YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Tuesday 2 September 2014

SAKATA LA MKE WA KAMANDA BARLOW, MAPYA YAIBUKA!



Sakata la madai kuwa mke wa aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, Stella Barlow (pichani)alitimuliwa ukweni kwa mapanga limechukua sura mpya baada ya ndugu wa mumewe kuibuka na kutoa ufafanuzi.
Mjane Stell Barlow wakati wa mazishi ya aliyekuwa mume wake, Kamanda Liberatus Barlow.
 Akizungumza kwa njia ya simu mwishoni mwa wiki iliyopita, ndugu wa marehemu Kamanda Barlow, aliyejitambulisha kwa jina moja la Lyimo alisema si kweli hata kidogo kuwa walimkimbiza kwa mapanga shemeji yao huyo. 
“Kilichotokea ni kwamba tulimuambia huyo mama kuwa hawezi kufanya chochote kwenye kaburi la mumewe mpaka akamuone kiongozi wa ukoo. Kimila tangu wakati kaburi linachimbwa, linakuwa chini ya uangalizi wa wanaume na hata baada ya kuzika haliwezi kuwa chini ya mwanamke, hilo tulimjulisha,” alisema Lyimo.
Kamanda Barlow enzi za uhai wake.
 Alifafanua kuwa wamewahi kufanya misa ya kumuombea marehemu Barlow na ndugu wengine na mama huyo aliarifiwa lakini hakuja. “Ujumbe wetu ni kwamba muambieni huyo mama  kuwa siyo vizuri kuchafua ukoo kwa sababu hatuna ugomvi naye na hakika kama ni wa kulaumiwa ni yeye siyo sisi wana ukoo,” alisema Lyimo.

NGOMA MPYA KALI: USHAWAHI MSIKIA DIAMOND AKICHANA?! HUYU HAPA AKIWA AKIWA NA GODZILLA!



BONYEZA DOWLOAD AU PLAY HAPA CHINI..
U

WARAKA WA MAKANISA KUHUSU KATIBA MPYA WAZAGAA MITAANI




Iringa. Waraka uliotolewa juzi na Jukwaa la Wakristo Tanzania wakitaka mchakato wa Katiba Mpya usitishwe, jana ulisomwa katika baadhi ya makanisa na sasa utasambazwa katika jumuiya ndogo za Kanisa Katoliki.
Akizungumzia waraka huo katika Ibada ya Jumapili, Paroko wa Parokia ya Mkwawa ya Kanisa Katoliki Jimbo la Iringa, Padri Oscar Rutechura alisema amechukua uamuzi huo ili kuwawezesha waumini kuelewa vizuri tamko la viongozi wao wa dini kuhusu mchakato wa katiba unaoendelea.
“Katika ibada hii ya leo nitatoa mahubiri kwa muda mfupi, nitafanya hivyo ili niweze kufanya mambo mengi yaliyoko mbele yangu,” alisema Padri Rutechura kabla ya kusoma waraka huo.
Waraka huo ulitolewa kwa pamoja na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (FPCT) na Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA).
Padri Rutechura alitaja mapendekezo sita yaliyomo kwenye waraka huo ambayo ni: Kuitaka Serikali irudishe tovuti ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kulitaka Bunge kuboresha maoni ya wananchi yaliyomo kwenye rasimu ya Katiba na kuacha kuyadharau na kuyapuuza.
Mengine ni kutaka mchakato wa Katiba usitishwe, Bunge la Katiba liendeshwe kwa mujibu wa kanuni, wananchi waendelee kusoma na kufuatilia mchakato na Tume ya Mabadiliko ya Katiba ihusishwe na kupewa mamlaka ya kujibu maswali yanayojitokeza.
Padri Rutechura alisisitiza kuwa ametumiwa waraka huo na Askofu wa Jimbo la Iringa, Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa ambaye kwa sasa ndiye Rais TEC kwa ajili ya kuusoma kwa waumini wote.
Alisema baada ya kuusoma angetoa nakala na kuzigawa kwa viongozi wa jumuiya ndogondogo ili waumini wote wa parokia hiyo wapate fursa ya kuusoma na kuuelewa na watoe uamuzi sahihi.
Padri Rutechura aliwataka waumini kuhakikisha wanajiandikisha kwa wingi kwenye daftari la kudumu la wapigakura pindi Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) itakapotangaza kuanza kuandikisha upya wapigakura.
Alisema hatua hiyo itawasaidia waumini hao kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kupiga kura ya maoni kupata Katiba Mpya au kuipinga, kuchagua viongozi wanaofaa katika uchaguzi wa serikali za mitaa na Uchaguzi Mkuu wa mwakani.
Wakati huohuo, polisi wilaya mpya ya kipolisi, Mbalizi mkoani Mbeya wamewakamata waumini 16 wa Kanisa la Katoliki, Parokia ya Songwe kwa madai ya kutaka kufanya vurugu kwenye kanisa lao.
Paroko wa Parokia hiyo, Ernest Mwashiuya alisema waumini hao walikamatwa jana na kwamba taarifa zaidi zitatolewa na polisi.
Baadhi ya waliokamatwa walisema tukio hilo lilitokea Jumamosi saa 12 jioni wakati wanajadili sehemu ya kusalia ibada ya Jumapili baada ya kutokuwa na imani na paroko wao. Walisema hatua hiyo ilichukuliwa baada ya Paroko Mwashiuya, Jumapili ya Agosti 24 kutamka kwamba waumini wasio na imani naye wasifike kanisani hapo tena.
“Polisi walifika nyumbani kwa Emmanuel Kalomba tulikokuwa tukisali na kutukamata,” alisema mmoja wa waumini waliokamatwa na kuachiwa kwa dhamana.

