YOUR MOST FAVORITE BLOG.

YOUR MOST FAVORITE  BLOG.
Calvin

Wednesday, 15 August 2012

0
.
Ishu ya utoroshaji wa wanyama pori ambayo juzi imefanya watumishi watatu wa maliasili kupigwa chini iliingia kwenye page nyingine bungeni Aug 14 2012 baada ya msemaji rasmi maliasili na utalii mchungaji Peter Msigwa kuhoji uhalali wa kutokamatwa kwa ndege iliyobeba wanyama hao.
Amesema pamoja na kwamba Waziri wa maliasili na utalii ametangaza kuwafukuza kazi maafisa watatu, bado sio suluhisho la kudhibiti ujangili kwani mtandao ulioipitisha ndege ya jeshi la Qatar ni mkubwa na unahusisha wafanyakazi wa uhamiaji, Polisi na baadhi ya vigogo serikalini.
“serikali inahusika kwa sababu kuna wakubwa juu yake na kuwatoa wale ni kafara, watupe taarifa ilikuja hapa kufanya nini na ilipotoka hapa ilikwenda wapi, anadanya umma sasa hivi eti anataka kwenda Qatar, anahitaji kwenda Qatar? – Mch Peter Msigwa
Kwenye mistari mingine, mbunge huyu wa Iringa mjini 92.9 amesema hajahusika kuwatetea baadhi ya wamiliki wa vitalu vya wanyamapori kufuatia kuwa na hisa katika miradi hiyo.
2
.
Mara yako ya mwisho kumsikia Profesa Jay kwenye his new single ni lini? ……najua ni time kidogo toka atoe ‘Kamili gado’ ambapo this time karudi na new single ambayo Dully Sykes ametoa baraka zake na kuuza voco kwenye chorus, hii ni time yako kusikiliza mashairi, beat na ujuzi mwingine humu ndani.
Baada ya kuisikiliza.. hakikisha kabla hujaondoka umeacha comment juu ya mapokezi yako kuhusu this new single mtu wangu wa nguvu!
1
.
Huku michuano ya Olympic ikiwa imemalizika tayari, Kituo cha television cha CNN kimeripoti kwamba mwanamichezo Valerie Adams wa New Zealand mwenye umri wa miaka 31, ameshtushwa baada ya kupigiwa simu akiwa njiani kwenye gari yake kueleka nyumbani na kuambiwa kwamba yeye ndio bingwa mpya wa mchezo wa kurusha tufe kwenye michuano ya Olympic 2012.
.
Nadzeya Ostapchuk wa Belarus ambae alishinda hiyo medali ya Gold imegundulika kwamba alitumia dawa za kuongeza nguvu hivyo akaagizwa arudishe hiyo medali.
Kutokana na hiyo ishu, China imepanda kwa kupata tena medali nyingine ya bronz na kupata jumla ya medali 88 kwenye michuano ya Olympic iliyomalizika jumapili iliyopita London Uingereza ambayo kwa mwaka 2016 itafanyika nchini Brazil ikiwa ni nchi ya kwanza ya Amerika Kusini kuwa mwenyeji.
.
0
.
Siku nane zilizopita stori kubwa ya siku area 254, ni Mkali wa muziki wa genge Nonini Mgenge true kutangaza kusain dili la kuwa presenter kwenye radio moja Nairobi yani One Fm.
Baada ya kutangaza hilo dili ilitangazwa kwamba mshkaji atakua Gerald Hando wao kwenye show ya asubuhi kuanzia saa 12 asbh mpaka saa nne ambapo alichukua nafasi ya mtangazaji mwingine aliehamishiwa kwenye show nyingine.
Wengi wanadhani Nonini hii ndio mara yake ya kwanza kufanya kazi kama mtangazaji lakini ukweli ni kwamba alishawahi kufanya hiyo kazi siku kadhaa zilizopita YFM ambayo sasa hivi inaitwa hot 96.
Toka tumepata stori kwamba mshkaji amesain dili la kuwa mtangazaji, nilikua natamani sana kumsikia akiwa mbele ya mic atatema vipi madini, sasa nimefanikiwa kumdaka saa 12 asbh akiwa hewani live August 14 2012… unaweza kumsiliza kidogo akitangaza hapo chini.

kwa hapa Tanzania nakumbuka ni wasanii wawili tu wamewahi kuniambia waliipenda kazi ya kuwa watangazaji japo hawakuwahi kuifanya, ni Izzo Biznes a.k.a Emanuel Simwiga na Hemed Suleiman.’
0
.
.
.
.

