YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Thursday 18 April 2013

TUPIA MACHO UCHAFU UNAOTENDEKA COCO BEACH NI ZAIDI YA SODOMA NA GOMOLA...



Matukio yanayotokea Dar es Salaam usiku ni balaa, yaliyotendeka enzi za Sodoma na Gomora ni cha mtoto! Oparesheni Fichua Maovu ya Global  kwa mara nyingine imenasa ufuska wa ajabu unaofanyika katika Ufukwe wa Coco, Masaki jijini Dar usiku wa saa 9:00..

Timu ya Risasi ikiwa mzigoni mwishoni mwa wiki iliyopita, usiku tajwa hapo juu na kuendelea hadi kunakucha iliwakuta watu wa kada mbalimbali wakifanya ngono hadharani katika ufukwe huo.

UFUSKA NAMBA MOJA
 
Katika eneo la wazi lenye mwanga hafifu mchangani, walinaswa mwanamke na mwanaume wakifanya ngono kwa kupakatana bila kujali watu waliokuwa wakikatiza usiku huo kupunga upepo wa Bahari ya Hindi.


Wawili hao walisikika wakitoa miguno ya kimapenzi hadi waliposhtushwa na mwanga wa kamera.

NGONO LAIVU KWENYE GARI
 
Baada ya kutibua matukio mengine ya kifuska kutokana na mwanga wa kamera, kikosi kazi kiliondoka ufukweni na kwenda kutega kwenye maegesho ya magari.


Katika eneo hilo la maegesho, mwanaume na mwanamke walishtukiwa wakifanya mapenzi bila kujali watu waliokuwa wamelizunguka gari hilo aina ya Toyota Prado, ambalo halikuwa hata na vioo vyeusi (tinted) hivyo mchezo mzima ulishuhudiwa laivu bila king’amuzi hadi polisi wa doria walipofika na kuwagongea, wakaacha ‘kubanjuka’ kwa aibu.

AWAMU YA PILI MCHANGANI
 
‘Patroo’ ya timu yetu ilitimba kwa awamu ya pili upande wa baharini mchangani ambapo mabinti wa chini ya umri wa miaka 18 walibambwa na ‘mijibaba’ wakiwaridhisha kimapenzi bila kujali wengine ni sawa na baba zao.


Mita chache kutoka pale mabinti hao walipokuwa wakigawa dozi ya mapenzi kwa waliowatoroka wake zao majumbani, kulikuwa na wapenzi waliokuwa ‘wakidendeka’.

FUMANIZI
 
Wakati hayo yakiendelea eneo hilo, kule chini wanapouza mihogo kulisikika kelele za mwanamke aliyekuwa akilalamika kumfumania mumewe lakini kabla timu yetu haijafika wote walitimua na magari yao waliyokuwa wameyaegesha barabarani.

‘KUKU WATAMU’ WA KUMWAGA
 
Uchunguzi wetu ulibaini kuwepo kwa mashoga ‘kuku watamu’ wengi pale Coco ambao huzurula maeneo hayo kusaka wanaume.


Wengi wa mashoga hao ni vijana watanashati wa Kiarabu ambao tayari wameshaambukiza tabia hiyo kwa vijana wa Kitanzania.

USAGAJI
 
Habari za uhakika ni kwamba kuna wanawake wengi ambao hukusanyika eneo hilo usiku kucha wakisaka mabinti wadogo kwa ajili ya kukidhi haja zao za kimapenzi.


Ili kuthibisha hilo, Risasi Mchanganyiko ilishuhudia mwanamke mmoja akimchezea ‘kifua’ mwenzake huku wote wakitoa miguno ya kimahaba.

 
UBAKAJI
Uchunguzi huo ulibainisha kuwa mara kadhaa katika eneo hilo, wanawake hubakwa na vijana ambao wapo pale muda wote kwa ajili ya kuwafundisha kuogelea.

Kuna kisa cha hivi karibuni cha wasichana wawili ambao walileweshwa madawa ya kulevya, wakabakwa na baadaye walitelekezwa ufukweni hapo.

Uvutaji bangi na unga ufukweni hapo si jambo jipya kwani ukifika kule mchangani, unakaribishwa na harufu ya ‘kitu cha Arusha’.

Pamoja na ulinzi  kuimarishwa na jeshi la polisi bado kuna matukio mengine ya kutisha kama ukabaji, uporaji, biashara kubwa ya ngono na madawa ya kulevya.
Global publisher

PICHA ZA DIAMOND AKILA BATA NA BAADHI NDUGU NA JAMAA ZAKE JANGWANI SEA BREEZ WEEKEND HII HIZI HAPA







ESMA PLATNUM....
QBOY SHEM LAKE......
FARIDAH & QBOY MNYAMA.....