INASIKITISHA LAKINI INAFUNDISHA PIA, KUTANA NA MTU HUYU ALIYEZALIWA KICHWA CHAKE KIKIWA MGONGONI


A man born with physical disabilities so severe his head is Upside-down has defied the odds to become an inspirational public speaker.

Claudio Vieira de Oliveira, 37, was born with his neck folded back on itself, as well as badly deformed legs and almost no use of his arms and hands. Doctors told his mother to stop feeding him as a newborn as they believed he had no chance of survival. But Claudio from Monte Santo, Brazil, has overcome his extreme disadvantages to graduate as an accountant and become a public speaker. 
"Since I was a child I've always liked to keep myself busy and work - I don't like to depend totally on other people. I do a bit of accounting, research for clients and consulting. I have learned to turn on the TV, pick up my cell phone, turn on the radio, use the internet, my computer - I do it all by myself." he said.
Claudio types with a pen held in his mouth, operates phones and a computer mouse with his lips and has specially made shoes that allow him to move around town. His determined independence saw him succeeding at school and qualifying as an accountant from the State University of Feira de Santana.

When Claudio was born, doctors told his mother Maria Jose he would not be able to survive. Maria Jose said:
"People started saying 'the baby is going to die' because he could barely breathe when he was born. Some people would say: 'Don't feed him, he is already dying'. But there's only happiness now. Claudio is just like any other person - that's how he was raised in this house. We never tried to fix him and always wanted him to do the normal things everyone else does. That's why he is so confident. He is not ashamed of walking around in the street - he sings and he dances."
At eight years old, Claudio, who had previously been carried everywhere, began to walk on his knees.

His family had to change the floor of the house so he could walk around without injuring himself.
Claudio's bed, plugs and lights had to be made lower so that he could do things for himself without asking for help.

He cannot use a wheelchair because of his unusual shape, making it hard for him to be independent outside the home - but he begged his mother to be allowed to go to school and learn with the other children. Doctors have recently diagnosed him with a rare condition called congenital arthrogryposis.

They believe he has multiple joint contractions in his legs and arms which mean they cannot extend properly. Claudio said:
"Throughout my life I was able to adapt my body to the world. Right now, I don't see myself as being different. I am a normal person. I don't see things upside-down. This is one of the things I always talk about in my interventions as a public speaker.
"Nowadays it's much easier to deal with the public, I'm not afraid of it anymore and I can say that I am a professional, international public speaker and that I receive invitations from all over the world."

AJALI: [PICHAZ] MWANAMKE AGONGWA NA DALADALA UBUNGO MAJI



Raia wakijaribu kuokoa maisha ya dada aliyegongwa na gari (daladala) maeneo ya Ubungo maji wakati akivuka bara bara.
 
Majeruhi (dada huyo) akichukuliwa kwenye gari na wasamaria wema.
 
HiIi ndilo gari aina ya Toyota Coaster lenye namba za usajili T454 BBV lililomgonga dada huyo.
 