BONGE LA JOKA KUBWA LAKAMATWA HUKO AMAZONI, not comfirmed story.

Mitambo iliyotumika kumkamata nyoka mwenyewe..

WATU WANGU WA MANCHESTER UNITED, HII YA WELBECK MSIACHE KUICHEK!



1
Danny Welbeck kushoto.
Hii ni goooooood news kwa fans wa Manchester United kwa sababu yule mkali Danny Welbeck ambae mkataba wake unaisha mwaka kesho kuichezea Man U, amekubali kuongeza mkataba wa miaka mitano wa kuendelea kuishi kwa Sir Ferguson.
Toka mwaka 2008 alipojiunga na Man U, Danny (21) ameshapiga goli zake kumi na kwenye timu zake za taifa za

Story kubwa za magazeti ya leo...

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

MASWALI MANNE YALIYOJIBIWA NA PREZZO IKIWEMO MSHAHARA ANAOLIPWA SASA HIVI KAMA BALOZI.

Najua utakua umesikia sana stori mbalimbali za mshindi wa pili wa Big brother Africa Cmb Prezzo kutoka Kenya lakini nyingine hazina ukweli wowote.

Haya ni maswali manne aliyoyajibu kupitia AMPLIFAYA ya CLOUDS FM Aug 14 2012.
1. Ni kweli kuhusu taarifa zilizoandikwa kwamba unalipwa shilingi milioni nne za Kenya kutokana na kuchaguliwa kuwa balozi?
“ningependa kumfahamisha kila mtu kwamba hii One campaign sio kampeni ya michuzi, ni kampeni ambayo mtu mwenyewe unajitolea kujaribu kuwasaidia kwenye ujumbe wao wanaousambaza, kama leo nimeona kwenye gazeti nikaangalia nikasema ehhh naomba kweli ingekua hivyo, sio kweli kwa sababu mshahara wangu ni kuona watu wanalala wamekula chakula na sio kulala njaa” – Prezzo
2. Kwa time hii kuna uwezekano ukaingia studio kurekodi single yoyote? utatumia studio gani pia?“sasa hivi nimepewa muda wa siku tatu za kupumzika kwa hiyo nazitumia kadri ya uwezo wangu ila baada ya hapo kazi lazima iendelee.. mi huwa sibagui studio lakini sanasana nitakua homeboys studios” – Prezzo
Unakwenda kwenye Consert ya Jay Z Marekani, kuna chochote umepanga kufanya nae?
“Kati ya watu ambao nawaheshimu Jay Z ni mmoja wao so huwezi kujua mwenyezi Mungu kapanga nini mbele ya safari, naamini Mungu anasababu yake kunifanya nipate nafasi kama hii, Mungu alikua ana sababu yake mimi kushinda namba mbili na Keagan kuwa wa kwanza” – Prezzo
Ni kazi gani utakua unafanya kwenye huu ubalozi wa kampeni ya One Campaign?
“Kama balozi wa One Campaign kwa miaka mitatu hivyo nitakua nasafiri kwa nchi tofauti kwenda kuangalia na kuwasaidia watu wenye upungufu wa chakula, lengo ni kumaliza ukame ambapo licha ya malipo kuna njia nyingi tu ambazo unaweza ukalipwa na kama tukiweza kufanikisha kila mtu akawa na chakula nadhani hakuna

