YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Thursday 30 August 2018

DC MURO APATANISHA WACHUNGAJI NA MAASKOFU ARUMERU


Leo August 30 2018 Serikali imemaliza mgogoro wa Kanisa la African Mission Evangelism Church ( AMEC TANZANIA ) Arusha uliodumu kwa zaidi ya miaka 13.
Kumalizika kwa mgogoro huo kunatokana na viongozi wakuu wa kanisa hilo waliokuwa kwenye mgogoro kukubaliana kumaliza tofauti zao baada ya serikali kuamua kuingilia kati kulinusuru kanisa hilo.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro amesema mgogoro huo haukuwa na tija kwa kanisa wala wananchi waliokuwa wakipata Huduma za kiroho na ulihatarisha amani na usalama kwa waumini wa kanisa.
Pia amesema mahusino mabovu ya serikali na kanisa hilo yamechangia kudhoofisha kanisa hilo Tanzania kwa zaidi ya miaka 13.
DC Muro amewapongeza viongozi wakuu wa kanisa hilo kwa kukubali kukaa katika Meza ya mazungumzo na kumaliza tofauti zao, ambapo amewataka viongozi hao wakuu kufanya ibada ya pamoja ya toba ambayo itawahusisha waumini wote wa kanisa hilo.
Serikali ya Rais John Magufuli itayalinda makubaliano haya pamoja na kuwapa ushirikiano wa kutosha katika kutekeleza majukumu yenu,”amesema.



No comments:

Post a Comment

gfjythfghgfhdfgergdfgbvdfgrfdgdfrgdrgdfrgrdegedrgdrfg