YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Saturday 1 September 2012

WAASI WATEKA NA KUHARIBU VITUO CHA NDEGE ZA JESHI SYRIA



 

SYRIA,
Waasi wameteka kituo kimpja cha jeshi la anga la Syria na kuharibu vituo vingine viwili mashariki mwa Syria asubuhi ya leo. Mashambulizi hayo yamekuwa ni ya kulipiza mashambulizi ya majeshi ya serikali ambayo kwa sasa yameongeza masahambulizi ya anga dhidi ya waasi hao.

Kwa mujibu wa mashuhuda Waasi hao wameteka kituo cha ndege za kijeshi na kuwakamata mateka 6 na vifaa vya kijeshi katika jimbo la Deir al- Zor karibu na mpaka wa nchi hiyo na Uturuki huku pia wakishambulia na kuaribu vituo vingine viwili vya Hamdan na Albu Kamal mashariki mwa Syria karibu na mpaka wa nchi hiyo na Iraq.

Katika taarifa nyingine imedaiwa kuwa waasi hao wameitungua na kuiangusha helkopta ya kijeshi pamoja na ndege aina ya Jet Fighter zote za jeshi la serikali.

Waasi wameendeleza mashambulizi dhidi ya majeshi ya serikali ambayo yameongeza kasi ya kuwashambulia kwa ndege baada ya kupata upinzani mkubwa katika mapigano ya ardhini.

Rais Al Assad amekuwa katika upinzani mgumu kutoka kwa wananchi na sasa waasi kwa takribani miezi 17 ambapo watu zaidi ya 20,000 wameuawa.

No comments:

Post a Comment

gfjythfghgfhdfgergdfgbvdfgrfdgdfrgdrgdfrgrdegedrgdrfg