YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Tuesday 24 December 2013

MAITI YA DENTI WA CHUO CHA BIASHARA CBE YAZUA KASHESHE





KWELI dunia ina mambo! Kijana Abel Dafe 21, (pichani) mkazi wa Kayenze, Mwaloni jijini Mwanza amezua sintofahamu ya aina yake baada ya kudaiwa kufariki dunia na maiti yake kuzikwa wiki chache zilizopita na baadaye kuonekana akiwa hai, bali denti wa Chuo cha Biashara (CBE) Tawi la Mwanza ndiye akidaiwa kufa.


Desemba 2, mwaka huu, Abel alidaiwa kufa maji akiogelea katika Ziwa Victoria na mwili wake kuthibitishwa na mjomba’ake, mwili ukapelekwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando kabla ya kusafirishwa Sengerema kwa maziko Desemba 4.


Akizungumza na waandishi wetu juzi, mtu wa karibu wa Abel aliyejitambulisha kwa jina la Emmanuel alisema baada ya kumaliza mazishi, familia ilirudi Kayenze, Lakini yeye Desemba 17  mwaka huu ghafla alionana na Abel akiwa mzima wa afya maeneo ya Mwaloni.


Alisema alimuweka chini ya ulinzi na kumpeleka Kituo cha Polisi cha Kayenze na kutoa taarifa kwa ndugu waliokuwa Sengerema ambao walifika na kujionea marehemu akiwa hai!
Kituoni hapo, Abel alikataa katakata kuwa yeye hakufa alikuwa kwenye misele yake ila alipoteza simu ndiyo maana hakuwa na mawasiliano na nduguze.


Ndugu hawakuyaamini mwaelezo hayo, wakati mwingine walitaka asiwakaribie maana ni mzimu, lakini wakiwa katika maswali mengi juu ya Abel yupi aliyezikwa, walipata taarifa kituoni hapo kuwa maiti waliyemzika Sengerema anaitwa Manyama Chimwejo na nduguze  wamepatikana.


Polisi wakaitaka familia hiyo ya Abel kukaa na familia ya Manyama kujadili hatima, kama watafukua maiti hiyo na kwenda kumzika upya Kigoma au watamwacha hukohuko Sengerema alipozikwa awali.


Akizungumza kwa simanzi, Abel (aliyedhaniwa kufa) alisema ndugu zake wanachojua waliyemzika ndiye Abel bali amefufuka.


Ndugu zangu hawaamini kama mimi ni mzima hivyo napata tabu sana kwa kuwa kila mtu ananipigia simu kuniuliza. Mimi sikufa, nilikuwa nyumbani kwangu, tatizo lilikuwa ni mawasiliano, nilipoteza simu,” alisema Abel.

Kwa upande wa pili, kaka wa marehemu aliyejitokeza kudai maiti ya mdogo wake aliyezikwa kimakosa aliyejitambulisha kwa jina la Christopher Chimwejo alimtaja Manyama Chimwejo (20) kuwa kweli alikuwa mwanafunzi wa Chuo cha Biashara (CBE), Tawi la Mwanza mwaka wa kwanza na alifika kuishi naye mapema mwezi huu baada ya chuo kufungwa.

Alisema Manyama alitoweka nyumbani kwake ghafla maeneo ya Mwaloni na baada ya hapo hakumuona tena jambo lililomfanya atoe taarifa polisi.

Hata hivyo, sakata hilo lilimalizika Desemba 21, mwaka huu katika Kituo cha Polisi Kirumba D ambapo pande zote mbili zilikutana na kukubaliana kuacha kaburi la marehemu Manyama liendelee kuwa Sengerema licha ya kwamba familia hiyo haiamini kama mwanafunzi huyo alifariki dunia.

Hapa kuna kitu, sisi hatujafiwa na ndugu yetu, tumechezewa. Kama ndugu yenu aliyekufa amerudi hata ndugu yetu pia atarudi tu, ngojeni kwanza tukatambike kwetu Kigoma,” alisema kaka huyo wa marehemu

SAMAHANI KWA PICHA ZA KUTISHA...MCHAWI APIGWA HADI KUFA MBEZI NI BAADA YA KUDONDOKA NA UNGO



WANANCHI wenye hasira kali wamempiga hadi kumuua mtu mmoja mwanaume aliyesadikiwa kuwa ni mchawi baada ya kuanguka akiwa amepanda ungo maeneo ya Mbezi Luis jijini Dar es Salaam, Mtanzania limeshuhudia.



