YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Tuesday 9 April 2013

R.I.P BROTHER:MAZISHI YA MWANANCHUO ALIYESOMA UDOM ''FRANK CHAULA'' (BA-ECONOMICS) YANAFANYIKA KESHO TAREHE 10/04/2013


 
Marehemu Frank Chaula enzi za uhai wake

Alikukuwa  amemaliza shahada ya kwanza ya UCHUMI katika  CHUO KIKUU CHA DODOMA mwaka 2011/12. Baada ya kumaliza chuo alipata kazi katika benki ya AccessBank Tanzania Limited kitengo cha Loans Officer lakini ndoto yake ilikuwa bado akaamua kwenda kujiunga na JKT ambapo alipangiwa kwenda kushiriki mafunzo ya jeshi huko Tabora na ndipo mauti yalipomkuta. 
Kufuatana na msiba wa ndugu yetu  pendwa FRANK/GOD CHAULA ukiwa kama classmate/Rafiki/Ndugu/Schoolmate unaweza kutuma rambirambi yako kupitia M-PESA YA JORAM KIBONA 0752494763 AU KWA TIGO PESA 0712867869 YA GABRIEL ULAYA na pia mazishi yanatarajia kufanyika kesho tarehe 10/04/2013  katiaka kijiji cha Ilembo kata ya Vwawa, Wilaya Mbozi, mkoani Mbeya.

Kiukweli kama mimi mpaka sasa siamini kama Frank Chaula ametutoka maana nakumbuka mwezi wa pili niliwasiliananae akaniambia yuko benki ila ndoto yake anataka kuwa mwanajeshi. Na pia nimesoma naye couse za uchumi.
 

Kama unataka kumjua zaidi bofya hapa

Uongozi wa PAMOJAPURE BLOG unaungana na familia ya marehemu Katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao FRANK CHAULA
 
Bwana ametoa Bwana ametwaa Jina lake Lihimidiwe.

No comments:

Post a Comment

gfjythfghgfhdfgergdfgbvdfgrfdgdfrgdrgdfrgrdegedrgdrfg