YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Friday 3 August 2018

MOISE KATUMBI AZUIWA KUINGIA DR CONGO

Moise Katumbi aliondoka DRC mnamo Mei 2016, siku moja baada ya kutolewa waranti ya kukamatwa kwake
Haki miliki ya pichaREUTERS
Msafara wa kiongozi wa upinzani nchini DR Congo Moise Katumbi umerudi nchini Zambia baada ya serikali ya DR Congo kumzuia kuingia nchini humo.
Alikuwa amekwama mpakani kati ya mataifa hayo mawili kwa saa kadhaa .
Mwandani huyo wa karibu wa rais Kabila amekuwa akiishi mafichoni kwa miaka miwili na alikuwa na matumaini ya kurudi nyumbani ili kuwania urais.
Awali kiongozi huyo alikuwa amevuka na kuingia eneo lisilodhibitiwa na nchi yoyote kati ya mpaka wa zambia na taifa la DR Congo huku maelfu ya wafuasi wake wakielekea katika eneo hilo kumlaki.
Alikuwa katika mji wa Kasumbalesa, kulingana na mwandishi wa BBC Anne Soy. Awali tuliwanukuu wafuasi wake wakisema kuwa alikuwa amevuka mpaka na kuingi nchini DR Congo.
Mji wa Kasumbalesa upo takriban kilomita 95 karibu na nyumbani kwao Lubumbashi.
Vikosi vya DR Congo vilifyatua risasi hewani kuwatawanya wafuasi wake waliosubiri kumkaribisha akijaribu kuvuka mpaja kulingana na mwandishi wa BBC Poly Muzalia.
Wafuasi wake wanasema alikuwa amevuka mpaka na kuingia nchini humo akiabiri gari lililotoka Zambia licha ya utawala wa taifa hilo kutishia kumkamata iwapo angejaribu kurudi nyumbani.
Kundi la chama cha bwana Katumbi Ensemble pour le Changement, lilichapisha kanda ya video ya bwana katumbi akiwa katika eneo la Kasumbalesa , mji wa mpakani nchini DR Congo.
Moise Katumbi, alikuwa amezuiwa kurudi nchini kugombea urais katika uchaguzi mkuu Desemba mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

gfjythfghgfhdfgergdfgbvdfgrfdgdfrgdrgdfrgrdegedrgdrfg