YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Thursday 6 March 2014

NI AIBU SANA...!!! WAFUMANIWA WAKIFANYA MAPENZI NDANI YA GARI..


Mke wa mtu alivyonaswa na njemba wakifanya uzinzi kwenye gari.
KUFUATIA vitendo vya usaliti wa ndoa, uasherati, ufuska na ukiukwaji wa maadili ya Kitanzania kwa wanandoa, wiki iliyopita Ijumaa liliendelea na Operesheni Fichua Maovu kwa kuzunguka jijini Dar usiku wa manane na kunasa tukio la mke wa mtu akifanya uzinzi ndani ya gari.
KINONDONI YAONGOZA 

Kabla ya kufanya operesheni hiyo, gazeti hili liliambiwa kwamba Wilaya ya Kinondoni jijini Dar ndiyo inayoongoza kwa wake na waume za watu kufanya vitendo vya ngono kwenye magari.
Maeneo yaliyodaiwa kwamba wazinzi hao hupenda kuyatumia ni Coco Beach, Leaders Club, Mlimani City na sehemu kubwa ya vitongoji vya Sinza na Mwenge, Dar.
WAMO WASANII
Mbali na waume na wake za watu, wengine wanaotajwa kufanya vitendo vya ngono ndani ya magari ni mastaa wakubwa ambao wanaogopa kwenda kukodi vyumba mahotelini na gesti wakihofia watajulikana kutokana na umaarufu wao.
IJUMAA MZIGONI
Kwa muda wa wiki nzima, timu ya Ijumaa ilikuwa barabarani kwa ajili ya opresheni hiyo ya kufichua uovu huo.
JUMATATU, 3 2014
January 3, mwaka huu, waandishi wa Ijumaa walianza mchakato wa kutembelea vitongoji walivyoezwa kwamba, watu hususan wake na waume za watu hupenda kuvitumia kufanyia ufuska.
COCO BEACH
Waandishi wetu walitinga kwenye Ufukwe wa Coco uliopo Oysterbay, Dar ambako walishuhudia wasichana wengi waliokuwa wakifanya biashara ya kujiuza ‘machangudoa’ katika viunga hivyo.
Mbali na wasichana hao, pia kulikuwa na vibaka wengi waliokuwa wakiwalinda machangudoa hao ili wasipate matatizo.
Pia, wanaume wengi walikuwa wakifika na wanawake ndani ya magari yao na kupozi kwenye maegesho, wengi wao hawakuonekana kama ni watu na wake zao.
USALAMA MDOGO
Hata hivyo, Ijumaa lilibaini kwamba magari mengi yanayotumiwa katika eneo hilo ni yale yenye vyoo vyeusi ‘tinted’ hivyo ni vigumu kujua kinachoendelea ndani yake.
Kwa ujanja, Ijumaa lilibaini kwamba ‘pea’ nyingine zilikuwa zikifanya vitendo vya ‘kudendeka’ na wengine kufika mbali zaidi lakini Ijumaa lilishindwa kuwavaa kutokana na usalama mdogo katika eneo hilo.

Jamaa akijaribu kuvaa nguo baada ya kunaswa.
Wakiwa wamepigwa butwaa ndani ya gari.
Wakiwa na aibu baada ya kukutwa ndani ya gari.
 
Mwanaume naye akivaa pensi yake baada ya aibu hiyo.

SAA 8:05 USIKU, LEADERS CLUB
Ijumaa lilihamishia mtego wake Leaders Club, Kinondoni mida ya saa 8:05, baada ya kupiga misele ya hapa na waandishi walifanikiwa kumbamba mmoja wa wazinzi.
AWATOROKA WAANDISHI
Waandishi walitulia baada ya kuliona gari aina ya Toyota Land Cruiser (namba tunazo) likiwa katika eneo la maficho nje ya viwanja hivyo.
Gari hilo lilikuwa likitikisika kuonesha kwamba mchezo ulikuwa ukiendelea ndani yake.
Wakati waandishi wakijipanga kulivamia, ghafla waliokuwa ndani walishtuka na kupozi kwa muda.
Hata walipoachiwa ili waendelee, machale yaliwacheza na kuwasha gari kisha kuondoka kwa kasi.
 
Mwanamke akivaa chupi yake.
JUMATATU HADI JUMAPILI
Pamoja na kulikosakosa tukio hilo, waandishi hawakukata tamaa, kuanzia Jumatatu hadi Jumapili waliendelea na utaratibu wa kutembelea viwanja husika.
KABAANG!
Jumapili iliyopita baada ya kutembelea viwanja vyote kusaka ‘wahalifu hao’, hatimaye mtego ulinasa ‘kabaang!’
January 3, JUMAPILI SAA 9:20 USIKU
‘Patroo’ ikiwa kazini maeneo ya Mwenge, Dar jirani kabisa na hoteli moja inayopata umaarufu mkubwa siku za hivi karibu, ghafla gari aina ya Toyota Corona likiwa limepaki kwenye eneo la giza, chini ya mti lilikuwa likitikisika kuonesha kwamba kulikuwa na watu waliokuwa wakifanya ngono.
Safari hii, bila kufanya makosa, waandishi wetu waliwasogelea ambapo na wao hawakuonekana kujali wapita njia

NI AIBU SANA...!!! WAFUMANIWA WAKIFANYA MAPENZI NDANI YA GARI..


