YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Sunday 3 March 2013

Matukio punde yanapojiri:Uchaguzi Kenya



 4 Machi, 2013 - Saa 05:31 GMT
Wapiga kura tayari kwa foleni katika mtaa wa Kibera
Hii leo wakenya wanapiga kura katika uchaguzi wa kihistoria chini ya katiba mpya. Foleni tayari zimeanza kushuhudiwa katika vituo.
Kinyang'anyiro ni kikali kati ya Muungano wa Cord na Jubilee wa Raila Odinga na Uhuru Kenyatta.
Kwenye ukurasa huu tutakupasha matukio kila yanapojiri hadi upigaji kura utakapokamilika mwendo wa saa kumi na moja jioni.
Unaweza kututumia maoni yako kuhusu uchaguzi unavyokenda kwenye ukursa awetu wa Bofyafacebook

08:30 @smugera anasema kwamba kupiga kura kunachukua takriban dakika 12 minutes. #bbcnewsday
08:25 Hassan Majid pia mwandishi wa BBC anasema kuwa polisi wamepata mwili mmoja wa mtu aliyeuawa na mwingine kujeruhiwa kwa kukatwa panga katika eneo la Moshomoroni

08:24 Mwandishi wa BBC mjini Mombasa, Karen Allen anasema kuwa polisi wamepata maiti za polisi wanne ambao wameuawa katika eneo la eneo la Changamwe , Kaskazini mwa Mombasa. Hana taarifa zaidi kwa sasa

08:16:Frawaso Kimutai kupitia Bofyafacebook yuko katika kituo cha Menengai mjini Nakuru kura ilianza kupigwa saa moja asubuhi na foleni ni ndefu ingawa inakwenda polepole mwendo wa kobe
08:15: Fatma Sanbur yuko mtaani Kibera na anasema watu ni wengi sana lakini hakuna mbinu ya kupanga foleni. Anasema watu wanapangwa kwa orodha ya majina na hata baada ya saa moja tangu waanza kupangga foleni saa kumi na moja, shughuli yab upigaji kura ilikuwa haijaanza

07:11 James Mwangi: Kwenye ukurasa wa Facebook wa Bofyabbcswahilianasema yuko kwenye foleni na habanduki
07:14 Hison Nyakundi : Yuko mjini Eldoret kwa Foleni tayari kupiga kuraBofyabbcswahili
07:24 Kips Oscar: Kupitia Facebook yuko katika kaunti ya Marsabit anasema upigaji kura unaendelea bila wasiwasi na kuwa wanatarajia shughuli itakamilika kwa muda bila wasiwasi
Usalama ulidhibitiwa asubuhi na mapema wakati upigaji kura ulipoanza
07:28: Mgombea mwenza wa Uhuru Kenyatta, William Ruro amepiga kura mjini Eldoret

07:32: William Ruto anasema kuwa anajivunia uchaguzi wa Kenya unafanyika kwa amani licha ya dukuduku la wengi. Anasema anawataka wapinzani kukubali matokeo ya uchaguzi vyovyote matokeo hayo yatakavyokuwa.

07:43 Upiga kura bado haujaanza katika baadhi ya sehemu za Kenya. Wapiga kura wanalalamika kuwa katika vituo kadhaa tarakilishi zimegoma na kwa hivyo watasubiri muda kabla ya kupiga kura zao

07:47 Eco Seyar Papa akiwa mjini Nairobi anasema Wakenya wamejitokeza kwawingi jijini Nairobi katika eneo la Dagoreti. Foleni zilianza kupigwa kuanzia saa tisa usiku tangu kuanzishwa kwa demokirasia ncini Kenya watu waeneo hili hawajawai kujitokeza kwa mapenzi kama inavyo onekana.
07:50 Mwandishi wa BBC Ann Mawathe yuko mjini Kisumu na anasema ameona foleni ndefu sana watu wakiwa hamasa kupiga kura. Wamepiga foleni tangu saa nane usiku.

Foleni ya watu mjini Mombasa
07:52 Mombasa eneo la Kaloleni mpiga kura mmoja amesema hadi kufikia sasa upigaji kura haujaanza kwani maafisa wa tume ya uchaguzi bado hawajawasili na vifaa vyao

No comments:

Post a Comment

gfjythfghgfhdfgergdfgbvdfgrfdgdfrgdrgdfrgrdegedrgdrfg