Kijana huyo mkazi wa Mwanza anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 20 hadi 25, alianguka jana saa 12 asubuhi maeneo hayo baada ya kudai kuwa alikuwa kwenye safari zake za kishirikina.
Kabla ya kufariki alisema “mimi nilikuwa na wenzangu sita, wanaume watatu na wanawake watatu ambapo tulikuwa tunatoka Mwanza kuelekea kwenye mkutano wetu”.
“Lakini mimi kwa bahati mbaya nilikiuka masharti tuliyopewa na mkuu kwa kufungua macho ndipo ghafla nilianguka na kupata kadhia hii inayopelekea mauti yangu”.
 
Hata hivyo kutokana na vurugu zilizokuwapo eneo hilo la tukio, ambapo wananchi wa eneo hilo walikuwa wanataka kumuua, kijana huyo alishindwa hata kutaja jina lake kutokana na kipigo alichokuwa anakipata kutoka kwao.

 Kwa mujibu wa mashuhuda wengine wa tukio hilo walisema baada ya kuanguka eneohilo walimkimbiza hadi ndani kwa mtu na kumtoa pamoja na zana zake za kichawi ambapo walizichoma kwanza moto ikiwa pamoja na ungo wenyewe ndipo wakaendelea kumpiga kwa mawe hadi mauti yalipomkuta.

 “Huyu jamaa bwana, ameanguka hapa, sasa kwakuwa sisi hatuna mzaha na watu kamahawa tumemtoa huko alikokimbilia na kumhalalisha kwa vijana wa kazi hapa baada ya kuhakikisha zana zake zote tumezichoma moto” alisema mkazi mmoja wa maeneo hayo. Hata hivyo baadhi ya wananchi walielekeza lawama zao kwa Jeshi la Polisi (Kituo cha Polisi Kimara) kilichopo Mbezi kwa Yusuph kwa kuchelewa kuja kumuokoa kija huyo ingawa walipewa taarifa mapema. 
 
“Sisi tumepiga simu kituoni hapo hata kabla huyu mchawi hajaanza kushambuliwa, lakini angalia tukio limeanza saa 12 asubuhi wanakuja baada ya masaa mawili, huu nu uzembe” alisema mkazi wa eneo hiloaliyejitambulisha kwa jina moja la Ali.

Ingawa katika tukioa hilo kulitokea mkazi mmoja aliyekuwa na silaha aina ya bastola na kufyatua risasi hewani kwa lengo la kuwatawanyisha wananchi hao wenye hasira kali, haikusaidia kitu kwani waliendelea kumpiga hadi wakahakikisha amekufa.

Mtanzania lilibisha hodi katika kituo cha Polisi Kimara ambacho mwili wake ulipelekwa ili kupata uthibitisho zaidi lakini askari wa zamu waliokuwa mapokezi walisema hawana mamlaka ya kutoa maelezo hadi mkuu wa kituoa au mkuu wa makosa ya kieupelezi wa kituo hicho ndiyo wenye dhamana.

 Aidha wakuu hao OC CID (ASP) M. Mganga pamoja na Mkuu wa kituo wote hawakuwapo kituoni wakati Kamanda wa kipolisi wa Kinondoni, Elias Kalinga hakuweza kupatikana ili kudhibitisha tukio hilokutokana na namba yake ya simu kuita bila kupokelewa

SAMAHANI KWA PICHA ZA KUTISHA...MCHAWI APIGWA HADI KUFA MBEZI NI BAADA YA KUDONDOKA NA UNGO



WANANCHI wenye hasira kali wamempiga hadi kumuua mtu mmoja mwanaume aliyesadikiwa kuwa ni mchawi baada ya kuanguka akiwa amepanda ungo maeneo ya Mbezi Luis jijini Dar es Salaam, Mtanzania limeshuhudia.