Mke wa mtu alivyonaswa na njemba wakifanya uzinzi kwenye gari.
KUFUATIA vitendo vya usaliti wa ndoa, uasherati, ufuska na ukiukwaji wa maadili ya Kitanzania kwa wanandoa, wiki iliyopita Ijumaa liliendelea na Operesheni Fichua Maovu kwa kuzunguka jijini Dar usiku wa manane na kunasa tukio la mke wa mtu akifanya uzinzi ndani ya gari.
KINONDONI YAONGOZA 

Kabla ya kufanya operesheni hiyo, gazeti hili liliambiwa kwamba Wilaya ya Kinondoni jijini Dar ndiyo inayoongoza kwa wake na waume za watu kufanya vitendo vya ngono kwenye magari.
Maeneo yaliyodaiwa kwamba wazinzi hao hupenda kuyatumia ni Coco Beach, Leaders Club, Mlimani City na sehemu kubwa ya vitongoji vya Sinza na Mwenge, Dar.
WAMO WASANII
Mbali na waume na wake za watu, wengine wanaotajwa kufanya vitendo vya ngono ndani ya magari ni mastaa wakubwa ambao wanaogopa kwenda kukodi vyumba mahotelini na gesti wakihofia watajulikana kutokana na umaarufu wao.
IJUMAA MZIGONI
Kwa muda wa wiki nzima, timu ya Ijumaa ilikuwa barabarani kwa ajili ya opresheni hiyo ya kufichua uovu huo.
JUMATATU, 3 2014
January 3, mwaka huu, waandishi wa Ijumaa walianza mchakato wa kutembelea vitongoji walivyoezwa kwamba, watu hususan wake na waume za watu hupenda kuvitumia kufanyia ufuska.
COCO BEACH
Waandishi wetu walitinga kwenye Ufukwe wa Coco uliopo Oysterbay, Dar ambako walishuhudia wasichana wengi waliokuwa wakifanya biashara ya kujiuza ‘machangudoa’ katika viunga hivyo.
Mbali na wasichana hao, pia kulikuwa na vibaka wengi waliokuwa wakiwalinda machangudoa hao ili wasipate matatizo.
Pia, wanaume wengi walikuwa wakifika na wanawake ndani ya magari yao na kupozi kwenye maegesho, wengi wao hawakuonekana kama ni watu na wake zao.
USALAMA MDOGO
Hata hivyo, Ijumaa lilibaini kwamba magari mengi yanayotumiwa katika eneo hilo ni yale yenye vyoo vyeusi ‘tinted’ hivyo ni vigumu kujua kinachoendelea ndani yake.
Kwa ujanja, Ijumaa lilibaini kwamba ‘pea’ nyingine zilikuwa zikifanya vitendo vya ‘kudendeka’ na wengine kufika mbali zaidi lakini Ijumaa lilishindwa kuwavaa kutokana na usalama mdogo katika eneo hilo.

Jamaa akijaribu kuvaa nguo baada ya kunaswa.
Wakiwa wamepigwa butwaa ndani ya gari.
Wakiwa na aibu baada ya kukutwa ndani ya gari.
 
Mwanaume naye akivaa pensi yake baada ya aibu hiyo.

SAA 8:05 USIKU, LEADERS CLUB
Ijumaa lilihamishia mtego wake Leaders Club, Kinondoni mida ya saa 8:05, baada ya kupiga misele ya hapa na waandishi walifanikiwa kumbamba mmoja wa wazinzi.
AWATOROKA WAANDISHI
Waandishi walitulia baada ya kuliona gari aina ya Toyota Land Cruiser (namba tunazo) likiwa katika eneo la maficho nje ya viwanja hivyo.
Gari hilo lilikuwa likitikisika kuonesha kwamba mchezo ulikuwa ukiendelea ndani yake.
Wakati waandishi wakijipanga kulivamia, ghafla waliokuwa ndani walishtuka na kupozi kwa muda.
Hata walipoachiwa ili waendelee, machale yaliwacheza na kuwasha gari kisha kuondoka kwa kasi.
 