Huyu ni mama wa makamo.....aliposikia diamond yupo pande hizi akusita
 kuja
HATUNA TATIZO NA MTU....


PEACE N LOVE...!!




HAPPY FOREVER ......!!






Baada ya kumaliza kuogelea ikawa time ya kupata soft drink kabla ya kupata
chakula.....
watu wakifanya yao kwenye maswala ya makulaji....!!
muziki aukuwa nyuma nao....watu walicheza bila kikomo....!!

BREAKING NEWZ!!! MLIPUKO TENA WATOKEA MAREKANI TEXAS



Mamia ya watu wanahofiwa kufariki kutokana na mlipuko huo
Zaidi ya watu 100 wamejeruhiwa katika mulipuko uliotokea kwenye kiwanda cha mbolea kilichoko Kaskazini Magharibi mwa eneo la Waco, jimbo la Texas. Wengi wamekwama ndani ya majengo yanayendelea kuteketea kufuatia mulipuko huo.
Meya wa Mji kulitokea mulipuko huo, Tummy Muska ameelezea kutokea moto mkubwa uliolipuka sawa na bomu. Mulipuko huo umeharibu majengo ya kiwanda hicho, makaazi ya karibu kikiwemo kituo kimoja cha afya.
Wazima moto, magari ya kubebea wagonjwa na helikopta sita zimetolewa kushughulikia majeruhi na kutuliza hali ya sasa.
Majengo kadhaa yameendelea kuteketea karibu na kiwanda hicho cha mbolea.Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinasema zinasea kuna watu waliopoteza maisha.
Dean Wilson wa idara ya usalama ya Texas amesema nyumba 75 karibu na jengo hilo ziliharibiwa kabisa.
Amesema kufikia sasa hawezi kuthibitisha vifo vyovyote. Watu 38 wameripotiwa kua katika hali mahututi. Makundi ya wokozi yameanza kufika nyumba hadi nyingine kuwaokoa majeruhi na kutoa huduma ya kwanza.
Kituo cha Dharura kimewekwa kwenye uwanja wa mpira ulioko karibu.Gavana wa Texas amesema afisi yake imetoa raslimali zake kusaidia katika juhudi za wokozi.

Wednesday 17 April 2013

AJARI!!! AJARI!!!! WATU watatu wamefariki dunia na wengine wawili wa familia moja kujeruhiwa baada Gari aina ya Scania kuvamia Nyumba yao wakiwa ndani jana Usiku. Ilongo wilayani Mbarali mkoani Mbeya


Gari aina ya scania yenye nambali za usajiri T578 ALS likiwa na tela nambli T125 AGM lililobomoa nyumba na kusababisha vifo vya watu 3 wa familia moja

Tunaomba radhi kwa kuonyesha picha hizi hii ni miili ya watu walifariki kwa gugongwa na roli hilo













Wananchi wa kijiji cha Ilongo wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya wakiwa msibani
WATU watatu wamefariki dunia na wengine wawili wa familia moja kujeruhiwa baada Gari aina ya Scania kuvamia Nyumba yao wakiwa ndani jana  Usiku. Ilongo wilayani Mbarali mkoani Mbeya
  
Tukio hilo lilitokea jana majira ya saa Tatu na Robo usiku katika Kijiji cha Ilongo Wilaya ya Mbarali Mkoani hapa.


Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, Barakael Masaki amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa ajali hiyo ilihusisha  magari kugongana na kugonga nyumba na kusababisha vifo na majeruhi.


Alisema chanzo cha ajali kilitokana na Gari lenye namba za usajili T578 ALS likiwa na tela lenye namba za usajili T125 AGM aina ya Scania likiendeshwa na dereva ambaye hakuweza kutambulika liligonga  kwa nyuma  gari lenye namba T959 ASC aina ya Scania.
  
Alisema gari hilo lilikuwa likiendeshwa na dereva Juhudi Saimon(34)Mnyiha mkazi wa Dar Es Salaam kisha gari hilo  kugonga nyumba mali ya Matia  Mwagala mkazi wa Kijiji cha Ilongo.
  
Aliwataja matrehemu kuwa ni Asia Yahaya (52)mkulima na Msangu, Abubakari Yahaya(8) Msangu na mwanafunzi darasa la pili  aliyekuwa anasoma katika Shule ya msingi Ilongo na Fatuma Yahaya (6) Msangu mwanafunzi wa darasa la kwanza  Shule ya Msingi Ilongo wote wakazi wa kijiji hicho.

Aidha aliwataja majeruhi wa ajali hiyo kuwa ni pamoja na Abuu  Fadhil (22)Mzigua mkazi wa Dar Es Salaam ambaye ni tingo wa gari lililogonga Nyumba pamoja na Steven  Chiwa (26) mbembe raia na mkazi wa Nchi jirani ya Zambia ambaye ni msindikizaji wa gari hilo ambao wamelazwa katika Hospitali ya Misheni ya Chimala.
  