Kijana huyo mkazi wa Mwanza anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 20 hadi 25, alianguka jana saa 12 asubuhi maeneo hayo baada ya kudai kuwa alikuwa kwenye safari zake za kishirikina.
Kabla ya kufariki alisema “mimi nilikuwa na wenzangu sita, wanaume watatu na wanawake watatu ambapo tulikuwa tunatoka Mwanza kuelekea kwenye mkutano wetu”.
“Lakini mimi kwa bahati mbaya nilikiuka masharti tuliyopewa na mkuu kwa kufungua macho ndipo ghafla nilianguka na kupata kadhia hii inayopelekea mauti yangu”.
 
Hata hivyo kutokana na vurugu zilizokuwapo eneo hilo la tukio, ambapo wananchi wa eneo hilo walikuwa wanataka kumuua, kijana huyo alishindwa hata kutaja jina lake kutokana na kipigo alichokuwa anakipata kutoka kwao.

 Kwa mujibu wa mashuhuda wengine wa tukio hilo walisema baada ya kuanguka eneohilo walimkimbiza hadi ndani kwa mtu na kumtoa pamoja na zana zake za kichawi ambapo walizichoma kwanza moto ikiwa pamoja na ungo wenyewe ndipo wakaendelea kumpiga kwa mawe hadi mauti yalipomkuta.

 “Huyu jamaa bwana, ameanguka hapa, sasa kwakuwa sisi hatuna mzaha na watu kamahawa tumemtoa huko alikokimbilia na kumhalalisha kwa vijana wa kazi hapa baada ya kuhakikisha zana zake zote tumezichoma moto” alisema mkazi mmoja wa maeneo hayo. Hata hivyo baadhi ya wananchi walielekeza lawama zao kwa Jeshi la Polisi (Kituo cha Polisi Kimara) kilichopo Mbezi kwa Yusuph kwa kuchelewa kuja kumuokoa kija huyo ingawa walipewa taarifa mapema. 
 
“Sisi tumepiga simu kituoni hapo hata kabla huyu mchawi hajaanza kushambuliwa, lakini angalia tukio limeanza saa 12 asubuhi wanakuja baada ya masaa mawili, huu nu uzembe” alisema mkazi wa eneo hiloaliyejitambulisha kwa jina moja la Ali.

Ingawa katika tukioa hilo kulitokea mkazi mmoja aliyekuwa na silaha aina ya bastola na kufyatua risasi hewani kwa lengo la kuwatawanyisha wananchi hao wenye hasira kali, haikusaidia kitu kwani waliendelea kumpiga hadi wakahakikisha amekufa.

Mtanzania lilibisha hodi katika kituo cha Polisi Kimara ambacho mwili wake ulipelekwa ili kupata uthibitisho zaidi lakini askari wa zamu waliokuwa mapokezi walisema hawana mamlaka ya kutoa maelezo hadi mkuu wa kituoa au mkuu wa makosa ya kieupelezi wa kituo hicho ndiyo wenye dhamana.

 Aidha wakuu hao OC CID (ASP) M. Mganga pamoja na Mkuu wa kituo wote hawakuwapo kituoni wakati Kamanda wa kipolisi wa Kinondoni, Elias Kalinga hakuweza kupatikana ili kudhibitisha tukio hilokutokana na namba yake ya simu kuita bila kupokelewa

SAMAHANI KWA PICHA ZA KUTISHA...MCHAWI APIGWA HADI KUFA MBEZI NI BAADA YA KUDONDOKA NA UNGO



WANANCHI wenye hasira kali wamempiga hadi kumuua mtu mmoja mwanaume aliyesadikiwa kuwa ni mchawi baada ya kuanguka akiwa amepanda ungo maeneo ya Mbezi Luis jijini Dar es Salaam, Mtanzania limeshuhudia.



Kijana huyo mkazi wa Mwanza anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 20 hadi 25, alianguka jana saa 12 asubuhi maeneo hayo baada ya kudai kuwa alikuwa kwenye safari zake za kishirikina.
Kabla ya kufariki alisema “mimi nilikuwa na wenzangu sita, wanaume watatu na wanawake watatu ambapo tulikuwa tunatoka Mwanza kuelekea kwenye mkutano wetu”.
“Lakini mimi kwa bahati mbaya nilikiuka masharti tuliyopewa na mkuu kwa kufungua macho ndipo ghafla nilianguka na kupata kadhia hii inayopelekea mauti yangu”.
 
