YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Wednesday 3 April 2013

BREAKING NEWZZZZZZZZZZZ~ HALI NI MBAYA HUKO TUNDUMA....MABOMU KILA MAHALI NA WATU WAMEAMRIWA WASITOKE NJE


Wednesday, April 3, 2013



Masaa takribani matano mabomu ya machozi na risasi za moto zinasikika mataili yamechomwa barabarani maduka yote yamefungwa...
Ni mshikemshike kati ya vyombo vya dola na raia hadi sasa msikiti mmoja umechomwa moto maeneo ya mwaka na kisimani 
Hali ni mbaya zaidi kwan mabomu ya mochozi yanapigwa hadi vyumbani. 
Imetollewa amri watu wote walale majumbani kwao
Chanzo cha tatizo ni waislam na wakristo.Wametofautiana juu ya swala la kuchinja.

MAGAZETI YA UDAKU YA LEO 3/4/2013





UDAKU WA LEO KWENYE MAGAZETI April 3, 2013





Maghorofa 100 Dar feki, Serikali ina kigugumizi


Wananchi waliliondoa gari lililoangukiwa na jengo la ghorofa 16 wiki iliyopita na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 35. Picha na Ibrahim Yamola 
Dar es Salaam.
Kuporomoka jengo lililopo Mtaa wa Indira Gandhi Jijini Dar es Salaam, huenda ikawa mwanzo tu wa kuporomoka majengo mengine zaidi hasa kufuatia matokeo ya tume iliyoundwa mwaka 2006 iliyobaini zaidi ya majengo 100 Jijini Dar es Salaam yamejengwa bila kuzingatia viwango.
Kwanini Serikali haichukui hatua kwa majengo hayo 100 yaliyobainika kuwa hayajajengwa kwa kuzingatia viwango? Wenye akili timamu wanaweza kuendelea kujiuliza maswali mengi zaidi na kujibu wanavyoweza.
Wapo wanaoweza kusema rushwa ndio inasababisha mambo mengi kutofanyiwa kazi kwa ufasaha, lakini mbele ya sheria utaombwa utoe ushahidi, hapo bila shaka patafanya wengi kubadili maneno kwamba aaah labda Serikali inaendelea kufanya mchakato, mpango mkakati, mkakati yakinifu nk dhidi ya majengo hayo.
Kubomoa jengo lenye ghorofa 16 au hata chini au zaidi ya hapo baada ya kulibaini halijazingatia viwango, ni lazima uwe na uso mgumu. Baadhi ya wananchi wanasema wenye majengo bila shaka hawawezi kutulia wakisubiri sheria ifanye inachotakiwa kufanya, hapo ndipo ugumu unapoanzia.
Pinda analo na kujibu
Baadhi ya watu wanafikiri kuondolewa madarakani kwa viongozi walio katika wizara husika na sakata hili akiwemo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye ofisi yake ilichunguza na kubaini maghorofa zaidi 100 kuwa ni feki, kunaweza kuwa ni mojawapo ya mambo muhimu kwa sasa.
Mke na watoto wafukiwa
Licha kwamba jengo hilo liliporomoka saa 2.30 asubuhi, baadhi ya watu waliofukiwa na kifusi cha jengo hilo walikuwa wakiwasiliana na jamaa zao kwa njia ya simu na wengine wakipiga kelele za kuomba msaada.
Idd Baka ambaye alikuwa akiwasiliana na mkewe ambaye aliegesha gari huku ndani kukiwa na watoto wake wawili alikwenda dukani kununua bidhaa, mara jengo hilo likaporomoka, alikuwa akiwasiliana nae hadi majira ya mchana simu ya mke wake haikuwa inapatikana.
Vifaa duni
Ni dhahiri kwamba endapo kungekuwapo na vifaa vya kutosha katika zoezi la uokoaji lingewezaa kufanikiwa kwa  muda mfupi na kwa kiasi kikubwa hivyo kuwapata majeruhi wakiwa hai.  
Katapila latumika
Cha  ajabu na aibu kwa taifa kutokuwa tayari kwa kuwa na vifaa vya kuokolea kwani tangu saa 2:30 hadi ilipofika saa 4.30 ndipo lilipatikana katapila moja ambalo nalo halikuwa na tija kutokana na kuwapo kwa uwezekano wa kuwakandamiza au kuwajeruhi zaidi  watu waliofukiwa na kifusi hicho.
Kutokana na kutokuwepo na vifaa vya kukatia nongo waokoaji iliwachukua takribani dakika 15 kukata nondo zilizokuwa zimemkandamiza.
Umati wa watu ulivamia kifusi na kuanza kukisomba kwa mikono  ili hali jambo hili lilikuwa kama mchezo wa kuigiza ambao umegharimu uhai wa watu zaidi ya 35 pamoja na kuharibu magari yaliyobondwa na kuwa kama chapati takribani matano.
Mashuhuda
Ali Mparang’ombe mmoja wa mafundi wa jengo hilo anasema kudondoka kwa jengo hilo ni mtiririko wa majengo mengine kutokuwa katika viwango vinavyotakiwa.