 
Mwanamke mmoja (jina halijafahamika) aliyekuwa anavuka barabara ya Morogoro maeneo ya Ubungo maji kutoka ng'ambo ya tank na kuelekea upande wa Tanesco amegongwa na gari ya daladala aina ya Toyota Coaster lililodaiwa kuvunja sheria likiwa  linapita kwenye barabara ya magari ya mwendo kasi.
 
Katika ajali hiyo dereva wa basi(daladala) hakupatikana kwani alikimbia baada ya ajali.

MFANYABIASHARA ADAIWA KUMCHARANGA MAPANGA ALBINO MKOANI MOROGORO


Wakati Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro likimshikilia mkazi wa wilayani Mvomero, Johnson Damian Mkude kwa msala wa kumchinja mdogo wake na kupeleka kichwa kwa mganga wa kienyeji ili awe bilionea, jeshi hilo linamshikilia mfanyabiashara mwingine maarufu mkoani hapa aitwaye Lyimo kwa tuhuma za kumcharanga mapanga Damas Valeniani (36) ambaye ni  mlemavu wa ngozi (albino).
Jamaa huyo maarufu kwa jina la Mangi, anadaiwa kutenda unyama huo wiki iliyopita usiku wa manane kwenye Msitu wa Milima ya Uluguru, Mtaa wa Bingwa Kiwasi Juu, Kilakala, wakati mlemavu huyo, akiwa amelala.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, mlemavu huyo alisema:

“Nilikuwa nimelala, ghafla nikasikia mtu akiingia akiwa ameshika panga na kuanza kunikatakata huku akitaka kuninyofoa masikio yangu. Nilimtambua kuwa ni Lyimo ambaye ni jirani yetu.”
 
Eneo la tukio ambalo Bw. Damas Valeniani alishambuliwa kwa mapanga.
Alisema kuwa baada ya kuona hali hiyo, alijitetea vya kutosha na kufanikiwa kuchomoka, kwa bahati nzuri mpwa wake, Mathias John alitokea na kumsaidia huku wakipiga kelele za kuomba msaada lakini tayari alikuwa amshamcharanga panga kichwani na kusababisha atokwe na damu nyingi.

Alisema kuwa kutokana na woga alioupata, aliogopa kulala hivyo alikimbilia kwa mjumbe wa mtaa wao, Filemon Gyuna ambako alipatiwa huduma ya kwanza.
 
Dada wa Damas Valeniani.
 “Kulipokucha ndipo tukaenda kuripoti polisi na kupewa jalada la kesi namba MOR/RB/5122/2014-SHAMBULIZI.

“Polisi walifika nyumbani na kumkamata mtuhumiwa na kumfikisha kwenye mkono wa sheria na mimi nikapewa PF-3 kwa ajili ya matibabu kwenye Hospitali ya Mkoa wa Morogoro,” alisema Damas kwa maumivu makali.
 
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, SAC Leonard Paul akifafanua jambo.

Akihojiwa na mwandishi wetu juu ya tukio hilo, mwenyekiti wa mtaa huo, Ally Malekela alikiri kutokea kwa tukio hilo na kueleza kwamba Lyimo alipewa saa 24 za kuhama kwenye mtaa huo.
Wananchi mbalimbali waliozungumza na Ijumaa Wikienda, walisema Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, SAC Leonard Paul, anatakiwa kufanya kazi ya ziada ili kukabiliana na matukio kama hayo.

Kwa upande wake, mwenyekiti wa Chama cha Maalbino Mkoa wa Morogoro, David Mganga alisema: “Natoa wito kwa jamii ielewe kuwa kiungo cha albino hakiwezi kumpa mtu utajiri au mafanikio, waache kututesa sisi maalbino

JESHI LA POLISI KAHAMA LIMELAZIMIKA KUFYATUA RISASI ZA MOTO, BAADA YA WANANCHI KUCHOMA MOTO WATUHUMIWA


Maafisa wa jeshi la Polisi wilaya ya Kahama wakiwa katika eneo la tukio katika kwaajili ya kuuchukua mwili wa Marehemu.

Inasemekana watuhumiwa hao walivamia chumba ya mkazi mmoja wa mtaa wa Muhungula Kahama na kujeruhi kwa mapanga watoto wawili ussiku wa kuamkia leo.
 
 
 
 
 
 
Endelea kufatilia mtandao huu na muda si mrefu tutawaletea taarifa Kamili.