Hata hivyo kutokana na vurugu zilizokuwapo eneo hilo la tukio, ambapo wananchi wa eneo hilo walikuwa wanataka kumuua, kijana huyo alishindwa hata kutaja jina lake kutokana na kipigo alichokuwa anakipata kutoka kwao.

 Kwa mujibu wa mashuhuda wengine wa tukio hilo walisema baada ya kuanguka eneohilo walimkimbiza hadi ndani kwa mtu na kumtoa pamoja na zana zake za kichawi ambapo walizichoma kwanza moto ikiwa pamoja na ungo wenyewe ndipo wakaendelea kumpiga kwa mawe hadi mauti yalipomkuta.

 “Huyu jamaa bwana, ameanguka hapa, sasa kwakuwa sisi hatuna mzaha na watu kamahawa tumemtoa huko alikokimbilia na kumhalalisha kwa vijana wa kazi hapa baada ya kuhakikisha zana zake zote tumezichoma moto” alisema mkazi mmoja wa maeneo hayo. Hata hivyo baadhi ya wananchi walielekeza lawama zao kwa Jeshi la Polisi (Kituo cha Polisi Kimara) kilichopo Mbezi kwa Yusuph kwa kuchelewa kuja kumuokoa kija huyo ingawa walipewa taarifa mapema. 
 
“Sisi tumepiga simu kituoni hapo hata kabla huyu mchawi hajaanza kushambuliwa, lakini angalia tukio limeanza saa 12 asubuhi wanakuja baada ya masaa mawili, huu nu uzembe” alisema mkazi wa eneo hiloaliyejitambulisha kwa jina moja la Ali.

Ingawa katika tukioa hilo kulitokea mkazi mmoja aliyekuwa na silaha aina ya bastola na kufyatua risasi hewani kwa lengo la kuwatawanyisha wananchi hao wenye hasira kali, haikusaidia kitu kwani waliendelea kumpiga hadi wakahakikisha amekufa.

Mtanzania lilibisha hodi katika kituo cha Polisi Kimara ambacho mwili wake ulipelekwa ili kupata uthibitisho zaidi lakini askari wa zamu waliokuwa mapokezi walisema hawana mamlaka ya kutoa maelezo hadi mkuu wa kituoa au mkuu wa makosa ya kieupelezi wa kituo hicho ndiyo wenye dhamana.

 Aidha wakuu hao OC CID (ASP) M. Mganga pamoja na Mkuu wa kituo wote hawakuwapo kituoni wakati Kamanda wa kipolisi wa Kinondoni, Elias Kalinga hakuweza kupatikana ili kudhibitisha tukio hilokutokana na namba yake ya simu kuita bila kupokelewa