Ufisadi mkubwa kampuni za simu


Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe akiwauliza maswali viongozi waTCRA naTRA wakati kamati hiyo alipokutana nao kwenye ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Deo Filikunjombe. Picha na Venance Nestory 


Posted  Jumanne,Aprili2  2013  saa 22:36 PM
KWA UFUPI
“Misamaha kwa kampuni za mawasiliano ni miaka mitano na TIC inaweza kuongeza miaka mingine mitatu. Kutokana na hali hiyo tunahitaji marekebisho ya sheria ili tuweze kuzibana hizi kampuni ziweze kulipa kodi na kuchangia pato la ndani,” alisema Zitto.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Zitto Kabwe hakuwa tayari kueleza maeneo ambayo Serikali imekuwa ikipunjwa kodi na kampuni hizo na badala yake amesema wameunda kamati ndogo ya watu watatu kwa ajili ya kuchunguza wizi huo.

Kamati hiyo ilibaini madudu hayo baada ya kukutana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), Mamlaka ya Bandari (TPA) na Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA).

Akizungumza na waandishi wa habari, Zitto alisema wameitaka TRA kuandika mapendekezo ya kufanyiwa marekebisho ya sheria ya fedha ya 2012, ili iwe na uwezo wa kuhakiki uwekezaji wa kampuni za simu na kufanya ukaguzi wa miradi husika ili kubaini kama inafanana na kodi inayotozwa.

Alisema kampuni hizo zina misamaha mikubwa ya kodi ambayo inatolewa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) bila kushirikisha wadau mbalimbali na kwamba hivi sasa Serikali inapata Sh300 bilioni tu kwa mwaka kama fedha za mapato ya kampuni hizo.

“Misamaha kwa kampuni za mawasiliano ni miaka mitano na TIC inaweza kuongeza miaka mingine mitatu. Kutokana na hali hiyo tunahitaji marekebisho ya sheria ili tuweze kuzibana hizi kampuni ziweze kulipa kodi na kuchangia pato la ndani,” alisema Zitto.

Zitto alisema mbali na mapendekezo hayo, pia wamemtaka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kukagua misamaha yote ya kodi inayotolewa na TIC ili kujiridhisha kabla ya kutoa uamuzi wa kuendelea nayo ama vinginevyo.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa PAC, Deo Filikunjombe alisema: “Kuna fedha zinakatwa kienyeji tu na kampuni hizi, mfano kwa watu 5 milioni kwa siku wanapata Sh1.8 bilioni, sasa kama kampuni hii itakuwa na wateja zaidi inapata kiasi gani, fedha hizi hazipo katika mlolongo wa ukatwaji wa kodi.