Saturday, 11 August 2012

Al-Shabaab kuwaua wanachama wake kunaashiria matatizo makubwa



Na Mahmoud Mohamed huko Mogadishu

Julai 30, 2012
Uamuzi wa Al-Shabaab wa kuwaua wanachama wake watatu kwa tuhuma za kupeleleza kwa ajili ya serikali za kigeni kunaonyesha ukosefu wa imani ndani ya vyeo vya kikundi cha wapiganaji, wachambuzi wa kisiasa na waangalizi wanasema
  • Mpiganaji wa al-Shabaab amesimama akilinda wakati mamia ya wakazi wakiangalia adhabu ya kukatwa viungo hadharani. Al-Shabaab hivi karibuni iliwaua wanachama wake watatu kwa tuhuma za kupeleleza kwa niaba ya serikali za kigeni. [Mustafa Abdi/AFP]
    Mpiganaji wa al-Shabaab amesimama akilinda wakati mamia ya wakazi wakiangalia adhabu ya kukatwa viungo hadharani. Al-Shabaab hivi karibuni iliwaua wanachama wake watatu kwa tuhuma za kupeleleza kwa niaba ya serikali za kigeni. [Mustafa Abdi/AFP]
Al-Shabaab ilisema watu watatu -- Ishaq Omar Hassan,miaka 22, Yasin Osman Ahmed,miaka 23, na Mukhtar Ibrahim Sheikh, miaka 33 -- walikuwa wanapeleleza kwa ajili ya Shirika la Upelelezi la Marekani na Shirika la Upelelezi la Uingereza MI6.
"Hassan na Ahmed wote wawili walihusika na vifo vya Bilal al-Berjawi na wengine watatu [wanachama wa al-Shabaab]," shirika hilo linalohusiana na al-Qaeda lilisema katika mtandao wake wa Twitter tarehe 22 Julai. "Wawili hao waliweka vifaa vya ufuatiliaji katika magari ya al-Berjawi & kaka zake ambayo waliyaongoza makombora yaliyoshambulia vitongoji vya Mogadishu."
Al-Berjawi, mwenye uraia wa nchi mbili za Lebanon na Uingereza ambaye alivuliwa uraia wa Uingereza, aliuawa katika shambulio la kombora mwezi Januari nje ya Mogadishu. Iliripotiwa kuwa alikuwa kamanda msaidizi wa al-Qaeda nchini Somalia.
Waliyoshuhudia huko Marka walisema watu hao watatu waliuawa na kikosi chenye silaha katikati ya mji.
"Wapiganaji wa al-Shabaab ilitumia vipaza sauti vilivyofungwa katika malori kuwaita watu kushuhudia mauaji na watu walipokusanyika uwanjani, dazani ya wapiganaji waliyofunika nyuso zao waliwafunga vitambaa machoni watu hao watatu na kisha kuwapiga risasi, wakiwaua hapo hapo," mkaazi wa Marka Mohamed Said, miaka 34, aliiambia Sabahi

Tatizo la Al-Shabaab la kujiamini.

Omar Dahir, mkurugenzi wa Kituo kilichopo Mogadishu cha Marekebisho na Mjadala, alisema matatizo ya al-Shabaab yanatokana na kuongezeka kwa mgawanyiko miongoni mwa wanachama na kunaweza kusababisha kusambaratika kwa haraka kwa kikundi katika siku karibu zijazo.
"Kuna kutojiamini ndani ya al-Shabaab, kwa kuwa kikundi hakiwaamini wanachama wake na sasa viongozi wake hawaaminiani," Dahir aliiambia Sabahi. "Uamuzi wa al-Shabaab kuwaua wanachama wake watatu huko Marka unaonyesha ukosefu wa imani ambao unakikabili kikundi."
"Hii inaweza kuwa mwanzo wa kuvunjika kwa mipango ya mapigano iliyoandaliwa ndani ya kundi hilo, ambalo tayari linasumbuliwa na mgawanyo mkubwa," Dahir alisema.
Alisema al-Shabaab inaweza kukimbilia kuwaua kwa siri wengi wa wanachama wake kwa kuogopa kuwa kufanya mauaji mara mingi mbele ya wananchi kunaweza kuyumbisha umoja wa kundi hilo.
"Kundi hili litamuua mwanachama yeyote anyeshukiwa kuwa na uhusiano na pande za nje kwa sababu wanaogopa kuwa mashirika ya upelelezi ya Ulaya yanaweza kupenyeza kwenye kundi hilo na kuwalenga viongozi wao wanaotakiwa," Dahir said.
Al-Shabaab ilisema katika mtandao wa Twitter kuwa imezindua kampeni kubwa ya kukabili upelelezi ili kusafisha nchi kutokanana na majasusi hao .
Mwaka uliopita , kiongozi wa al-Shabaab Mualim Hashi Mohamed Farah alisema Kitengo cha upelelezi cha Ulaya kimepenyeza kwenye safu ya maaskari wa al-Shabaab, na mawakala wa pande mbili wanaojifanya kuwa wapigananaji wa vita vitakatifu.
Huu sio muda pekee kwa al-Shabaab kuwaua washirika wake waliotuhumiwa kwa kupeleleza kwa niaba ya mawakala wa upelelezi wa Kimagharibi. Al-Shabaab ilimuua makamu wa kiongozi wao mkuu wa upelelezi, Ahmed Ali Hussein, pia anajulikana kama Ahmed Keyse,mwaka 2010 kwa "upelelezi " wa serikali za kigeni.
Tarehe 27 Julai, al-Shabaab ilisema iliwakamata "wapelelezi watatu wa TFG" ambao kwa sasa wanahojiwa. "Kama watatiwa hatiani watu hao watatu watauawa hadharani," al-Shabaab ilisema katika Twitter.

