YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Thursday 11 April 2013

MAMBO 10 MUHIMU YA KUFAHAMU KUHUSU shuledirect.co.tz YA FARAJA NYALANDU

0
.
Naibu Waziri wa Elimu Philipho Mulugo ndio alikua mgeni rasmi.
1. Faraja Nyalandu ambae alikua Miss Tanzania 2004 maarufu kama Faraja Kota ndio mwanzilishi wa mfumo wa Wanafunzi Tanzania  kujisomea masomo mbalimbali kupitia Internet kupitia shuledirect.o.tz .
2. Ni mfumo wa kitaaluma wa Wanafunzi, ni zaidi ya mtandao wa kawaida kwa sababu pamoja na kwamba ukiingia unaweza kusoma masomo mbalimbali, pia unaweza kuchat na watu mbalimbali, 3. Masomo yanayopatikana ni ya Sekondari kuanzia form I mpaka IV.
4. Mwanafunzi anayo nafasi ya kuchat na walimu, kuuliza maswali na kujibiwa, 5. Mpango wa kuongeza walimu upo, kwa sasa wako tisa ambapo kila mmoja anayo degree na uzoefu usio wa chini ya miaka mitano, 6. Kutakua na Quiz ambayo Mwanafunzi anaweza kujibu na ikasahihishwa na Walimu na kurudishiwa majibu.
7. Wizara ya Elimu imeridhia na kuipa baraka zote shuledirect.co.tz  8. shuledirect.co.tz ni huduma ya bure kwa kila mmoja, kinachotakiwa ni kujisajili tu, 9. Vinapatikana vitabu ambavyo wakati mwingine sio rahisi kupatikana mtaani, 10. kutakua kukifanyika mashindano kwenye sehemu mbalimbali ikiwemo mijadala nia ikiwa pia ni kuitangaza zaidi shuledirect.co.tz
.
.
Kama na wewe umeguswa kumsupport Faraja, naomba nione like yako hapo chini pamoja na tweet yako ya hii post…. kwa info zaidi pia unaweza kumsikiliza Faraja Nyalandu akiongea hapa chini…

No comments:

Post a Comment

gfjythfghgfhdfgergdfgbvdfgrfdgdfrgdrgdfrgrdegedrgdrfg