Mwanamke akivaa chupi yake.
JUMATATU HADI JUMAPILI
Pamoja na kulikosakosa tukio hilo, waandishi hawakukata tamaa, kuanzia Jumatatu hadi Jumapili waliendelea na utaratibu wa kutembelea viwanja husika.
KABAANG!
Jumapili iliyopita baada ya kutembelea viwanja vyote kusaka ‘wahalifu hao’, hatimaye mtego ulinasa ‘kabaang!’
January 3, JUMAPILI SAA 9:20 USIKU
‘Patroo’ ikiwa kazini maeneo ya Mwenge, Dar jirani kabisa na hoteli moja inayopata umaarufu mkubwa siku za hivi karibu, ghafla gari aina ya Toyota Corona likiwa limepaki kwenye eneo la giza, chini ya mti lilikuwa likitikisika kuonesha kwamba kulikuwa na watu waliokuwa wakifanya ngono.
Safari hii, bila kufanya makosa, waandishi wetu waliwasogelea ambapo na wao hawakuonekana kujali wapita njia

PICHA ZA FUMANIZI:MKE WA MTU AFUMWA LIVU NA MWANAMME MWINGINE CHUMBANI KWA MUMEWE MCHANA KWEUPE


Mwanamke aliyetambulika kwa jina moja la Mwanahamisi au mama Daudi, mkazi wa Pugu-Kajiungeni, Dar, amejikuta akipata aibu ya karne baada ya kudaiwa kuingiza mwanaume mwingine chumbani kisha kufumaniwa na mumewe.
 
MSAMAHA: 
Mwanahamisi ambaye ni mke wa mtu akiomba samahani baada ya kunaswa.
Tukio hilo la kufedhehesha lilijiri hivi karibuni, mchana kweupe nyumbani kwa wanandoa hao maeneo hayo.
ILIKUWAJE?
Kwa mujibu wa mtu wa karibu wa wanandoa hao, mume wa Mwanahamisi aitwaye Mashaka au baba Daudi ana rafiki yake aliyetajwa kwa jina moja la Paulo ambaye alidai kusumbuliwa na shemeji yake (mama Daudi) kwa muda mrefu.
Ilidaiwa kuwa mama Daudi alikuwa akimtumia Paulo ujumbe wa mapenzi kupitia simu hadi wakati mwingine kufikia hatua ya kumbana na kumkumbatia pale anapokutana naye njiani.
Ikaelezwa kwamba Paulo alimwambia baba Daudi kuwa alikuwa ameshamtumia zaidi ya SMS 240 za kimapenzi.
Baada ya kuona kero zimezidi huku rafiki yake akimlalamikia kutomuelewa mke wake aliyezaa naye mtoto mmoja ambaye bado hata hajaacha kunyonya, Paulo aliamua kuvunja ukimya na kumuonesha ujumbe anaotumiwa na shemeji yake huyo ili wamkomeshe.
AIBU YA USALITI: 
Mke wa mtu pamoja na njemba aliyokuwa nayo wakiwa na aibu baada ya kunaswa live chumbani.
Ilisemekana kwamba baada ya kufanya tathmini ya SMS hizo, baba Daudi na Paulo waliweka mtego huku wakimshirikisha mke wa Paulo ambaye aliwahi kugombana na mama Daudi kwa kitendo cha kumtambia ovyo.
Ilielezwa kuwa baada ya mpango kukamilika huku Paulo akimwambia shemeji yake kuwa amemkubalia, mama Daudi alimuaga mumewe kuwa baba yake ni mgonjwa huko Yombo-Buza, Dar hivyo anakwenda kumuona na siku hiyo atarudi saa 12:00 jioni akijua kuwa kwa mwanya huo ataweza kwenda gesti maeneo ya Ukonga-Mombasa, Dar na Paulo kama walivyokubaliana.
Ilisemekana kuwa baada ya Paulo kuona gesti patakuwa na shida ya kumshikisha adabu mama Daudi, alimshawishi wakutane chumbani kwa mumewe (baba Daudi) ili iwe rahisi kumfumania.
Ilifahamika kwamba ili kusaliti chumbani kwa mumewe, alimpigia simu baba Daudi kujua alipokwenda.
Kwa kuwa baba Daudi alijua mchezo, alimwambia mkewe kuwa amekwenda kufuatilia kitambulisho cha kazi kisha atakwenda Kigogo, Dar kwenye mishemishe nyingine.
Ilidaiwa kuwa majibu hayo yalimfurahisha mama Daudi ambaye alimwalika Paulo chumbani kwa mumewe bila kujua aliwekewa mtego.
KIPONDO: Mke wa mtu akipokea kichapo baada ya kubambwa. 
SAA 7:OO MCHANA KWEUPE
Mishale ya saa 7:00 mchana, Paulo aliondoka nyumbani kwake na kuwaacha wafumaniaji wakiwa tayari, alipofika kwa mama Daudi naye akainua simu kumpigia baba Daudi kumhakikishia Mwanahamisi kuwa mume wake harudi muda huo, akamwambia kuwa amekwenda mbali wataonana saa 12:00 jioni.
Ilidaiwa kuwa ili wafaidi mambo vizuri, mama Daudi alimuondoa mtoto wake na mdogo wake kwa kuwapa fedha ya kwenda kulipia kuangalia ‘tiivii’ kibandani ili abanjuke na Paulo kwa raha zake.
Nusu saa kabla ya tendo, Mwanahamisi alikuwa ameshasaula nguo zote mwilini ndipo Paulo alipomtaarifu baba Daudi kuwa mchezo tayari anaweza kufumania.
OFM, BABA DAUDI
Baba Daudi, huku akiambatana na makamanda wa Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers alitimba chumbani kwake na kumbamba mkewe ‘live’ kitandani kwake, tayari kusaliti ndoa.
Huku OFM ikishuhudia, mama Daudi alishtuka na kukimbilia khanga kisha akaanza kutoa lawama kwa Paulo kwa kumtia mtegoni.
Katika utetezi wake, mama Daudi alilia kwa uchungu na kusema kuwa ni shetani na tamaa ya fedha ndiyo iliyomponza kwani alijua angelamba mshiko kutoka kwa Paulo.
“Yaani naumia sana kwa mume wangu kunifumania tena na rafiki yake, naomba msamaha, ni shetani tu alinipitia,” alisema mama Daudi huku akimpigia magoti baba Daudi.
Pamoja na utetezi wake, mama Daudi alikula kichapo cha nguvu kutoka kwa mke wa Paulo ambaye aliunganishwa kwenye mtego.
Baada ya mtiti wa nguvu, mama wa Mwanahamisi aliitwa ambapo alipofika na kujionea aibu ya mwanaye, presha ilimpanda, akashindwa kuongea. Hata hivyo, fumanizi hilo liliisha baada ya mmoja wa majirani kusuluhisha ugomvi huku akiwaongoza ibada ya toba kisha akawaomba wasameheane.
Mwanahamisi akamuangukia mumewe na kumuomba msamaha, maisha yakaendelea

