1. Mkalama - Jackson Jonas Masako
2. Manyoni - Mwembe Idephonce Geofrey
3. Singida - Elias Choro John Tarimo
4. Ikungi  - Fikiri Avias Said
5. Iramba - Emmanuel Jumanne Luhahula
SONGWE
1. Songwe - Samwel Jeremiah
2. Ileje  - Joseph Modest Mkude
3. Mbozi  - Ally Masoud Maswanya
4. Momba - Juma Said Irando
TABORA
1. Nzega  - Geofrey William Ngudula
2. Kaliua  - Busalama Abel Yeji
3. Igunga  - Mwaipopo John Gabriel
4. Sikonge - Peres Boniphace Magiri
5. Tabora - Queen Mwashinga Mlozi
6. Urambo - Angelina John Kwingwa
7. Uyui  - Gabriel Simon Mnyele
TANGA
1. Tanga  - Thobias Mwilapwa
2. Muheza - Mhandisi Mwanaisha Rajab Tumbo
3. Mkinga - Yona Lucas Maki
4. Pangani - Zainab Abdallah Issa
5. Handeni - Godwin Crydon Gondwe
6. Korogwe - Robert Gabriel
7. Kilindi  - Sauda Salum Mtondoo
8. Lushoto - Januari Sigareti Lugangika
Wakuu wote wa Wilaya walioteuliwa wanapaswa kufika Ikulu Dar es salaam siku ya Jumatano tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi kwa ajili ya kiapo cha maadili ya uongozi na maelekezo mengine kabla ya kuapishwa na wakuu wa mikoa watakaporejea katika mikoa yao.

WAZEE WA ULAYA TIMU YA ITALIA WATOA DOZI KWA SPAIN.

TIMU YA TAIFA YA ITALIA JIONI YA LEO IMEIFUNGASHIA VILAGO MABINGWA WATETEZI WA KIKOMBE CHA UBINGWA WA ULAYA.


Tuesday 21 June 2016

MAMBO MUHIMU KATIKA KUTUMA MAOMBI YA CERTIFICATE NA DIPLOMA



TETESI ZA USAJIRI BARANI ULAYA.


Mabingwa wa Ulaya Real Madrid wameanza mazungumzo ya kumsajili kiungo wa Ufaransa, Paul Pogba, 23, kutoka Juventus, kwa mujibu wa wakala wake (Marca), mabingwa wa EPL Leicester wako tayari kulipa pauni milioni 30 kumsajili mshambuliaji wa Watford Troy Deeney, 27, baada ya dau lao kukataliwa mara mbili (Mirror), kocha msaidizi wa Manchester United Ryan Giggs ambaye anatarajiwa kuondoka Old Trafford, huenda akawania kazi ya kuifundisha Nottingham Forest (Mirror), hata hivyo taarifa nyingine zinasema Giggs hana mpango wa kwenda Forest ambayo wamiliki wake wanamtaka meneja wa zamani wa Olympiakos Michel (Nottingham Post), meneja mpya wa Chelsea Antonio Conte anapanga kumsajili winga wa Lazio Antonio Candreva, 29, pamoja na beki wa Juventus Leonardo Bonucci, 29 (Sun), meneja wa Pari St-Germain Laurent Blanc ataondoka wiki hii (Europe 1), Liverpool wanapanga kupanda dau kumtaka winga wa England na Newcastle Andros Townsend, 24 (Mirror), Manchester City pia wanamtaka Townsend ambaye ada yake ni takriban pauni milioni 10.5 (Telegraph), Everton wameanza mazungumzo ya kumsajili mshambuliaji kutoka Cameroon, Vincent Aboubakar, 24, kwa pauni milioni 16 kutoka Porto (Daily Mail), West Brom wanataka kumsajili kiungo Moussa Sissoko, 26, kutoka Newcastle (Birmingham Mail), meneja wa zamani wa Manchester United Louis van Gaal, meneja wa zamani wa Ajax, Frank de Boer na Andre Villas-Boas wanawania kazi ya kuifundisha AC Milan (La Gazzetta dello Sport), mshambuliaji wa AC Milan Fernando Torres, 32, anatarajiwa kusaini mkataba wa mwaka mmoja Atletico Madrid (Marca), Crystal Palace, Aston Villa na Norwich wanataka kumsajili kiungo wa Reading Aaron Tshibola, 21 (GetReading), Swansea wako tayari kuwapa mikataba mipya Leon Britton na Angel Rangel (South Wales Evening Post), meneja wa Sheffield Wednesday Carlos Carvalhal hawanii nafasi ya umeneja Southampton (Sheffield Star), mshambuliaji wa Manchester City Kelechi Iheanacho, 19, huenda akakosa mwanzo wa msimu baada ya kuitwa na timu ya taifa ya Nigeria kushiriki michuano ya Olimpiki mjini Rio (Manchester Evening News). Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa.