Hata hivyo wa dereva wa gari lililosababisha ajali alikimbia na gari mara baada ya tukio ambapo Kaimu Kamanda  anatoa rai kwa yeyote mwenye taarifa juu ya mahalialipo dereva wa gari lililosababisha ajali hiyo azitoe katika mamlaka husika ili akamatwe na sheria ichukue mkondo wake, vinginevyo ajisalimishe mara moja.
  
Wakati huo huo  Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya linamshikilia  Asajile Mwamtina (46) mkazi wa kijiji cha Syukula Wilaya ya Rungwe mkoani hapa akituhumiwa kufanya mapenzi na binti yake wa miaka 13.
  
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa lilitokea juzi  majira ya saa Kumi na Mbili jioni baada ya kumvizia binti huyo (jina limehifadhiwa) ambaye aliacha shule akiwa darasa la tano mwaka 2011 kwa matatizo ya ugonjwa wa kifafa akiwa anapika.
  
Alisema mtuhumiwa alipata mwanya wa kufanya unyama huo kutokana na mkewe  ambaye  mama mzazi   wa mhanga huyo Tumikigwe Samalinga akiwa kijiji cha Kiwira kuuguza mgonjwa na kuongeza kuwa taratibu za kumfikisha mahakamani zinafanyika.
  
Aidha katika tukio lingine eneo la Makunguru Jijini Mbeya Vyumba 12 vya biasharaa viliteketea kwa moto jana majira ya saa Tano asubuhi vilivyokuwa vimetoka kujengwa  mali ya Dominick Mbinga Mkazi wa Dar Es Salaam.


Hata hivyo hakuna madhara ya kibinadamu yaliyojitokeza baada ya moto huo kudhibitiwa kwa ushirikiano baina ya kikosi cha zima moto na uokoaji na wananchi.


Thamani halisi ya uhalibifu bado kujulikana pamoja na chanzo ingawa kwa mujibu wa majirani walisema inawezekana ikawa ni hitilafu ya umeme kutokana na muda huo wapangaji wa nyumba hiyo kutokuwepo wakati moto ukitokea ambao ulijulikana baada ya majirani kuona.

YALIYOJIRI KWA PICHA KWENYE MSIBA WA BI. KIDUDE NYUMBANI KWAKE


 Gari ikiwa na Mwili wa marehemu Bi. Kidude ukiusafirisha kutoka katika Kijiji cha Kihinani kuupeleka nyumbani kwake Rahaleo kwa matayarisho ya mazishi kesho mchana na kuzikwa Kitumba. Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.(Picha zote kwa hisani ya Othman Maulid wa ZanZinews)
 Mwili wa marehemu ukishushwa katika gari wakat ukiwasili nyumbani kwake Rahaleo kwa taratibu za mazishi kesho mchana na kuzikwa Kitumba.
Ndugu na Jamaa wakiubeba mwili wa marehemu Bi.Kidude wakati ulipowasili nyumbani kwake Rahaleo kwa ajili ya mazishi  kesho.
Mrajisi wa Baraza la Sanaa Zanzibar Khadija Batashi akizungumza na Waandishi jinsi alivyoupokea msiba wa Bi. Kidude
 Matayarishi ya mazishi ya Bi. Kidude yakitayarishwa katika Nyumba yake Rahaleo.
 Mjuukuu wa Bi Kidude Omar Ameir akiwasiliana na jamaa kuwajulisha msiba wa Marehemu Bi. Kidude, baada ya kuwasili katika nyumba yake kwa matayarisho ya mazishi kesho mchana saa saba baada ya sala ya adhuhuri na kuzikwa Kitumba.   
 Bi.Maryam Hamdani akilakiwa na Bi Sihaba baada ya kuwasili katika makazi ya bikidude rahaleo , akiwa na majonzi.  
 Waandishi wa habari wakizungumza na Mfadhili Mkubwa wa Bi Kidude Maryam Hamdan,kuhusiana na marehemu ambaye yeye alikuwa ni mtayarishaji na mratibu wa safari za Bi Kidude nje ya Nchi katika matamasha mbalimbali aliyokuwa akihudhuria nje ya nchi katika uhai wake.
Meneja wa Sauti ya BUSARA Zanzibar Stella Steven, akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na marehemu Bi Kidude ambaye alikuwa akidhaminiwa na BUSARA katika matamasha mbalimbaliyaliokuwa yakiandaliwa na Busara.jinsi walivyopokea kifo chake kwa masikitiko makubwa na kuacha pengo katika tasnia ya muziki wa taarab asilia Zanzibar.