TAZAMA HAPA YALOJIRI USIKU WA VIGODORO...!JIONEE MWENYEWE HAPA...


Kwenye hii video utamuona mkali wa vigodoro anaitwa Msagasumu akiwapagawisha mashabiki wake ndani ya Dar Live ambapo kulifanyika uzinduzi wa movie ya Kigodoro.

Kitu kingine ni pale Wema Sepetu alipoimba verse ya Diamond kwenye wimbo wa Letadutigite akiwa na Linex.
Shilole kahusika pia kwenye hii video bila kuiacha sehemu ambayo Wema alipoamua kuvua pete zote baada ya kupoteza pete moja akiwasalimia mashabiki wake.
CHEKI VIDEO HAPA CHINI..

TUPILIA MBALI DIAMOND NA JAYDEE , HUYU NDIYE BILLIONEA WA KITANZANIA,,MFAHAMU HAPA


Diamond-Lady-jaydee


Hapa duniani kwasasa kuna mabilionea 1645 , kutokana na takwimu zilizotolewa na Forbes. Kwa mwaka jana bara la Afrika lilikua na mabilionea 20 lakini kwa mwaka huu wameongezeka mabilionea 9 na mmoja wapo ni mtanzania. Kwa upande wa sanaa ya hapa Bongo basi tunaweza kusema Diamond na Lady jaydee ndio wanaongoza kwa mkwanja labda ni kwasababu ya uwekezaji wao wanaofanya na kila kukisha kutuonesha mapesa na magari wanaomiliki lakini sio mbaya ukamjua tajiri namba moja Tanzania na namba mbili kwa Afrika mashariki akiachwa na Sudhir Ruparelia kutoka Uganda mwenye utajiri wa bilioni  1.1 za kimarekani .
Diamond-Lady-jaydee
Anaitwa Rostam Aziz, 53 ndio bilionea pekee Tanzania. Anamiliki asilimia 35 ya mtandao wa Vodacom, Mtandao mkubwa zaidi nchini wenye watumiaji zaidi ya millioni 10.Pia Rostam anamiliki mgodi wa Caspian Mining.pia anamilikia asilimia fulani kwenye bandari ya Dar-es-salaam. Na pia anafanya biashara za nyumba nchi za Tanzania, Dubai, Oman and Lebanon. Rostam ana utajiri wenye thamani ya bilioni 1 za kimarekani.
Rostam-Aziz-Forbes-vibe-co-tz
Ikumbukwe kwamba Akon ndio msanii tajiri kuliko wote Afrika na utajiri wake ni dola za kimarekani milioni 80 na kwa mwaka huu ameanza kampeni ya kuzipa mwanga nyumba zaidi ya milioni moja katika nchi za afrika magharibi na afrika ya kati.
Akon
Tujiulize ni lini wasanii wa kibongo watafika level kama alizofika Akon na sio kwa kipato bali kwa ile hali ya kurudisha shukrani kwa jamii na kuacha kuturingishia utajiri wao.

