YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Thursday 30 August 2018

KATIBU MKUU WA CCM DR. BASHIRU AUNGURUMA


August 30, 2018 Katibu Mkuu wa CCM Dr. Bashiru Ally amesema kuwa amemuita mmoja wa mawaziri wa Serikali ya awamu ya tano aeleze kuhusu tuhuma za kumiliki ardhi ya ekari elfu moja (1,000) ili aeleze amezipataje.
Nilikuwa Morogoro akatajwa Waziri mmoja kuwa ana ekari elfu moja watu wanataka kujua amezipataje, na nitamuita anieleze amezipataje. Hatuwezi kuwa na viongozi ndani ya chama tunachokiita chama cha wanyonge alafu baadhi yetu tunapora ardhi ya wanyonge. Ni suala la kuchagua kati ya kuwa kiongozi wa CCM au kuwa mporaji wa ardhi.” –Dr. Bashiru Ally

DC MURO APATANISHA WACHUNGAJI NA MAASKOFU ARUMERU


Leo August 30 2018 Serikali imemaliza mgogoro wa Kanisa la African Mission Evangelism Church ( AMEC TANZANIA ) Arusha uliodumu kwa zaidi ya miaka 13.
Kumalizika kwa mgogoro huo kunatokana na viongozi wakuu wa kanisa hilo waliokuwa kwenye mgogoro kukubaliana kumaliza tofauti zao baada ya serikali kuamua kuingilia kati kulinusuru kanisa hilo.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro amesema mgogoro huo haukuwa na tija kwa kanisa wala wananchi waliokuwa wakipata Huduma za kiroho na ulihatarisha amani na usalama kwa waumini wa kanisa.
Pia amesema mahusino mabovu ya serikali na kanisa hilo yamechangia kudhoofisha kanisa hilo Tanzania kwa zaidi ya miaka 13.
DC Muro amewapongeza viongozi wakuu wa kanisa hilo kwa kukubali kukaa katika Meza ya mazungumzo na kumaliza tofauti zao, ambapo amewataka viongozi hao wakuu kufanya ibada ya pamoja ya toba ambayo itawahusisha waumini wote wa kanisa hilo.
Serikali ya Rais John Magufuli itayalinda makubaliano haya pamoja na kuwapa ushirikiano wa kutosha katika kutekeleza majukumu yenu,”amesema.



MAKUNDI YA UEFA CHAMPIONS LIGUE HAYA HAPA


Staa zamani wa club ya Man United ya England ambaye anaichezea club ya Juventus ya Italia kwa sasa Cristiano Ronaldo atarudi kucheza katika nyasi za uwanja wa Old Trafford kwa mara ya nyingine tena  msimu huu wa 2018/19.
Cristiano Ronaldo ambaye aliondoka mara ya mwisho Old Trafford kama mchezaji wa Man United mwaka 2009 na kujiunga na club ya Real Madrid ya Hispania hivyo leo baada ya kuchezeshwa droo ya makundi na Man United kupangwa Kundi H na Juventus atarudi tena hapo.
Ronaldo atarudi Old Trafford kucheza mechi yake ya makundi akiwa na Juventus ambao amejiunga nayo msimu huu akitokea Real Madrid, hivyo kupangwa kwao Kundi H na timu za Man United, Valencia na Young Boys kutampa nafasi ya kucheza tena Old Trafford.

Makundi yote ya UEFA Champions League msimu wa 2018/2019.

KWENYE MTANDAO WA TWITTER MBUNGE NAPE ANENA HAYA.


Mbunge wa Mtama Nape Nnauye ameandika katika ukurasa wake wa Twitter asubuhi ya leo August 31, 2018 “Barabara inapokua na shida, usikate tamaa na kuacha safari. Badili viatu na kusonga mbele!”
Alichoandika Nape wengi hawajafahamu ana maanisha nini? ila aliambatanisha na picha yenye maneno ya kizungu ambayo yeye aliyatafsiri katika caption.