YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Friday 8 August 2014

STYLE YA NYWELE YA MKE WA RAISI WA CAMEROON GUMZO MAREKANI

Picha: Mtindo wa Nywele wa mke wa rais wa Cameroon wazua gumzo Marekani

posted 4 hours ago by admin
Mke wa rais wa Cameroon Paul Biya, anaefahamika kwa jina la Chantal Biya ni miongoni mwa wake wa viongozi walioungana na wenza wao kuhudhuria mkutano na Rais Obama kuhusu maendeleo na Ustawi wa bara la Afrika.
Lakini jicho la wengi limeanguka kwenye nywele za mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 43 ambazo zimewenakishiwa na kuwekwa katika mtindo wa aina yake ambao huonekana zaidi kwa mabinti wanaotamba katika urembo.
Bi Chantal Biya, yeye haoni haya kuweka mtindo huo hata alipokutana na papa au katika mkutano kama huo wa marais ambapo hawategemei kuona mtindo kama huo katikati yao lakini huo ndio mtindo wake daima. ‘Forever Young!’
Wengine wameanza kuhoji kama mtindo huo wa nywele unaweza kuwa sehemu ya kielelezo cha tabia yake, huku wengine wakipinga mtazamo huo

No comments:

Post a Comment

gfjythfghgfhdfgergdfgbvdfgrfdgdfrgdrgdfrgrdegedrgdrfg