Tuesday 4 March 2014

AJABU NA KWELI, CHATU AMSHINDA MAMBA NGUVU....


Nyoka huyo alijipinda kwa Mamba na kumbana hadi akafa

Nyoka alimvuta Mamba na kumtoa ndani ya Maji

Chatu huyo alianza kumla Mamba na kushangaza wakazi

Baada ya mlo huo mkubwa Nyoka alijiendea zake
Chatu ameshinda vita vikali dhidi ya Mamba Kaskazini mwa mji wa QueensLand, kupigana na Mamba, kumpinda na kisha kumla.
Tukio hilo lilishuhudiwa katika ziwa Moondarra, karibu na mlima Isa na kunaswa kwa kamera na wakazi wa eneo hilo siku ya Jumapili.

Nyoka huyo mwenye urefu wa futi 10, alijipinda kwa Mamba na kuanza kupambana naye majini.
Hatimaye, Nyoka huyo alifanikiwa kumshinda Mamba na kumtoa nje ya maji na kisha kumla.
Tiffany Corlis,mkazi wa eneo hilo, alishuhudia pambano hilo na kupiga picha hizi.
"lilikuwa jambo la ajabu sana, '' aliambia BBC
"Tulimuona Nyoka akipambana na Mamba , alifanikiwa kumbana mamba hasa katika sehemu ya miguu ya ili kumdhibiti.''
"Pambano lilianzia ndani ya maji. Mamba alikuwa anajaribu kuweka kichwa chake juu ya maji wakati mmoja ingawa Nyoka alikuwa amembana sana.''
"Baada ya Mamba kufa nyoka alijikunjua, na kuja mbele ya Mamba huyo na kuanza kumla,'' alisema Tifanny.
Bwana Corlis alisema kuwa ilimchukua nyoka muda wa robo saa kumla mamba huyo.
''Bila shaka Nyoka huyo alishiba vyema, na hatujui alikokwenda, baada ya mlo wake,'' alisema mama huyo ambaye hakutaka kusuburi kumuona Nyoka tena.
Mtu mwingine aliyeshuhudia pambano hilo Alyce Rosenthal, alisema kuwa wanyama hao wawili walipambana kwa karibu saa 5. Hatimaye wote walionekana kuchoka.
''Sio kitu unachoweza kuona kila siku,'' alisema Alyce.
BBC SWAHILI

TAZAMA PICHA YA MSANII LORD EYEZ AKIWA MBALONI KWA TUHUMA YA WIZI












































Msanii kutoka kundi La Weusi ‘Lord Eyez’ amekumbwa na Tuhuma ya wizi wa Laptop aina ya ‘Dell’ ikiwa ndani ya gari.
Utafiti huo ulimbaini msanii huyo akiwa na wenzake waliovunja kioo cha gari katika Hoteli ya Shiva ya jijini Arusha na kuiba Laptop aina ya Dell, baada ya wahusika kutoa taarifa kituo cha polisi na uchunguzi ulianza siku ya ijumaa.
Mtego huo ulipo kamilika na kugundulika ndipo Lord Eyez ndiye muhusika akakamatwa na Polisi usiku wa Jumamosi kuamkia Jumapili, hadi sasa msanii huyo bado yupo Lumande akiisaidia polisi

UNAAMBIWA TAJIRI NAMBA MOJA DUNIANI ATUA ARUSHA... BAJETI YAKE NI MARA NNE YA TANZANIA, AONGOZANA NA WATU 50 KIMYA KIMYA BILA MBWEMBWE




TAJIRI namba moja duniani, Bw. Mukesh Ambani (53) (pichani) raia wa India amewasili nchini jana alfajiri kimyakimya kwa safari ya
kitalii.

Tajiri huyo aliwasili juzi saa 10.15 alifajiri Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akiwa na ndege nne binafsi akifuatana na wafanyabiashara wakubwa zaidi ya 50.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na mmoja wa waratibu wa safari hiyo hapa nchini, Bw. Godfrey Famandes zimeeleza kuwa lengo la safari yake ni kutembelea hifadhi za taifa, hususan Hifadhi ya Serengeti.

Bw. Ambani kwa mujibu wa mitandao mbalimbali ya kimataifa ndiye tajiri namba moja akimiliki dola za Marekani bilioni 63.2 (zaidi ya sh. trilioni 90), akifuatiwa na Carlos Slim Helu kutoka Mexico mwenye dola za Kimarekani bilioni 62.2993 na Mmarekani William Bill Gates akifuatia kwa karibu akimiliki dola za Marekani bilioni 62.29.