SHEIKH PONDA AIANGUKIA MAHAKAMA



NA KULWA MZEE, DAR ES SALAAM

KATIBU wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda, ameiangukia Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kwa kuiomba itumie busara kusimamisha kesi ya uchochezi inayomkabili mkoani Morogoro.
Maombi hayo yaliyokwama mara kadhaa kutokana na sababu za kisheria, yaliwasilishwa jana kupitia wakili wake, Juma Nassoro, wakati rufaa yake ya kupinga hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iliyomtia hatiani kwa kuingia kwa jinai katika kiwanja cha Chang’ombe Markaz na kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja nje, ikisikilizwa.
Wakili Nassoro akiwasilisha maombi hayo mbele ya Jaji Augustine Shangwa, aliiomba mahakama hiyo isimamishe kesi ya uchochezi inayomkabili Ponda katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, hadi itakapotoa uamuzi wa rufaa hiyo.
“Mheshimiwa jaji endapo Mahakama ya Morogoro ikimtia hatiani Ponda na kumhukumu wakati Mahakama Kuu ikikubali hoja zake za rufaa na kutengua hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, itaishushia hadhi mahakama.
“Mahakama ikisimamisha kesi ya Morogoro, upande wa Jamhuri hautaathirika kwa kuwa ndio waliofungua kesi, naomba mahakama yako tukufu itumie busara kusimamisha kesi hiyo,” alidai Nassoro.
Katika rufaa hiyo, Ponda anadai hakukuwa na ushahidi wa kutosha kumtia hatiani kwa mashtaka yaliyokuwa yakimkabili.
Ponda na wenzake walikuwa wakikabiliwa na mashtaka ya kula njama, wizi wa mali yenye thamani ya Sh milioni 59.6 na kuingia kijinai kwa nia ya kujimilikisha isivyo halali eneo la ardhi inayomilikiwa na Kampuni ya Agritanza Ltd na uchochezi.
Katika hukumu iliyotolewa Mei 9, 2013, Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa wa Mahakama ya Kisutu alimtia hatiani Ponda peke yake kwa kosa la kuingia kijinai katika eneo la Agritanza Ltd, na ikawaachia huru washtakiwa wengine wote.

Jaji Shangwa aliahirisha kesi hiyo hadi Septemba 10, mwaka huu kwa ajili ya upande wa Jamhuri kujibu hoja za Sheikh Ponda

MSHINDI WA TMT MTOTO MWANAAFA SASA ATEMBEA NA MABAUNSA WAWILI WAWILI... MTAANI KARIAKOO AWA KIVUTIO






Mfanyakazi wa TMT, Happy Ngatunga (Kushoto) akitoa maelekezo kwa Mabaunsa na Mshindi wa TMT aliyejinyakulia Kitita Cha Shilingi milioni 50 katika fainali ya Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa Mlimani City Mwanaafa Mwinzago wakati walipokuwa katika matembezi Kariakoo.
Baadhi ya wafanyabiashara wa Kariakoo wakimpungia Mikono kama ishara ya kumpongeza kwa kuibuka mshindi wa fainali ya Tanzania Movie Talents (TMT) Star wa TMT 2014 kutoka Mtwara, Mwanaafa Mwinzago Wakati alipokatiza kwenye mitaa ya Kariakoo pindi alipokwenda kununua zawadi kwaajili ya wazazi wake
Star Wa TMT 2014, Mwanaafa Mwinzago (katikati) akiwa na furaha mara baada ya kupongezwa na mashabiki waliopata nafasi ya Kumsalimia na kumpongeza wakati akikatiza mitaa ya Kariakoo pindi alipokwenda kununua Zawadi kwaajili ya Wazazi wake 
Wanafunzi wa Shule ya Msingi wakimpongeza Star Wa TMT 2014, Mwanaafa Mwinzago kwa kuweza kuibuka mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 kwa kuwabwaga mwenzake 9 na kuondoka na Kitita Cha Shilingi Milioni 50 za kitanzania wakati walipomuona katika moja ya mitaa ya Kariakoo wakati Star Huyo wa TMT 2014 alipokwenda Kununua Zawadi kwaajili ya kuwapatia wazazi wake ikiwa kama ishara ya Upendo na shukrani kwao.
Matron wa Kambi ya TMT 2014, Kemmy akichagua baadhi ya vitenge kwa Niaba ya Star Wa TMT 2014 Mwanaafa Mwinzago wakati alipopelekwa Kariakoo kwaajili ya Kununua Vitenge kama zawadi kwa wazazi wake.