UJUMBE WA RAISI KWA WABUNGE.

Rais John Magufuli ametuma ujumbe bungeni kuwa yeye ni mbunge namba moja na anataka mapato yake yote yakatwe kodi stahiki, hatua inayofuata ni kutoachwa kwa mtu yeyote katika suala la kodi ya mapato.Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alitangaza ujumbe huo wa Dk Magufuli kwamba alipewa mapema alipopeleka pendekezo la kukata kodi ya mapato katika kiinua mgongo cha wabunge. Kwa mujibu wa Dk Mpango, kabla hata ya kuwasilisha mapendekezo ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017, alipeleka mapendekezo hayo ya kwa Rais Magufuli.“Nataka niwaambie, nilipopeleka hili (kukata kodi kiinua mgongo cha wabunge) kwa Rais, alinishangaa na kisha akasema yeye ni Mtanzania na ni lazima Watanzania wote walipe kodi kwa ajili ya kuendeleza nchi yao. “Rais alisema yeye ni mbunge wa kwanza wa Tanzania mpya na anapenda awe wa kwanza kukatwa kodi stahiki katika mapato yake, hivyo sasa kiinua mgongo cha Rais kitakatwa kodi,” Dk Mpango aliwaambia wabunge wenzake jana wakati akifanya majumuisho ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2016/17.Kutokana na kauli hiyo ya Rais, Dk Mpango alisema hata Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa viinua mgongo vyao lazima vikatwe kodi. Alimgeukia Naibu Spika, Dk Tulia Ackson, akamwambia kuwa na yeye lazima akatwe kodi kisha akawageukia mawaziri, akawakumbusha kuwa wao ni wabunge na kwa dhamana waliyopewa kuwa mawaziri, wanapaswa kuongoza kwa mfano katika kukatwa kodi ya mapato katika mapato yao.Hatua hiyo, kwa mujibu wa Dk Mpango, inashuka katika ngazo zote za uongozi, kwa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya, ambao nao pia kiinua mgongo chao, lazima kikatwe kodi. Akifafanua hatua hiyo ya serikali kukata kodi ya mapato kwa kila mtu, waziri alisema sheria inataka vyanzo vyote vya mapato vikatwe kodi na kiinua mgongo ni moja ya vyanzo vya mapato vinavyotambulika na sheria hiyo.Alisema kila Mtanzania amekuwa akikatwa kodi hiyo isipokuwa wachache na hatua hiyo ya serikali inalenga kutoa haki sawa katika utozaji kodi kwa jamii yote. Baada ya muda, Naibu Spika, Dk Tulia alitania mbona Mwanasheria Mkuu George Masaju na Spika Job Ndugai hawajatajwa au wao wamesamehewa; na katika jibu la ishara, Dk Mpango alionesha kutikisa kichwa kueleza kuwa hawajasamehewa, bali nao watakatwa kodi hiyo.

DEREVA WA HALIMASHAURI AGEUKA MUHASIBU.

Upungufu wa watumishi katika kituo cha afya cha Likombe manispaa ya Mtwara Mikindani, kimepelekea dereva wa kituo hicho Ally Mchanyambi kutumika kukusanya mapato ya kituo,hali iliyowashangaza madiwani wa halmashauri hiyo na kutoa agizo kwa mkurugenzi  wa manispaa hiyo kumuondoa kwenye nafasi hiyo mara moja  na nafasi ijazwe na mtumishi mwenye sifa za uhasibu .

MANENO YA ABDUL JUMA MCHEZA WA YANGA MARA BAADA YA KUPOTEZA MECHI.