Katika kundi hilo dogo la matajiri watano duniani nafasi ya nne inashikiliwa na Warren Buffett kutoka Mexico ambaye anamiliki dola 55.9 na kufuatiwa na Lakshmi Mittal wa India mwenye kitita cha dola bilioni 50.9.
 
Akizungumza na njia ya simu jana, Bw. Famendes ambaye ni Mkuu wa Oparesheni wa Kampuni ya Gapco Tanzania ambaye pia ndiye msemaji wa kampuni hiyo na mwenyeji wa
tajiri huyo, alikiri kuwasili kwa tajiri huyo na kusita kuzungumzia safari hiyo zaidi.

 Safari yenyewe ni ya binafsi zaidi, hivyo sina cha kukueleza zaidi ya kukuthibitishia kuwa ni kweli amewasili…sina uhakika na idadi ya wafanyabiashara aliofuatana nao, alisema Bw. Famendes kwa njia ya simu.

Habari zaidi kuhusiana na safari hiyo zimeeleza kuwa tajiri huyo pamoja na wenzake wamewasili Hifadhi ya Serengeti, ambayo ina hadhi ya urithi wa dunia, na tayari jana walifanya mzunguko wa kwanza wa kutembelea hifadhi hiyo na kujionea maajabu ya dunia ya hifadhi hiyo.
 
 Kuja kwa mfanyabiashara huyo na wenzake na fahari kubwa kwa Tanzania, kwani ni kielelezo kuwa tayari dunia imeanza kujua vivutio tulivyo navyo, nchini na umuhimu wake duniani, alisema mmoja wa wakurugenzi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) huku akisizitiza kuwa hana habari lakini akiahidi kufuatilia ujio huo.

Bw. Ambani alizaliwa Aprili 19 mwaka 1957, huko Aden (Colony of Eden) sasa Yemen akiwa na uraia wa India. Kwa sasa anaishi Antilia, Mumbai Maharashtra na mke wake Nita Ambani, wakiwa na watoto watatu, Akash, Anant na Isha

Alisoma Chuo Kikuu cha Mumbai na baadaye Stanford, Uingereza. Kwa sasa ni Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Reliance Industries chini ya Ambani Group of Campanies. 
 
 
CHANZO: MAJIRA

KWELI HALISI...HAWA NDIO WANACHAMA WA FREEMASON TANZANIA...!SOMA ZAIDI HAPA.....


Tanzania ina wanachama hai zaidi ya 600 wa kundi la watu wenye imani ya siri ya Freemasons wakiwa wanatokana na watu wa kada mbalimbali wakiwemo maarufu, huku ikielezwa kwamba miongoni mwao hakuna viongozi wakuu wa serikali.
Hayo yalibainishwa na Kiongozi wa kundi la Freemasons katika eneo la Afrika Mashariki, Jayantilal Keshavji Chande maarufu kama Sir Andy Chande.
Kiongozi huyo Mtanzania mkazi wa Dar es Salaam mwenye asili ya Kiasia, alisema licha ya Tanzania kuwa na wanachama hao, kwa sasa idadi ya wanachama duniani inapungua tofauti na inavyoonekana sasa kuwa wanaongezeka kutokana na kuibuka maneno mengi kuhusu kundi hilo. Alisisitiza kuwa si rahisi kumjua mwanachama wa kundi hilo, bali wenyewe ndio wanaofahamiana, akisema ni siri na kwamba wenyewe wanakutana katika vikao mbalimbali mara moja kwa mwezi au zaidi. 

Alisema nchini kuna wanachama zaidi ya 600 wakiwemo wafanyabiashara, watumishi serikalini, walimu pamoja na wanataaluma mbalimbali wanaoheshimika sana na kusisitiza kuwa kuna maneno mengi yanayosemwa kuhusu kundi hilo, ambayo siyo ya kweli. 

Alisema idadi ya wanachama wake duniani inazidi kupungua kutoka milioni nane hadi sasa wako milioni sita, tofauti na wengi wanaodhani kuwa idadi hiyo inaongezeka. 

Chande alizungumza na mwandishi wa habari hizi katika Shule ya Sekondari ya Shaaban Robert ambako yeye ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule alipozungumzia maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake.

Alisema duniani kuna watu wazito wengi ambao ni wanachama wa kundi hilo kama majaji wakubwa na hata Binamu wa Malkia Elizabeth wa Uingereza ni kiongozi mkubwa wa kundi hilo.

Akizungumzia masharti ya kujiunga na kundi hilo, Chande alisema ni lazima mwanachama huyo awe anaamini katika Mungu bila kubagua iwapo ni Mkristo au Muislamu.

Alisema pia ni lazima anayetaka kujiunga awe na umri unaozidi miaka 21 na walio chini ya umri huo hawaruhusiwi kujiunga na lazima familia ya anayetaka kujiunga na wanandugu wafahamu kuwa umejiunga na kundi hilo.