Tuzo yazidisha tatizo ndani kati ya al-Shabaab

"Vurugu za kujiamini zimetawala katika sura ya nchi ndani ya kundi la al-Shabaab,ambazo zimesababisha mauaji ya washirika wake," alisema Abdirahman Mohamud, mwangalizi wa makundi yenye msimamo mkali.
Tangu Marekeni ilipotangaza tarehe 7 Juni kwamba itatoa zawadi ya hadi Dola za Marekeni milioni 33 kwa taarifa zinazowahusu wapi walipo viongozi saba wa ngazi ya juu wa al-Shabaab, viongozi wanaotafutwa wamejificha dhidi ya sio tu kikosi cha upelelezi lakini pia dhidi ya macho ya jamii na washirika wao.
"Viongozi wa al-Shabaab sasa wana wasiwasi kwamba Marekeni kutoa tuzo ya fedha kutasababisha kutoa msukumo kwa baadhi ya washirika wa kundi, ambao watahamasishwa na uroho waa pesa, kuwasaliti viongozi wao na kutoa taarifa kuhusu walipo ili wajipatie zawadi za fedha," Mohamud aliiambia Sabahi.
"Kwa maoni yangu huo ni motisha kwa uamuzi wa al-Shabaab hivi karibuni kuwaua washirika wake watatu kwa tuhuma za kufanya upelelezi kwa niaba ya mawakala wa kipelelezi wa Marekani na Uingereza," alisema.
Mohamud alisema al-Shabaab imegawanyika katika kambi mbili, na kila moja "itafanya ukatili" dhidi ya nyingine.
Mwezi Machi, kiongozi wa al-Shabaab Hasan Dahir Aweys alilaumu kikundi cha wanamgambo kwa kuwaua wananchi bila ya malengo kwa jina la kiislamu na kwa kushirikishwa kwake na al-Qaeda. "
Kundi lenye msimamo mkali la al-Shabaab lilifanya mauaji mengi katika miaka michache iliyopita, yakilenga sio tu washirika wake lakini pia na wananchi wengi wa Somalia waliotuhumiwa wakifanya kazi na upelelezi kwa ajili ya mawakala wa upelelezi wa Kimagharibi au wakishirikiana na majeshi ya serikali ya Somalia au Umoja wa Afrika," alisema Abdullahi Osman, mchambuzi wa masuala ya kisiasa na mtaalamu katika masuala ya vikundi vya waislamu wenye msimamo mkali nchini Somalia.
Osman aliiambia Sabahi kwamba al-Shabaab wanawafanyia ugaidi wananchi wa Somalia na wanatishia kuwaua wale ambao wanashirikiana na serikali au Umoja wa Afrika waliopo nchini Somalia.
Alitoa wito kwa serikali ya Somalia kuimarisha jitihada zao ili kuyakomboa maeneo yaliyobakia chini ya udhibiti wa al-Shabaab kumaliza uhalifu wa kuchukiza unaofanywa na kikundi hicho.
"Al-Shabaab itaendelea kufanya vurugu za kutokuwa na hadhari na kutochagua kwa uangalifu dhidi ya wananchi wa Somalia hadi kundi hilo litakapotolewa nchini," alisema.

TEMBO AVAMIA MAKAZI YA WATU, NAO WAMFAIDI NYAMA.

Hallow people...

STORY KUBWA ZA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI TAREHE 12/8/2012