YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Friday 7 September 2012

MBWIGA NA SHAFFIH WASHINDWA KUTAMBIANA MJINI TABORA.



Mchezo maalum wa kuzipatanisha timu za Rhino Rangers na Police za hapa mjini Tabora umemalizika kwa timu hizo kufungana bao 1:1.
Mchezo huo ulioandaliwa na kampuni ya Clouds Media Group ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za tamasha la Fiesta linalotarajiwa kufanyika jioni ya leo kwenye uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora.
lengo la kuzikutanisha timu hizo lilikua ni kuondoa uhasama uliokuwepo hapo awali baina ya timu hizo mbili uliokuwa umedumu kwa muda sasa,watangazaji wa vipindi vya michezo vya Clouds Media Group bwana Shaffih Dauda (Polisi ) na Mbwiga Mbwiguke (Rhino Rangers ) walizichezea timu hizo ikiwa ni sehemu ya kuonyesha kwamba upinzani kwenye mchezo wa soka huwa ni uwanjani na mara baada ya hapo maisha mengine huendelea kama kawaida.
Lengo lingine la mchezo huu lilikua pia kuzichangia timu hizi pesa kwa ajili ya maandalizi ya ligi daraja la kwanza inayotaraji kuanza siku chache zijazo,o.
mapato ya mchezo huo yalikuwa ni Tsh 1,2170,000 kutokana na kiingilio cha tsh 1,000 kwa wakubwa na 500 kwa watoto.

    Dauda na Mbwiga wakisalimiana kabla ya mchezo.

   Hapa huyu jamaa alijipendekeza nikampiga kikoi kwa kutumia guu langu la dhahabu kama unavyoona hapo.
    Mbwiga kama anapigaaaaaaaaaa, anafinyaaaaaaaaaaaa
    sehemu ya mashabiki waliohudhulia mpambano huo.


   Bonge nae alikuepo kushow luv na wadau wake.
    Mgeni wa heshima akiikagua Rhino Rangers




 Hapa nilikua nawaeleza wachezaji wa timu zote mbili dhumuni hasa la mchezo huu!
 Kikosi cha Shaffih (POLICE TABORA )

No comments:

Post a Comment

gfjythfghgfhdfgergdfgbvdfgrfdgdfrgdrgdfrgrdegedrgdrfg