“Pia tutahitaji maelezo ya jinsi mnavyodhibiti meseji za chuki ambazo tunaziona kila siku katika simu zetu, pia kampuni hizi zimekuwa zikibadili majina kila baada ya muda fulani jambo ambalo pia linakosesha nchi mapato.”

TRA na TCRA
Mkurugenzi Mkuu wa TRA, Harry Kitilya alisema kinachowakwamisha ni sheria zilizopo, kwamba wanashindwa kukusanya mapato kwa kuwa kampuni hizo zina misamaha ya kodi.
“Misamaha hii ndiyo inatupa wakati mgumu kukusanya mapato, ila kama sheria hii ya misamaha ya kodi itafanyiwa marekebisho tutaweza kuingia kiasi kikubwa cha kodi,” alisema Kitilya.

Naye Profesa Nkoma alisema ili kuzibana zaidi kampuni za simu kuanzia mwezi Julai mwaka huu utafungwa mtambo maalumu wa kudhibiti mawasiliano (TTMS).
Kuhusu wizi wa mafuta bandarini, Zitto alisema kamati hiyo itafanya kazi kwa muda wa mwezi mmoja ikiwa ni pamoja na kuhoji wadau mbalimbali wanaohusika na suala hilo ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

Alisema wizi huo umekuwa ukifanywa kutokana na kuchezewa kwa mabomba (flow meters) ya kupakua mafuta kutoka kwenye meli na kwamba WMA pamoja na TRA wamethibitisha kwamba vipimo hivyo havifai kwani vinasoma tofauti na kiasi cha ujazo wa mafuta.

Aliongeza kuwa kitendo cha kuzuia mashine hiyo kutofanya kazi kumezidisha wizi wa mafuta bandarini, jambo ambalo limesababisha kuongezeka kwa malalamiko.

Alisema katika mazingira hayo mkakati wa Serikali wa kuongeza mapato kupitia vyanzo vya ndani hauwezi kufanikiwa, hivyo wabunge wana wajibu wa kuchukua hatua ili kuhakikisha hali hiyo inafanyiwa kazi.

Marekani yaongeza kasi ya vita Korea



SHARE BOOKMARKPRINTEMAILRATING
Magari ya kivita yakiwa yameegeshwa katika mji wa Panju nchini Korea ya Kaskazini tayari kabisa kwa mashambulizi yanayotarajiwa kufanywa na Korea Kusini inayosaidiwa na Marekani.Picha na AFP  

Tuesday 2 April 2013

Maafa juu ya maafa, Dar 36 Arusha 20


Kile kilichodhaniwa kuwa kilele cha sikukuu ya pasaka, kimegeuka msiba baada ya wachimba kokoto 20 kufukiwa katika kifusi Jijini Arusha.
Hiyo ilikuwa ni kama ndimu katika kidonda kibichi, kwani ni ijumaa iliyopita tu wakati watu wakijiandaa kwa sikukuu ya Pasaka jengo la ghorofa 16 lilidondoka Jijini Dar es Salaam na kuua watu 36.
Vifo hivi vilivyotokea katika msimu wa sikukuu vimeweka idadi ya watu waliopoteza maisha kufikia 56 hivi, ndani ya  siku nne tu.
Watu waliofukiwa na kifusi mkoani Arusha, walikuwa wakichimba kokoto katika eneo la Moshono.
 Imeelezwa kuwa ni maiti 14 tu ndizo zilizoopolewa na watu wengine bado wanahofiwa kuwa ndani ya kifusi hicho.
 Ilikuwa ni saa tano asubuhi, juzi, gema la kokoto liliporomoka kisha kuwafunika wote waliokuwamo ndani, sababu kubwa ikielezwa kuwa ni mvua kubwa zilizokuwa zikinyesha mjini Arusha.
 Vilevile magari mawili yaliyokuwa yamepaki pembeni kwa ajili ya kubeba mzigo huo yalizama ndani ya shimo hilo kubwa la kokoto.

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KUTOKA SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA



Ukitaka kuangalia nafasi za kazi bofya hapo chini

 

Bofya hapa chini