YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Wednesday 15 August 2012

Mtandao wa freemasonry


UNAJUA NINI KUHUSU FREEMASON?
Kwa karne kadhaa sasa kumekuwa na hofu, gumzo na minong’ono  juu ya mitandao inayoendesha siasa za Ulimwengu kwa siri. Mitandao hiyo ni Freemansory na Mafya  ambayo yote iko chini ya nguvu za uzayuni wa kimataifa. Ukurasa wetu huu utajikita  katika kujaribu kuielezea mitandao hiyo zaidi kikiwa kimejikita katika ule mashuhuri wenye jina la “Freemasonry” au kwa utohozi usiyo rasmi “Frimansori”.  Mtandao huu umejengwa na watu walioamuwa kujitowa muhanga wenye kuzingatia miiko na tahadhari zote ili kufanikisha lile walilolikusudia. “Frimansonri” ni tafsiri  inayogeuza kidogo matamshi, inatanguliza n kabla ya s na kisha n. Freemansonry-Frimansori. Katika Ukurasa wetu huu tutatumia tafsiri hii pamoja na neno Mafya.
Walimwengu wamekuwa wakiushutumu mtandao wa  “Freemasonri”  kutokana na matendo yake maovu na ya uhalifu. Kwa sababu hiyo “Frimansori” ni jina linalochukiza masikioni mwa wengi. Hata hivyo, wenye mtandao, badala ya kujibu shutuma, wameendelea kupiga kimya huku wakijitahidi kuupa haiba ya asasi ya kawaida ya kijamii. Wamekuwa makini sana katika kuujenga mtandao huo ambao sasa unaweza kujitapa kuwa umeweza kudhibiti siasa na uchumi wa dunia kwa sura mbali mbali. Maudhui haya yanajaribu kuiweka wazi sura halisi ya “Frimansori”.
Ama  Chachu ya umoja wa kimafiya ni ile falsafa yao ambayo yaweza kuelezwa kwa maneno ya Usekula. Umoja wa kimafyoso au Umafya umejengwa kwa falsafa potofu iliyojengwa kwa dhanna zisizo sahihi au nadharia zenye walakini. Hii ndiyo nukta muhimu ya mwanzo  ambayo “Frimansori”  inakosolewa kwayo. Kwa kutumia rejelea kadhaa kutoka kwa waandishi mbali mbali walioandika kuhusu “Frimansori”  itawekwa bayana hapa kuwa ukosowaji huwo ni muhimu si tu kwa kuwaelimisha watu wasiohusika na shirika hili bali pia kuwapa changamoto wahusika wauone ukweli. Katika hao wapo wanaojua malengo ya ndani ya shirika hilo na wapo wasiojua lolote zaidi kuhusika ili kujipatia manufaa ya kibiashara. Bila shaka Wananchama wa “Frimansori” , kama walivyo watu wengine wako huru kujiamulia mambo yao na hivyo wanaweza kufuata mtazamo wowote wautakao Duniani na wakaishi kwa mujibu wa mtazamo huo. Hii ni haki yao ya kimaumbile. Hata hivyo wengine nao wana haki ya kubainisha makosa yao. Tunazingatia kanuni zilezile za ukosoaji kama tunavyozikosoa jamii nyingine.
Ukurasa huu unakosoa misingi na malengo ya harakati na  shughuli za shirika hili. Pia kwa muhtasari tunaelezea mapisi ya  mapambano ya “Frimansori”  dhidi ya dini zinazoamini Mungu. Frimansori imetoa mchango mkubwa sana katika hila ya Ulaya kujitoa katika dini na katika kuunda utaratibu mpya wa maisha kwa msingi wa falsafa za kumkana Muumba . Aidha “Frimansori”  imeshiriki katika kupandikiza itikadi za kukana Muumba  katika jamii zisizokuwa za kimagharibi kupitia mitalaa ya elimu kwa kuhakikisha inakuwa na watu wake katika sekta hiyo kila nchi. Ukumbi wetu huu pia utaelezea mbinu na njama ambazo Mafia, Mazayuni na Mayahudi kwa ujumla wamekuwa wakizitumia  kusaidia kusimamisha na kudumisha mfumo wa jamii uliojengwa kwa dhana hizi. Inatazamiwa kuwa mambo muhimu yatakayoelezwa katika ukumbi huu yatatoa changamoto ambayo kwayo wengi wakiwemo wadau wa shirika hilo wataweza kuuangalia ulimwengu kwa mtazamo sahihi zaidi. Baada ya kusoma mfululizo wa mada hizi  maalumu kwa watu wanaotaka kuufahamu mtandao huu wataweza kutumia tafakuri na kuyachambua mambo mbali mbali yatokeayo ulimwenguni kwa uoni mpana zaidi. Wataelewa misingi na mielekeo ya itikadi za kisiasa, falsafa, utitiri wa  vyombo vya habari na hasa yale magazeti yanayoandika na kuchapisha habari na picha za ovyo yaliyojazana mitaani hivi na kubaini  malengo yaliyofichikana ndani yake.

No comments:

Post a Comment

gfjythfghgfhdfgergdfgbvdfgrfdgdfrgdrgdfrgrdegedrgdrfg