KABLA YA CHRISTIMAS HIVI NDIVYO DIAMOND ALIVYO AMUA KUKATIZA MITAANI YA DAR ES SALAAM KWA MIGUU









SAMAHANI KWA PICHA YA KUTISHA KATIKA OPERATION YA TOKOMEZA UJANGILI..ILIYO SABABISHA MAWAZIRI 4 KUONDOLEWA


Uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete kuwaachisha kazi mawaziri wanne Ijumaa, juma lililopita, umemsaidia kuiokoa serikali yake dhidi ya kupigiwa kura na wabunge ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu wake. Kama asingechukua hatua hiyo, Rais angekabiliwa na tatizo la au kuvunja serikali yake au yeye mwenyewe kupigiwa kura hiyo na hivyo kulipeleka taifa katika uchaguzi mkuu wa kuchagua serikali nyingine. Mawaziri ambao Rais alitengua kuendelea kusimamia wizara zao ni aliyekuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo, bwana David Mathayo, aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na
Jeshi la Kujenga Taifa, bwana Shamsi Vuai Nahodha, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, bwana Emmanuel Nchimbi na aliyekuwa Waziri wa Mali asili na Utalii, Balozi Hamisi Kagasheki. Hata hivyo bwana Kagasheki ambaye ni mwanadiplomasia kwa taaluma, anaelekea ‘alitonywa’ na Rais kuwa ataondolewa hivyo akatumia mahusiano yake hayo ya karibu na Rais kutangaza kujiuzulu kwake bungeni kabla Rais hajatangaza uamuzi wake wa kuwaondoa mawaziri wengine watatu Ijumaa hiyo. Pengine jambo la kusikitisha ni utetezi uliofanywa bungeni na aliyekuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo, bwana Mathayo ambaye alidiriki kudai kuwa anaonewa! Huyu ni Waziri ambaye alipewa maagizo tisa na rais mwaka 2006, lakini mpaka alipoachishwa kazi Ijumaa alikuwa hajatekeleza hata agizo moja! Kwa kujitetea kwake bungeni, Waziri huyo ameonyesha bayana kwanini hakupaswa kupewa kazi ya uwaziri! Katika utetezi wake bungeni, bwana Mathayo, alidai kuwa Wizara yake kuanzia mwaka 2006 imekuwa ikipewa fedha kidogo tofauti na zile ambazo ilikuwa ikiomba. Lakini kwa bahati mbaya hakuonesha ni kwa namna gani amekuwa akitumia fedha hizo kidogo katika kutatua moja ya maagizo hayo tisa aliyopewa na rais! Hata hivyo, uamuzi wa Rais kuwaondoa mawaziri hao wanne hautakuwa na tija kama hatawaondoa pia viongozi wa Vyombo vya Dola ambavyo vimelaumiwa Ijumaa na wabunge kwa kuhusisha uvunjaji wa haki za binadamu; vitendo ambavyo vinafanana na vile ambavyo vilikuwa vikifanywa na makaburu wa serikali ya kibaguzi ya Afrika Kusini! Viongozi wa Taasisi hizo wanaopaswa pia kufutwa kazi ni pamoja na Mkuu wa Jeshi la Wananchi na Jeshi la Kujenga Taifa, Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi, Mkugurugenzi wa Usalama wa Taifa na Kamanda wa Askari wa Wanyamapori. Viongozi hao toka Taasisi nne nilizotaja, wanapaswa pia kuwajibishwa kutokana na usimamizi wao mbaya wa Vyombo vya Dola vilivyohusika moja kwa moja na utekelezaji wa Operesheni Tokomeza. Serikali pia inapaswa kuwashughulikia Makatibu Wakuu wote na wakurugenzi wao wa Wizara nne husika, pamoja na ile inayosimamia Utawala Bora, Wizara ambayo pia inasimamia Usalama wa Taifa. Hata hivyo serikali pia inapaswa kuchunguza kwa kina yale ambayo yamekuwa yakiendelea, hususan katika Wizara ya Mali asili na Utalii, hasa katika eneo la vitalu vya uwindaji na kadhalika. Kumekuwa na madai lukuki ya rushwa katika eneo hili! Ikumbukwe pia kuwa ni viongozi waandamizi wa wizara hiyo hiyo waliodaiwa kuhuhusika na utoroshaji wa wanyamapori kwenda Jamhuri ya Kifalme ya Uarabuni, UAE, mwezi Septemba, mwaka 2010 wakati umakini wa viongozi wa nchi ulikuwa umemezwa na shughuli za uchaguzi mkuu! Kadhalika ni viongozi hao hao wambao walidaiwa kuhusika, kwa namna moja au nyingine na kashifa ya kuitenga Loliondo na kakabidhi sehemu nyeti ya eneo hilo kwa waarabu chini ya mkataba tata! Suala la Liliondo linalokaliwa na mtoto wa mfalme wa UAE linapaswa kutafutiwa ufumbuzi sasa kwani wakati utakuja wakati Rais wa Tanzania wakati huo atapaswa kuwajibika! Swali ambalo tunapaswa kujiuliza ni; Kwanini viongozi waandamizi katika wizara hii wana kiburi cha kutisha cha hata kutompa ushirikiano aliyekuwa waziri wa wizara hiyo, Balozi Kagasheki? Wabunge siku ya Ijumaa walihoji Usalama wa Taifa walikuwa wapi wakati yote haya yalikuwa yakitokea. Mimi nauliza, Waandishi wa Habari na Vyombo vya Habari walikuwa wapi? Tutafakari! - See more at: http://www.fikrapevu.com/operesheni-tokomeza-serikali-kuwafukuza-mawaziri-wanne-kazi-haitoshi
source-jamiiforums

Sunday 22 December 2013

JAMAA AKIMBIA GESTI AKIWA MTUPU BAADA YA KUFUMANIWA NA MKEWE AKIWA NA KIMADA WAKIVUNJA AMRI YA SITA...!!