" Wachezaji tumeumia sana kwa matokeo ya kufungwa dhidi ya MO Bejaia, goli tulilofungwa lilitokana na walinzi kukosa mawasiliano kuukabili mpira uliopigwa kuelekea lango letu ___ Timu yangu ilicheza vizuri sana sema tu tukashindwa kutumia nafasi za kufunga tulizokuwa tumezipata

"Siwezi sema tumefungwa kwa sababu mimi sikuwepo hapana, pengo langu kwa kiasi fulani lilionekana maana washambuliaji akina Ngoma na Tambwe walikosa zile krosi walizozoea ambazo huwa nawalisha, mchezo ujao ni dhidi ya TP Mazembe ambayo ni timu kubwa barani Afrika wao pia wanatambua Yanga ni timu kubwa kwa sasa hivyo utakuwa ni mchezo mgumu na lazima tupambane tupate matokeo na naamini tutafuzu hatua inayofuata

"Bado sijaanza mazoezi mepesi nataraji kuanza kesho au Alhamisi itategemea na ushauri wa daktari, hapa naelekea kuonana naye ili anipe maendeleo ya jeraha" Alimalizia Juma Abdul,mlinzi wa Yanga aliyeko majeruhi.

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI ATOA TAMKO KWA WALIMU.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Salum Hapi, amesema walimu wote ambao hawaridhiki na mishahara yao ni bora watafute shughuli nyingine za kufanya.

Kwa mtazamo wako kauli hii unadhani ni sawa?

KUNDI LA ALSHABAAB LADAI KUFANYA MASHAMBULIZI


WABUBGE WANAPOTOKA NJE YA UKUMBE WA BUNGE

HUWAKILISHI WA WANANCHI UPO WAPI?  HASWA PALE WABUNGE TULIOWACHAGUA WANAPOAMUA KUTOKA NJE YA UKUMBI WA BUNGE.  HATA HIVYO HAKI IK9 WAPI PALE BUNGENI?  KWA SABABU MALALAMIKO MENGI YAMEKUWA YAKITOLEWA NA KAMBI RASMI YA UPINZANI KUHUSU MWENDENDO MZIMA WA VIKAO VYA BUNGE.  TAFAKARI Na chukua hatua



UTATA WA MATUMIZI YA KADI ZA MABASI YA MWENDO KASI


Utata katika matumizi ya kadi za kupandia mabasi ya DART.  Haya ni baadhi ya mambo ambayo bado wananchi wangepende kuelekezwa haswa katika matumizi ya kadi za kupandia magari ya DART.  Mtumiaji wa card anapaswa kuelezwa ni wakati gani haswa ambapo ataweza kuswap kadi yake je ni akiwa anaingia kwenye basi au anatika kwenye basi?  Na vipi kuhusu makato na salio la kiasi kilichobakia kwenye card yake atawrza kutambuaje?  Maswali mengine muhimu unaweza kushare na sisi katika comment..... 

WABUNGE KUHAIDI KUFANYA MIKUTANO YA SIASA NCHI NZIMA.


Monday 20 June 2016

Thursday 18 February 2016

BAADHI YA WANAFUNZI NA WALIMU WA SHULE YA SEKONDARI KAIZIREGE WAKISHANGILIA BAADA YA SHULE YAO KUSHIKA NAFASI YA KWANZA KITAIFA




OFFICIAL LISBON BUSINESS COLLEGE YOUTUBE PAGE



Hallow people...

OFFIAL ADVERT PAGE ON YOUTUBE FOR LISBON BUSINESS COLLEGE


Dec 2015 tv advertisement

FIRST LADY AKIAGWA RASMI NA SHULE ALIYOKUWA AKIFUNDISHA,


Mke wa Rais John Pombe Magufuli  Janeth Magufuli February 17 2016 alirudi katika shule aliyofundisha kwa miaka 15 kabla ya JPM hajawa Rais wa Tanzania.

SHOO NA TEKNO NA WASANII WA BONGO FLEVA JIJINI MWANZA WATISHA


Ni show ambayo ilifanyika February 13 2016 Mwanza Tanzania ikikutanisha mastaa wa muziki kutoka Tanzania ( Juma Nature na Ommy Dimpoz ) na Nigeria ( Tekno na Seyi Shay )

ISKILIZE HAPA BARUA KUTOKA GEREZANI YA JACKY CLIFF.


Jackie Cliff ni Mtanzania ambaye alihukumiwa kwenda jela miaka miwili iliyopita hukoMacao China baada ya kukamatwa uwanja wa ndege akijaribu kuingiza dawa za kulevya, kwenye hii video amemtumia Millard Ayo barua ambayo anataka Watanzania wasomewe.