YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Saturday 7 September 2013

JINSI MSANII BATULI ALIVYONASWA LIVE NA SLIMU OMARY WAKIWA SEHEMU TATA....!!


Msanii wa bongo movie Yobi nesh au Batuli katika pozi
 Hivi ndivyo thesuperstarstz ilivyowanasa wasanii hawa maarufu katika maeneo ambayo ni ngumu kuwakuta wawili hao,mwanzoni mwandishi wa habari hizi alijua wana rekodi filamu ila alipowasogelea  akagundua hapakuwa na kamera yoyote katika eneo lile kitu kilichompa maswali mengi sana na kujikuta akipata hamu ya kutaka kujua kulikoni wawili hawa kuwa close namna ile.

Mwandishi wa tsstz alijibanza asijulikane kama yupo eneo lile na hapo alimshuhudia slim omari msanii wa bongo movie akizidi kumsomesha Batuli ili akubaliane na anachomueleza japo hatukupata bahati ya kusikia walichokuwa wanaongea kwani wangejua nipo eneo lile.

Mara baada ya kupata picha za uhakika thesuperstarstz iliwafuata wawili hao na walipomuona muandishi wetu waliachina mikono haraka na kuanza kucheka huku slimu akionyesha kutokuamini kama  amebambwa na muandishi wetu na kisha wakaondoka haraka eneo lile nakuingia katika mlango flan kwa staili ya kumkwepa muandishi wetu na tulipowafuata tulizuiliwa na ungozi wa eneo lile kwa madai ya kuwabuguthi wateja wao.
Hapa ni mwanzo Batuli alionekana kufurahiya maneno ya slimu
Bado thesupestarstz inalifuatilia swala hili kwa kina kutaka kujua kulikoni maana hata simu hawapokei hata tulipojaribu kubadili namba tulimpata Batuli na tulipomsomea mashtaka yake alicheka na kusema wacha zako bwana hiyo ni kikazi zaid wala hakuna jipya  tulipombana zaidi alisema tumtafute hawezi kuongea kwenye simu
baada ya kukata simu tulipigiaslimu na  kwa upande wake hakutaka kupokea simu yetu
Hapa Slim Anaonyesha aliongeza utamu wa maneno na kumfanya Batuli aanze kuingia mkenge kwa maneno yake
Endelea kuwa nasi tutahakikisha tunakuletea kilichojiri kwani kazi yetu ni kukupa habari popote pale ulipo nataka ujue hii sio filamu mdau ni tukio la kweli kaaa na sisi

No comments:

Post a Comment

gfjythfghgfhdfgergdfgbvdfgrfdgdfrgdrgdfrgrdegedrgdrfg