DUNIA ina mambo jamani! Mfanyabiashara wa madini aliyefahamika kwa jina moja la Jimmy amejikuta katika wakati mgumu baada ya kufumaniwa na mkewe akiwa na kimada gesti.
Tukio hilo lililofunga mtaa kwa kujaza wambea kibao, lilitokea hivi karibuni ndani ya gesti hiyo (jina tunalo) Kinondoni jijini Dar es salaam ambapo mke wa mfanyabiashara huyo (jina halikupatikana mara moja), alimnasa mumewe  akijiandaa kuvunja amri ya sita ya Muumba.
Mke wa mfanyaiashara (kulia) baada ya kumfumania kimada akiwa na mumewe gesti maeneo ya Kinondoni, jijini Dar.
Wadakuzi waliokuwa eneo la balaa walitonya kuwa, siku hiyo ya tukio, Jimmy ambaye ni mkazi wa jijini Arusha, alifika Dar kibiashara na baadaye alimsaka kimada huyo wa siku nyingi na kwenda kujirusha naye bila kujua mkewe alishatonywa juu ya usaliti wake.
Awali chanzo makini kinachojua nini maana ya habari kiliwatonya mapaparazi wetu mara baada ya kupata mchongo wa fumanizi kutokea Sinza ya Kumekucha lililoandaliwa na mke wa Jimmy.

“Nyie njooni tu hapa Sinza-Kumekucha ndipo mkewe alipotonywa na dereva wa mumewe kuwa anaibiwa na kimada. Kuna gesti moja ipo ndani kidogo upande wa kushoto kama unaelekea Shekilango,” kilisema chanzo.
Timu ya mapaparazi ilifika katika gesti hiyo lakini bahati mbaya waliambiwa kuwa, Jimmy na kimada huyo walihamisha kiwanja cha starehe na kwenda Kinondoni.
                                               Kimada aliyefumaniwa na mume wa mtu.
Mapaparazi walipofika katika gesti hiyo ya Kinondoni, walimkuta mke wa Jimmy hivyo wakaambatana naye pamoja na askari polisi wawili kwa ajili ya kwenda kufumania.
Jimmy kabla ya kuingia gesti inadaiwa alijipumzisha katika grosari iliyo karibu na Mango Garden Bar, baadaye akaenda kwenye gesti hiyo ya jirani bila kujua mkewe alikuwa akitua mguu kila pale yeye aliponyanyua, akazama ndani ya gesti hiyo na kuanza kujiandaa kwa zinaa.
Mke wa Jimmy hakuwa mbali, baada ya kujiridhisha mumewe amezama chumbani, dakika kadhaa na yeye alitokea na kugonga mlango wa chumba hicho kufuatia kutonywa na mhudumu mmoja wa gesti hiyo.
Jimmy alikutwa tayari ameshavua nguo zote na kubakiwa na ‘boksa’ huku kimada naye akiwa na ‘kufuli’ pekee.
Kilichofuata hapo ni kipigo, mke wa Jimmy alianza kumtembezea kipigo yule kimada. Mapaparazi walivamia na kutandika picha za timbwili ambapo Jimmy alifanikiwa kupenya mlangoni na kukimbia bila kujali nguo nyingine.
Kutokana na kelele za timbwili hilo, majirani wa eneo hilo walifika kuhoji kulikoni ambapo mfumaniaji huyo alitoboa siri kwamba amekuwa akimfuatilia mumewe kwa siku nyingi baada ya kuambiwa ana kimada Dar.
“Huyo malaya akome kutembea na waume za watu. Nimekuwa nikimfuatilia mume wangu kwa muda mrefu. Nimetoka Arusha mpaka Dar kwa ajili yake. Kweli za mwizi ni arobaini, leo nimewanasa,” alisema mwanamke huyo huku akiondoka eneo la tukio na kutokomea kusikojulikana.
Wakati pakichimbika, kimada huyo alisikika akimlaumu Jimmy kwamba amemuingiza kwenye mkenge akijua mkewe ni mdodosaji wa mambo na anaweza kufika Dar madai ambayo hayakuwa na wa kuyajibu.
Taarifa zaidi zilidai kuwa ndugu mmoja wa mwanamke huyo ndiye aliyekuwa na mchoro mzima