FREEMASON WATUA KANISANI,WAINGIA NA MKOBA WENYE VIFAA VYAO


WATU wanaodaiwa kuwa ni wa imani ya Freemason wametua ndani ya ibada katika Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima, Uwazi lina ‘ei tu zedi’ ya tukio hilo.
Baadhi ya vitu vilivyokutwa kanisani kwa Gwajima.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, Freemason hao wawili waliingia kwenye ibada hiyo iliyofanyika Februari 23, mwaka huu ndani ya kanisa hilo lenye makao makuu yake katika Viwanja vya Tanganyika Peckers, Kawe jijini Dar wakiwa na mfuko wa rambo wenye vitu mbalimbali vikiwa na alama zao.
GWAJIMA MADHABAHUNI
Habari zilidai kwamba wakati neno likiendelea kunenwa na Mchungaji Gwajima, watu hao walifunua mfuko huo ambapo baadhi ya waumini waliokuwa karibu yao walihoji kulikoni kuwa kwenye ibada na vitu vyenye viashiria ya Freemason.
Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima.
“Wengine tulishangaa sana kwani baadhi ya vitu vilionekana kuwa na thamani kubwa, tukadhani labda wameleta zawadi kwa mtumishi wa Mungu (Gwajima),” kilisema chanzo hicho ambacho kinaabudu katika kanisa hilo.
MFUKO WANASWA NA WALINZI
Mtiririko wa tukio hilo unazidi kuwekwa wazi kwamba, haraka sana walinzi wa kanisa hilo walifika eneo lenye mfuko huo na kuunasa huku watu walioingia nao wakipotea au kujichanganya miongoni mwa waumini wengine.
WASIWASI WATANDA
Kufuatia tukio hilo, baadhi ya waumini wa kanisa hilo walipozungumza na Uwazi baada ya ibada kumalizika walisema wanaamini watu hao walifika kanisani hapo kwa nia mbili, kujisalimisha au kuzijaribu nguvu za Gwajima ambaye ni maarufu kwa kuibua misukule.
Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima akiongoza ibada.
MFUKO WENYE VITU
Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa, ndani ya mfuko wa watu hao kulikutwa saa ya rangi ya fedha, pete ya dhahabu, cheni 2 za fedha, bangili, fulana nyeupe na shati jeusi, vyote vikiwa na picha zenye alama mbalimbali za Freemason kama mafuvu, nyoka na bikari.
“Lakini mimi naamini wale watu nia yao hasa ilikuwa kumjaribu mtumishi wa Mungu ambaye ni kinara wa kuwarudisha watu waliokufa katika mazingira ya mazingara (misukule),” kilisema chanzo kimoja na kujitambulisha kwa jina moja la Isaya.
IMANI KWA GWAJIMA YAKAZIWA
“Mimi ninavyomjua Gwajima sidhani kama wangefanikiwa, ni vigumu sana. Kuna majambazi waliwahi kujaribu kumuua lakini waliambulia patupu, wakapigwa na upepo wa kisurisuri, sembuse Freemason? Ninachokijua mimi watamjaribu lakini hawataweza,” kilisema chanzo kingine.
UWAZI MZIGONI, WALINZI WAWA MBOGO
Wakati sakata hilo likiendelea, mmoja wa waandishi wa Uwazi alipata taarifa ambapo aliwahi tukio hilo na kujaribu kupiga picha lakini mlinzi mmoja (jina tunalo) alimkataza licha ya kufanya jitihada kubwa.
Mlinzi huyo alimnyang’anya kamera mwandishi wetu na kuishikilia kwa muda huku akitishia kufuta picha zote hata kama hazikuwa za tukio hilo.
GWAJIMA KIMYA
Baada ya kuinyaka ishu hiyo nzima, Uwazi lilitumia siku tano kumsaka Mchungaji Gwajima ili kupata mtazamo wake juu ya tukio hilo ambalo huenda ni la kwanza kwenye kanisa hilo la kiroho jijini Dar es Salaam lakini bila mafanikio kutokana na kukwamishwa na wasaidizi wake.
Awali, ilikuwa Februari 25, mwaka huu ambapo hakupatikana kanisani kwake na hata kwa njia ya simu.
Baada ya kumkosa mtumishi huyo kwa kutopokea simu, Uwazi lilimtumia ujumbe wa simu (SMS) na kumuuliza kuhusu tukio hilo na ikiwezekana kukutana ambapo alijibu kwamba alikuwa kwenye kikao cha viongozi wa Kikristo, Kurasini jijini Dar, hivyo asingeweza kuonana na wanahabari.
Ijumaa ya Februari 28, mwaka huu, waandishi wa gazeti hili walitumia saa tano kumsubiri Gwajima kanisani kwake bila mafanikio.
MSIKILIZE MSEMAJI WAKE
Baadaye msemaji wa kanisa hilo, Mchungaji Yeconia Bihagaze alipoulizwa juu ya sakata hilo aliliambia gazeti hili kuwa, matukio kama hayo hutokea mara kwa mara licha ya kuchukua muda mrefu ikilinganishwa na hili la juzikati.
“Mambo ya Freemason kujisalimisha hapa mbona ni ya muda sana! Mimi naona kama yamepitwa na wakati, tukio hilo unalolisema mimi sijalisikia. Kanisa letu ni kubwa, mambo mengine ni madogomadogo hivyo siyo lazima yafike kwenye uongozi wa juu.
“Kwa nini msiandike misukule tunaowafufua hapa kila siku? Kwa nini msichukue matukio makubwa kwenye mtandao wa kanisa letu? Ninyi wanahabari wakati mwingine huwa mnatuvunjia heshima ndiyo maana huwa tunaamua kuwapotezea,” alisema Mchungaji Bihagaze. 

Monday 3 March 2014

Sikiliza Magazeti ya leo March 03 yakisomwa Redioni.


tv+studio+on+airKila siku kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa millardayo.com inakupa nafasi ya kusikiliza magazeti yakichambuliwa redioni,hii ni kwa sababu pengine muda wa kusikiliza magazeti ulikuwa busy kidogo hivy0 kwa kutumia teknolojia ya sasa nakurekodia na kukuwekea hapa.
Sikiliza kupitia 104.4 Clouds Fm Dodoma.
Bonyeza play kusikiliza.

U

MFANYABIASHARA MKUBWA WA MADAWA YA KULEVYA TANZANIA AKAMATWA


Dar es Salaam. Anti-drugs police have arrested a man believed to be the country’s most wanted drug kingpin. Ali Khatibu Haji, popularly known as Shikuba, was arrested at Julius Nyerere International Airport (JNIA) last Sunday after two years of an intensive manhunt. The 44-year-old is considered one of the most powerful and influential drug barons in Tanzania. He is said to be the leader of a cartel operating principally in East Africa but with a reach as far as China, Brazil, Canada, Japan, the United States and the United Kingdom.

He was charged last week with trafficking in a record 210 kilograms of heroin worth around Sh10 billion. Police seized the drugs in Lindi in January 2012 and have linked him with the haul. Shikuba reportedly fled to South Africa the same day the drugs were seized and has since been in hiding.

It is not clear how he sneaked into the country and managed to get a new passport but on February 28, the manhunt paid off. Investigators had been on his trail in Dar es Salaam before cornering him at the airport as he prepared to leave the country.

He had been at the airport for an hour before officers from the anti-drugs task force descended on him and arrested him at around 1 p.m. as he was about to board a South African Airways flight. The head of the Anti-Drugs Unit (ADU), Mr Godfrey Nzowa, told The Citizen on Sunday: “It’s true that we got him. His arrest is a major milestone in our efforts to nab the big fish. He is among the suspected powerful and influential traffickers.”

Entries in his passport indicate that Shikuba had in the past two years frequented Canada, the United Kingdom, the United States, China, Japan and Brazil. The passport was issued in Zanzibar in June last year.

Shikuba has also been charged with the murder in 2007 of a young Tanzanian who died in China after reportedly swallowing drugs. According to police reports, Shikuba used the victim as a courier. He was acquitted, though, after the Director of Public Prosecution dropped the charges for lack of sufficient evidence.

Two years later, officers from ADU arrested Shikuba and asked the Ilala district court to place him under the watch of the police and courts because they had reliable information that he was a notorious drug dealer operating in and outside the country. The court ordered him to report to ADU once a month for a year. One of the security officers who took part in the arrest told The Citizen on Sunday that the suspect was “big-headed” upon his arrest. He reportedly refused to cooperate with the police and told them he would only speak in court.

After his arrest, Shikuba was driven to Central Police Station under tight security. He was taken to Lindi the following morning and charged with trafficking in drugs.

The Citizen on Sunday has reliably learnt that authorities in US and UK are also on his trail over similar accusations. Shikuba was among 12 people appearing on the list of suspected notorious drug dealers released by a Tanzanian prisoner in Hong Kong last year. He is also among 122 suspected drug dealers who were arrested between 2007 and 2008 and put under court and police supervision.

Anti-drugs officials in Tanzania have for the past year intensified the war against drug trafficking and registered significant success at transit points such as airports. Dozens have been arrested in the past year at JNIA and Kilimanjaro International Airport. Early last month, authorities impounded 201 kilograms of heroin worth $5.5 million (Sh9 billion) hidden in an Iranian ship. The development came just a few weeks after the Canadian military ship Toronto impounded 265 bags of heroin weighing more than 280kgs aboard a vessel while patrolling the Indian Ocean